Hataki kuchukua mahari yake nifanyeje??

Hataki kuchukua mahari yake nifanyeje??

Status
Not open for further replies.
Hasira hizo ndo wanakwake wanakimbilia huko! Wanadhani wanamkomoa mwanaume?
Ndo maana anasema akitokea mwanaume mwingine akitoa mahari hakuna shida?

Mwambie ukishapigwa mhuri "kuzalishwa" uwezekano wa kuolewa lazima utumie mbinu za kujeshi
Ndio wanaume mnavyojidanganya hivyo kwamba ukishazaa uwezekano wa kuolewa ni mdogo? Na ndio manatumia kama silaha ya kuwatesa baby mama zenu ili muendelee kuwanyanyasa...
 
Mpaka tabia yako umeiweka wazi...kwa andiko hilo tu...
Pole sana mkuu nimegundua una stress ndio maana unaropoka yasiyokuwepo. nakushauri ungetulia na familia yako achana na mambo ya michepuko huo ndio umalaya sasa[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Kama hauko kwenye mahusiano mapya tulia basi haraka ya nini?

Usikute jamaa bado anajifikiria hasa mtoto wake .

Unataka uachane nae saivi halafu baadae uje kuleta vilio vya kisingo maza hapa wakati mambo umeyataka mwenyewe .

We tulia jamaa ubongo uformat upya aanze kukuona malaika .

Ni mtazamo tu
Yaani nitulie nimsubiri afomart upya ubongo wake kisa kaniacha bila sababu?? Niendelee kumbembeleza sababu naogopa kuwa single maza?? Mimi mtoto wangu ni zawadi yangu kama baba aliamua kuondoka aende na mimi pia maisha yaendelee aisee
 
Uyo unae uyo mahari kagoma kuchukua na hakika atakuharibia na pengine anakupima tu kuona upepo wako cha msingi kuwa na busara Lea mtoto wako wala usiwe na maneno mengiiii nae fika wakati muulize kuhusu ndoa n.k

MTU alie sirias kuvunja uhusiano angechukua mahari yake alafu in mchaga wee uyo anakupima tu
 
Ndio wanaume mnavyojidanganya hivyo kwamba ukishazaa uwezekano wa kuolewa ni mdogo? Na ndio manatumia kama silaha ya kuwatesa baby mama zenu ili muendelee kuwanyanyasa...
Ni bora usuluhishe ndoa yako muendele kulea mtoto wenu huko uendako ni giza unaweza kuolewa mtoto akanyanyasika au wewe
 
asante kwa ushauri angalau kuna watu wanaelewa ninachotaka kujua sio wanaokurupuka kunitukana tuu
Uyo unae uyo mahari kagoma kuchukua na hakika atakuharibia na pengine anakupima tu kuona upepo wako cha msingi kuwa na busara Lea mtoto wako wala usiwe na maneno mengiiii nae fika wakati muulize kuhusu ndoa n.k

MTU alie sirias kuvunja uhusiano angechukua mahari yake alafu in mchaga wee uyo anakupima tu
 
Ni bora usuluhishe ndoa yako muendele kulea mtoto wenu huko uendako ni giza unaweza kuolewa mtoto akanyanyasika au wewe
Sasa mkuu utasuluhisha vipi na mtu ambae hataki? Nimejitahidi sana mpaka nikafikia hatua ya kumove on. Sababu kiukweli hakukuwa na kubwa lolote la kusema tuachane kwa kuwa aliamua basi haina budi kukubali. Imefika hatua hadi watu wananisema najibembeleza kwa mtu ambae hanitaki sababu ya kupigania familia yangu mwishowe nikakubali matokeo.
 
Kuachana/kutengana kwa wazazi mkiwa tayari mna mtoto/watoto ni ubinafsi.

Kama wote mngeweka ubinafsi pembeni na kumfikiria mtoto wenu mdogo (ndo kwanza miezi saba) hakika mngeyasuluhisha na maisha yaendelee.

Fikiria mtoto anaenda kulelewa na mzazi mmoja, atakuwa na malezi gani? Atafikiaje malengo yake ukubwani? Atakuwa mtoto wa aina gani? Kwa nini mnamkatili mtoto haki yake ya msingi ya kulelewa na wazazi wote wawili kwa upendo?

Mnaanza kumjengea mazingira magumu ya ukuaji kwa kujifikiria nyinyi (ubinafsi) aje alelewe na mzazi wa kambo, apate mateso, akue kwa shida na taabu nyingi, akose elimu bora, upendo wa wazazi kisa tu nyie mnashindwa kutatua matatizo yenu? Ni kweli hayatayuliki na mkaendelea kupendana na kulea mtoto wenu?

Hebu mfikirieni huyo malaika kwanza kabla hamjarudishiana mahali
 
Kwa haraka Haraka Hapa..Wewe Bibie Unaonekana Unataka Sana Kuachana Na Jamaa..Aingii Akilini Miezi Miwili Unataka kurudisha Mahari..Ushauri wangu ni Kwamba Tulia ujitafakari kwanza..

Mpaka Jamaa Alikubali Kutoa Mahari Ni Kwamba Amekubali kuishi Na Wewe.

Kiukweli Vijana Now ..Wamebadilika sana..Mabiti wamekuwa Na Viburi kuanzia kwenye Hatua Za Uchumba ..Na Kwa Haraka Haraka Wewe Utakuwa ni wa kutokea Kusini ama Kaskazini Mwa Tanzania.una Sound ivyo kitabia

Jitafakari mtoto Bado mdogo Na Uyo Ni mzazi Mwenzio.
 
Habari wanajf na heri ya pasaka.

Niende kwenye lengo la uzi...mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miezi 7 nina miaka 26. Miezi 3 iliyopita nilitengena na mzazi mwenzangu ambaye alishanitolea mahari na kunivalisha pete ya uchumba kwa sasa nipo nyumbani na mtoto wangu.

Mwanzoni nilipata wakati mgumu sana kukubali kwamba tumetengana lakini namshukuru Mungu sasa hivi nimekubaliana na hali na nipo vizuri kabisa.
Baba mtoto wangu alikataa kabisa kuchukua mahari yao na pia kuwashirikisha wazazi juu ya kutengana kwetu kwa madai tulikutana wawili tuu wakati pete tulivalishana mbele ya wazazi na ndugu wa pande zote.
Swali langu ni je naweza kuingia kwenye mahusiano mapya wakati yeye hajachukua mahari yake? Na je kwa mfano mtu akataka kuja kutoa mahari inakuwaje kuhusu mahari yao ya mwanzo haitakuwa na shida yoyote maana hataki kuchukua kabisa na watu wanasema kubaki na mahari yake itanifunga sababu kimila bado nitakuwa mke wake. Ninachohofu mbeleni asije leta shida akasema ni mchumba wake halali sababu temetengana kienyeji sana. Naombeni msaada wa mawazo juu ya hili.
Asanteni kwa mchango wenu.

Mpesa
 
aliyenitolea mahari ndie alivunja uhusiano. Nadhani watu wengi huwa hawasomi mada wakelewa wanakimbilia kucoment. Sababu nimeuliza madhara ya kukaa na mahari yake haina shida kwa baadae coment nyingi zinashutumu nakimbilia kuolewa
Kwani kuzaa au kuchumbiana lazima.muoane? Kama kumetokea mazonge zonge si bora kuachana kabla hamjaingia kwenye ndoa, kuvunja uchumba ni rahisi sana kuliko ndoa
 
Umeshaanzisha balaaa hta huyo atakuacha pia
 
Matatizo ya watanzania hawasomi wakaelewa kabisa. Wapi nimesema nimeingia au ninaingia kwenye mahusiano mapya?? swali lilikuwa je kubaki na mahari yake haina shida kama kutakuwa na mtu atataka kutoa mahari kwa baadae? Sikuchepuka wala sina hiyo tabia aliniacha kwa sababu hakutaka nirudi kwetu baada ya kujifungua.
Wengine hawasomi Uzi vizuri wanakimbilia comments za watu watu wengi hawapendi kusoma hujasikia ukitaka kumficha kitu mbongo kiweke kwenye kitabu hata gundua kamwe
 
Kuachana/kutengana kwa wazazi mkiwa tayari mna mtoto/watoto ni ubinafsi.

Kama wote mngeweka ubinafsi pembeni na kumfikiria mtoto wenu mdogo (ndo kwanza miezi saba) hakika mngeyasuluhisha na maisha yaendelee.

Fikiria mtoto anaenda kulelewa na mzazi mmoja, atakuwa na malezi gani? Atafikiaje malengo yake ukubwani? Atakuwa mtoto wa aina gani? Kwa nini mnamkatili mtoto haki yake ya msingi ya kulelewa na wazazi wote wawili kwa upendo?

Mnaanza kumjengea mazingira magumu ya ukuaji kwa kujifikiria nyinyi (ubinafsi) aje alelewe na mzazi wa kambo, apate mateso, akue kwa shida na taabu nyingi, akose elimu bora, upendo wa wazazi kisa tu nyie mnashindwa kutatua matatizo yenu? Ni kweli hayatayuliki na mkaendelea kupendana na kulea mtoto wenu?

Hebu mfikirieni huyo malaika kwanza kabla hamjarudishiana mahali
Mkuu nimejaribu sana kusuluhisha lakini baba mtoto hajakubali kabisa mpaka nikamuuliza kosa langu ni kurudi nyumbani au kuna lingine nijue hana jibu. Unajua wakati mwingine huwezi jua Mungu anatuepushia nini katika maisha yetu
 
Kwa haraka Haraka Hapa..Wewe Bibie Unaonekana Unataka Sana Kuachana Na Jamaa..Aingii Akilini Miezi Miwili Unataka kurudisha Mahari..Ushauri wangu ni Kwamba Tulia ujitafakari kwanza..

Mpaka Jamaa Alikubali Kutoa Mahari Ni Kwamba Amekubali kuishi Na Wewe.

Kiukweli Vijana Now ..Wamebadilika sana..Mabiti wamekuwa Na Viburi kuanzia kwenye Hatua Za Uchumba ..Na Kwa Haraka Haraka Wewe Utakuwa ni wa kutokea Kusini ama Kaskazini Mwa Tanzania.una Sound ivyo kitabia

Jitafakari mtoto Bado mdogo Na Uyo Ni mzazi Mwenzio.
mkuu yeye ndio aliniacha na miezi 3 imeshapita toka tumetengana ndio maana. Mimi asili yangu sina kiburi na ni mvumilivu sana aisee
 
Ndio wanaume mnavyojidanganya hivyo kwamba ukishazaa uwezekano wa kuolewa ni mdogo? Na ndio manatumia kama silaha ya kuwatesa baby mama zenu ili muendelee kuwanyanyasa...
Wanaolewa sana na unaweza kuta kuna mabinti kibao sehemu hiyo lakini single mother anaolewa na Mme ambaye hajawahi kuoa wala kuzaa, kuolewa ni bahati ya mtu
 
Nimeshapitia nyuzi nyingi hapa nimegundua anachouliza mhusika na coment zinakuja tofauti sababu watuhawataki kusoma wakaelewa. Unakuta mtu anaanza kutukana ukijiuliza hakuna hata sababu
Wengine hawasomi Uzi vizuri wanakimbilia comments za watu watu wengi hawapendi kusoma hujasikia ukitaka kumficha kitu mbongo kiweke kwenye kitabu hata gundua kamwe
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom