Huijui Tanzania yote. Kama wewe hujawahi au huwezi usiseme haiwezekani. Na huu uzi nimefungua kuwatahadharisha wanaofanya hivyo ni hatari kwao na watumiaji mengine wa barabara.Ulisha ambiwa Tanzania hatuna barabara za kuendesha 300kms.
Highway zetu ZIMEJAA MATUTA na hapo bado kona kila kms 2-5 hiyo 300 utaendeshea wapi labda angani...
Ilikuwa inasoma ngapi Mkuu?Adrenaline rush.
Baadae wakishayakanyaga, waulize kwa nini ulikumba mbio hivyo?
Majibu hawana.
Kuna magari automatically ukiwa unaendesha upo speed, lakini chuma bado inaita. Huoni tofauti kabisa.
Kuna siku, nilikuwa naendesha.
Sioni kama nakimbia, baadae nachungulia dashboard na mawani yangu, nipo speed ambayo kwa hakika sikuitarajia.
Ilinibidi nisimame, niheme kwa nguvu. I was worried. Nisingethubutu kufika huko kama my eyes were on the speedometer.