Hamisi Kigwangalla juu ya Boda Boda Arusha!

Wacha uwongo wewe hata kama wewe ni mmja wa beneficiaries hao.

Waheshimiwa hao walipewa hela hizo kama mkopo usio na interest kwa ajili ya kununulia magari makubwa ya kuwahikishia usafiri salama. Sheria iliyotumika kuwapa mkopo huo inabainisha wazi kuwa zitatumika kununulia magari kwa ajili ya usafiri wa wabunge katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku; na kila siku wanalipiwa mafuta kwa ajilia ya usafiri huo huo. Majukumu ya wabunge siyo tu kuzunguka jimboni kwake bali ni pamoja na kuzunguka sehemu nyingine nchini kulingana na atakavyotumwa na bunge. Ndiyo maana hata wabunge wa kuteuliwa wasiokuwa na majimbo walipewa hela hizo, na pia wanapewa hela za mafuta.

Ni kweli sina uhakika sawasawa kuwa walipewa kiasi gani kwa vile namba kamili huwa inafichwa, hata hivyo miaka kadhaa iliyopita tuliambiwa ni milioni themanini. Iwapo walipewa zaidi ya hapo, basi ni kwa nini watembelee na bodaboda; je wakianguka juu ya mabodaboda hayo sakaumia bado bunge letu litawahudumia matibabu yao?

Kumbe unakubaliana na mimi kwamba walikopeshwa na SI KWAMBA WALIPEWA. Au bado umeshikilia kwamba walipewa? Na pia unakubali kwamba wabunge hawana limit ya mahala pa kwenda ilimuradi ni Tanzania na kwa ajili ya ya wananchi! Halafu unaposema wanapewa pesa za mafuta sikuelewi! Maana allowance ya mafuta ni mojawapo ya malipo yaliyomo kwenye payroll. Yaani ni sawa na marupurupu unayolipwa wewe hapo TPDC! Kwa hiyo si ajabu kumwona mbunge ana gari lake Singida wakati yeye ni mbunge wa Songea. Suala la wabunge kupanda bodaboda si issue maana kama anaweza kuzunguka Tanzania kwa bodaboda mimi sina la kusema, isipokuwabaadaye wakianza kutembelea bajaji au bodaboda msije kusema wamevunja sheria.....
 
Kumbe unakubaliana na mimi kwamba walikopeshwa na SI KWAMBA WALIPEWA. Au bado umeshikilia kwamba walipewa? Na pia unakubali kwamba wabunge hawana limit ya mahala pa kwenda ilimuradi ni Tanzania na kwa ajili ya ya wananchi! Halafu unaposema wanapewa pesa za mafuta sikuelewi! Maana allowance ya mafuta ni mojawapo ya malipo yaliyomo kwenye payroll. Yaani ni sawa na marupurupu unayolipwa wewe hapo TPDC! Kwa hiyo si ajabu kumwona mbunge ana gari lake Singida wakati yeye ni mbunge wa Songea. Suala la wabunge kupanda bodaboda si issue maana kama anaweza kuzunguka Tanzania kwa bodaboda mimi sina la kusema, isipokuwabaadaye wakianza kutembelea bajaji au bodaboda msije kusema wamevunja sheria.....

Kwani marupurupu maana yake ni nini. Mafuta hayo ni sehemu ya marupurupu kusudi aweze kufanya kazi yake ya kutembelea sehemu mbalimbali za kazi. Kwa asiyatumia kama inavyotakiwa kisheria? Unadhani ni halali kwake kutumia pesa hiyo kununulia mafuta halafu akayauza kwa namna yoyote ili ajipatie faida?

Halafu mkopo usiokuwa na interest ni mkopo gani kama si kupewa tu; wewe unajua time value of money na kwa nini kuna kitu kinaitwa interest?

Kwa vile kazi yake inamruhusu kuzunguka sehemu yoyote Tanzania, na mkopo wa gari aliopewa ni kwa sababu hiyo, kwa nini asilitumie?


Hili ni mojawapo ya mambo niliyowahi kujadili hapa kuhusu watanzania na ethics za kazi;tunapenda sana kujifanyia mambo ambayo hayalingani na maadili ya kazi zetu. Kupanda boda boda na kuacha kutumia gari alilopewa kikazi ni mojawapo ya ukiukwaji wa ethics za kazi; ni sawa kabisa na kutumia gari hilo kufanyia biashara. Hata kama alikopeshwa, ni lazima ijulikane kuwa mkopo huo ulikuwa na malengo yake, na umetolewa kutokana na kodi yetu.
 
8E9U1428 (1).JPG
jk ndani ya shangingi lake
 
Ndugu, Nzega huwa natembea kwa miguu kabisa, achilia mbali pikipiki (mbona hiyo anasa kabisa!) na mara nyingi tu huwa natumia baiskeli...nitapiga picha nikiwa jimboni na baiskeli, sijui hapo utahoji nini tena!

Nzega huwa nakula mahindi na wapiga kura wangu, huwa nakunywa uji, ama chai na mihogo na karanga, ama kahawa na wazee wangu kwenye vijiwe vya jioni ama vya asubuhi na mapema na kupiga soga na wapiga kura wangu na wameishazoea hilo na wala si jambo la maonyesho. Nimesema mimi huwa si-pretend, nafanya mambo kwa uhalisia na wala siyo kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa - mimi siyo mtoto wa kishua, ni mtoto wa jalalani na kwa wananzega hili si jambo geni kwao maana wananifahamu fika na wanafahamu nimekulia wapi kwa hiyo siwezi kuwadanganya leo eti mimi ni mtoto wa uzunguni wakati ni wa uswazi!

Wakatabahu,
HK.

Umekosa shuhuli ya kufanya?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
mimi najiuloza na uwauliza pia... So angetumia shangingi lake kwenda kutafuta hio ATM?

Ivuga,
Hiyo ni political stunt (cheap popularity), ingawa yeye mwenyewe kajitetea kwenye thread aliyoianzisha kuhusu hiyo picha. Yeye na January Makamba ujana unawasumbua sana.
 
Kwani marupurupu maana yake ni nini. Mafuta hayo ni sehemu ya marupurupu kusudi aweze kufanya kazi yake ya kutembelea sehemu mbalimbali za kazi. Kwa asiyatumia kama inavyotakiwa kisheria? Unadhani ni halali kwake kutumia pesa hiyo kununulia mafuta halafu akayauza kwa namna yoyote ili ajipatie faida?

Halafu mkopo usiokuwa na interest ni mkopo gani kama si kupewa tu; wewe unajua time value of money na kwa nini kuna kitu kinaitwa interest?

Kwa vile kazi yake inamruhusu kuzunguka sehemu yoyote Tanzania, na mkopo wa gari aliopewa ni kwa sababu hiyo, kwa nini asilitumie?


Hili ni mojawapo ya mambo niliyowahi kujadili hapa kuhusu watanzania na ethics za kazi;tunapenda sana kujifanyia mambo ambayo hayalingani na maadili ya kazi zetu. Kupanda boda boda na kuacha kutumia gari alilopewa kikazi ni mojawapo ya ukiukwaji wa ethics za kazi; ni sawa kabisa na kutumia gari hilo kufanyia biashara. Hata kama alikopeshwa, ni lazima ijulikane kuwa mkopo huo ulikuwa na malengo yake, na umetolewa kutokana na kodi yetu.

Kwa hiyo wewe hoja yako iko wapi? Kwamba mkopo usio na riba ni sawa na kupewa bure? Unajua kwa nini mkopo unakuwa na interest? Elimu ya Financial Management unayo kidogo ili niingie deep kukupiga shule? Infact, mimi ninachojua si kosa kutokulitumia gari ulilokopeshwa maana ni lako!! Tafsiri unayotaka kuionesha ni kwamba wabunge ni LAZIMA watumie magari yao popote na saa zote.... Huko siko mkuu. Hoja tunayoijadili si kupewa mafuta (au fedha ya kununulia mafuta) kisha kuyauza. Hakuna thread yoyote inayosema wabunge huuza mafuta wanayopewa. Tunajadili wabunge kukopeshwa magari na si dhana kwamba magari hayo wamepewa. Nilitaka kuondoa dhana kwamba milioni themanini ama zaidi walizokopeshwa wabunge ili wanunue magari si hisani au msaada ni mkopo ambao unalipwa kwa kukatwa kila mwezi. Kutokutozwa riba hiyo si issue maana ni makubaliano ya mwajiri na mwajiriwa. Mtu akikopeshwa fedha bila kudaiwa riba maana yake si kwamba deni hilo halipo la hasha..... Riba ni mojawapo ya incentives zilizo katika sheria za kazi na maadili (ethics) unazozizungumzia wewe. Soma vizuri sheria za kazi, sheria za kodi, sheria za mikataba, sheria za fedha na kibenki na kanuni za maadili ya utumishi wa umma natumai utaelewa na kugundua kwamba wabunge hawajapendelewa kupewa magari ama posho za kuwezesha magari yao kuwa barabarani.
 
Kwa hiyo wewe hoja yako iko wapi? Kwamba mkopo usio na riba ni sawa na kupewa bure? Unajua kwa nini mkopo unakuwa na interest? Elimu ya Financial Management unayo kidogo ili niingie deep kukupiga shule? Infact, mimi ninachojua si kosa kutokulitumia gari ulilokopeshwa maana ni lako!! Tafsiri unayotaka kuionesha ni kwamba wabunge ni LAZIMA watumie magari yao popote na saa zote.... Huko siko mkuu. Hoja tunayoijadili si kupewa mafuta (au fedha ya kununulia mafuta) kisha kuyauza. Hakuna thread yoyote inayosema wabunge huuza mafuta wanayopewa. Tunajadili wabunge kukopeshwa magari na si dhana kwamba magari hayo wamepewa. Nilitaka kuondoa dhana kwamba milioni themanini ama zaidi walizokopeshwa wabunge ili wanunue magari si hisani au msaada ni mkopo ambao unalipwa kwa kukatwa kila mwezi. Kutokutozwa riba hiyo si issue maana ni makubaliano ya mwajiri na mwajiriwa. Mtu akikopeshwa fedha bila kudaiwa riba maana yake si kwamba deni hilo halipo la hasha..... Riba ni mojawapo ya incentives zilizo katika sheria za kazi na maadili (ethics) unazozizungumzia wewe. Soma vizuri sheria za kazi, sheria za kodi, sheria za mikataba, sheria za fedha na kibenki na kanuni za maadili ya utumishi wa umma natumai utaelewa na kugundua kwamba wabunge hawajapendelewa kupewa magari ama posho za kuwezesha magari yao kuwa barabarani.

Unaangalia maneno badala ya kuangalia hoja. Hoja iliyopo hapa ni kuwa wabunge wanapewa pesa hizo siyo asante kwao na wala siyo kwa sababu wao ni bora kuliko wananchi wengine, bali ni kwa sababu ya kuhitaji wawe na usafiri wa kuaminika ili waweze kufika popote wakati wa kazi zao. Vile vile wanapewa hela ya kuliendesha gari hilo kwa vitu kama mafuta na matunzo kwa sababu hiyo hiyo.

Hoja hapa nikuhusu diversion ya matumizi ya pesa hizo, ndiyo maana nikakupa mifano kama kuuza mafuta au kutumia magari hayo kufanyia biashara kama mfano wa diversion. Unapoangalia neno moja moja na kutoa conclusion ni dalili ya kushindwa kuangalia mambo kwa mapana kama vile huwezi kuprocess information nyingi kwa pamoja.


Kama kweli unajua Finance Management basi unajua hakuna mkopo wa bure, kila mkopo una thamani yake inayoitwa interest. Mikopo inayoitwa soft loans au interest free loans huwa ni misaada, siyo mikopo. Yaani wakopeshwaji wanakuwa wanaruhusiwa kulipa kidogo kuliko walichokopeshwa kwa vile thamani ya fedha hukua na wakati, siyo static. Kwa hawa wabunge wtu kupewa mkopo wa shilingi milioni 80 (kama ni hizo) interest free kwa miaka mitano wakati uchumi wetu unadai interest rate ya 20% na zaidi ni kama wamepewa bure zaidi ya milioni 119 (za interest) kutokana na mkopo huo wa milioni 80 usiokuwa na interest
 
No ni uongo hakuwa anatafuta ATM, NILIONA TUKIO ZIMA. YEYE ALIKUWA NA MAMBO YAKE MTAA WA MNAZI MMOJA KARIBU NA BENKI YA NBC ILIYOKO KATIKA JENGO LA MEGA COMPLEX NA SIM ALIYOTUMIA NI BLACKBERRY ALIKUTANA NA DEREVA TOYO UNAYEMWONA HAPO KAMA DEREVA AKAONGEA NAE KUWA ANATAKA KUPIGA PICHA AKIWA KWENYE PIKIPIKI NA MWENYE TOYO AKAMKUBALIA NDIPO AKAIPIGA HIYO PICHA. MUDA HUO ULIKUWA NI MAJIRA KATI YA SAA KUMI NA MOJA NA NUSU HADI SAA KUMI NA MBILI JIONI

Dah,shame up on him kwahyo mpiga picha alikua nani??
 
Unaangalia maneno badala ya kuangalia hoja. Hoja iliyopo hapa ni kuwa wabunge wanapewa pesa hizo siyo asante kwao na wala siyo kwa sababu wao ni bora kuliko wananchi wengine, bali ni kwa sababu ya kuhitaji wawe na usafiri wa kuaminika ili waweze kufika popote wakati wa kazi zao. Vile vile wanapewa hela ya kuliendesha gari hilo kwa vitu kama mafuta na matunzo kwa sababu hiyo hiyo.

Hoja hapa nikuhusu diversion ya matumizi ya pesa hizo, ndiyo maana nikakupa mifano kama kuuza mafuta au kutumia magari hayo kufanyia biashara kama mfano wa diversion. Unapoangalia neno moja moja na kutoa conclusion ni dalili ya kushindwa kuangalia mambo kwa mapana kama vile huwezi kuprocess information nyingi kwa pamoja.


Kama kweli unajua Finance Management basi unajua hakuna mkopo wa bure, kila mkopo una thamani yake inayoitwa interest. Mikopo inayoitwa soft loans au interest free loans huwa ni misaada, siyo mikopo. Yaani wakopeshwaji wanakuwa wanaruhusiwa kulipa kidogo kuliko walichokopeshwa kwa vile thamani ya fedha hukua na wakati, siyo static. Kwa hawa wabunge wtu kupewa mkopo wa shilingi milioni 80 (kama ni hizo) interest free kwa miaka mitano wakati uchumi wetu unadai interest rate ya 20% na zaidi ni kama wamepewa bure zaidi ya milioni 119 (za interest) kutokana na mkopo huo wa milioni 80 usiokuwa na interest

Kumbe Financial Management huijui na wala business law huijui. Licha ya hivyo, hata sheria za mikopo huzijui. Umesema kukopeshwa mkopo usio na riba ni msaada, je kama kweli umesoma uchumi, msaada huwa unalipwa kwa kukatwa katika mshahara? Mbona kitu unachokiongelea hakiendani na theme iliyobandikwa kwenye JF kumhusu Kigwangala? Rudi katika point kisha tuendelee.
 
Kumbe Financial Management huijui na wala business law huijui. Licha ya hivyo, hata sheria za mikopo huzijui. Umesema kukopeshwa mkopo usio na riba ni msaada, je kama kweli umesoma uchumi, msaada huwa unalipwa kwa kukatwa katika mshahara? Mbona kitu unachokiongelea hakiendani na theme iliyobandikwa kwenye JF kumhusu Kigwangala? Rudi katika point kisha tuendelee.

Yaani ndugu yangu wewe hujui kuwa kupewa kitu bila malipo yoyote ni msaada, na wala huamini kabisa function ya interest rates katika financial markets. Unanitia shaka na uelewa wako kama huoni kuwa interest wanayosamehewa wabunge kutokana na mkopo huo ni gharama kubwa sana kwa taifa. Nimekuwekea hesabu za haraka haraka kuwa katika miaka mitano hiyo wabunge watakuwa wamechukua karibu milioni 120 kutoka kwa walipa kodi kutokana na mkopo huo wa milioni 80; kama wewe huzioni hizo milioni 120 ila unaangalia hela wanazurudisha basi elimu yako ya uchumi inatia shaka sana.

Katika swala hili hapa hakuhitajiki knowledge ya Business Law wala Financial Management bali ni kitu kidogo sana katika Managerial Economics kinaitwa time value of money.
 
Yaani ndugu yangu wewe hujui kuwa kupewa kitu bila malipo yoyote ni msaada, na wala huamini kabisa function ya interest rates katika financial markets. Unanitia shaka na uelewa wako kama huoni kuwa interest wanayosamehewa wabunge kutokana na mkopo huo ni gharama kubwa sana kwa taifa. Nimekuwekea hesabu za haraka haraka kuwa katika miaka mitano hiyo wabunge watakuwa wamechukua karibu milioni 120 kutoka kwa walipa kodi kutokana na mkopo huo wa milioni 80; kama wewe huzioni hizo milioni 120 ila unaangalia hela wanazurudisha basi elimu yako ya uchumi inatia shaka sana.

Katika swala hili hapa hakuhitajiki knowledge ya Business Law wala Financial Management bali ni kitu kidogo sana katika Managerial Economics kinaitwa time value of money.

Basi bwana mimi naona tuishie hapo maana umeacha kujadili hoja unaingia kwenye mambo binafsi. Roho inakuuma sana kwa wabunge kukopeshwa bila riba milioni 80 za kununua magari. Unawalaumu wabunge badala ya kutaka kujua ni kigezo gani kilitumika kuwasamehe riba. Mbona wewe kampuni yako ya TPDC inaponunua vifaa vya vya kuchimbia mafuta inasamehewa kodi na ushuru mbona roho haikuumi? Unaona wabunge tu.... Wewe ni mbinafsi.... Kwa heri.
 
Basi bwana mimi naona tuishie hapo maana umeacha kujadili hoja unaingia kwenye mambo binafsi. Roho inakuuma sana kwa wabunge kukopeshwa bila riba milioni 80 za kununua magari. Unawalaumu wabunge badala ya kutaka kujua ni kigezo gani kilitumika kuwasamehe riba. Mbona wewe kampuni yako ya TPDC inaponunua vifaa vya vya kuchimbia mafuta inasamehewa kodi na ushuru mbona roho haikuumi? Unaona wabunge tu.... Wewe ni mbinafsi.... Kwa heri.


(1) Sijaingilia mambo yako binafsi, ila nimepima hoja zako na kuziona pumba tu. Ni afadhali usingeniambia kuwa unajua Business Law na Financial Management wakati hujui kutumia knowledge hiyo, tungejadiliana kama laymen tu.

(2) Hii mentality ya kuona kuwa kukemea watumishi wa umma wanaotumia raslimali za umma vibaya ni kuwaonea wivu ndiyo inayosababisha Tanzania tusiendelee hadi leo, na ndiyo inayohalalisha watu kuiba mali za umma tena kwa kiwango kikubwa na kuzihamishia nje. Mambo yote makubwa huanza kama mambo madogo kabla hayajua; tabia za wabunge kutumia raslimali za umma kinyume na sheria inavyotaka ni makosa, wala siyo kuwaonea wivu.

(3) Ukiwa mtalaam wa Financial Management na Business Law, nadhani utakuwa unafahamu pia kuwa kwenye Public Finance, kusamehewa kodi kwa sababu yoyote ile huwa ni gharama kwa taifa husika, ila katika kutunga monetary policies za nchi, wakati mwingine serikali husamehe kodi fulani fulani ili kupanua eceonomic activities ambazo kwa pamoja kuongeza tax base ya nchi. Kwa hiyo mimi kampuni yangu ya TPDC kusamehewa kodi kwa ajili ya kuingiza vitendea kazi ni kwa sababu itakuwa inaongeza economic activities ambazo zitasababisha watu wengi waajiriwe na vile vile kuwa na value added products nyingi za mafuta, vyote kwa pamoja vikiwa vinaongeza wigo wa kodi kwa Taifa. Kusamehe kodi wabunge hakuongezi economic activities zozote!
 
(1) Sijaingilia mambo yako binafsi, ila nimepima hoja zako na kuziona pumba tu. Ni afadhali usingeniambia kuwa unajua Business Law na Financial Management wakati hujui kutumia knowledge hiyo, tungejadiliana kama laymen tu.

(2) Hii mentality ya kuona kuwa kukemea watumishi wa umma wanaotumia raslimali za umma vibaya ni kuwaonea wivu ndiyo inayosababisha Tanzania tusiendelee hadi leo, na ndiyo inayohalalisha watu kuiba mali za umma tena kwa kiwango kikubwa na kuzihamishia nje. Mambo yote makubwa huanza kama mambo madogo kabla hayajua; tabia za wabunge kutumia raslimali za umma kinyume na sheria inavyotaka ni makosa, wala siyo kuwaonea wivu.

(3) Ukiwa mtalaam wa Financial Management na Business Law, nadhani utakuwa unafahamu pia kuwa kwenye Public Finance, kusamehewa kodi kwa sababu yoyote ile huwa ni gharama kwa taifa husika, ila katika kutunga monetary policies za nchi, wakati mwingine serikali husamehe kodi fulani fulani ili kupanua eceonomic activities ambazo kwa pamoja kuongeza tax base ya nchi. Kwa hiyo mimi kampuni yangu ya TPDC kusamehewa kodi kwa ajili ya kuingiza vitendea kazi ni kwa sababu itakuwa inaongeza economic activities ambazo zitasababisha watu wengi waajiriwe na vile vile kuwa na value added products nyingi za mafuta, vyote kwa pamoja vikiwa vinaongeza wigo wa kodi kwa Taifa. Kusamehe kodi wabunge hakuongezi economic activities zozote!


Hapo kwenye "red". (1) Hivi wabunge wamevunja sheria gani maana sera iliyopo ni kuwa wanasamehewa riba na si kwamba "wanajisamehe riba". Kwa kuwa mimi nilipokuambia najua financial management lakini kila ukiongea hoja zako unaongea off point na financial management principles mimi nikanyamaza-kisha wewe ukatumia nafasi hiyo kunionesha kwamba unazijua, basi kwa kuwa wewe ni mtaalamu wa sheria hizo na unazijua mfano, umeonesha unajua Public Finance... basi nakuomba unieleze wabunge wamevunja sheria gani. Yaani kifungu gani kilichovunjwa nawao kama wabunge kisha tuendelee kujadili. Toa kifungu kwa format ifuatayo: Kifungu (mfano) 24(1)(b) cha sheria fulani kisha ukibandike kifungu hicho kama kinavyosomeka. Hapo utakuwa umetenda vema sana na utaalamu wako utajulikana kwa watu wote humu JF.
(2) Kwa hilo la kutoongeza economic activities zozote, naona niliache kwanza kwa sasa.... Ila nakupa pole.
 
[/COLOR]
Hapo kwenye "red". (1) Hivi wabunge wamevunja sheria gani maana sera iliyopo ni kuwa wanasamehewa riba na si kwamba "wanajisamehe riba". Kwa kuwa mimi nilipokuambia najua financial management lakini kila ukiongea hoja zako unaongea off point na financial management principles mimi nikanyamaza-kisha wewe ukatumia nafasi hiyo kunionesha kwamba unazijua, basi kwa kuwa wewe ni mtaalamu wa sheria hizo na unazijua mfano, umeonesha unajua Public Finance... basi nakuomba unieleze wabunge wamevunja sheria gani. Yaani kifungu gani kilichovunjwa nawao kama wabunge kisha tuendelee kujadili. Toa kifungu kwa format ifuatayo: Kifungu (mfano) 24(1)(b) cha sheria fulani kisha ukibandike kifungu hicho kama kinavyosomeka. Hapo utakuwa umetenda vema sana na utaalamu wako utajulikana kwa watu wote humu JF.
(2) Kwa hilo la kutoongeza economic activities zozote, naona niliache kwanza kwa sasa.... Ila nakupa pole.

Pumba tupu!
 
Back
Top Bottom