Hataki kuchukua mahari yake nifanyeje??

Hataki kuchukua mahari yake nifanyeje??

Status
Not open for further replies.
Dada imebidi nisome uzi wako wa mwanzo.
Sababu yako ni nyepesi mno na umewadharau mume na mkwe wako ungekaa palepale.
Wao hawakukukataa.
Walitaka ulee mtoto akiwa kwao.

Nb
Kama ni mkristo ukiposwa, pande zote mbili za wazazi wakakubali, tena mkazaa na mtoto na mahari na pesa ya uharibifu ikalipwa wewe ni MKE tayari na usimuone jamaa mjinga kutochukua hiyo mahari anajua anachokifanya....hakuna mtu atakayejua story yako halafu atake kukuoa ikiwa mahari jamaa hajachukua.

What to do!
Go back kwa mama yako mkwe!
 
Kwani huyo mwenzako anaetaka kurejesha mahari kuna mahali amesema alikuwa ananyanyaswa au wewe ndo una stress....mana unaonekana uliwahi kupitia hayo mambo na huko ulipoenda ulitegemea utasahau yaliyopita lakin ukakuta ni yale yale ya "wanaume wote ni mbwa"

Tumia basi akili sio kukurupuka kama mkojo wa asubuhi umesoma comments mbili tu unaleta utumbo hapa vyote alishaeleza huko usiniletee stress zako nyie ndiyo mnakuwa wanyanyasaji wa wanawake kisa umezaa naye
 
Mmevalishan mbele ya wazazi ndugu..mkazaa sa hv mnatengana kwa sababu ambazo naona dah...ila jamaa hana cha kupoteza itakuwa ashahesabu mtoto anaye anahudumi....kuzaa kwemye uchumba nayo ni challenge sana..au bila ndoa
 
Eti 'mimi ni mvumilivu'

Miezi mitatu tu unataka kurudisha mahari!!!!!!!!!!!! Alafu unajiita mvumilivu....mvumilivu my foot.
Kweny masuala ya mahusiano jitahid sana kutatua changamoto zako bila kusikiliza watu wengine wanasema nini hata kama ni wazazi.
Nyie wabena, wasangu, wahehe kweny mahusiano mna kawaida ya kusikiliza nyumban wamesemaje, yani baba au mama kasema nini na sio kile kilichopo akilini mwenu.
Eti baba na mama wanasema najibembeleza sana kwa uyo mwanaume...aiseee!!!!
Sasa walitaka ujibembeleze kwa nan? Wenzako ndoa wanazipigania miaka wewe miezi mitatu tu chaliiii eti umechoka.
We sema tu kuwa umeshapata mtu mwengine ndan ya mda mfupi now unataka maoni ya wadau ili moyo wako upate aman wakat unajua sio sawa.
Kabla ya yote jiulize kwanini ataki kuchukua mahari yake??? .......Ni kwa sababu anajua tayari mna mtoto na kipaumbele chake ni mtoto sio wewe hivyo haoni haja kuchukua mahari ila wewe unajistukia mana tayari unataka kuleta ingizo jipya wakati jamaa amekaa kmyaaaa anakusoma tu.
Mkuu mpaka nataka kurudisha mahari yake nmevumilia mengi sana. Mpaka mahusiano yamwfika hapa kuna mengi nmevumilia na hadi nataka kurudisha mahari yake nmeridhia kwamba hatakuja kubadilika kuwa yule mume mwenye maamuzi yake binafsi kama baba wa nyumba
 
Matatizo ya watanzania hawasomi wakaelewa kabisa. Wapi nimesema nimeingia au ninaingia kwenye mahusiano mapya?? swali lilikuwa je kubaki na mahari yake haina shida kama kutakuwa na mtu atataka kutoa mahari kwa baadae? Sikuchepuka wala sina hiyo tabia aliniacha kwa sababu hakutaka nirudi kwetu baada ya kujifungua.
Sasa kwann urudi kwenu mzee mama wakati hapo ulipo ndipo kwenu?

Makabila mengine hasa langu mwanamke akizingua tunawezafuata mahari maana inakuwa ni gharama kubwa na ndiyo utaratibu.

Wewe kabila gani na jamaa kabila gani?
 
Hata mimi pia sijapoteza kitu mkuu sababu mtoto wangu ni zawadi nzuri sana na sijutii kumzaa ananipa furaha sana. Mengine Mungu anapanga mwenyewe.
Mmevalishan mbele ya wazazi ndugu..mkazaa sa hv mnatengana kwa sababu ambazo naona dah...ila jamaa hana cha kupoteza itakuwa ashahesabu mtoto anaye anahudumi....kuzaa kwemye uchumba nayo ni challenge sana..au bila ndoa
 
Kama hauko kwenye mahusiano mapya tulia basi haraka ya nini?

Usikute jamaa bado anajifikiria hasa mtoto wake .

Unataka uachane nae saivi halafu baadae uje kuleta vilio vya kisingo maza hapa wakati mambo umeyataka mwenyewe .

We tulia jamaa ubongo uformat upya aanze kukuona malaika .

Ni mtazamo tu
Ndiyo maana ndoa hazidumu.

Wamegombana tu wanakimbilia kuachana. Uvumilivu haupo.

Wanashindwa kuelewa ugomvi ni sehemu ya ubinadamu wanaweza kuyasahau yaliyopita maisa yakaendelea.
 
Matatizo ya watanzania hawasomi wakaelewa kabisa. Wapi nimesema nimeingia au ninaingia kwenye mahusiano mapya?? swali lilikuwa je kubaki na mahari yake haina shida kama kutakuwa na mtu atataka kutoa mahari kwa baadae? Sikuchepuka wala sina hiyo tabia aliniacha kwa sababu hakutaka nirudi kwetu baada ya kujifungua.
Nini kilikulazimu kurudi kwenu baada ya kujifungua ?Kulikuwa na ulazima wowote?
 
Sasa kwann urudi kwenu mzee mama wakati hapo ulipo ndipo kwenu?

Makabila mengine hasa langu mwanamke akizingua tunawezafuata mahari maana inakuwa ni gharama kubwa na ndiyo utaratibu.

Wewe kabila gani na jamaa kabila gani?
naomba usome coment 138 utaelewa kwanini nimerudi nyumbani...Mimi ni mbena na mwenzangu mchaga.
 
Nini kilikulazimu kurudi kwenu baada ya kujifungua ?Kulikuwa na ulazima wowote?
Nimeelezea kwenye coment namba 138 sababu za kurudi nyumbani nililazimika kurudi
 
Mtoto alishalipa hela ya uchafuzi maana mahari alitoa kipindi nina ujauzito. Mimi nahitaji kujua je kubaki na mahari yake haitaleta shida?? na vile hataki tuvunje uchumba mbeleni hawezi kuleta shida kwamba huyu ni mchumba wangu halali??
Kwani kwenye uchumba kunatolewaga vyeti vya uhalali?
 
Wewe kaka unaweza kuwa huna akili timamu na stress za maisha yako zinakusumbua. Labda nikwambie kwa ufupi utaelewa kwanini nilirudi nyumbani.
Nilipotolewa mahari ndugu zake walisema inabidi nikae na mama kwe nikijifungua nikaenda na nilipojifungua mama mkwe alikuja kunihudumia lakini aliondoka baada wa wiki mbili tuu akaniacha na dada wa kazi. Hapo ulikuwa uzazi wangu wa kwanza na nilikuwa sijui chochote.
Kuna wakati nilikuwa nashinda njaa while mtoto anahitaji kunyonya unakuta siwezi kujipikia au dada wa kazi ananipikia chakula kibichi. Nilimweleza mwenza wangu lakini hakuna measure ya maana iliyochukuliwa nadhani labda utapata picha kwa nn nililazimika kurudi nyumbani. Ikafika hatua nikapata homa baada ya uzazi na sikuwa nna msaada wa maana.
Upande wa tabia za familia yangu no familia ya kikristo na wameshika dini.Huyo mwenza wangu toka ilipotolewa mahari mwaka jana mwezi wa 6 mpaka leo hata kuwasalimia wakwe zake kwa simu hajawahi. Mimi binafsi sina kiburi ni mvumilivu sana sababu mpaka tumefika hapa tulipofika nmemvumilia sana na bado nikawa napigania familia isivunjike kwa ajili ya mtoto wetu.
Siku nyingine usikurupuke kutukana watu wakiomba ushauri sababu hujui amepitia wapi na hawezi eleza kila kitu katika maisha yake.Jifunzeni kuwa na busara.
Hata uandike kitabu hili la kusema unataka rejesha mahari halivumiliki....
Si kitu cha kawaida kabisa Mwanamke kuongea. Chunga ulimi wako.
Na kama umeshalitamka hili kwa huyo jamaa umemkosea adabu sana sana saanaa... Na ni lazima umuombe msamaha.

Haya uliyoyaongea hapo yote yanazungumzika. Just in one night. Sasa sielewi ni utoto unakusumbua au kuna watu wanakushauri vibaya.

Wahenga waliposema "kuwa uyaone..." hawakumaanisha magorofa.. Ila changamoto kama hizo za maisha.
Kukua na kukomaa akili ni kuzitatua kwa busara na sio kufikia maamuzi kama ambavyo umshaamua.

Utataabika sana.
 
Yaani nitulie nimsubiri afomart upya ubongo wake kisa kaniacha bila sababu?? Niendelee kumbembeleza sababu naogopa kuwa single maza?? Mimi mtoto wangu ni zawadi yangu kama baba aliamua kuondoka aende na mimi pia maisha yaendelee aisee
Nadhani unatuchora...huwezi kuongea kwa kibri hivi. Dunia haihitaji watu wenye viburi vya namna hii. Ukija kuwa mkubwa utajutia maamuzi uliyokuwa unayafanya ujanaani.

Be humble..usitumie jazba, kibri na umwamba kufanya maamuzi. Haijawahi kuleta faida..unailisha ego ikishashiba unajutia...
 
Kaka yangu laiti ungemjua mkwe wali alivyo usimgenishauri nirudi hapa naandika kwa kifupi tuu na pia natunza heshima ya mwemzangu sababu yupo humu na nafwatilia sana ila nngeandika kila kitu ungeungana na mm kurudi nyumbani au ungehamia kumshauri mwenzangu jinsi ya kuishi na familia yake
Kumbe yupo humu!
Basi pia unachofanya kitakuwa na athari ataona unafuata ya mtandaoni na si ushauri wake.
Ila ki msingi we ni bado mke wake mpaka sasa.

Tumia njia nyingine ya kupatana wachagga ni watu poa sana when it comes for family ila ni wagumu kubadili misimamo ya maamuzi yao pale ambapo anahisi amedharauriwa( from experience) Solve this please na utaenjoy ndoa yako. Pia, kila unalosoma changanya na za kwako.

Kama jamaa upo humu please do the needful this usiache mke kirahisi hivi.
Kwaharaka haraka kulikuwa na external force, solve this like a man. Najua unapita kama Trudie akivyosema.
All the best both of you.
Mungu anachukia kuachana.
Pasaka njema kwenu.
 
Kwa haraka Haraka Hapa..Wewe Bibie Unaonekana Unataka Sana Kuachana Na Jamaa..Aingii Akilini Miezi Miwili Unataka kurudisha Mahari..Ushauri wangu ni Kwamba Tulia ujitafakari kwanza..

Mpaka Jamaa Alikubali Kutoa Mahari Ni Kwamba Amekubali kuishi Na Wewe.

Kiukweli Vijana Now ..Wamebadilika sana..Mabiti wamekuwa Na Viburi kuanzia kwenye Hatua Za Uchumba ..Na Kwa Haraka Haraka Wewe Utakuwa ni wa kutokea Kusini ama Kaskazini Mwa Tanzania.una Sound ivyo kitabia

Jitafakari mtoto Bado mdogo Na Uyo Ni mzazi Mwenzio.
Mkuu afadhali umesema.


Vijana wamejaa viburi saana....wanaonyeshana umwamba.
 
Nimeelezea kwenye coment namba 138 sababu za kurudi nyumbani nililazimika kurudi
Nimesoma pole sana,Ina maana kwenu mtu akitolewa mahali tu...mchezo unakua umekwisha? Mbona kama mliamua kuishi bila kufuata utaratibu?
 
Hapo kuna mambo kadhaa yanaleta mkanganyiko. lakini naweza ng'amua yafuatayo

1. Kama jamaa hakupendi na hakutaki angeichukua hiyo mahari.
wewe ni Mkristo au muislam??.
Kama ni Mkristo mahari si walipewa wazazi wako. Wewe huna jukumu lolote la kuirudisha mahari bali wazazi ndio wahusika. Au umeshaongea nao??.

2. Mtoto anamiezi saba unawaza habari za kuchumbiwa upya kwa kutolewa mahari. Ndio maana unahofia huko mbeleni mshikaji asije kukuharibia mpango mzima. Kama wewe si mwenye tatizo mbona unaulizia habari za kurudisha mahari mapema yote hii kama mtu anayejihami.

3. Inaonekana alikupa mimba kwa starehe tuu. Aidha hukumpenda au hakukupenda. Yaani ilikuwa ni bahati mbaya. Na ndipo akalazimika kutoa pesa ya kukuchafua na mahari juu ili kuua Soo. Kama ni hivyo hapa unapaswa uwe makini zaidi kwani ukicheza unaweza shangaa ukapewa mimba ya pili mpaka ya tatu na wanaume tofauti tofuati kama Mbwa.

4. Kama wote ni Wakristo na mnafanana kitabaka na kihadhi yaani elimu na hali ya uchumi. Sidhani kama hili ni jambo kubwa la kutengana. Lakini kama hamfanani na mlikutana kukidhi haja ya mwili basi kuna ugumu kidogo.


Ushauri; Kuolewa ukiwa single Mama kuna athari kubwa sana. Usijidanganye wala asikudanganye mtu. Kama hutanyanyasika wewe basi mtoto atanyanyasika. Mimi nimeishi maisha hayo. Naelewa ninachokisema. Kama hakuna ulazima wa kuachana Fight huyo mshikaji awe mumeo.

Sababu ya kuachana hakuna. Kumbuka sababu kubwa ya kutengana ni Kufumaniwa, Au mwanaume/mwanamke kupatwa na matatizo makubwa ya kiakili.

Pia huna ushahidi kuwa jamaa kakuacha. Hivyo hapa unatafuta ruhusa ya kuharibu future yako au ya mtoto.
 
naomba usome coment 138 utaelewa kwanini nimerudi nyumbani...Mimi ni mbena na mwenzangu mchaga.
Kwa hiyo ulirudi nyumbani ili afuate utaratibu wa kufunga nawe ndoa?
 
Nimesoma pole sana,Ina maana kwenu mtu akitolewa mahali tu...mchezo unakua umekwisha? Mbona kama mliamua kuishi bila kufuata utaratibu?
Hapana ndoa waliahidi iwe mwezo huu wa nne ila baada ya kutoa mahari walisema wao mila zao lazima nijifungue kwa uangalizi wa mama mkwe ndio maana nikaedna kujifungua huko.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom