Shoctopus
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 3,435
- 1,995
Ninyi wote tatizo lenu ni kutaka kuvuna bila kupanda. Tangu lini value added tax ikatozwa kwenye hela? Tena ni hela ya mshahara au pensheni ya mtu iliyokatwa kodi kabla ya malipo! Hivi mamilioni waliyoficha ugaibuni wangekuwa wanakatwa vat wangefurahia kweli? Tusidanganyane lengo la kodi nchi hii ni kuwafilisi masikini tu! Beno nisikilize! Hii kodi inatozwa kwenye mapato ya benki yatokanayo na service charge, wewe unataka alipe "mlaji" eti kwakuwa inaitwa 'vat' tu? Ungeeleweka kama ungesema isiitwe 'vat' vinginevyo nia yako ni kukwepa kodi. Au ufute service charge kabisa kwasababu sisi wengine tunalazimishwa kupokea mishahara au vijipensheni vyetu kupitia vibenki vyenu ambako hatulipwi riba (interest) badala yake tunatozwa hiyo service charge! Huku ndiyo nasema ni kuvuna bila kupanda. Narudia: mshahara umeshakatwa kodi, halafu unanilazimisha nikaupate benki ili nitozwe service charge! Hii ni nini kama sio wendawazimu? Yule unyenilazimisha nimpelekee pesa yangu ndiye anayepaswa kunipa asante sio kuninyanyasa. Hebu nikuulize bwana BOT Gavana, Yale mamilioni ya epa na escro waliyogawana wakubwa angalau walilipa kodi yeyote? Tena baadhi yao wako bungeni wanapitisha sheria za kuwanyonya zaidi wanyonge wa nchi hii!Kama vi VAT lazima mlaji wa mwisho ndio atailipa.
Kama ni makato si benki wanayalipia kodi kwenye jumla ya faida yao wanapokabidhi mahesabu kwa tra.
Najua makato katika huduma za kibenki ni sehemu ya mapato ya taasisi za fedha ambayo mwisho wa siku kodi yake hulipwa na hayo mabenki.
Haiwezekani mabenki yakalipa kodi mara mbili, alafu wao input Vat, itakua ni output tu sasa wao watadai refund kama hakuna imput vat?
Nadhani serikali ilichemka kwenye hili. Haya ndio matatizo ya kila kitu ndio bungeni bila kuwaza.