Freeman Mbowe, Sugu, Msigwa na Lema

Freeman Mbowe, Sugu, Msigwa na Lema

Status
Not open for further replies.
Umejitahidi sana kujionesha ulivyo mjinga na drs lako la saba, yaani unadhani uongozi ni vyeti na cv za ubabaishaji je Mandela ndiye msomi kuliko wote Africa? Je mikataba feki imetiwa saini na watu ambao hawakwenda shule, ni kilaza hadi unatia aibu
 
hili sio swala jipya na wala halihitaji ushahidi wa kiasi hicho..
we angalia matendo yao tu utajua hawa wanaendeshwa na yale majani aliyokuwa anapenda kuyatumia ROBERT NESTA MARLEY
 
Lakini wanajituma sana kuliko hao wenye CV iliyojaa kibiriti. Tatizo ni katiba, ati inatosha alimradi anajua kusoma na kuandika!
 
Nimegundua kisa cha vijana wengi kuiba mitihani na kufoji vyeti !
 
kwa elimu hizi za hawa watu kweli chadema hakifiki kokote kumbe kimejaa wajinga kiasi hiki.
 
Hii hoja haina mashiko, elimu ni kitu tofauti na uongozi,
Hebu tujiulize, Kawawa alikuwa na elimu gani,? mzee Mwinyi ana elimu gani? Baba Karume alikuwa na elimu gani? etc, etc na walishika madaraka gani kwenye hili Taifa? Ni viongozi wangapi kwenye hili taifa wenye elimu za Prof, Phd ambao wanafanya vitu vya ajabu_?

Hebu tuwekee elimu ya Prof Maji Marefu na Ole Sendeka hapa
 
Siasa na uongozi ni vipaji kutoka kwa mwenyezi mungu,elimu ni fursa ya kidunia,kipaji hakijifichi usipokuwa na elimu kubwa,na mara zote kiongozi bora ni yule asiyekua na elimu kubwa maana anashaulika kulikoni msomi anahisi anajua kila kitu.mwisho wa siku linganisheni kati ya viongozi wenye elimu kubwa na wasio na elimu kubwa kiutendaji,utashi na busara
 
Kwani mkuu babayako wewe ni mgeni hapa Tanzania?

Hao uliowaorodhesha wote wanajulikana ni "vilaza".

sasa mkunga na zile cv za uprofesa za mawaziri na wabunge wa ccm zimetusaidia nn miaka 50 baada ya uhuru...?????
 
Last edited by a moderator:
Uongozi ni kipawa kinachotoka kwa mwenyezi mungu bila kujali kiwango cha elimu yako.Unaweza ukawa na elimu kubwa lakini uongozi ukakushinda kwa sababu hujachaguliwa na mungu kuongoza.Na ndiyo maana hakuna hata Taifa moja hapa duniani ambalo linaongozwa na viongozi wenye cv ambazo zinafanana kila kiongozi ana umuhim wake kulingana na nafasi yake aliyopo kwa kuzingatia umuhim wa kila mtu mungu alimnyima mtu mwingine elimu akampa uwezo wa kuongoza ili amsaidie aliyempa elimu kubwa pia mwenye elimu kubwa kanyimwa uongozi ili atumie elimu yake kumsaidia kiongozi wake ambae amenyimwa elimu ya kawaida lakini uwezo wa kuongoza anao.Kwa ujumla ni kwamba uongozi ni kitu ambacho kinaendeshwa kwa kutegemeana bila kujali elimu ya mtu.
 
Naomba CV ya Chenge, Ngeleja, Tizeba, Makinda, Ndugai, Serukamba, Mulugo, Nkamia...
 
mimi nawapongeza sana hawa watu kwa elimu hii wamewaacha mbali sana chenge,balali,yona,pro kapuya na mafisadi wanaosaini mikataba kama wamelala.je wangekuwa na elimu za juu si ingekuwa balaa?
 
sasa mkunga na zile cv za uprofesa za mawaziri na wabunge wa ccm zimetusaidia nn miaka 50 baada ya uhuru...?????

zimetusaidia kujenga miundombinu na mtandao wa barabara za lami nchi nzima, shule za sekondari kila kata, vyuo vikuu kila mkoa, hospitali za rufaa kila mkoa na za kawaida kila kijiji na kazi inaendelea kutuletea katiba mpya, demokrasia ya kweli nk
 
JamiiForums siku hizi imeingiliwa!!
Hawa joiners wa mwaka huu wote inabidi wapewe orientation kidogo. Wawe wanasearch kwanza mada kama ilishawahi kujadiliwa hapa kabla ya kuja nayo tena. Hizi CV za hawa watu tumeshaziscuss kwa zaid ya miaka 3. Kila mtu anafahamu hawana shule na sidhani kama kuna jipya tena . Mods, muwe mnafanya kazi yenu ya kuziunganisha bana!!



Yap! Rejao habari ya siku tele Mkubwa!
Nakwambia hawa watumwa wanaonaingia humu jamvini bila kupekuwa kwanza yani ni giza tupu humu!
 
Last edited by a moderator:
Nyimbo za Ugaidi,Ukabila ,Udini na ukanda zimechuja sasa unakuja kwenye cv, uongozi siyo cv ni kipaji kutoka kwa mungu,ni madudu mangapi yanafanywa na watu wanao jiita wana Phd, mirambo alikuwa na cv ipi mbona ni shujaa na atakumbukwa na vizazi vyote.Hebu tupatie cv yako

Tuko pamoja mkuu
!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom