FC Barcelona (Barça or Blaugrana) | Special Thread

FC Barcelona (Barça or Blaugrana) | Special Thread

Unahitaji kuwa na akili za babu Ferguson kuweza ku-manage aging stars na kuhakikisha kwamba wanapunguziwa majukumu kadri umri unavyosogea.

Otherwise unajikuta uko kwenye wakati mgumu kama huu.

Barca haina sauti mbele ya huyu mwamba, ni kama imewekwa mateka.

Xavi na Iniesta muda ulipofika busara kubwa ilitumika na wao wakapisha, hawakuwa wabinafsi na waliweka maslahi ya timu mbele.

Messi ni mbinafsi.
Hivi unajua Messi ni zaidi ya mchezaji wa Barça?

Hivi unajua La Liga nzima kwa sasa inabebwa na Messi?

Hivi unajua dunia nzima Inamwangalia Messi?

Yaani upuunzi wa Uongozi kufanya sajili za Kibuuzi mzigo umwangukie Messi
Ubinafsi wa Messi upo wapi? Kuendelea kubaki kwenye team ndo ubinafsi?

Messi anayeongoza kwa Assists unawezaje sema Mbinafsi...

Pamoja na ubovu wa Barça Messi bado yupo kwenye Performance nzuri, unawezaje sema yeye ndo sababu?

Ninadhani tuendelee kuchambua mipira ya bongo ya simba na Yanga..
 
Mnaosema Messi asiondoke mnatafakar kwa mapana? Messi atakaa hapo milele?

Leo hii twaishuhudia Madrid ilivyo baada ya kuondoka Ronaldo, tuachane na Ronaldo, turudi ktk Barca hii hii.

Kwanini Iniesta na Xavi mpaka leo nafasi yao inaonekana kuwa haijazibwa?

1. Tuliwaacha wacheze kwa miaka mingi, wakiwa ktk age ya 32 wangeweza kuuzwa.

2. Hatukuamini vijana ambao tulitarajia wangerithi nafasi zao au niseme hatukuwapa nafasi.

Leo hii timu kila ikishambulia ni lazima imtazame Messi, hii inafanya kila mchezaji ndani ya Barca asiwe na uhuru zaidi wa yeye kufanya atakacho ila ni lazima atazame nafasi ya Messi.
Aliyesema Messi kashuka kiwango nani?

Mchezaji anayeongoza Ufungaji kwenye League unawezaje sema aondoke?

Messi anaongoza kwa Assists unawezaje mnalaumu?

Unataka Messi akawe baki? Kiungo hadi goalie?

Tatizo lipo wazi board ya Barça iachie ngazi
 
Hivi unajua Messi ni zaidi ya mchezaji wa Barça?

Hivi unajua La Liga nzima kwa sasa inabebwa na Messi?

Hivi unajua dunia nzima Inamwangalia Messi?

Yaani upuunzi wa Uongozi kufanya sajili za Kibuuzi mzigo umwangukie Messi
Ubinafsi wa Messi upo wapi? Kuendelea kubaki kwenye team ndo ubinafsi?

Messi anayeongoza kwa Assists unawezaje sema Mbinafsi...

Pamoja na ubovu wa Barça Messi bado yupo kwenye Performance nzuri, unawezaje sema yeye ndo sababu?

Ninadhani tuendelee kuchambua mipira ya bongo ya simba na Yanga..

Father time is unbeatable bro.

Nakubaliana na wewe, tuendelee kujadili mpira wa Simba na Yanga.
 
Aliyesema Messi kashuka kiwango nani?

Mchezaji anayeongoza Ufungaji kwenye League unawezaje sema aondoke?

Messi anaongoza kwa Assists unawezaje mnalaumu?

Unataka Messi akawe baki? Kiungo hadi goalie?

Tatizo lipo wazi board ya Barça iachie ngazi

Unaweza kuweka statistics za magoli ya Messi msimu kwa msimu toka 2008 mpaka sasa?
 
Tukiongelea zama hizi hapa duniani timu bora ya muda wote ni Barcelona mchezaji bora wa dunia ni Messi..na hili kila Mtu analijua
Sio mbaya tumepoteza na si ajabu ikatokea tusifanye vema kwenye uefa lakini hayo yote yatapelekea kutusukuma kurekebisha mapungufu ktk kikosi
watu bwana
 
Tukiongelea zama hizi hapa duniani timu bora ya muda wote ni Barcelona mchezaji bora wa dunia ni Messi..na hili kila Mtu analijua
Sio mbaya tumepoteza na si ajabu ikatokea tusifanye vema kwenye uefa lakini hayo yote yatapelekea kutusukuma kurekebisha mapungufu ktk kikosi
Acha Utani Weweeeee
 
Hivi unajua Messi ni zaidi ya mchezaji wa Barça?

Hivi unajua La Liga nzima kwa sasa inabebwa na Messi?

Hivi unajua dunia nzima Inamwangalia Messi?

Yaani upuunzi wa Uongozi kufanya sajili za Kibuuzi mzigo umwangukie Messi
Ubinafsi wa Messi upo wapi? Kuendelea kubaki kwenye team ndo ubinafsi?

Messi anayeongoza kwa Assists unawezaje sema Mbinafsi...

Pamoja na ubovu wa Barça Messi bado yupo kwenye Performance nzuri, unawezaje sema yeye ndo sababu?

Ninadhani tuendelee kuchambua mipira ya bongo ya simba na Yanga..
kwa ninavyomfahamu Don Clericuzio hawezi kuhoji kiwango cha mtakatifu messi kwa sababu anafahamu fika ya kwamba bado jamaa ana uwezo wa kucheza timu kubwa yeyote licha ya kwamba takwimu zake za kiufungaji zimeshuka sana msimu huu ila bado contributions yake kwenye sekta nyenginezo zimeendelea kuiweka kwenye ramani ya kiushindani klabu ya barcelona.

nadhani hoja yake ya kwanza ipo kwenye ishu ya umri alionao lionel messi pamoja na wachezaji wenzake ambao wamedumu pamoja kwa takribani miaka 10 ya mafanikio, mpaka mchana wa leo kikosi cha kwanza cha barcelona kinaundwa na Pique (33), Alba (31), Busquets (31), Rakitic (32), Vidal (33), Messi (33), Suárez (33) na muongezee Pjanic (30)

kabla ya corona pato la barcelona limekuwa likiongezeka mara kwa mara mpaka wamefikia hatua ya kushika nafasi ya kwanza kwa mujibu wa deloitte (barcelona wanahesabu pato la klabu mpaka kwa dili za mauzo ya wachezaji, pia barcelona inasemekana wanazalisha jezi zao wenyewe) lakini pia deni la barcelona limeendelea kuongezeka na hata cash reserves hairidhishi, yawezekana barcelona wanakusanya revenue kubwa sana lakini operating cost kwa upande wao imekuwa ikiongezekana na sababu kubwa ya kwanza ni wage bill structures inayokula asilimia kubwa sana ya net profit.

hao wachezaji wote saba niliokutajia wanavuta hela ndefu sana kwa mwaka wakiongozwa na huyo lionel messi ambaye inasemekana pale barcelona anakusanya €1.3m per week, Griezmann €850k per week, Suarez €450k per week, De Jong €300k per week, Busquets €300k per week, Coutinho, Rakitic, Pique, Dembele na Umtiti wanakusanya €250k per week each, Roberto €200k per week, Vidal €180k per week, Alba na Ter Stegen €165k per week na wote hao wana mkataba wa muda mrefu (vyanzo vya taarifa vinatofautiana hivyo basi naruhusu masahihisho)

Njia pekee ya kuondokana na tatizo hilo ni kubana matumizi kwa kufanya overhaul ya kuwaondoa wachezaji ambao upo uwezekano mkubwa wa kuzibwa nafasi zao kwa hali ya soko lilivyo kwa cheap price and salary au kupandisha wachezaji kutoka academy, kinyume chake barcelona watakuwa wanakaribisha hali ngumu ya kifedha ambayo imeshaanza kujionyesha (nakukumbusha kwa mujibu wa raisi wa barcelona msimu huu walichukua mkopo kwa dhumuni la kumsjaili griezmann)

Bartomeu says, as quoted by Samuel Marsden: "Paying Griezmann's €120 million release clause was a complex deal. Barcelona have had to take out a loan of €35m to pay the fee outright."

ukija kwenye sera yao ya usajili wa galacticos nayo pia imekuwa ni kituko kwa miaka hii ya karibuni, unalipaje paundi milioni 100 au zaidi kwa wachezaji watatu ambao huna uhakika wa kuja kufiti kwenye mfumo wa team yenu (dembele, griezmann na coutinho), zipo stori za chini ya kapeti zinadai ya kwamba hata team captain messi amekuwa na nguvu kwenye ishu ya usajili (huu unabaki kuwa ni uvumi uliokosa uthibitisho)
1595075679470.png
 
Messi akicheza kama suarez unahisi kwa akili ya kawaida hayo magoli yangefika?

Messi wasasa ni kama midfielder ni jambo la ajabu kulinganisha stats zake na zile za enzi za kulishwa na akina iniesta..

Tuache umamluki
Nazijua, zinaniambia Messi hana tena uwezo wa kuscore magoli mengi kama alivyokuwa anafanya zamani.

Na mpaka Messi ana retire, UEFA hatakaa aiguse tena.
 
Messi akicheza kama suarez unahisi kwa akili ya kawaida hayo magoli yangefika?

Messi wasasa ni kama midfielder ni jambo la ajabu kulinganisha stats zake na zile za enzi za kulishwa na akina iniesta..

Tuache umamluki

Kwa mtazamo wako, yuko productive sasa hivi anavyocheza kama midfield au zamani alipokuwa anacheza kama striker?
 
Kwa mtazamo wako, yuko productive sasa hivi anavyocheza kama midfield au zamani alipokuwa anacheza kama striker?
Atachezaje kama striker na hakuna creative mids!? Barca ingefika wapi...!!

Messi ni productive zaidi kuliko mchezaji yoyote laliga.. na alikua productive ktk kikosi cha nyuma..

Productivity imebadilika kutokana na role anazocheza katika vipindi vyote.. kwa mtazamo huo messi aachwe tu ametoa 100% yake kila siku
 
kwa ninavyomfahamu Don Clericuzio hawezi kuhoji kiwango cha mtakatifu messi kwa sababu anafahamu fika ya kwamba bado jamaa ana uwezo wa kucheza timu kubwa yeyote licha ya kwamba takwimu zake za kiufungaji zimeshuka sana msimu huu ila bado contributions yake kwenye sekta nyenginezo zimeendelea kuiweka kwenye ramani ya kiushindani klabu ya barcelona.

Umezungumzia kitu ambacho kuna siku nilitaka kukiandika humu ila nikaishia kusema Messi ni mbinafsi kwa Barca.

Swala la mshahara wa Messi; ni kweli jamaa ni Star wa timu, hakuna yeyote anayeweza kupinga umuhimu wa Messi pale Barca.

Swali linakuja kulinganisha umri, performance na mshahara. Alipokuwa kijana, say 22 to 29 years old, mchango wake kipindi hicho ulileta makombe La Liga, UEFA, Kombe la Mfalme, Kombe la Dunia kwa Vilabu etc. Kipindi hiki alilipwa shilingi ngapi kwa wiki?

Leo hii pamoja na umuhimu wake, yeye kuwa kiungo muhimu kwenye timu, mafanikio ya timu ni sawa na kipindi kile? Analipwa shilingi ngapi? Unaweza kulinganisha mshahara wake na mafanikio ya timu kwa sasa?

Kitu ambacho watu tunachanganya, ni kwamba we are talking about the former Messi/Barcelona vs this Messi/Barcelona. Standards walizoziweka vs wanachokifanya sasa hivi.

Kwa wale wafatiliaji wa NBA, hili liliwakuta LA Lakers kwenye misimu ya mwisho ya Legend Kobe Bryant, walijikuta wanamlipa mshahara mkubwa sana wakati production yake ilishaisha, na hivyo ikawa hata kupata wachezaji Star ikawa ngumu. Wamekaa muda bila kucheza Playoffs mpaka alivyo retire wakaanza rebuild.

Messi lazima aelewe nafasi yake kwa kuisaidia timu, not holding the team hostage.
 
Atachezaje kama striker na hakuna creative mids!? Barca ingefika wapi...!!

Messi ni productive zaidi kuliko mchezaji yoyote laliga.. na alikua productive ktk kikosi cha nyuma..

Productivity imebadilika kutokana na role anazocheza katika vipindi vyote.. kwa mtazamo huo messi aachwe tu ametoa 100% yake kila siku

Unapimaje productivity?

Mimi binafsi napima productivity kutokana na makombe timu inayopata, na pia kutokana na games muhimu timu inazoshinda.
 
Umezungumzia kitu ambacho kuna siku nilitaka kukiandika humu ila nikaishia kusema Messi ni mbinafsi kwa Barca.

Swala la mshahara wa Messi; ni kweli jamaa ni Star wa timu, hakuna yeyote anayeweza kupinga umuhimu wa Messi pale Barca.

Kitu ambacho watu tunachanganya, ni kwamba we are talking about the former Messi/Barcelona vs this Messi/Barcelona. Standards walizoziweka vs wanachokifanya sasa hivi.

Messi lazima aelewe nafasi yake kwa kuisaidia timu, not holding the team hostage.
teh teh teh
kwenye hii forum ya barcelona kuna muhuni fulani amekichafua vibaya sana kama wewe,
sijui hii makala ameitolea wapi
FC Barcelona Finances - Page 67
 
Nazijua, zinaniambia Messi hana tena uwezo wa kuscore magoli mengi kama alivyokuwa anafanya zamani.

Na mpaka Messi ana retire, UEFA hatakaa aiguse tena.
Messi sasa hivi hasimami pale centre lkn pamoja na kutokea nyuma bado anatikisa kwa ufungaji na assist
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom