Hamisi Kigwangalla juu ya Boda Boda Arusha!

Hamisi Kigwangalla juu ya Boda Boda Arusha!

... kama vile amejiandaa kupigwa picha! Ngoja niinote ID ya mleta mada, huenda ametumwa na Kigwangwalla kuja kuuza sifa za kijinga humu!

..Halafu usikute aliyeleta huu uzi ni yuleyule aliyeleta ule uzi wa makamba ndani ya bajaj.
 
tumetoka kushuhudia picha ya Januari Makamba akiwa ndani ya Bajaji, leo sasa kuna kali ya mwaka Mbunge wa Nzega ame-post kwenye ukurasa wake wa FB picha akivinjari mitaa ya A-town kusaka ATM kwa kutumia usafiri wa Pikipiki, pamoja na kutaka kujionyesha wako karibu na maisha ya kila siku ya wananchi, nadhani Mbunge huyu amehatarisha maisha yake kwa kiasi kikubwa kwa kutokuvaa protective gears, hebu cheki mwenyewe hapa chini:





























12210_10151534580468243_1030950183_n.jpg



....ina maana bodaboda inaenda huku mwendeshaji anaburuza miguu chini? acheni njaa ndugu zangu. Mtu anaonekana amepozi kabisa kupigwa picha.....aarghh!!
 
Hata kama ndie, haina tofauti na January Wa Kamba, maana pikipiki yenyewe imesimama tu.
Pili kama kiongozi katika jamii alipaswa awe mfano katika kuvaa PPEs but anatufundisha nini hapo sasa??
 
Laiti huyo dereva angejua uyo ndo Dr.Vitumbua angeangusha iyo pikipiki kwa maksudi.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Hata Upumbavu ni Kipaji , Mwl Julius K Nyerere
 
Hii ni sehemu gani Arusha?
Afu mbona sio the so called Kigwangalla?

Ni Kagwangala mwenyewe. halafu anaongelea safety huku yeye mwenyewe ameshindwa kuvaa helmet!! mjanja sana huyu jamaa, alijua itafika tu huku JF.

kig.JPG
 
tumetoka kushuhudia picha ya Januari Makamba akiwa ndani ya Bajaji, leo sasa kuna kali ya mwaka Mbunge wa Nzega ame-post kwenye ukurasa wake wa FB picha akivinjari mitaa ya A-town kusaka ATM kwa kutumia usafiri wa Pikipiki, pamoja na kutaka kujionyesha wako karibu na maisha ya kila siku ya wananchi, nadhani Mbunge huyu amehatarisha maisha yake kwa kiasi kikubwa kwa kutokuvaa protective gears, hebu cheki mwenyewe hapa chini:

12210_10151534580468243_1030950183_n.jpg


Acheni tu wananchi wawazomee magamba, sasa kupanda bodaboda kama hivi kunasaidiaje wananchi kupata dawa hospitalini, kupata maji ya uhakika, kupata masoko ya uhakika kwa mazao ya mashamba? Ni kama CCM hawana fikra mbadala zaidi ya kuhakikisha Mtanzania wa hali duni anabaki huko huko kwenye uduni. Unafiki mtupu!
 
Jamaa alijiandaa na pia hakuwa amekuja kwenye atm kama anavyosema na alipigwa picha ya kwanza ikawa mbaya akamwambia airudie ndiyo hiyo ikatoka na unafuu na ni majira ya jioni saa 11 na nusu hadi 12 na ukiangalia kwa makini dereva bodaboda amesimama na yeye mwenyewe amejiandaa na ndiyo maana sura imevutwa ili aonekane vizuri na pia jana hapakuwa na shida ya mawasiliano katika atm zozote hapa jijini arusha
 
Kwanin picha hiyo haikupigiwa Nzega?! Au ndo kuonyesha watu wa Arusha wana shida ya usafir na ATM kuliko Nzega?! Alifuata nin Arusha, ndg jamaa na marafik ama siasa?! Kama ni siasa nan kamtuma?!
 
Ndugu zangu,

Vyovyote vile mtakavyosema lakini napenda kuhoji yafuatayo: hivi kupanda pikipiki ni sifa? Hivi kuwa maskini ni sifa? Hebu jaribuni kufikiria kwa sauti.

Kwa mtu kama mimi kupanda pikipiki siyo jambo la ajabu sana na wala siyo la kuzua mjadala, maana nimekulia kwenye umaskini wa hali ya juu lakini siupendi umaskini na ndiyo maana napambana nao kila kukicha mimi binafsi na katika jamii, na ninapenda kuhakikisha umaskini wa kutupwa hapa Tanzania unatoweka - huo ndiyo mchango ninaoendelea kuutoa ili kulipa fadhila kwa nchi yangu kwa kunipa fursa ya elimu na ya ajira. Kwa sisi tuliokulia kwenye shida za umaskini, tuliowahi kupitia maisha ya mlo mmoja kwa siku, kwenda shule bila viatu, kucheza mpira bila viatu tunaelewa kwa nini tupigane kuondoa umaskini kwa watu wote. Na wala kupanda pikipiki siyo jambo la maonesho, eti la kujidaisha naishi maisha ya chini sawa na 'ordinary citizen', kwangu mimi ntahoji who is ordinary na who is extra-ordinary, na why these classes? Na je kuna uhalalai wowote ule wa kuwa na watu wa kawaida na wale wasio wa kawaida? Naamini mimi nimepewa fursa hii si kwa ajili ya kuendelea kuwa na raha bali kwa ajili ya kutoa mchango utakaowapa wengine kama mimi kupata fursa za kuboresha maisha yao. Na siwezi kuwa mtu wa ku-pretend kuwa na watu wa 'kawaida' kwa faida za kisiasa. Take it or leave it, wengine tuko orijino na tuna sababu za kuwa hivi tulivyo!

Pili: napenda kutoa taarifa kwa wanaopinga kwamba, hiyo picha ni ya kwangu na nilipigwa kwa maksudi wala siyo kwa bahati mbaya...na nimeiweka mwenyewe kwenye facebook page yangu na sidhani kama hilo ni kosa.

Wakatabahu,
HK.
 
Kama ameomba apigwe picha ili akauze nyago kwa wananchi Nzega
 
Kwanin picha hiyo haikupigiwa Nzega?! Au ndo kuonyesha watu wa Arusha wana shida ya usafir na ATM kuliko Nzega?! Alifuata nin Arusha, ndg jamaa na marafik ama siasa?! Kama ni siasa nan kamtuma?!

Ndugu, Nzega huwa natembea kwa miguu kabisa, achilia mbali pikipiki (mbona hiyo anasa kabisa!) na mara nyingi tu huwa natumia baiskeli...nitapiga picha nikiwa jimboni na baiskeli, sijui hapo utahoji nini tena!

Nzega huwa nakula mahindi na wapiga kura wangu, huwa nakunywa uji, ama chai na mihogo na karanga, ama kahawa na wazee wangu kwenye vijiwe vya jioni ama vya asubuhi na mapema na kupiga soga na wapiga kura wangu na wameishazoea hilo na wala si jambo la maonyesho. Nimesema mimi huwa si-pretend, nafanya mambo kwa uhalisia na wala siyo kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa - mimi siyo mtoto wa kishua, ni mtoto wa jalalani na kwa wananzega hili si jambo geni kwao maana wananifahamu fika na wanafahamu nimekulia wapi kwa hiyo siwezi kuwadanganya leo eti mimi ni mtoto wa uzunguni wakati ni wa uswazi!

Wakatabahu,
HK.
 
Jamaa alijiandaa na pia hakuwa amekuja kwenye atm kama anavyosema na alipigwa picha ya kwanza ikawa mbaya akamwambia airudie ndiyo hiyo ikatoka na unafuu na ni majira ya jioni saa 11 na nusu hadi 12 na ukiangalia kwa makini dereva bodaboda amesimama na yeye mwenyewe amejiandaa na ndiyo maana sura imevutwa ili aonekane vizuri na pia jana hapakuwa na shida ya mawasiliano katika atm zozote hapa jijini arusha
Utafikiri ulikuwepo vile!
 
Ndugu, Nzega huwa natembea kwa miguu kabisa, achilia mbali pikipiki (mbona hiyo anasa kabisa!) na mara nyingi tu huwa natumia baiskeli...nitapiga picha nikiwa jimboni na baiskeli, sijui hapo utahoji nini tena!

Nzega huwa nakula mahindi na wapiga kura wangu, huwa nakunywa uji, ama chai na mihogo na karanga, ama kahawa na wazee wangu kwenye vijiwe vya jioni ama vya asubuhi na mapema na kupiga soga na wapiga kura wangu na wameishazoea hilo na wala si jambo la maonyesho. Nimesema mimi huwa si-pretend, nafanya mambo kwa uhalisia na wala siyo kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa - mimi siyo mtoto wa kishua, ni mtoto wa jalalani na kwa wananzega hili si jambo geni kwao maana wananifahamu fika na wanafahamu nimekulia wapi kwa hiyo siwezi kuwadanganya leo eti mimi ni mtoto wa uzunguni wakati ni wa uswazi!

Wakatabahu,
HK.
Ulishaumaliza ugomvi wako na Bashe ?
 
Back
Top Bottom