Makongo;
Kuna mtu alikuwa mtata sana anaitwa Afande Miraji(RIP) alikuwaga NA kawaida ya kupita kitaan kwetu saa 1 usku kila akiwa anatoka job kwake Makongo sec school ...sasa mzee wangu NA mm mili ilikuwa inaendana kdgo alikuwaga naye mjeda NA alikuwa anapenda sana kukaa nje mida hiyo usiku....siku Miraji alipopita nikiwa nimekaa mm pale nje mzee hakuwepo jamaa akatoa shikamo kama kawaida yake NA mm nikaitikia marahaba kumbe akaishtukia ile saut sio ya mshua akaenda zake kimya kimya ...kesho yake jamaa alikuja nichomoa darasan akanipeleka ofisin kwake niliporud joints zote mwilin hazifany kaz maana push ups,kichura chura ndio zilikuwa adhabu zake wiki nzima najisaidia aja kubwa nimesimama maana kuchuchumaa siwez ,...Bas toka siku hiyo nikawa sikae nje ya home kwetu ikifika SAA 1 usku
Kigonsera Sec School
1.Kulikuwaga kuna kajamaa kamoja kutoka Mbeya kalikuwa kanawaingilia wanaume wenzake kishirikina,Aliweza kuwaingilia wanafunzi wengi sana(Mm hakuwahi nigusa hata chembe)...Sasa siku akaingia anga za dogo mmoja (nahisi naye alikuwa ninja ) kutoka Rukwa ndipo alipodakwa kichapo alichopata nusu wamuue ikabid baadae wamuhamishe shule ndio ikawa salama yake
2. kuna Teacher mmoja Yank flan hiv alikuwa anatoka Songea mjin anakuja Mbnga(kigonsera) kutupigia practical za chemistry NA Bios NA kesho yake anageuza, Yy alikuwa rafik wa wanafunzi kwahiyo akawa analala kwenye madom ya wanafunz ...Kulikuwa kuna Teacher mmoja kila ikifa SAA 12 kasoro anapita Dom hadi Dom kuamsha wale ambao hawajasmka, NA kawaida yake akiingia tu akakukuta umelala anatandika bakora hapo hapo juu bila hata kukustua ww unakuja shtukia kitu paaah! ...Sasa siku akaingia room ambapo teacher alikuwa kalala NA wanafunz ndan ahahahahaha jamaa alimtandika fimbo moja ya nguvu yule mwalimu akiwa usingzin ,teacher ikabid apige kelele "mm mwalimu wa practicaaaaaal sio mwanafunz"
Pugu Sec School.
1.Baada ya kukimbia Kigonsera kutokana NA barid Kali nikajiunga Pugu.....Huku identity ya kwamba huyu ni mwanafunz wa Pugu ilikuwa ni kujikuna sehem za siri kwa7bu ya fungus kutokana NA shida ya maji MTU alikuwa anaoga ikifika ijumaa au jmos akiwa anadrop kwenda town maji pale yalikuwa ya pond...
2. Tulikuwa NA kawaida ya kuwa NA magroup ya wanafunz wasiozid 10 katika kugawana chakula,wali au ugali NA mboga zinajazwa kwenye sufuria mbili kubwa kisha anateuliwa mmoja kuwagawia member wa group ambao sahan zao zimetandazwa chini....sasa siku nikachelewa dining bwana alafu ilikuwa siku ya wali nyama(ilikuwa kama sikukuu Siku hii maana attendance inakukuwa nzur hata wale watoro waliokubuhu wanakuwepo) ...Baada ya kukosa kwenye group letu nikaona kuna group linatafuta chimbo ili waanze kugawana menu ikabidi niunge walipotandaza sahaan chin NA mm nikaweka yangu katkat ....Bas yule group leader(jamaa nahis alikuwa NA roho ya Nduli) maana alisambaza chakula Sahan zote tena zimejaa mpaka zinamwagika nyama tatu tatu huku sahan yangu ikiwa nyeupe haina kitu, nilipomuuliza kwann imekuwa hivyo jamaa akanijibu " group letu mzamiaji hana nafasi" daah ikabid niwe mpole tu
3. Tulikuwa tunashindana kupiga msuli PCB darasa letu ...msuli unaanza SAA 4 usiku mpaka pale mshindi anapopatikana ....Masharti ya shindano member wote mnachangishana mia 2 NA pesa inayopatikana inanunuliwa mikate inawekwa mezani mshind anapewa, ni mikate sababu Pugu chai ilikuwa inachemshwa ila vitafunwa unajininulia mwenyewe......,Sharti la pili ukisinzia tu umejitoa unapewa red card NA msimamiz ambaye naye alikuwa sio mshindani anaruhusiwa kusinzia NA walikuwa wanapeana shift saa 4,6 & 8.....Bas kuna jamaa akikuwa anaitwa Mwisho Wa Lami alichukua mikate for 4 consecutive days maana alikuwa anafika mpaka SAA 11 asbhi peke yake cha ajabu kwenye parade 1 lazima umkute wakat sisi wengine tulikuwa tukifanikiwa kufika sana bas SAA 8 au 9 ndio pumzi zinaishia(usingizi) inabid ukalale tu japo mikate unaitaman NA kuamka kwake ujue ni SAA 4 mda wa chai....Headmaster alimpatiaga zawadi huyu jamaa baada ya kuzisikia habar zake.