Hamisi Kigwangalla juu ya Boda Boda Arusha!

-Kuwa karibu na wananchi kivipi?Yeye ni mwakilishi wa wananchi lakini inaonekana anawakilisha wavunja sheria za barabarani na wahalifu.Hapa anastahili kuchukuliwa hatua za kisheria mara moja

-Pia hoja ya kuwa karibu na wananchi kutafuta ATM kwa kupanda Bodaboda mjini ni kutafuta cheap popularity na ku-expose fikra zilizochusha na kwa kuwa huyu ni msomi mwenye MBA anajua umuhimu wa huduma ya kibenki vijijini.Sasa kule Nzega ameshapigana kwa kiasi gani kuhakikisha huduma hiyo inawafikia wananchi vijijini?

-Nilidhani hiyo ndiyo inge-reflect ukaribu wake kwa wananchi kuliko jitihada hizi anazofanya mjini za kuvunja sheria za usalama barabarani na kuwadhalilisha wananchi waliomchagua kwa jaribio hili la kuonyesha yeye ni mwakilishi asiyezingatia sheria na anayerudisha nyuma harakati za kukabiliana na ajali za barabarani

Nd. Ben,

You have put forward some good points here that I feel obliged to address.

1. Kuwa karibu na wananchi - nimeeleza kwa urefu dhana hii kwenye mchango wangu mwingine hapa so soma kule.

2. Kuhatarisha maisha yangu - I totally agree with you kwamba kwa kiasi fulani nimehatarisha maisha yangu kwa kutokuvaa protective gears, lakini sina hakika kama kuna sheria nimevunja kwa kuwa sikuwa mwendeshaji na ndiyo maana kwenye mchango wangu kule FB (kuna mtu ameuleta hapa) nimeeleza kwamba pengine kuna haja ya kutunga sheria itakayolazimisha wapanda pikipiki wote (uwe mwendeshaji ama abiria) ni lazima wavae protective gears, na hii kazi nitaifanya. Naomba radhi kwa kutokuwa mfano mzuri kwa kuvaa protective gears ukizingatia kuwa mimi ni Daktari Bingwa niliyebobea kwenye fani ya Injury Prevention and Safety Promotion na zaidi kwa kuwa mimi ni Mbunge na kiongozi katika jamii - mara nyingi nikiwa Nzega huwa natumia protective gears na majuzi tu nimewagawia reflective tops waendesha bodaboda wote jimboni.

3. Huduma za kibenki - pale kwetu Nzega mjini kwa sasa tuna matawi ya benki za NBC na NMB, na tumefanya mazungumzo na uongozi wa benki ya CRDB watuletee tawi lao pale na wameishakubali - tayari tumewapa kiwanja. Benki vijijini - tunaelekea kuanza mchakato wa kuanzisha Benki ya Maendeleo ya Jamii Nzega (Nzega Community Development Bank) ambayo itafungua matawi kwenye tarafa zote nne za wilaya ya Nzega, kwa kuanzia; na itaanza kwa kufanya kazi na SACCOS za kila kata ambazo tumezianzisha. Mtaji tumeupata kutokana na ushuru wa huduma (service levy) tuliyoidai kwa mbinde kutoka kwa wawekezaji wa kampuni ya Resolute (mgodi) ambayo haikuwahi kulipwa kwa zaidi ya miaka 14.

Wakatabahu,
HK.
 
Utafikiri ulikuwepo vile!

nitake radhi kama ni uongo ubishe mbele ya mwenyezi mungu. Aliyekupiga ni kijana mmoja ambaye hata kutumia simu yako hajui vizuri alikuwa amevaa shati la mikono mifupi la rangi nyeusi na draft nyeupe, si mweusi sana ni mrefu wa wastani na mwembamba wastani ulipigia karibu na mlango wa kuingilia bank. KATAA KAMA SI KWELI NA KAMA UNAYOONGEA NI HAKI MBELE YA MUNGU
 
nitake radhi kama ni uongo ubishe mbele ya mwenyezi mungu. Aliyekupiga ni kijana mmoja ambaye hata kutumia simu yako hajui vizuri alikuwa amevaa shati la mikono mifupi la rangi nyeusi na draft nyeupe, si mweusi sana ni mrefu wa wastani na mwembamba wastani ulipigia karibu na mlango wa kuingilia bank. KATAA KAMA SI KWELI NA KAMA UNAYOONGEA NI HAKI MBELE YA MUNGU
Nimeamini jambo moja tu kwamba, kweli kuna watu mna vipaji vya kutengeneza mambo. Hii picha ilipigwa mara moja tu na haikurudiwa.
 
Boflo,

Boflooooooooo................. .....



Ila hili kosa la kutovaa hiyo Kofia Kinga kichwani, tumefanya/tunafanya/tutafanya wengi sana.
 
Last edited by a moderator:
Nimeamini jambo moja tu kwamba, kweli kuna watu mna vipaji vya kutengeneza mambo. Hii picha ilipigwa mara moja tu na haikurudiwa.

unakataa kwamba sikuwepo ili ajulikane mwongo nani lidhibitishie hili jukwaa ni wapi ulipopiga hii picha na mimi nikipata mda naenda eneo la tukio napiga picha na kuiwakilisha hapa kwa mtu yeyote anayepafahamu ukiangalia nyuma ya hamis kuna generator na pia ni sehem ambayo kuna parking ya winch
 
sina hakika kama kuna sheria
Mtunga sheria unasema hujui kama hiyo sheria ipo ama haipo!

Nchi za watu una resign hapo hapo! Mbunge huna exposure na safety standards za dunia ya leo masikini ya Mungu, umekulia Nzega huko umezaliwa Malawi sijui Burundi umesoma Muhimbili, huna exposure kiasi kwamba unapitwa hata na mwananchi wa kawaida muendesha pikipiki anaeelewa umuhimu wa safety precautions kuliko Mbunge. Surreal!

Halafu savvy za damage control nazo zero, bora ungeuchuna, unakiri kwamba hujui kama kuna sheria au hakuna!
 
Yaani wabongo kweli tumechoka,yaani eti hii nayo ni mada tunajadili
 
Kubanda Bajaj au Bodaboda kinahusianaje na mabadiliko ya hali ngumu ya maisha tuliyonayo sisi wakesha hoi? kama wanaitumia kuchukua mirupo yao sisi tutajuaje? Kama wanaona kwao ni fashion basi wamuulize Mchungaji Mtikira kwani yeye amepanda sana hadi Baiskeli.
HAPA HAKUNA JIPYA WANATUSANIFU TU.
 
Unafiki mtupu huo!

Kama wanasafiiri kwa bodaboda au pikipiki za kukodi basi warudishe zile milioni themanini walizopewa kununulia mashangingingi. Kisheria pesa zile walipewa ili zitumike kununulia magari imara yatakayowafikisha popoe walipo wapiga kura wao; na wala hazikuwa zawadi kwao kutumia watakavyo kama wabunge.

Iwapo walitumia pesa hizo nje ya malengo yake ya kisheria basi inatakiwa washtakiwe kwa kuvunja sheria inayotawala matumizi ya pesa hizo.

Jamani sisi ni great thinkers, au mmesahau? Nani alikwambia wabunge walipewa milioni themanini?.... Walikopeshwa tena zaidi ya kiasi unachokisema na kila mwezi wanakatwa kwenye mishahara yao.... Yaani kimsingi yale magari ni yao na wala si fadhila (japo sera ni ya Serikali kwamba mashangingi ndo yatumike kama chombo cha usafiri kwa wabunge-hii ni kutokana na hali ya miundombinu yetu na jiografia yetu. Huwezi kusafiri jimbo la Tabora kaskazini lenye kilomita (mzunguko) elfu 2 mia tatu na thelathini na tisa kwa kutumia gari aina ya corola). Halafu mtu anagonga like kwa mtu alieongea kitu asichokijua.... This is strange!!!! Jifunze kwanza kuhusu kitu kisha ndo useme ili uwe na haki!!!!!
 
Jamani sisi ni great thinkers, au mmesahau? Nani alikwambia wabunge walipewa milioni themanini?.... Walikopeshwa tena zaidi ya kiasi unachokisema na kila mwezi wanakatwa kwenye mishahara yao.... Yaani kimsingi yale magari ni yao na wala si fadhila (japo sera ni ya Serikali kwamba mashangingi ndo yatumike kama chombo cha usafiri kwa wabunge-hii ni kutokana na hali ya miundombinu yetu na jiografia yetu. Huwezi kusafiri jimbo la Tabora kaskazini lenye kilomita (mzunguko) elfu 2 mia tatu na thelathini na tisa kwa kutumia gari aina ya corola). Halafu mtu anagonga like kwa mtu alieongea kitu asichokijua.... This is strange!!!! Jifunze kwanza kuhusu kitu kisha ndo useme ili uwe na haki!!!!!

Wacha uwongo wewe hata kama wewe ni mmja wa beneficiaries hao.

Waheshimiwa hao walipewa hela hizo kama mkopo usio na interest kwa ajili ya kununulia magari makubwa ya kuwahikishia usafiri salama. Sheria iliyotumika kuwapa mkopo huo inabainisha wazi kuwa zitatumika kununulia magari kwa ajili ya usafiri wa wabunge katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku; na kila siku wanalipiwa mafuta kwa ajilia ya usafiri huo huo. Majukumu ya wabunge siyo tu kuzunguka jimboni kwake bali ni pamoja na kuzunguka sehemu nyingine nchini kulingana na atakavyotumwa na bunge. Ndiyo maana hata wabunge wa kuteuliwa wasiokuwa na majimbo walipewa hela hizo, na pia wanapewa hela za mafuta.

Ni kweli sina uhakika sawasawa kuwa walipewa kiasi gani kwa vile namba kamili huwa inafichwa, hata hivyo miaka kadhaa iliyopita tuliambiwa ni milioni themanini. Iwapo walipewa zaidi ya hapo, basi ni kwa nini watembelee na bodaboda; je wakianguka juu ya mabodaboda hayo sakaumia bado bunge letu litawahudumia matibabu yao?
 
Back
Top Bottom