Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Gavana yupo sahihi. Tuache siasa kwenye mambo ya kitaalamu.

Ukweli ubaki kuwa ukweli hata kama unauma. Prof. yuko sahihi, mlaji wa mwisho (end user) ndio mlipaji wa VAT. Ktk hili tukubali kwamba watumiaji wa huduma za kibenki ndio tunabeba mzigo.
 
Mkuu wengi hawajui na hawana elimu ya kodi. Hawataki kuuliza wanaingia kichwa kichwa tu kujadili kitu wasichokijua. Hakuna mtu anayeweza kujua kila kitu. Lakini hapa JF kuna watu wanataka kila uzi wachangie hata kwa mambo wasiyoyajua. Tujifunze na kuuliza kwa wanaojua, humu JF wapo wataalamu pia wa mambo yanayohusu kodi. Tusome comment zao tuelimike.

Nakubaliana na wewe 100%. Kila mmoja ni mtaalamu kwenye eneo fulani humu JF, ni vema wale ambao si wataalamu wa eneo hilo tukasoma michango ya wabobezi ili tujifunze. Sio vema kutanguliza ushabiki wa kisiasa kwenye issues za kitaalamu. Kuna baadhi ya comments zinashangaza na kuacha maswali mengi juu ya IQs zetu
 
Duh....hawa TRA wamepatwa na nini? Taaluma yao wameweka pembeni? Ni vema siasa wakawaachia wanasiasa!

Kama serikali ilitaka kukusanya kodi kwenye miamala ya benki na simu, wangetumia sheria nyingine lakini sio sheria ya excise au VAT kwa sababu hizi mbili ni consumption tax na anayepaswa kubeba mzigo ni mlaji.

Prof Ndullu yupo sahihi na kwa kweli atatunza heshima yake zaidi akiendelea kusimama kwenye ukweli kama anvyofanya katika suala hili.
 
Prof. huyu ni JIPU toka kitambo!! Escrow, EPA, Richmond, Hati fungani STANBANK, Tshs imetoka US $1=Tshs 1000 (2005) to US $1=Tshs2280 (2015) chini yake-hela haina thamani kabisaa, Money Laundering chini ya utawala wake- tatizo lipo juu sana, nk na sasa VAT zote chini ya utawala wake! Lengo lake ni kuhakikisha Rais anafeli!! Huwa yuko Against na President na kila kitu.

Ana dharau sn kwa Rais. Angalia agizo la Rais kuhusu wafanyakazi hewa, wasio na sifa na mrundikano wa wafanyakazi BoT (karibia 2800 wakati wana wana matawi 4 tu nchi nzima) na response yake kesho yake!! Always negative against the President!! "Kama wana sifa kwa nn wasiajiriwe? Hapa BoT hatuna mfanyakazi hewa"

Anne Kilango alikosea moja tu akatemwa, huyu ana makosa lukuki tena yote yaliyo ligharimu TAIFA. MAGUFULI tumbua huyu katumwa kukukwamisha!!!

Mkuu haya mambo hayahitaji hasira, unahitaji utulivu kidogo tuu ili uelewe kuwa yote uliyoyataja hayamhusu Prof. Kama jambo huna hakika nalo kuwa mpole. Hivi kwanini huyo Prof. hadi leo hajatumbuliwa? Humjui prof mkuu
 
Tuliwambia waungwana humu kuwa iwe vyovyote itakavyokua hizo gharama zinabebwa na wananchi. Pinduka, ruka galagala ila namba lazima isomwe tu tena na vyama vyote.
 
Mabenki yanaweza kufanya jambo dogo tu. Kuondoa service charges zote kwenye miamala na kuongeza 1% kwenye riba ya mikopo. Kwisha. Hiyo itakuwa tax avoidance, sio evasion

Uko sahihi kabisa, au wanaweza kuongeza hizo tozo na kuwa kubwa kufidia kodi zote, either inclusive or exclusive. Tuelewe kuwa hakuna sheria yeyote inayoweka bei elekezi kwenye tozo za mabenki.
 
Huyo prof naye hajui. TRA wamesema mabenki yalikuwa yakusanya bila kulipa. Sio new makato. Mwee
Bado mlipaji ni mlaji. Mabenki ni mawakala tu. Ni kweli hapatakiwi kuwa na makato mapya lakini kama hapo awali walikuwa hawalipi vat sasa watalipa na hivyo kupunguza hapo kwa kiasi kidogo faida yao.
 
Huyu gavana hana msaada wowote nchini..ndio maana BOT ina mauzauza kibao..atoke tu hizi nyakati zimemzidi uwezo.
Atokeje wakati ana msada kwa setokali ya chama chake cha CCM katika suala zima la ukusanyaji wa kodi ya serikali?
 
Kwani ukilipa ada za shule za watoto kwa kuingiza pesa kwenye account ya shule unalipia huo maumala?

Mkuu ndio tunalipia 1000 mimi nililipa CRDB,
Lakini tuwe wakweli hivi benki zikibadilisha bank charges huwa zinatutaarifu , mfano ilikuwa 300.. 500..600 na sasa inachezea kati 800 na 1000 je walikuwa wanaongeza kwa kigezo kipi na je walikuwa wanatujulisha?
 
Lengo la gvt ni kodi na italipwa period,wanajua wanachofanya ndo sababu yakuptsha budget kwa mpera mpera.Ni Jambo Jema katka mwongezeko wa pato la gvt ingawa wananchi joto yake tutaiona
 
Back
Top Bottom