Let us be objective. Makonda anaweza kuwa alifoji cheti/vyeti. Kwa maelezo ya Gwajima, anamfahamu tangu kijijini kwao alikosoma au kwa maana nyingine sakata hilo analifahamu siku nyingi kwa sababu Makonda hakuwa mafichoni. Ni mwanasiasa amekuwa majukwaani akionekana na wanaomfahamu, akina Gwajima walimuona siku nyingi, huku wakifahamu siyo anayeitwa Makonda.
Swali kwa Gwajima ni kwa nini alikaa kimya miaka yote hiyo, Makonda akapewa ukuu wa Wilaya na akapewa ukuu wa mkoa. Akaanza na mapambano ya ukahaba, Ushoga na shisha Gwajima akiwa kimya! Makonda akaja na mapambano ya madawa ya kulevya na hapo ndo Gwajima na wenzake wakaja juu! Hafai! hafai! hafai! Amefoji! namjua tangu Kolomije, ajitokeze.
Kwa Gwajima huu ni unafiki. Kwa kiongozi wa dini anayejinasibu ni mtumishi wa Mungu, hafai. Hata kama Makonda kafoji, Gwajima ameona asimamie haki, pale tu yeye anapoguswa. Walipoguswa wengine aliona ni sawa. Tunaomba atulie na naona busara haijamuingia ndo maana anafikia hatua ya kujikuza kiasi hicho. Bahati mbaya kwa maoni yangu, mchango wake ktk taifa hili hauonekani. Wapo viongozi wanaostahili kuteta na serikali kwa michango yao kwa miasha ya wananchi. Wanajenga shule, wanajenga hospitali, wanasaidia wenye njaa, nk. Not this self-styled askofu!