Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Prof. Ndulu yuko sahihi!


Prof Ndulu nafikiri anatakiwa aende tena chuo cha kodi walau akapate cheti ktk hii tasnia ili ajue kama mtu/taasisi ilikuwa haitozwi kiwi ktk huduma, inapoanza kutozwa haitakiwi kuhamisha burden kwa mlaji bali ni katika kiwango kile kile bila kuathiri kiasi kinatozwa kodi,, ninachokiona bank hawataki kupunguza mapato yao ndio maana wanaongeza hilo ongezeko, nafikiri serikali ina kila sababu ya kuchukua hatua na ikiwezakana hata huyu prof atoke tu ili waingie wengine yeye kashindwa kazi kwani TRA ndio kila kitu hata hiyo bot isipokuwepo kwani inategemea mapato ya tra ktk uwepo wake.
 
Kamishna kaaibisha profession.

Kasema kwenye bank charges ya Shs. 1000 wao wanachukua Shs. 153 na Bank Shs. 847.

Swali, tarehe 30 June bank charge ilikua Shs. 1000 au Shs. 847?
Hivi ni kwa nini 18% ya 1,000/= inakuwa 153/= aliyosema Kamishna wa TRA badala ya 180/= ????
 
kama vat analipa mlaji inamana hata waliotunga sheria walikua wanafaham kua huu mzigo ni kwa wananchi still no mercy acha tuisome
 
Mmekuwa mking'ang'ana kila siku "TuLILIPE KODI" sasa kodi wamewaletea tena nzuri itayofanya tuifikie haraka tz ya viwanda mmeanza lalamika tena duh! Tumeipenda wenyewe, chaguo letu milele, acha tuisome namba eeeeeh. hahahahahaaaah!
 
Kama namuelewa Prof, sidhani kama ni mkulupukaji , maana niliona hata kipindi cha wafanyakazi hewa kuna hoja Zake alizisimamia na mpaka leo nadhani ana zitekeleza, sina ujuzi wa mambo ya KODI, ila nakubali kua VAT is a load of final consumer
 
Nyinyi mashabiki wa JPM mnamuabisha mtukufu wenu,angalau kaeni kimya kuficha umbumbu wenu kuliko kuchangia na kuabika hivi. Aliyekwambia VAT inalipwa na mtoa huduma ni nani?Haya ndo matokeo ya kufuata pushups badala ya sera.
Prof Ndulu nafikiri anatakiwa aende tena chuo cha kodi walau akapate cheti ktk hii tasnia ili ajue kama mtu/taasisi ilikuwa haitozwi kiwi ktk huduma, inapoanza kutozwa haitakiwi kuhamisha burden kwa mlaji bali ni katika kiwango kile kile bila kuathiri kiasi kinatozwa kodi,, ninachokiona bank hawataki kupunguza mapato yao ndio maana wanaongeza hilo ongezeko, nafikiri serikali ina kila sababu ya kuchukua hatua na ikiwezakana hata huyu prof atoke tu ili waingie wengine yeye kashindwa kazi kwani TRA ndio kila kitu hata hiyo bot isipokuwepo kwani inategemea mapato ya tra ktk uwepo wake.
 
Hivi ni kwa nini 18% ya 1,000/= inakuwa 153/= aliyosema Kamishna wa TRA badala ya 180/= ????

Kidata, kamishna TRA anajiumauma kwamba ndani ya bank charges ya Shs. 1,000 kulikuwa na VAT ya Shs. 153.

Huo ni uongo kwa sababu VAT ilikuwa exempted kwenye bank charges hivyo hakukuwa na hiyo Shs. 153.

Ndulu anachosema ni kwamba kama bank charges ilikuwa ni Shs. 1,000 basi sasa itakuwa ni Shs. 1,180. Hiyo Shs. 180 ni ongezeko linalotokana na VAT atakalolipa mtumiaji/mlaji.

Ni kitu very simple lakini TRA wanaeka siasa kwenye profession. Wanatia aibu.
 
Nadhani badala ya kumshambulia gavana Ndulu, tuujue ukweli. Bunge limepitisha sheria. Mabeki ni mawakala wa kukusanya VAT na kuipeleka TRA. Kama walikuwa wanakusanya tangu mwanzo bila kuipeleka TRA kama wanavyodai, wachukuliwe hatua za kisheria kwa kuikosesha serikali mapato kwa kipindi chote walichokusanya.
 
Hahahahaha jana nilijua tunaingizwa chaka na T. R. A

Tangu lini V. A. T akalipa mfanya biashara. V. A. T ni consumption tax.

Nchi ya miujiza hiii. Tangu lini kuwe na double standards kwamba bank ndo zilipe VAT ila biashara zingine mteja ndo alipishwe.

Yani tumefikia pabaya sana kama taasisi kubwa hivi za kuaminika zinapishana kauli hadharani.


Ni kweli kabisa mkuu .
Hata TANESCO wanakata VAT 18% mteja anaponunua umeme.
Mzigo huo unamwangukia mteja.
Basi waende na kule TANESCO ambalo ni shirika la umma wafanye marekebusho ya kisiasa kama hayo ya mitandao ya CCM.
 
Hivi yule dogo wa Ilala Boma anaitwa Rashid si bado yupo? Basi inabidi Kidata wa TRA aende review class pale [emoji23][emoji23][emoji23]
 
kitendo cha ile kodi kuiita VAT,Basi mzigo unaenda moja kwa moja kwa mlaji.Labda ibadilishwe jina na isiwe VAT.Profesa yuko sahihi.TATIZO HII NCHI KWA SASA MAAMUZI YA TULIOWAPA DHAMANA YANATOLEWA KWA HOFU YA KUTUMBULIWA.
Ni kweli VAT ni kodi inayolipwa na mlaji wa meisho. Lakini ni kweli vilevile kuwamba mabenki na mitandao walikuwa wanapata fedha nyingi tozo hizi. Ili Serikali ipate mapato katika eneo hili wanaweza wakabadilisha Sheria. Pia ni muhimu kupitia viwango cha tozo kama vitaonekana ni vikibwa ni sahihi viwango hivyo vijumuishe VAT (VAT onclusive). Kwenye mafuta Serkali imeweza kwa nini eneo hili ishindwe
 
Mkuu haya mambo hayahitaji hasira, unahitaji utulivu kidogo tuu ili uelewe kuwa yote uliyoyataja hayamhusu Prof. Kama jambo huna hakika nalo kuwa mpole. Hivi kwanini huyo Prof. hadi leo hajatumbuliwa? Humjui prof mkuu
mpaka leo nashangaa sana prof .Ndullu bado yuko ofisini...huyu anapingana sana na kauli za magufuli..anaikwamisha sana serikali bila shaka atakuwa mfuasi wa Lowasa
 
Atokeje wakati ana msada kwa setokali ya chama chake cha CCM katika suala zima la ukusanyaji wa kodi ya serikali?
kodi inakusanywa na TRA Ndullu anachofanya ni kukwamisha ukusanyaji wa kodi anaihujumu sana serikali labda katumwa na Lowasa sina Imani kabisa na huyu gavana
 
Hivi yule dogo wa Ilala Boma anaitwa Rashid si bado yupo? Basi inabidi Kidata wa TRA aende review class pale [emoji23][emoji23][emoji23]
haah haah kabla ya kwenda kwa Rashid ajisomee notisi za tax zilizo kwenye web ya TRA
 
Hawa Jamaa naona kama wako confused ila professor anaonekana yuko right Kwani bima tangu mwaka jana vat imeingizwa anaelipa mlaji na Hii hivyo ivyo imekula kwa mlaji umeumia
 
Prof Ndulu nafikiri anatakiwa aende tena chuo cha kodi walau akapate cheti ktk hii tasnia ili ajue kama mtu/taasisi ilikuwa haitozwi kiwi ktk huduma, inapoanza kutozwa haitakiwi kuhamisha burden kwa mlaji bali ni katika kiwango kile kile bila kuathiri kiasi kinatozwa kodi,, ninachokiona bank hawataki kupunguza mapato yao ndio maana wanaongeza hilo ongezeko, nafikiri serikali ina kila sababu ya kuchukua hatua na ikiwezakana hata huyu prof atoke tu ili waingie wengine yeye kashindwa kazi kwani TRA ndio kila kitu hata hiyo bot isipokuwepo kwani inategemea mapato ya tra ktk uwepo wake.
duh...wajinga mko wengi
 
Hawa Jamaa naona kama wako confused ila professor anaonekana yuko right Kwani bima tangu mwaka jana vat imeingizwa anaelipa mlaji na Hii hivyo ivyo imekula kwa mlaji umeumia
VAT ni consumption tax...tra wanajua sema kuna mtu wanamuumbua
 
Back
Top Bottom