Ni mchanganyiko fulani wa upatu ktk forex na km betting fulani controlled na computer. Hella wanazopata ni vizo wanazolipishwa ktk membership fee, na hela kibao za kufundishwa.Zinazungushwa kiakili ktk formula za computer jamaa wanapewa kidogo kidogo cha kuendelea.Km ingekuwa biashara yenye faida halisi ya soko.wenye mtandao wasingeweka malipo ya mwezi wanayapa amjina fulani ila ukweli wanazirudisha hizo hela ktk mgao. kawaida ya upatu wanaoingia mwanzoni wengi wanajua kuwa haitokula kwao.Na wanajua wanapiga mandezi.Wengine huwalinda watumwa wao kwa kuwaambia usiongee na watu wenye akili ndogo,wapinga maendeleo,huko kutoongea kunasadia hata watu wa dini ili kulinda watu watu wao wasishawishike kutoka, na hata wakipigwa au game likianza fikia pagumu karibia na kuanguka.huwa wanaanza walaumu wateja wao kuwa shida sio upatu ,ila wao ndio wavivu.
Ni km forever living ,wanadanganyaw atu ni biashara ,kumbe wanataka kula hela yao, na mavitu wanayowauzia wanawaambia hakuna shida hata ukitumia tuu sio shida ,ila ingiza watu.Watu wanakuwa wateja wakimini kuwa ni wajasiria mali. wanakwenda gombana na rafiki na ndugu wanapopeana hasara au ndugu wakikataa kuingia ktk huo upuuzi.Wauzaji dili za upatu ni wanyonyaji wa mahusiano,anakutumia wewe kuweka uhsino wako rehani ili umuaminishe anayekuamini kununua bidhaa kwa faida yao.Na siku zote husema mafanikio ya uongo kuliko waliyo nayo. Nawajua wengi wamejenga kwa mikopo ila wanawaambia watu kuwa ni forever living, wakishakosa watu wanawapasha kiporo moto wale wale kwa kuwadhalilisha kuwa ni wao tuu hawakomai warudie km hawataona mafanikio. Watoto w ashule wengi ndio wanajiunga bila kujua.Na wafanya kazi wa serikali wasiopenda kuumia ktk bisahra halisi.