Baada ya kukosa namba kikosi cha kwanza licha ya kununuliwa kwa bei mbaya, Jurgen Klopp amemuita Ousmane Dembele katika kikosi cha Liverpool.
Dembele alijiunga na Barcelona kwa Pauni95 milioni, lakini ameshindwa kuvaa viatu vya Neymar aliyetimkia Paris Saint Germain (PSG).
Klopp anamtaja mshambuliaji huyo wa zamani wa Borussia Dortmund ni mchezaji mwenye kiwango bora anayestahili kucheza Liverpool.
Dembele aliyepata maumivu ya misuli iliyomuweka nje uwanja muda mrefu, hajarejea katika kiwango chake.
Dembele mwenye miaka 20, ameshindwa kuendana na aina ya mfumo wa Barcelona tangu alipotua Now Camp katika usajili wa majira ya kiangazi.
Kocha huyo wa Liverpool anataka kumsajili Dembele kuboresha safu ya ushambuliaji.
“Dembele kwani yupo sokoni? Ndio ninamtaka,”alisema kocha huyo aliyewahi kuifundisha Dortmund.
Mchezaji huyo anakabiliwa na mazingira magumu Barcelona, baada ya kucheza mechi moja ya ligi kwa dakika zote licha ya kuanza katika michezo tisa akiwa amefunga bao moja.
Barcelona imeanza mkakati wa kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Antoine Griezmann majira ya kiangazi