Ben T
JF-Expert Member
- Sep 18, 2013
- 245
- 263
. iNGEKUW AMNAFANYA FOREX HIZO HELA ZA KUGAWANA KTK PYRAMIDS ZISINGEKUWEPO.NA UKIACHA MALIPO YA MWEZI ULIPASWA ACCOUNT YAKO IWE HAI NA UPOKEE FAIDA ZAKO KM KAWAIA KWA VILE UNAINGIZA HELA.UKWELI NI KWAMBA WANAKUCHOMOA NA HUPEWI HELA ILIYOBAKI.KWA VILE NI DANGANYA TOTO, hizo hela mnazogawana ktk ada za kijinga .
Nicholaus umeandika maneno mengi sana lakini suala la msingi hujaligusa hata kidogo, ngoja mimi nikupe ufafanuzi ufuatao:
TMT (The Million Team) imeunda baada ya mchakato mrefu sana wa kuitangaza Biashara ya Forex hapa Tanzania, kimsingi biashara hii ilikuwa inafanyika lakini kwa watu wachache sana ambao walikuwa wanaifahamu na hawakutaka kushare na Watanzania wenzao. Kilichofanyika kwanza Mr Ontario aliitangaza hapa JF na alipata mwitikio mzuri kutoka kwa Wanajamii wa Forum hii.
Kilichofanyika ni kuhamasisha watu wasome vitabu kwa wingi ili wapate kufahamu undani wa Forex na kweli hilo lilifanyika kwa kiwango kikubwa vitabu vilitumwa vingi tu na hata wewe ukivihitaji utatumiwa nawe pia uvisome.
Baada ya hatua hiyo kilichofuata ni watu kupata mafunzo ya wiki moja lakini Mr Ontario alitoa Offer kwa watu 300 wa mwanzo ambao wangejisajili TMT kuwa angetoa mafunzo kwa ada ndogo tu ya Tshs 65,000/= ili kulipia gharama ndogi ndogo za uendeshaji wa Ofisi na kufacilitate watoa mafunzo. Watu walishiriki vizuri sana na kumaliza mafunzo hayo ya awali.
Baada ya mafunzo ya awali kukamilika Mr Ontario akasema mafunzo yatakayo endelea kwa anae hitaji atachangia kama ada Tshs 130,000/= na ni mafunzo ya siku 5 na mara nyingi yanaanza Jumatatu hadi Ijumaa. Unachokipata katika mafunzo hayo kwanza ni kuifahamu Forex, pili kufahamu njia sahihi ya jufanya uchambuzi wa soko la Forex muda gani wa kuingia na muda gani wa kutoka na mengineyo, lakini la muhimu zaidi ni kupata Lifetime Mentorship huu ni kama muongozo wa jinsi ya kufanya Trades zako kwa maisha yako yote.
Naomna nikuweke wazi Mr Nicholaus hakuna kuchangizana fedha pale TMT kwa mtindo wa UPATU kama unavyodiriki wewe kuwaaminisha watu. Biashara ya Forex inafanyika kupitia kwa Brokers ambao si lazima mtu akuchagulie bali unachagua wewe mwenyewe na ukiridhika unamtumia fedha unafungua Live Account na unaanza kufanya biashara. Brokers wako regulated na Mamlaka zinazoangalia mambo yote yanayohosu Forex.
Mr Nicholaus ukiona kitu hukifahamu jitahidi sana kuuliza na si kuja na analysis yako na kuanza kuwasema watu kuwa wanaendesha UPATU hiyo si sawa. Ni kukumbushe tu kuwa wakati TMT inaanzishwa pale Jangid Plaza walishakuja Maofisa kadhaa wa Serikali wakiwa na Polisi baada ya kupokea wrong information kama hizi unazozizungumza wewe na walipewa maelezo ya kutosha na kuangalia vibali vyote na kuona kuwà hakukuwa na tatizo lolote.
Povu limekutoka sana ila unachokizungumza ni kitu tofauti kabisa na kinachofanyika, watu hawachangishwi fedha kama kwenye upatu, wanalipa ada ya kuhudhuria mafunzo na unapotaka kufanya biashara ya Forex wewe unakuwa na account yako ambayo haiingiliwi na mtu yoyote zaidi yako wewe na Broker wako tu.
Tujifunze kuweka akiba ya maneno kwa sababu si kila jambo unaweza kulifahamu kwa ufasaha wewe pekee yako wapo watu wengine wanajua mengine mengi uliza usibeze na kutoa lugha za kashfa haiyumkini wapo wenye kashfa zaidi yako.
Mwisho nikuase tu kuwa kinachokusumbua tunakifahamu acha hizo tabia wewe ni mtu mzima sana mapovu yanakutoka bila sababu na kama mtu huwezi kushindana nar basi jiunge nae, unakaribishwa sana TMT ili uje upate mafunzo. Pambana na Hali Yako!
Nawasilisha