Alinikubalia nirudi nyumbani lakini mama yake aliposikia akamlazimisha niende kwao Moshi na yeye wakati procedure za kwenda nyumbani zimekamilika. Nikamwomba tusogeze mbele kwenda Moshi kwakuwa ametaka ghafla ndipo mama yake alipokasirika. Na yeye akabadilika akawa hataki niondoke na akasema nikiondoka niende moja kwa moja
Inshort kuna mambo yaliyonilazimisha kwa kipindi kile nirudi nyumbani na mwenza wangu anamsikiliza sana mama yake hata kitu mkikubaliana wawili anamshirikisha mama akikataa basi na yeye anakubali tuu hadi mambo personal.
Mfano mzuri tulitaka kubadilisha dada wa kwazi sababu alikuwa ana mambo ya wanaume sana asingeweza kulea mtoto tukakubaliana na mwenzangu nikamwomba mama yangu atutafutie akampata kabisa ikabaki kumwagiza aje tunapokaa.Mwenzangu alipomshirikisha mama yake akakataa tusibadilishe nae akakubali kumbuka alishafatutwa mpya.
Je hakufukiria mtoto wake ataishije na dada anayeshinda kwa wanaume pale sisi tutakapoenda kazini? Hajui madhara yake?