Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

kuna mtu alifoji stam barua ikarudi ikasomwa assemble na headmaster alikuwa ameandika kwa demu wake ahahaaa eti nakupenda kama wali mchuzi
Sie ilisomwa moja nakumbuka maneno haya

"""EWE MPENZI WANGU ULIEUMBWA KWA SURA NA MFANO WA BIKIRA MARIA NIBUSU NA MIMI NIKUBUSU MAANA BUSU LAKO LANOGA KULIKO MZINGA WA NYUKI... ""

Sisahau mpaka leo hapo tulikua fom 1..... Ha ha ha ha spati picha voko za kijana yule kwa sasa
 
Daah maisha ya boarding raha sana kundi letu tulikuwa wahudhuriaji wazuri sana wa Matanga,harusi,na misiba na kufanya kazi zote ila target yetu ikiwa ubwabwa.
Disko vumbi na zile za usiku tulikuwa hatukosi.
Kila Ijumaa chumbani kwetu kulikuwa na mashindano ya Mieleka yanatandikwa magodoro chini zinapigwa hapo na mtu akitandikwa pakauma sana jua mchezo unageuka kuwa kweli wa kuja kuamua kaka mkuu au patron.
Ukiwa mwizi ukikamatwa kuna mawili uchoropoke utokomee usirudi au wazazi wako wapelekewe ripoti kuwa mwanenu yupo ICU
Kuna Mbabe huyo ye alikuwa anawatoza hela wadogo kwa kuwakusanya chumba kimoja kisha anaweka kapu katikati anawambia waimbe ule wimbo unaotumika makanisani kipindi cha kutoa sadaka unaimbwa hivi"toa ndugu toa ulichonacho...." ukiweka hela kubwa hakupi chenji hata ukiomba anakwambia kwani kanisani huwa unadai chenji.
Siku ya kula wali ndo watu tulikuwa tunaoga na mtu akiwa msafi ujue ana demu.
Bila kumsahau jamaa yangu mmoja ye alikuwa addicted na punyeto mpaka alipinda mgongo mana alikuwa mrefu akitaka kupiga lazima ainame kidogo.
Nina mengi ila kwa leo inatosha....boarding raha asee tena za mixer mana hata mwanao hawezi kuwa mzembemzembe wala punga..
 
Hii nakumbuka sana,nilivyofika form one, siku nimeenda prepo washkaji wa form three wakaja bwenini kwetu wakapiga tranka langu kipepeo wakaiba vijisenti kidogo.

Nilivyorudi nikakasirika sana, nikafanYa uchunguzi nikawagundua. Nikavizia siku form three wameenda shambani nikaingia bwenini kwao nami nikafungua matranka yao hao washkaji wawili.

Nikakuta hamna cha kuiba, hivyo nikaamua tu Kunya na kukojoa humo then nikasepa...
form one ulitoa wapi huu ujasiri
 
Hii nakumbuka sana,nilivyofika form one, siku nimeenda prepo washkaji wa form three wakaja bwenini kwetu wakapiga tranka langu kipepeo wakaiba vijisenti kidogo.

Nilivyorudi nikakasirika sana, nikafanYa uchunguzi nikawagundua. Nikavizia siku form three wameenda shambani nikaingia bwenini kwao nami nikafungua matranka yao hao washkaji wawili.

Nikakuta hamna cha kuiba, hivyo nikaamua tu Kunya na kukojoa humo then nikasepa...
duuuuuh umetisha khaa
 
Form one au New comer Ukiwa mzuri mzuri lazima usagwe tu na unaolewa kabisaaa. Uji wa bila sukari, kuvizia wanakijiji wakitoka shambani tunawaomba viazi vitamu au mahindi pia kutoroka kwenda sokoni siku za gulio na mnada pia kuchukua magodoro ya form one kuyapeleka chimbo.
 
Leo nimeona sio vibaya kila mtu akashiriki kusimulia matukio ambayo unayakumbuka ulipokua boarding school, either ya kusikitisha au kufurahisha.

Kwa uchache haya ni ya kwangu.

1.Tabia za kutokupenda kuoga: Kutokana na hali ya hewa kuwa baridi sana pale shuleni kwetu, wengi wa wanafunzi walikua wanapiga , " Passport" au " Kogo",kuosha sehemu chache tu za mwili, bila kuoga kabisa. Kuna mwanafunzi mwenzetu huyu yeye alikua na uwezo wa kutokuoga semester nzima. Yeye alikua ananawa uso tu na kwenda parade. Baada ya wanabweni wenzake kuona tabia yake. Kikakaa kikao kisicho rasmi ambacho maamuzi yake ilikua lazima jamaa aoge. Kwa pamoja wakamkamata mhusika na kumwogesha.

2. Tabia za kupigana makofi wakati wa kulala: Kulikua na tabia ya kila mwanafunzi mgeni kupata ukaribisho kwa kupigwa kofi usiku na kupakwa colgate mdomoni usiku wa kwanza anapoingia bording. Wanachumba wote kwa pamoja humtegea mgeni na kusubiri alale. Halafu taa huzimwa zote bweni zima. Mhusika hulishwa colgate akiwa amelala na kupigwa kofi la ukaribisho.

3. Utoro kwenda kwenye maulidi na harusi: Jamii ya watu walioizunguka shule wengi walikua wa dini ya kiislamu, hivyo kulikua na sherehe nyingi za maulidi, hivyo pale kunapotokea maulidi basi vijana usiku hutoroka na kurudi na mifuko na plastiki yenye pilau. Vile vile kila kunapotokea harusi maeneo ya jirani na shule basi usiku wa sherehe husika watu huzamia harusini, kubadilisha menyu.

Kwa uchache yangu ni hayo tu, karibuni nanyi mlete ya kwenu.
Makongo;

Kuna mtu alikuwa mtata sana anaitwa Afande Miraji(RIP) alikuwaga NA kawaida ya kupita kitaan kwetu saa 1 usku kila akiwa anatoka job kwake Makongo sec school ...sasa mzee wangu NA mm mili ilikuwa inaendana kdgo alikuwaga naye mjeda NA alikuwa anapenda sana kukaa nje mida hiyo usiku....siku Miraji alipopita nikiwa nimekaa mm pale nje mzee hakuwepo jamaa akatoa shikamo kama kawaida yake NA mm nikaitikia marahaba kumbe akaishtukia ile saut sio ya mshua akaenda zake kimya kimya ...kesho yake jamaa alikuja nichomoa darasan akanipeleka ofisin kwake niliporud joints zote mwilin hazifany kaz maana push ups,kichura chura ndio zilikuwa adhabu zake wiki nzima najisaidia aja kubwa nimesimama maana kuchuchumaa siwez ,...Bas toka siku hiyo nikawa sikae nje ya home kwetu ikifika SAA 1 usku

Kigonsera Sec School

1.Kulikuwaga kuna kajamaa kamoja kutoka Mbeya kalikuwa kanawaingilia wanaume wenzake kishirikina,Aliweza kuwaingilia wanafunzi wengi sana(Mm hakuwahi nigusa hata chembe)...Sasa siku akaingia anga za dogo mmoja (nahisi naye alikuwa ninja ) kutoka Rukwa ndipo alipodakwa kichapo alichopata nusu wamuue ikabid baadae wamuhamishe shule ndio ikawa salama yake

2. kuna Teacher mmoja Yank flan hiv alikuwa anatoka Songea mjin anakuja Mbnga(kigonsera) kutupigia practical za chemistry NA Bios NA kesho yake anageuza, Yy alikuwa rafik wa wanafunzi kwahiyo akawa analala kwenye madom ya wanafunz ...Kulikuwa kuna Teacher mmoja kila ikifa SAA 12 kasoro anapita Dom hadi Dom kuamsha wale ambao hawajasmka, NA kawaida yake akiingia tu akakukuta umelala anatandika bakora hapo hapo juu bila hata kukustua ww unakuja shtukia kitu paaah! ...Sasa siku akaingia room ambapo teacher alikuwa kalala NA wanafunz ndan ahahahahaha jamaa alimtandika fimbo moja ya nguvu yule mwalimu akiwa usingzin ,teacher ikabid apige kelele "mm mwalimu wa practicaaaaaal sio mwanafunz"

Pugu Sec School.

1.Baada ya kukimbia Kigonsera kutokana NA barid Kali nikajiunga Pugu.....Huku identity ya kwamba huyu ni mwanafunz wa Pugu ilikuwa ni kujikuna sehem za siri kwa7bu ya fungus kutokana NA shida ya maji MTU alikuwa anaoga ikifika ijumaa au jmos akiwa anadrop kwenda town maji pale yalikuwa ya pond...

2. Tulikuwa NA kawaida ya kuwa NA magroup ya wanafunz wasiozid 10 katika kugawana chakula,wali au ugali NA mboga zinajazwa kwenye sufuria mbili kubwa kisha anateuliwa mmoja kuwagawia members wa group ambao sahan zao zimetandazwa chini....sasa siku nikachelewa dining bwana alafu ilikuwa siku ya wali nyama(ilikuwa kama sikukuu Siku hii maana attendance inakukuwa nzur hata wale watoro waliokubuhu wanakuwepo) ...Baada ya kukosa kwenye group letu nikaona kuna group linatafuta chimbo ili waanze kugawana menu ikabidi niunge walipotandaza sahaan chin NA mm nikaweka yangu katkat ....Bas yule group leader(jamaa nahis alikuwa NA roho ya Nduli) maana alisambaza chakula Sahan zote tena zimejaa mpaka zinamwagika nyama tatu tatu huku sahan yangu ikiwa nyeupe haina kitu, nilipomuuliza kwann imekuwa hivyo jamaa akanijibu " group letu mzamiaji hana nafasi" daah ikabid niwe mpole tu

3. Tulikuwa tunashindana kupiga msuli PCB darasa letu ...msuli unaanza SAA 4 usiku mpaka pale mshindi anapopatikana ....Masharti ya shindano members wote mnachangishana mia 2 NA pesa inayopatikana inanunuliwa mikate inawekwa mezani mshind anapewa, ni mikate sababu Pugu chai ilikuwa inachemshwa ila vitafunwa unajininulia mwenyewe......,Sharti la pili ukisinzia tu umejitoa unapewa red card NA msimamiz ambaye naye alikuwa sio mshindani anaruhusiwa kusinzia NA walikuwa wanapeana shift saa 4,6 & 8.....Bas kuna jamaa akikuwa anaitwa Mwisho Wa Lami alichukua mikate for 4 consecutive days maana alikuwa anafika mpaka SAA 11 asbhi peke yake cha ajabu kwenye parade 1 lazima umkute wakat sisi wengine tulikuwa tukifanikiwa kufika sana bas SAA 8 au 9 ndio pumzi zinaishia(usingizi) inabid ukalale tu japo mikate unaitaman NA kuamka kwake ujue ni SAA 4 mda wa chai....Headmaster alimpatiaga zawadi huyu jamaa baada ya kuzisikia habar zake.


Leo nimeona sio vibaya kila mtu akashiriki kusimulia matukio ambayo unayakumbuka ulipokua boarding school, either ya kusikitisha au kufurahisha.

Kwa uchache haya ni ya kwangu.

1.Tabia za kutokupenda kuoga: Kutokana na hali ya hewa kuwa baridi sana pale shuleni kwetu, wengi wa wanafunzi walikua wanapiga , " Passport" au " Kogo",kuosha sehemu chache tu za mwili, bila kuoga kabisa. Kuna mwanafunzi mwenzetu huyu yeye alikua na uwezo wa kutokuoga semester nzima. Yeye alikua ananawa uso tu na kwenda parade. Baada ya wanabweni wenzake kuona tabia yake. Kikakaa kikao kisicho rasmi ambacho maamuzi yake ilikua lazima jamaa aoge. Kwa pamoja wakamkamata mhusika na kumwogesha.

2. Tabia za kupigana makofi wakati wa kulala: Kulikua na tabia ya kila mwanafunzi mgeni kupata ukaribisho kwa kupigwa kofi usiku na kupakwa colgate mdomoni usiku wa kwanza anapoingia bording. Wanachumba wote kwa pamoja humtegea mgeni na kusubiri alale. Halafu taa huzimwa zote bweni zima. Mhusika hulishwa colgate akiwa amelala na kupigwa kofi la ukaribisho.

3. Utoro kwenda kwenye maulidi na harusi: Jamii ya watu walioizunguka shule wengi walikua wa dini ya kiislamu, hivyo kulikua na sherehe nyingi za maulidi, hivyo pale kunapotokea maulidi basi vijana usiku hutoroka na kurudi na mifuko na plastiki yenye pilau. Vile vile kila kunapotokea harusi maeneo ya jirani na shule basi usiku wa sherehe husika watu huzamia harusini, kubadilisha menyu.

Kwa uchache yangu ni hayo tu, karibuni nanyi mlete ya kwenu.
 
Mwezi dume unatafuta hata kipande cha sabun shule nzima unakosa.
Ukiingia chooni unavua nguo zote kwanza kisa harufu kali vyooni
Kutoroka na madishi siku ya nyama na wali na kutokomea nayo porini.
Kuna jamaa alikua kiranja wa msosi siku ya nyama anachukua nyama kwenye kindoo na kuuza kinyango shs 200
Ukienda na mkate shuleni wewe ni mfalme..
 
Mwezi dume unatafuta hata kipande cha sabun shule nzima unakosa.
Ukiingia chooni unavua nguo zote kwanza kisa harufu kali vyooni
Kutoroka na madishi siku ya nyama na wali na kutokomea nayo porini.
Kuna jamaa alikua kiranja wa msosi siku ya nyama anachukua nyama kwenye kindoo na kuuza kinyango shs 200
Ukienda na mkate shuleni wewe ni mfalme..

dah hiyo ya kwenda chooni umevua nguo zote nahisi shule nying za serikal zinapitia
 
Hii nakumbuka sana,nilivyofika form one, siku nimeenda prepo washkaji wa form three wakaja bwenini kwetu wakapiga tranka langu kipepeo wakaiba vijisenti kidogo.

Nilivyorudi nikakasirika sana, nikafanYa uchunguzi nikawagundua. Nikavizia siku form three wameenda shambani nikaingia bwenini kwao nami nikafungua matranka yao hao washkaji wawili.

Nikakuta hamna cha kuiba, hivyo nikaamua tu Kunya na kukojoa humo then nikasepa...
Heheheee ujamaa upo boarding
 
Back
Top Bottom