babu na mjukuu
JF-Expert Member
- Jun 23, 2016
- 3,841
- 6,546
Kwani zito amepotea!?Hawa watu hasa huyu Mdee bado sijajua kwanini walikubali kudanganyika wakasaliti maamuzi ya chama chao, kama kilikuwa kiburi cha uwepo wa mwendazake pole yao.
Kinachomkuta sasa hivi hakuna yeyote mwanye akili atakayemuelewa na utetezi wake, walipewa ruhusa ya kujitetea kwenye KK wakagoma kwenda.
Kile kiburi walichoonesha pale ndio ulikuwa uhuni wenyewe, na ule uhuni ndio umeleta hii hasira kwa wajumbe wa Baraza Kuu "kuwachinjia baharini" kwa kura zakutosha toka kwenye kila kanda.
Kama walikuwa na nafasi ya kuomba msamaha ilikuwa ni wakati ule, pale anagalau wangeweza kusikilizwa, lakini kugoma kwao kwenda kwa kisingizia cha kitoto "usalama wao" 'ile ilikuwa ni dharau kwa wajumbe wa KK.
Hakuna mjumbe kichaa wa KK wa kuwafanyia fujo, wamevuna walichopanda, sasa waende mahakamani kama wakipenda, ingawa naamini wanajua hata huko mahakamani hawatavuna heshima yoyote, simply wameshapotea.
Hivi mnajikuta kina nani?
Sent from my SM-G5500 using JamiiForums mobile app