Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,705
- 36,154
Maskini ni kama mchawi tu maana hupenda sana habari mbaya.
Tena ukitaka afurahi zaidi asikie kuwa tajiri kafilisika, Boss kashushwa cheo. Hata wenyewe maskini hawapendani hasa pale maskini mmoja akionekana kupata chochote kitu.
Magufuli aliijua hii kanuni, akaanza kuwasumbua matajiri. Mioyo ya maskini ilifurahi sana bila kujali kuwa tajiri hawezi kafilisika kwa kiwango cha 0°.
Maskini walifurahi Magufuli alipowatumbua mabosi ambao walikuwa hawamtukuzi yeye na utawala wake, maskini walifurahi sana bila kujali kuwa zile nafasi hawatazirithi wao.
Magufuli mpaka kesho analiliwa na maskini , ukiwauliza kwanini mnampenda sana utawasikia eeh alikuwa mtetezi wa wanyonge, aliwanyoosha mafisadi . Kama alikuwa mtetezi wa wanyonge , je, miaka 6 ya utawala wake aliuondoa unyonge(umaskini) kwa Watanzania wangapi?
Aliongeza ufukara na umaskini miongoni mwa Watanzania maana wengi walikosa kazi kwakuwa mwajiri mkubwa (private sector) alimuua kwa mgongo wa kumnyoosha
Maskini wanaamini matajiri ni wezi wa pesa zao.
Maskini akisikia mtoto wa jirani kafeli form four moyo wake unakuwa mweupe hata soda anaweza kukununulia.
Roho ya "tukose wote" ni roho ya kichawi.
Maskini anafurahia tajiri kufungwa na kufilisiwa bila kujali kuwa bilionea mmoja analisha familia zaidi ya 1000 direct or indirect.
Ushauri : Tumia njia yoyote ila kuukimbia umaskini . Sijasema uue.
Tena ukitaka afurahi zaidi asikie kuwa tajiri kafilisika, Boss kashushwa cheo. Hata wenyewe maskini hawapendani hasa pale maskini mmoja akionekana kupata chochote kitu.
Magufuli aliijua hii kanuni, akaanza kuwasumbua matajiri. Mioyo ya maskini ilifurahi sana bila kujali kuwa tajiri hawezi kafilisika kwa kiwango cha 0°.
Maskini walifurahi Magufuli alipowatumbua mabosi ambao walikuwa hawamtukuzi yeye na utawala wake, maskini walifurahi sana bila kujali kuwa zile nafasi hawatazirithi wao.
Magufuli mpaka kesho analiliwa na maskini , ukiwauliza kwanini mnampenda sana utawasikia eeh alikuwa mtetezi wa wanyonge, aliwanyoosha mafisadi . Kama alikuwa mtetezi wa wanyonge , je, miaka 6 ya utawala wake aliuondoa unyonge(umaskini) kwa Watanzania wangapi?
Aliongeza ufukara na umaskini miongoni mwa Watanzania maana wengi walikosa kazi kwakuwa mwajiri mkubwa (private sector) alimuua kwa mgongo wa kumnyoosha
Maskini wanaamini matajiri ni wezi wa pesa zao.
Maskini akisikia mtoto wa jirani kafeli form four moyo wake unakuwa mweupe hata soda anaweza kukununulia.
Roho ya "tukose wote" ni roho ya kichawi.
Maskini anafurahia tajiri kufungwa na kufilisiwa bila kujali kuwa bilionea mmoja analisha familia zaidi ya 1000 direct or indirect.
Ushauri : Tumia njia yoyote ila kuukimbia umaskini . Sijasema uue.