Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,107
- 6,042
Hawa wakazi wa kusini naamanisha mikoa ya Lindi na Mtwara najua kabisa wana hamu kubwa sana ya mabadiliko. Kwa sasa mimi nipo mtwara, nilipita huko mtaani yaani hali inakatisha tamaa, hawa jamaa yaani wanahitaji mabadiliko haswa na isitoshe wana hamu sana ya kumsikia Dk Slaa. Na ijulikane kwamba CCM NA CUF imeshamiri sana pande za huku,isitoshe wiki kadhaa Dk Slaa alipanga kuja huku...watu toka vijijini na pande nyingine walikaa uwanja wa mashujaa tangu asubuhi mpaka pale walipopata taarifa kwamba ameghairisha kuja, watu wakaondoka na masononeko.
Kikubwa zaidi ambacho kinakatisha tamaa na kuvunja moyo tumesikia tetesi kwamba kwakuwa Dk Slaa anakubalika sana sana pande za Mbeya basi anatarajiwa afunge mikutano yake hukohuko ambako amesota mawiki kibao. Mi nadhani katusahau wapiga kura wa Lindi na Mtwara, na kwa mawazo yangu nilidhani angetumia muda mwingi huku ambako upepo wa kisaiasa uliotawala ni wa CCM na CUF.
Ningempa changamoto tu kwamba watu wa huku Mtwara kwa sasa wamekuwa ''upset' na 'fed-up' with u Dk. Wamechoka kukuona kwenye marunninga na wanakuhitaji sana,isitoshe nadhani uangalie tena ikibidi ufunge mbio za kampeni mikoa hii ya kusini kwani utawabadilisha kifikra sana wakazi wa huku kuliko unavyozidi kujisahau pande za mbeya,rukwa na iringa ambako asilimia kubwa mno wanakukubali, nadhani imetosha na sie wanaLindi na Mtwara kukuona Live. Nakerekwa sana na hili........
Kikubwa zaidi ambacho kinakatisha tamaa na kuvunja moyo tumesikia tetesi kwamba kwakuwa Dk Slaa anakubalika sana sana pande za Mbeya basi anatarajiwa afunge mikutano yake hukohuko ambako amesota mawiki kibao. Mi nadhani katusahau wapiga kura wa Lindi na Mtwara, na kwa mawazo yangu nilidhani angetumia muda mwingi huku ambako upepo wa kisaiasa uliotawala ni wa CCM na CUF.
Ningempa changamoto tu kwamba watu wa huku Mtwara kwa sasa wamekuwa ''upset' na 'fed-up' with u Dk. Wamechoka kukuona kwenye marunninga na wanakuhitaji sana,isitoshe nadhani uangalie tena ikibidi ufunge mbio za kampeni mikoa hii ya kusini kwani utawabadilisha kifikra sana wakazi wa huku kuliko unavyozidi kujisahau pande za mbeya,rukwa na iringa ambako asilimia kubwa mno wanakukubali, nadhani imetosha na sie wanaLindi na Mtwara kukuona Live. Nakerekwa sana na hili........