Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

Dah..mie nakumbuka jinsi tulivyoishi porini huku tukila mizizi na matundapori kwa miezi mitatu mimi na rafiki zangu wawili. Tulikuwa tunatafutwa kwa kuchoma moto malori mawili ya jeshi yaliojaa wanajeshi wakiwa na silaha zao 🙂
 
Ray C ktk ubora wake, kitu NIWE NA WEWE MILELE, nipo shule ya kidini, ya boys, Mwl mlezi, full unoko, kaikamata barua yng kutoka KILAKALA GIRLS, ticha si akaja kuisoma barua yote Assembly! Ticha anaisoma huku anapandisha mdadi. Masela wanamshangilia. Ilikuwa kesi ya kufukuzwa shule, thanks nilipenya tundu la sindano!
 
Kunywa pola,kudeki utumbo,kukata gogo,outdoor nadhana maneno aya wanayajua wenyewe
 
....niliibiwa tranka zima baada ya kutoka likizo nikiwa na mazagazaga kibao tena kwa kuchelewa unakuta wenzako wote wapo juu ya mawe, jamaa wakachokonoa mpaka likafunguka then wakabeba mazaga yote, likizo iliyofuata sikubeba kitu zaidi ya hela tu, katika kulipiza kisasi nilihakikisha kila mtu nmemliza, hakuna tranka nililokuwa siwezi fungua, nlkuwa na funguo kama 30 hv kipindikile kufuli zote ni tri-circle
We itakua uliku mchoyo haha mpka ukaibiwa tranka lote
 
1.kuto nunua vifaa kama vile sabuni mafuta dawa ya mswaki, kawaidah naamka mapema kugongea vya wengine

2.kusubiri chakula cha ziada baada ya muda wa kula kupita
 
Ulitokea ugomvi jamaa mmoja wa Six alikula mke ya mwanakijiji akakamatwa akachezea kichapo kesho yake jioni Mungu ndio anajua ,jamaa walitugawa kwenye platoons kikosi kikasonga mbele kwenda kijijini ,wanakijiji walichezea kichapo siku tatu mfululizo ,Jamaa wa CCP wakashindwa tuliza mtiti siku ya nne defender kama 30 hivi zikazingira shule ndio msala ukazimwa

Umenikumbusha nikiwa Form 5 kulikuwa na mechi ya A-Level na O-Level basi ikatokea O-Level wamshushia kichapo jamaa wa Form 5. Usiku mikakati ya kuwachapa ikapangwa, asubuhi tumeamka tunaona Polisi wanafanya Kwata nje ya Mabweni yetu. Tukaanza dialogue kwamba hakuna fujo inatokea, baada ya muda wakaondoka. Kilichotokea baada ya Assemble 0-Level walikula bakora sana na haikujalisha ulikuwepo uwanjani jana au lah. Vurugu ilitulizwa na Polisi ambao Kituo chao kipo mita 200 tu kutoka shuleni. Katika kukimbia nikaanguka kwenye matuta wenzangu wa nyuma wakanifanya daraja huku Polisi wanakuja jamaa wananikanyaga bahati nzuri nikaona shimo pembeni nikaingia humo ndio ikawa salama yangu.
 
1.tulikuwa tunachukua nyanya na viazi nakwenda kwenye poli la shule nakuni kupika Chui
2.wanafunzi wa boarding kuwaibia wale form one peanut butter siagi dawa ya mswaki pocket money navengine kwenye trucker
3.kwasababu tulikuwa karibu na beach tunatoroka kila time yajioni kwenda kuogelea na kula samaki kama unamkwanja sikuhio
4.kupiga kelele usikuu kisha patron akija nafimbo watu Libya
5.kutege prepo na Rafsanjani
6.kusingizia unaumwa ili uende home
We jamaaa umesoma lini hyo shule mbona unaandika kwa tress namna hyo
 
Makongo;

Kuna mtu alikuwa mtata sana anaitwa Afande Miraji(RIP) alikuwaga NA kawaida ya kupita kitaan kwetu saa 1 usku kila akiwa anatoka job kwake Makongo sec school ...sasa mzee wangu NA mm mili ilikuwa inaendana kdgo alikuwaga naye mjeda NA alikuwa anapenda sana kukaa nje mida hiyo usiku....siku Miraji alipopita nikiwa nimekaa mm pale nje mzee hakuwepo jamaa akatoa shikamo kama kawaida yake NA mm nikaitikia marahaba kumbe akaishtukia ile saut sio ya mshua akaenda zake kimya kimya ...kesho yake jamaa alikuja nichomoa darasan akanipeleka ofisin kwake niliporud joints zote mwilin hazifany kaz maana push ups,kichura chura ndio zilikuwa adhabu zake wiki nzima najisaidia aja kubwa nimesimama maana kuchuchumaa siwez ,...Bas toka siku hiyo nikawa sikae nje ya home kwetu ikifika SAA 1 usku

Kigonsera Sec School

1.Kulikuwaga kuna kajamaa kamoja kutoka Mbeya kalikuwa kanawaingilia wanaume wenzake kishirikina,Aliweza kuwaingilia wanafunzi wengi sana(Mm hakuwahi nigusa hata chembe)...Sasa siku akaingia anga za dogo mmoja (nahisi naye alikuwa ninja ) kutoka Rukwa ndipo alipodakwa kichapo alichopata nusu wamuue ikabid baadae wamuhamishe shule ndio ikawa salama yake

2. kuna Teacher mmoja Yank flan hiv alikuwa anatoka Songea mjin anakuja Mbnga(kigonsera) kutupigia practical za chemistry NA Bios NA kesho yake anageuza, Yy alikuwa rafik wa wanafunzi kwahiyo akawa analala kwenye madom ya wanafunz ...Kulikuwa kuna Teacher mmoja kila ikifa SAA 12 kasoro anapita Dom hadi Dom kuamsha wale ambao hawajasmka, NA kawaida yake akiingia tu akakukuta umelala anatandika bakora hapo hapo juu bila hata kukustua ww unakuja shtukia kitu paaah! ...Sasa siku akaingia room ambapo teacher alikuwa kalala NA wanafunz ndan ahahahahaha jamaa alimtandika fimbo moja ya nguvu yule mwalimu akiwa usingzin ,teacher ikabid apige kelele "mm mwalimu wa practicaaaaaal sio mwanafunz"

Pugu Sec School.

1.Baada ya kukimbia Kigonsera kutokana NA barid Kali nikajiunga Pugu.....Huku identity ya kwamba huyu ni mwanafunz wa Pugu ilikuwa ni kujikuna sehem za siri kwa7bu ya fungus kutokana NA shida ya maji MTU alikuwa anaoga ikifika ijumaa au jmos akiwa anadrop kwenda town maji pale yalikuwa ya pond...

2. Tulikuwa NA kawaida ya kuwa NA magroup ya wanafunz wasiozid 10 katika kugawana chakula,wali au ugali NA mboga zinajazwa kwenye sufuria mbili kubwa kisha anateuliwa mmoja kuwagawia member wa group ambao sahan zao zimetandazwa chini....sasa siku nikachelewa dining bwana alafu ilikuwa siku ya wali nyama(ilikuwa kama sikukuu Siku hii maana attendance inakukuwa nzur hata wale watoro waliokubuhu wanakuwepo) ...Baada ya kukosa kwenye group letu nikaona kuna group linatafuta chimbo ili waanze kugawana menu ikabidi niunge walipotandaza sahaan chin NA mm nikaweka yangu katkat ....Bas yule group leader(jamaa nahis alikuwa NA roho ya Nduli) maana alisambaza chakula Sahan zote tena zimejaa mpaka zinamwagika nyama tatu tatu huku sahan yangu ikiwa nyeupe haina kitu, nilipomuuliza kwann imekuwa hivyo jamaa akanijibu " group letu mzamiaji hana nafasi" daah ikabid niwe mpole tu

3. Tulikuwa tunashindana kupiga msuli PCB darasa letu ...msuli unaanza SAA 4 usiku mpaka pale mshindi anapopatikana ....Masharti ya shindano member wote mnachangishana mia 2 NA pesa inayopatikana inanunuliwa mikate inawekwa mezani mshind anapewa, ni mikate sababu Pugu chai ilikuwa inachemshwa ila vitafunwa unajininulia mwenyewe......,Sharti la pili ukisinzia tu umejitoa unapewa red card NA msimamiz ambaye naye alikuwa sio mshindani anaruhusiwa kusinzia NA walikuwa wanapeana shift saa 4,6 & 8.....Bas kuna jamaa akikuwa anaitwa Mwisho Wa Lami alichukua mikate for 4 consecutive days maana alikuwa anafika mpaka SAA 11 asbhi peke yake cha ajabu kwenye parade 1 lazima umkute wakat sisi wengine tulikuwa tukifanikiwa kufika sana bas SAA 8 au 9 ndio pumzi zinaishia(usingizi) inabid ukalale tu japo mikate unaitaman NA kuamka kwake ujue ni SAA 4 mda wa chai....Headmaster alimpatiaga zawadi huyu jamaa baada ya kuzisikia habar zake.
Nilikua pugu ujamaa 5 PCM miaka 90,umekumbusha mbali sana mambo ya pond, kudrop na mwisho wa lami, bus letu lilikua uda la kwenda kisarawe, tulikua tunapandia msimbazi
 
Wale wa Kantalamba tukutane Chanji kwa Mbombo ngafu au kwa mama kalekwa kwenye Wanzuki na kimpumu.
Na wale wa Jamhuri High school Dodoma tukutane 84 Club
Daaa umesahau chiluba na mazwi kupiga gongo,kidedi kuvutia ganja miksa chanji kwenda kuchi pilau j pili night
 
1. shuleni kwetu kulikuwa na tabia ya viongozi kupita mabwenini saa kumi na moja asubuhi kuamsha watu na atakayekutwa kalala bakora za kufa mtu. sasa siku moja tuka jipanga mtu mmoja akakaa mlangoni ile wamaingia tu mlango ukafungwa, asee tulikuwa na fimbo za kutosha na chaga tuliwachapa sana, na kesi tukashinda,

2. kuiba mahindi na kuchemsha kwenye ndoo kwa kutumia heater juu ya dari, yaani dari limejaa magunzi mpaka lina taka kuanguka
....hahahahahaaaa
 
Dah..mie nakumbuka jinsi tulivyoishi porini huku tukila mizizi na matundapori kwa miezi mitatu mimi na rafiki zangu wawili. Tulikuwa tunatafutwa kwa kuchoma moto malori mawili ya jeshi yaliojaa wanajeshi wakiwa na silaha zao 🙂
Nyie ni makomando aisee..au unatupa scenes za komando kipensi?
 
Hii nakumbuka sana,nilivyofika form one, siku nimeenda prepo washkaji wa form three wakaja bwenini kwetu wakapiga tranka langu kipepeo wakaiba vijisenti kidogo.

Nilivyorudi nikakasirika sana, nikafanYa uchunguzi nikawagundua. Nikavizia siku form three wameenda shambani nikaingia bwenini kwao nami nikafungua matranka yao hao washkaji wawili.

Nikakuta hamna cha kuiba, hivyo nikaamua tu Kunya na kukojoa humo then nikasepa...
Mh! wewe ni janga kabisa. yaaaaaaaaaa.......ni unafanya uchafuzi mkubwa hivyo kwenye masanduku ya wenzio. Wangekugundua 2 nadhani wao badala ya ku**** wangeharishia kwenye sanduku lako na kitanda.
 
form 1 mpaka form 4 nimesoma shule nne, na zote nilikuwa nahama siyo kwa kufail, bali ukorofi tuu, nakumbuka nilisoma Uchama nzega ikiwa shule yangu ya pili, kulikuwa na boga kubwa sana nyuma ya Labaratory, nafikiri lilikuwa kwa ajili ya experiment, kila siku tukawa tulapigia mikakati ya kuliiba maana lilikuwa sehemu ya wazi sana, siku ya kwanza tukaja na ndoo, lile boga likagoma kuingia kwenye ndoo, mara ya pili tukaja na begi la mgongoni (kipindi kile begi la volcano lilikuwa ndo bag kali la mgongoni) humo namo likagoma, safari iliyofata tukaenda na kisu cha jikoni tukalikata katikati then tukaenda kulichemsha usiku wa manane na ulila bweni zima.
kesho yake ikawa kesi, boga halionekani, tulichezea stick hatari
 
umenikumbusha kuna washkaji walichukua ugali uliobaki usiku wakauweka kwenye mfuko wa sembe wakauweka asubuhi yake wakapiga na uji...halafu ukiuita ugali wanakumaindi...wanataka uuite white bread
ha hahaha
 
Sie ilisomwa moja nakumbuka maneno haya

"""EWE MPENZI WANGU ULIEUMBWA KWA SURA NA MFANO WA BIKIRA MARIA NIBUSU NA MIMI NIKUBUSU MAANA BUSU LAKO LANOGA KULIKO MZINGA WA NYUKI... ""

Sisahau mpaka leo hapo tulikua fom 1..... Ha ha ha ha spati picha voko za kijana yule kwa sasa
nimecheka mpaka basi
 
Back
Top Bottom