FC Barcelona (Barça or Blaugrana) | Special Thread

FC Barcelona (Barça or Blaugrana) | Special Thread

Kuna mtu huwa haniangushi hata siku moja. Live long mtu mfupi,mzee baba,fundi mwenyewe Lionel Messi. Viva Barcelona viva
Naomba nikuzawadie hii pic
Screenshot_2018-02-20-21-08-56.png
 
Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi jana usiku amefanikiwa kuiokoa klabu yake kutoka kwenye kipigo kwa kuisawazishia goli 1-1 dhidi ya mabingwa wa Uingereza Chelsea kwenye mchezo wa klabu bingwa barani Ulaya.

Goli hilo la kusawazisha la Messi limevunja rekodi mbovu ya mchezaji huyo ya kutofunga goli lolote dhidi ya Chelsea pindi timu hizo zinapokutana akiwa na timu yake kwa zaidi ya miaka 7.

Imemchukua mchezaji huyo dakika 730 na mechi 9 kufunga bao lake la kwanza katika michuano ya Klabu Bingwa Barani Ulaya (UEFA).

Messi ambaye amekuwa yuko katika kikosi kimoja na Andres Iniesta tangu aanze kuichezea Barcelona mpaka sasa, alikuwa hajawahi kuzigusa nyavu za Chelsea, hadi Jana usiku ilipomlazimu kutumia dakika 75 uwanjani kupata goli hilo.

Iniesta ndiye aliyemsaidia Messi kufunga bao hilo kwa pasi safi ya mwisho kunako dimba la Stamford Bridge.
Goli la Chelsea lilifungwa na Willian kunako dakika ya 62 kwa shuti zuri lililopita miguuni mwa mabeki wa Barcelona.

Kwa sare hiyo Barcelona imekuwa na faida ya goli moja la ugenini, kabla timu hizo hazijakutana tena katika mchezo wa marudiano utakaochezwa kwenye Uwanja wa Camp Nou, Jumatano ya March 14 2018.
 
Naomba niseme yafuatayo kutokana na Game ya jana

1. Sijawahi kushuhudia Chelsea wakicheza ktk attention kubwa kama mechi ya jana dhidi ya Barcelona.
Chelsea walijua kuwa uzembe wowote ule ungewagharimu, na ni kweli, uzembe wa beki ulipelekea Messi akafunga, Chelsea waliamini heri matokeo ya kufungwa 2-0 pasipo kufungwa na Messi kuliko matokeo ya 1-1 na 1 lenyewe kufungwa na Messi.

2. Barca tunapaswa kusajili winga ya kushoto, tunapaswa kushoto kuwa na mtu makini wa kazi kama Hazard na sio wauza sura kama Neymar. Hazard jana kacheza mpira mmoja mzuri sana, alitulia na kupiga chenga na kutumia nafasi vizuri.

3. Goal la Chelsea kila mmoja wetu alivyoona Willian kapokea mpira alijua tu kuwa lile ni goli, Willians alionekana mara mbili akiachwa huru anapiga mipira kuelekea golini na zote kagongesha mwamba, mara anapokea mpira tena bila kukabwa anaachwa apige mpka anafunga, huu ulikuwa ni uzembe wa hali ya juu.

Solution Wakuu tupate Winga ya kushoto na kiungo mchezashi mmoja wa timu wa kueleweka, hawa akina Paulinho bado sana, walau Rakitic anajitahidi sana.
 
Naomba niseme yafuatayo kutokana na Game ya jana

1. Sijawahi kushuhudia Chelsea wakicheza ktk attention kubwa kama mechi ya jana dhidi ya Barcelona.
Chelsea walijua kuwa uzembe wowote ule ungewagharimu, na ni kweli, uzembe wa beki ulipelekea Messi akafunga, Chelsea waliamini heri matokeo ya kufungwa 2-0 pasipo kufungwa na Messi kuliko matokeo ya 1-1 na 1 lenyewe kufungwa na Messi.

2. Barca tunapaswa kusajili winga ya kushoto, tunapaswa kushoto kuwa na mtu makini wa kazi kama Hazard na sio wauza sura kama Neymar. Hazard jana kacheza mpira mmoja mzuri sana, alitulia na kupiga chenga na kutumia nafasi vizuri.

3. Goal la Chelsea kila mmoja wetu alivyoona Willian kapokea mpira alijua tu kuwa lile ni goli, Willians alionekana mara mbili akiachwa huru anapiga mipira kuelekea golini na zote kagongesha mwamba, mara anapokea mpira tena bila kukabwa anaachwa apige mpka anafunga, huu ulikuwa ni uzembe wa hali ya juu.

Solution Wakuu tupate Winga ya kushoto na kiungo mchezashi mmoja wa timu wa kueleweka, hawa akina Paulinho bado sana, walau Rakitic anajitahidi sana.
Umeongea ukweli mtupu sana mkuu, nashangaa sana Paulinho kwa uwezo wake kua first eleven ya Barcelona eti sub zetu ni Vidal na Gomez doh yan tuna masihara hatuwezi kua na timu yenye competition tukimtegemea mchezaji mmoja tu Messi. Jana nafasi ya Dembele ilikua wazi kabisa kuanza kucheza, ukiniambia hapana naomba niambie hivi unaweza mfananisha Vidal na Dembele kweli? Mie kwangu Dembele ni mchezaji nayemkubali sana na sioni wa kumweka benchi katika nafasi anayocheza katika timu yetu.
Katika Raktic mkuu naomba nipingane na wewe kidogo, katika match ya jana kiukweli Rakitic kaupiga mwingi mno katikati pale kama uliona Sergio alikua kama kapanda juu fulani hivi sababu ya shughuli aliofanya jana Raktic mana alikua anamsaidia Sergio pale kati.
 
Umeongea ukweli mtupu sana mkuu, nashangaa sana Paulinho kwa uwezo wake kua first eleven ya Barcelona eti sub zetu ni Vidal na Gomez doh yan tuna masihara hatuwezi kua na timu yenye competition tukimtegemea mchezaji mmoja tu Messi. Jana nafasi ya Dembele ilikua wazi kabisa kuanza kucheza, ukiniambia hapana naomba niambie hivi unaweza mfananisha Vidal na Dembele kweli? Mie kwangu Dembele ni mchezaji nayemkubali sana na sioni wa kumweka benchi katika nafasi anayocheza katika timu yetu.
Katika Raktic mkuu naomba nipingane na wewe kidogo, katika match ya jana kiukweli Rakitic kaupiga mwingi mno katikati pale kama uliona Sergio alikua kama kapanda juu fulani hivi sababu ya shughuli aliofanya jana Raktic mana alikua anamsaidia Sergio pale kati.
Nadhan inshu ya fitness na ukubwa wa mechi ndo ilikua sababu kubwa ya Dembele kua nje
 
Umeongea ukweli mtupu sana mkuu, nashangaa sana Paulinho kwa uwezo wake kua first eleven ya Barcelona eti sub zetu ni Vidal na Gomez doh yan tuna masihara hatuwezi kua na timu yenye competition tukimtegemea mchezaji mmoja tu Messi. Jana nafasi ya Dembele ilikua wazi kabisa kuanza kucheza, ukiniambia hapana naomba niambie hivi unaweza mfananisha Vidal na Dembele kweli? Mie kwangu Dembele ni mchezaji nayemkubali sana na sioni wa kumweka benchi katika nafasi anayocheza katika timu yetu.
Katika Raktic mkuu naomba nipingane na wewe kidogo, katika match ya jana kiukweli Rakitic kaupiga mwingi mno katikati pale kama uliona Sergio alikua kama kapanda juu fulani hivi sababu ya shughuli aliofanya jana Raktic mana alikua anamsaidia Sergio pale kati.
Mkuu, mm nimesema kwa Paulinho bado sana ila walau Rakitic anajitahidi. Rakitic ni mzuri ila kwa kuichezesha vilivyo bado aiseee.
 
Sergio jana kacheza offensive role ila jamaa apunguze kuchapa maana anapiga mno kiatu asije aka miss next match kama last years alivyo miss game ya juventus first leg hadi kukapigwa kizembe
Bila kupiga viatu ile mechi tungepoteza!

Sergio ni mmoja kati ya wachezaji wachache sana wanaocheza rafu za muhimu sana zenye kuokoa timu.

Unafikiri yule willian bila kupigwa viatu angetulia?

Anyway, kumkosa Sergio kwenye mechi zijazo za UEFA kunaweza kua sababu ya sisi kuanguka.

Let's pray that he doesn't mess it up!
 
Bila kupiga viatu ile mechi tungepoteza!

Sergio ni mmoja kati ya wachezaji wachache sana wanaocheza rafu za muhimu sana zenye kuokoa timu.

Unafikiri yule willian bila kupigwa viatu angetulia?

Anyway, kumkosa Sergio kwenye mechi zijazo za UEFA kunaweza kua sababu ya sisi kuanguka.

Let's pray that he doesn't mess it up!
Dembele akiwepo haitakuwa shida. ila mi napenda kwenye Right flank tungekuwa na RB ya semedo na RCM ya Roberto. ingefanya sana kazi naona kama tungeifanyia kazi kwenye ligi. lakini naona wanamlazimisha Paulinho acheze na kuvuruga mambo. ingekuwa amri yangu Paulinho angekuwa anaingia kuanzia dk ya 70 kwenda juu.
 
Naomba niseme yafuatayo kutokana na Game ya jana

1. Sijawahi kushuhudia Chelsea wakicheza ktk attention kubwa kama mechi ya jana dhidi ya Barcelona.
Chelsea walijua kuwa uzembe wowote ule ungewagharimu, na ni kweli, uzembe wa beki ulipelekea Messi akafunga, Chelsea waliamini heri matokeo ya kufungwa 2-0 pasipo kufungwa na Messi kuliko matokeo ya 1-1 na 1 lenyewe kufungwa na Messi.

2. Barca tunapaswa kusajili winga ya kushoto, tunapaswa kushoto kuwa na mtu makini wa kazi kama Hazard na sio wauza sura kama Neymar. Hazard jana kacheza mpira mmoja mzuri sana, alitulia na kupiga chenga na kutumia nafasi vizuri.

3. Goal la Chelsea kila mmoja wetu alivyoona Willian kapokea mpira alijua tu kuwa lile ni goli, Willians alionekana mara mbili akiachwa huru anapiga mipira kuelekea golini na zote kagongesha mwamba, mara anapokea mpira tena bila kukabwa anaachwa apige mpka anafunga, huu ulikuwa ni uzembe wa hali ya juu.

Solution Wakuu tupate Winga ya kushoto na kiungo mchezashi mmoja wa timu wa kueleweka, hawa akina Paulinho bado sana, walau Rakitic anajitahidi sana.
Huwa tunasema humu
Unamuachaje digne, dennis
Alaf leo hii yan sub ya barca n vidal,gomez
Kocha anafanya sub moja tu tena dk ya 88 cjui ile
 
Dembele akiwepo haitakuwa shida. ila mi napenda kwenye Right flank tungekuwa na RB ya semedo na RCM ya Roberto. ingefanya sana kazi naona kama tungeifanyia kazi kwenye ligi. lakini naona wanamlazimisha Paulinho acheze na kuvuruga mambo. ingekuwa amri yangu Paulinho angekuwa anaingia kuanzia dk ya 70 kwenda juu.
Sure!

Roberto ana impact kubwa sana kwenye attacking wakati huu akitokea right back. Sasa nawaza tukimsogeza kati kati akapunguziwa defensive roles itakuaje!

Tena nyuma yake akiwepo Semedo itakua balaa zaidi. Kati ya paulinho na rakitic anatakiwa kuanza mmoja wao.

Sergi Roberto bado hatumtumii ipasavyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom