Gen Z Mnakimbiza sana Magari!

Gen Z Mnakimbiza sana Magari!

Mimi niliwahi ona mwaka 2020 kwenye Golf GTI speed 200 ni kitu kidogo sana kwa gari zenye uwezo. Imagine tulifika 200+ na tukaachwa na gari fulanj hivi sikuijua jina lake ila inakaa watu wawili tu na ilipita kama upepo.
Huo mwendo kwa hayo magari unaona ni kawaida mpaka kitokee kitu ndio utajua ni mwendo wa hatari.
Siku hizi naweza kwenda Dar to Dom au Dar Arusha bila kuvuka 120kph. Halafu cha ajabu unatumia muda ule ule au tofauti ya dakika 10-30 na mtu anaeenda mwendo wa ngiri.
 
Hio picha yako ni edited. Lakini wapo vijana wanaendesha gari mpaka 300kph hapa hapa Tz. Kwani wewe unafikiri inachukua sekunde ngapi BMW M3 au Golf 7/8 R au Audi S3 kufika 250 au 300kph? Zipo video sitaki kuziweka hapa zitawa expose wenyewe.
Mkuu Kwakuwa sijaona hiyo video nikibishana bila kujua kama ilikuwa kwenye controlled environment mf. Drag race event kweli nitakuwa mbishi🙌
 
Mkuu Kwakuwa sijaona hiyo video nikibishana bila kujua kama ilikuwa kwenye controlled environment mf. Drag race event kweli nitakuwa mbishi🙌
Kuna barabara zimenyooka,hazina magari mengi ndio huwa wanatumia. Hii video nilioona BMW,VW na Golf wakienda 250-300kph kwa uzoefu wangu ni kipande cha Same-Mombo yale maeneo unakaribia Mombo barabara imenyooka,iko Smooth eneo tambarare una uwezo wa kuona mbali sana na haina magari mengi.
Hata mimi kipande nainjoi kuendesha gari ni Mombo-Same.
 
Huo mwendo kwa hayo magari unaona ni kawaida mpaka kitokee kitu ndio utajua ni mwendo wa hatari.
Siku hizi naweza kwenda Dar to Dom au Dar Arusha bila kuvuka 120kph. Halafu cha ajabu unatumia muda ule ule au tofauti ya dakika 10-30 na mtu anaeenda mwendo wa ngiri.
Sahihi
 
Video zao zipo Instagram na ukiingia Tu kwenye page zao utakutana na vichaa wa magari hawa watu hawana Kona wala tuta...
Kuna Toyota crown 2GR zimafanyiwa tuning zinagonga hadi speed 300, aisee huku barabarani usijaribu kufanya ligi na vijanaa
 
Mkuu huko highway wanakimbia sana. Vijana wanaendesha hadi 300kph na gari za Mjerumani. Nakumbuka zamani kuna kijana alijipost anaendesha Mark X 180kph ilionekana ni ajabu sana wakati sasa hivi ndio kawaida ya vijana wanaoendesha Toyota Crown
Mkuu wengi wanakimbizana mjini mara nyingi nakua na gari za kuuza au za wateja huwa sipendi kutuma picha ila ningekuonyesha wanavyosota huko wakifuata vyuma naporudi unamkuta mwingine ana Subaru au Mazda yake anaiamini balaa ukimpita anataka mbio ila baadae unaanza kumuona kwa mbali sana na hatokuja kukuta tena..
 
Sio magari tu,hata pikipiki wanakimbiza unakuta mtu amekalia tako moja alafu yuko moto mbaya
🤣🤣🤣Wakati tupo watoto tukitumia neno "motobati "
Mkuu wengi wanakimbizana mjini mara nyingi nakua na gari za kuuza au za wateja huwa sipendi kutuma picha ila ningekuonyesha wanavyosota huko wakifuata vyuma naporudi unamkuta mwingine ana Subaru au Mazda yake anaiamini balaa ukimpita anataka mbio ila baadae unaanza kumuona kwa mbali sana na hatokuja kukuta tena..
🤣🤣Wakikutana na wakongwe mkiwa kazini wanakula vumbi tu
 
Pamoja na kuwa una hoja ILA
magari yanayo fika 300km ni machache sana Tanzania
Lakini pia TANZANIA hatuna barabara ya kutembea kms 300 Barabara zetu nyingi ndani ya klm 2-5 unakuta kona hiyo mia tatu utatembelea wapi?; Kwa wenzetu kuna barabara unaenda umbali wa takribani km 60 ndio ukute cona-Hizo ndio wanatembea hizo klms
Unachokataa ww ni nn na video zimeonekana kabisa jamaa anavuka mpk 300 Tanzania hii hii sasa usiseme haiwezekan sema huwezi
 
Pamoja na kuwa una hoja ILA
magari yanayo fika 300km ni machache sana Tanzania
Lakini pia TANZANIA hatuna barabara ya kutembea kms 300 Barabara zetu nyingi ndani ya klm 2-5 unakuta kona, hiyo kms mia tatu utatembelea wapi?
Kwa wenzetu huko kuna barabara unaenda umbali wa takribani km 50-80 (express highway) ndio ukute Kona-hizo ndio wanatembea hizo kms
Uko sahihi kabisa.
 
Back
Top Bottom