Wakuu mfumo 4 4 2 na 4 3 3 kwa timu yetu upi unatoa matokeo mazuri,? kwa upande wangu huu mfumo wetu wa 4 3 3 aliouasisi Pep ndo mfumo bora kuwahi kutokea kwenye timu yetu ukilinganisha na huu wa sasa aliokuja nao Valverde, siudharau mfumo wa 4 4 2 maana hadi sasa umetufanya tusipoteze mchezo hata mmoja ila naona una mapungufu sana hasa upande wa ushambuliaji maana tunakuwa tunajilinda sana kuliko kushambulia kwa wale walioangalia mechi ya juzi dhidi ya Girona watakuwa mashahidi jinsi tulivyokuwa tunafanya mashambulizi mengi tulipoamua kuja na 4 3 3
Nina imani mchezo wa juzi dhidi ya Girona ulikuwa wa majaribio kwa ajili ya marudiano na Chelsea, kwa mfumo wa 4 4 2 chelsea watatusumbua sana maana hakuna mashambulizi na itawafanya wajiamini kuwa wanatuweza
Kama UEFA tutarudisha mfumo wa 4 3 3 basi kikombe tutakiweka kabatini