Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Vat kwenye services haya maajabu! Fedha inayotunzwa na benk yenyewe tu bado ina vat ndani yake maana ni income/revenue za watu na makampuni
 
Ni hatari sana kuendesha taasisi nyeti kama TRA kwa mizuka. Hivi kweli hao TRA hawajui maana ya VAT? Hiyo finance act iliyopitishwa hivi karibuni lengo lake ni kuzidi kuwakamua wananchi. Na ndipo utaliona tatizo la ushabiki wa wabunge wetu na mbwembwe ktk kuropoka "ndiyooo" kizuzu bila kupitia, kuisoma na kuichambua kwa kina miswada inayoletwa bungeni.
Mizuka na uchama vinatumaliza.

Kwa uelewa wangu mdogo ni kwamba VAT ni zigo la mlaji. Benki na Ndulu wako sahihi. Wacha tuisome hisabati kwa miaka takribani 10 tena labda tutazinduka.

Uchama hoyee!
Mizuka hoyee!
Udini hoyee!
Ukanda hoyee!
Asanteni kwa kusoma maoni yangu.

Katika hilo la VAT Uko sahihi kabisa
 
Hapa ndo nawaonea huruma watanzania maana hapa jf wachangiaji wengi n graduates lakin hawajuhi hata vat inalipwaje,benki ni wakala tu,akilipa vat ya kwenye faida mwisho wa mwaka atalipa vipi tena income tax?corporate tax?maana hzo services n source ya faida,hv tra hakuna watu smart au wanamharbia magufuri makusudi,nahisi magufuri ana hujumiwa maana kipindi hiki kuna makosa mengi ya kijinga ni km yanafanywa makusudi
 
I

Ikiwa huyajui haya mambo ni bora ukauliza kuliko kukurupuka. Sio hivyo mkuu.

TRA wamechemka, BOT iko sahihi
Mkuu wengi hawajui na hawana elimu ya kodi. Hawataki kuuliza wanaingia kichwa kichwa tu kujadili kitu wasichokijua. Hakuna mtu anayeweza kujua kila kitu. Lakini hapa JF kuna watu wanataka kila uzi wachangie hata kwa mambo wasiyoyajua. Tujifunze na kuuliza kwa wanaojua, humu JF wapo wataalamu pia wa mambo yanayohusu kodi. Tusome comment zao tuelimike.
 
Huyo prof naye hajui. TRA wamesema mabenki yalikuwa yakusanya bila kulipa. Sio new makato. Mwee
Hehehehehehehe eti prof nae hajui, akili uliyozaliwa nayo umepeleka wapi wewe,?? Yote umeiacha ccm, hapa umekuja na boga tuu??
 
Hii nchi imeshikwa pabaya. Kukosekana kwa wabunge wa ukawa kwenye bunge la bajeti effect yake imeanza kuoneka ndani ya siku moja.
Lusinde et al na huyo mvuliwa baraghashia nafasi mlizojitwalia zinaisababishia taifa madhara kwa kukubali kwenu kupitisha bajeti yenye migogoro kama hii. Wabunge wa ccm kuweni na tabia ya kusoma siyo mnasinzia tu. Naamini wabunge wa ukawa wangekuwepo haya yasingetokea.
 
Ila kwa sasa ile gharama tuliyokuwa tulipa kwa muamala 18% itakwanyuliwa na kupelekwa TRA. Iwapo wataruhusiwa kuongeza gharama za mihamala na serkali ikakubaliana nao ndio hapo watakuwa wamekula matapishi yao. Issue Bank walikuwa wanatoza hela kubwa na ni ajabu kwanini TRA walikuwa hawachukui chao, inabidi wapeleke mapato TRA. Aidha ni uzembe mkubwa ulifanywa na TRA kutotoza ushuru kwenye huduma hizo tangu awali. Haswa watu wa simu ndio wezi kupindukia, watu wamekariri huduma fasta ila ni wezi haswa wa pesa zetu tangu huduma za upigaji hadi za kifedha.
Acha story za vijiweni tafuta ukweli
 
huyo prof asituchanganye kabisaaaaa!!!swali hapo ni hili:je kutoa pesa au kutuma pesa ni huduma ?na huduma hii benk walikuwa walapeleka VAT serikalini?kama hapana maana yake serikali ilikuwa ikipoteza mapato ya kodi hii!!!maana yake walikuwa na msamaha Wa kodi hii!!hivyo serikali imeondoa msamaha huu!!Prof huyu kama haelewi basi ni jipu ajiuzulu haraka!!
Awali hakuna,hiyo ni sheria mpya,lazima gharama zipande ili kodi mpya ipatikane
 
Hapa ilitakiwa serkall iseme makato yanayofanywa na benki ni makubwa

Mfano kama ni tshs 1000
Basi kuanzia julaii makato yabaki ni 1000 na katika hiyo 750 iende bank na 250 iwe kusanyo la kodi.

Hapo bado anayelipa kodi bado ataendelea kuwa mlaji na faida kubwa ambayo benk ingepata itapungua

yaani waziri wa fedha ameshindwa kutumia mbinu kama hii.
 
TUACHE UKILAZA WATANZANIA, KODI SIKUZOTE ZIKIPANDA GARAMA ZA HUDUMA ZINAPANDA... SASA KUTOA PESA NI 800, KODI KWENYE KUTOA PESA NI ZAIDI YA 1000... BENKI ZITAFANYAJE KAZI KAMA HAWATAPANDISHA GARAMA ZA KUTOA PESA,... VIL.AZÀ NYIE. PROFESOR YUPO SAWA
 
Wizara ingekaa na Mabenki kujadili.....Wangekubaliana na kupata kodi stahili

Pia Wizara ya fedha ingekaa na M PESA, Airtel Money na Tigo Pesa kujadili na kukubadiliana -----TCRA ipo na inaona kila senti inayotumwa na kupokelewa

Mbona hii Serikali ina double standards? Wanakaa na mijamaa ya Migodi, wanakaa na mijamaa ya Mafuta...lakini kwingine inaonea watu

Uzuri Mmoja BOT inaona transaction zote zinazofanywa na Mabenki....kwa hiyo sio rahisi benki kudanganya

VAT duniani kote inajulikana ni consumption tax, Value ADDED tax

Hata kwenye Tourism, wamefanya Grave mistake......Madhara yake ni fatal kwa tourism, currency, employment and economy as large...

Serikali imefika hatua mpaka inacharge VAT pesa zake zenyewe....PARK entry fee ni PESA ya Serikali direct...
 
Gazeti la Mwananchi: Wakati TRA ikiitaka BOT izichukulie hatua bank zilizotangaza kuongeza gharama za huduma za kibenk, BOT imesema mabenki yapo sawa!

Prof.Ndulu anasema mabenk watakuwa mawakala wa TRA tu katika kukusanya VAT lakini si walipaji,kwa hiyo hawezi kuwachukulia hatua.

Beno Ndulu ametolea mfano unapokua unauza duka unakuwa wakala tu wa TRA na sio mlipaji.....KUMEKUCHA
Aondolewe kwasababu anapingana na (TRA ) mamlaka iliyotoa taarifa za ukwepaji wa kulipa kodi kwa mabenki na kututwisha mizigo sisi wananchi
 
Huyo prof naye hajui. TRA wamesema mabenki yalikuwa yakusanya bila kulipa. Sio new makato. Mwee
VAT ni Value Added Tax. Mfanyabiashara yeyote anapiotoa, anaihamimishia kwa mlaji. Kama serikali ilikusudia kukusanya kodi KWENYE MAPATO ya benki, basi isingekuwa VAT, ilipaswa iwe KODI YA MAPATO.

Shida moja bungeni wamebaki waomba minara, wanaoelewa wapi Magharibi wapi Kusini wamehujumiwa hadi wamesusa. Gavana yupo sahihi. Hakuna mfanyabiashara analipa VAT, yeye ni mkusanyaji tu. Hili tamko la kuwabana wenye mabenki limekuja baada tu ya malalamiko, wala hawakuwanalo akilini na ndio maana hawakutoa mwongozo.
 
Swali la msingi ni Je wizara husika walipopitisha kodi hii waliwashirikisha BOT,TRA na wahusika wengine kama watendaji wa juu wa Benki zilizopo Tanzania ili kufikikia makubaliano ya utekelezaji wa makusanyo haya?

Inashangaza kuona mamlaka mbili zilizopo chini ya serikali moja kutoa matamko tofauti kwenye swala moja linalowagusa/kuwaunganisha wakati utekelezaji wa maamuzi ya serikali umeshaanza na unawagusa wananchi moja kwa moja.

Kwa nini gavana wa BOT ama mabenki hawakutuonya/kutoa tamko kabla ya makusanyo hayo kuanza? Au hawakushirikishwa katika hatua za awali za uundaji wa utaratibu huu mpya wa ukusanyaji kodi na hivyo hawakuwa na namna ya kuzuia mfumo huo zaidi ya kukubaliana nao na kuhamishia gharama kwa mteja.

Either way hii haijakaa vizuri kwa serikali maana wananchi ndio wanaachwa katikati hawajui washike tamko la nani, cha msingi ni kujiandaa kisaikolojia kwa lolote sitashangaa nikisikia benki zilizopandisha tozo kufungiwa ama kunyang'anywa leseni maana lolote linaweza kutokea kutokana na maamuzi ya viongozi wetu ambayo hayajaona/hayajatambua madhara kamili ya utekelezaji wake.
 
Tusiwe wavivu wa kupata taarifa sahihi mabenki yapo sahihi na prof yuko sahihi tatizo tuna wabunge wengi wa ccm uelewa wao wa mambo ni mdogo saaana hawasomi.Naomba watu waaome income tax practise notice number 05/2013 iliyotiwa sahihi tarehe 1/11/2013 inayozungumzia business income ndio utajua sasa wakuu wameamua kwa makusudi kupindisha sheria za nchi . Na lazima tujue VAT as per international taxation laws mlipaji ni final consumer and not otherwise.kama tumeamua kuwa na ' VAT' ya definition ya kibongo kibongo well and good lakini is not health kwa elimu yetu watu wako vyuoni wanasoma hivi halafu in practices wanakuta vike its ridiculous and shame kwa watu walioshiriki kupitisha mambo ya hovyo kama haya
Tulilia maridhiano kati ya wabunge wa ukawa na NS kwa afya ya taifa...watu wakasema NS aendelee kuwanyoodha...naamini Kabisa ukawa wangekuwepo bungeni hii kitu ingeangaliwa kwa jicho la tatu Na huu mkanganyiko usingekuwepo...kila kitu kingewekwa sawa huko huko bungeni...ninachoshangaa zaidi ni pale commissioner Mkuu TRA mishipa ya shingo inamtoka akiongea kitu ambacho anajua kabisa sio sahihi...ila Jana nilipomuona akiongelea hili jambo nilihisi kitu kwani kichwa Na mdomo vilikiwa havina ushirikiano...Sijui aliambiwa tu nenda ukaseme hivi..
 
hv tra hakuna watu smart au wanamharbia magufuri makusudi,nahisi magufuri ana hujumiwa maana kipindi hiki kuna makosa mengi ya kijinga ni km yanafanywa makusudi

Jiulize kwanza anashaurika? Serikali hii inahitaji inputs za wataalamu?
 
nilivyosikia Bosi wangu wa zamani anaenda kuwa kamishna Mkuu TRA nikajua tu sasa tunaingia chaka! jamaa ni muoga sana na wa kujipwndekeza. ni mchumi asiejua mambo ya Kodi. BOT, Mabank wako sahihi, VAT analipa mlaji!
 
Back
Top Bottom