DSN
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 2,837
- 1,688
Regia Mtema Kwa Baba na Mama yake wamepoteza mtoto,kwa dada na kaka zake wamepoteza Dada kwa wanafamilia wamepoteza ndugu yao, kwa marafiki zake wamepoteza rafiki kipenzi,kwa chama chake Chadema wamepoteza Mwanachama na Kiongozi wao, kwa wanasiasa wenzie wamepoteza mshirika, kwa Jamii Forum [JF] wamepoteza mpiganaji na kwa Watanzania wamepoteza binti wa Nchi.
Tukipima siku za maisha yetu hapa dunia ni chache sana kwa kuishi, lakini ni nyingi sana kwa binadamu mwenye kumjua Mungu kwa kuwa Mungu ndiye mpangaji wa maisha yetu hivyo ulefu au ufupi ni kudra zake Mungu.Regia ameondoka lakini kaacha jina na jina hilo tafsiri yake inaonekana kwenye michango yetu ya maombolezo yetu humu ndani ya Jamii Forum, kwa kuwa Mungu anasema usitumaini akili zako bali mtumaini yeye Mungu kwa kuwa ndiye anayejua sababu ya uwepo wetu sisi wanadamu hapa duniani.
Mungu alisema anamuumba Mwanadamu kwa mfano wake,hivyo yaliyosemwa na sisi wote kama Wanajamii forum,Viongozi, Wanandugu na Wananchi wote juu ya Mtoto, Dada, Ndugu, Mwanasiasa, Kiongozi, Rafiki, Askari Mpiganaji huyu ni kielelezo tosha cha Mungu kuongea nasi jinsi gani Mungu alikusudia kuwapa Baba na Mama yake Regia mtoto mwema na ambae kwetu Watanzania alikuwa Mwanasiasa na Kiongozi aliyetutumikia kwa muda mfupi lakini, kwa sauti yenye mwangi mkubwa sana ambayo ilisambaa kwenye nyika na kufikisha ujumbe popote pale ilipostahiki.
Regia kaacha jina lake kwenye vinywa vyetu kwa kuwa katimiza kazi aliyotumwa na Mungu kwetu,ndio maana wanafalsa [Philosophers] wanasema kwa Wanasiasa na Viongozi wazuri duniani ubora na uzuri wa uongozi wao si kuacha mali kwa walithi wao,bali kuacha jina ambalo kila mtu akilisikia na kukumbuka anapata mwamko wa kufuata mazuri ambayo mwanasiasa au kiongozi huyo aliyapigania na kusimamia wakati wa wote wa uhai wake hapa duniani.Ndio maana kwa sisi vijana wa dotcom ambao hatukupata kuushuhudia utawala wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lakini wanadotcom hao wa sasa wanamjua na kumfuata nyayo zake kuliko wale Mwalimu aliowatumika na kuwafundishawakati wote wa maisha yake hapa duniani.
Hakika napata picha ya kibinadamu lakini ambayonatumani nawe ndiyo unayoijenga.Mungu alipomuita kiumbe wake Regia, wakati anaitikia wito wake kufika mbinguni Mungu nae ananena na mmoja wa makarani wake kwa Nchi yetu Tanzania [Baba wa Taifa] Mwalimu Nyerere.Maneno ya Mungu na mmoja wa makarani wake Mwalimu Nyerere,hakika mimi binafsi nayaona ni kama ifuatavyo:
Mungu: Julius
Julius: Naaaaaaaaam Bwana
Mungu: Kuna kiumbe wangu anakuja yuko upande wako wa wanasiasa kampokee
Julius: Ndio Bwana nitatenda ulivyonena Bwana.
Mungu: Utanena nae
Julius: Ndio Bwana
Mwalimu anaelekea langoni kule wageni wanakoingilia,naam katika tizama yake kutoka kundi la wageni anawaona kwenye mlango wa wanasiasa anashanga kuwa anaona binti,ambae kwa umri huo anamuona kwenye faili ni mjukuu wake.Kibinadamu Mwalimu amini kuwa binti aliye mlangoni mwake ni mgeni wake toka Tanzania hasa upande wa siasa, Mwalimu anaamua kupiga magoti na kunena na Bwana tena ili apate jibu kwa kuwa ajaamini.
Julius: Bwana Mungu wangu mbona mgeni ulie nena nami,ninae muona mbele yangu ni mjukuu wangu Bwana.
Mungu: Julius unaniuliza nini tena fuata nilichokuagiza
Julius: Ndio Bwana
Mwalimu anampokea Regia na kuanza kuelekea nae makazi ya Mwalimu,mazungumzo ya Mwalimu na Regia yanaanza kama ifuatavyo
Regia: Shikamoo Babu
Julius: Marahaba ujambo,karibu sana umefika hapa ndio kwenu nyumbani kwa maisha ya milele.
Regia: Asante Babu, nimepapenda kuzuri sana sijapata kuona mfano wake natamani Watanzania wangepaona.
Julius: Mshukuru Bwana Mungu aliyekufanya mteule kuja huku.
Baada ya mapumziko na kupumzika,jioni Mwalimu anamazungumzo na mjukuu wake huyo:
Julius: Regia mjukuu wangu ujambo na heri ya safari yako njema na salama,japo najua ugenini uko ulikotoka wanakulilia.
Regia: Babu Umekosea kule ndio Nyumbani,
Julius: Aaaaaaaaah mjukuu wangu Regia, kule sio kwenu huku ndio kwenu kule ni ugenini huku ndiko nyumbani kwenu.
Regia: Kumbe !!!!!!!,natamani hata walioko kule wangekuona kulivyo kuzuri.
Juliis: Baba na Mama yako, Bibi zako akiwemo Maria Nyerere natumai ni wazima ila najua wanakulilia
Regia: Wazima Babu.
Julius: Eeeeeeeeeeh Nchi yenu ikoje manake mimi mwenyewe,nimestuka sana pale Bwana aliponena nami na kuniagiza nikapokee mgeni,lakini wewe katika makarabrasha yangu ya wanasiasa niliowafundisha na kuwaagiza kufuata maadili ya UTU NA KUTENDA HAKI, HASA KWA MASKINI NA WANYONGE nakisha nikawaachia jukumu la kuongoza maisha ya Watanzania na vizazi vyao, viumbe wa Bwana, wewe ulikuwa kichanga tena wakati mimi naaawachia madaraka wao wewe ulikuwa na umri wa miaka mitano.
Regia: Mmmmmmh Babu kwani wewe ujui!!!!!!!!!.
Julius: Regia mimi nitajulia wapi mjukuu wangu,kwa kuwa kuna ukuta mkubwa sana kati yangu mimi na watu walioko Duniani,na mwenye funguo za mawasiliano hayo ni Bwana, ambae nyie duniani mnamuita Mungu.Sana sana taarifa ya mwisho kuhusu huko kanipa Babu yako Rashid tena alitoka hapa asubuhi, karibu ataludi.
Regia: Aaaaaaaaah Kumbe!!!!!!!!. Na mimi nataka kumuona Bwana Mungu.
Julius: Aahhhhhhaaa Regia Bwana Mungu unae hapa hapa ulipo anakujua, anakusikia anakugusa wewe hata kabla ujafikiliwa utazaliwa na kwenda kuishi ugenini huko duniani na kisha yeye kukuita tena kwake,anakujua wewe tangu alivyokuumba yeye.
Regia: Babu mbona duniani walinimbia wanaokuja huku wanamuona Bwana Mungu.
Julius: Ndio hawakukosea unamuona Bwana Mungu yeye ni Alpha na Omega yani mwanzo na mwisho kwa kuwa wewe kuja kwako uku tayari umemuona ndio maana mimi na wewe tumeonana,na tunaongea, kwa kuwa yeye ndie aliyeyafanya haya yote.
Mara mlangoni aningia Sokoine, Mwalimu anamkaribisha ndani,
Sokoine: Shikamoo Mzee
Julius: Marahaba Edward karibu,tuna mgeni, kwani nilinena na Bwana akaniagiza nikampokee anaitwa Regia
Regia: Shikaamo nafurahi kukuona Baba
Sokoine: Aaaaaaaha Marahaba Regia,karibu sana Nyumbani. Kisha Sokoine anataka kutoka,kumuacha Mwalimu aendelee na maongezi yake na mjukuu wake Regia,Mwalimu anatoa kauli
Julius: Edward,usitoke ebu,twende hapo kilimani na mgeni huyu manake kaniuliza swali la mwisho hapa wakati wewe unaingia kumuhusu Bwana Mungu,ya kuwa anataka kumuona !!
Sokoine: Sawa Mzee
Wanatoka na kuelekea kilimani,wakati wakielekea huko Regia anavutiwa na uzuri wa maua na hali ya hewa ya mazingira ya wenyeji wake na sauti nzuri za ndege,wenye rangi nzuri za kuvutia kupita Tausi wa Ikulu, Regia amepapenda sana.Ghafla wanafika kilimani Regia anaona kwa mbali mwanga mkali wa moto na miale mikali ambayo kwa macho yake hakuna athari zozote anazopata ila inatisha kwa kuangalia.Mwalimu anatumia muda huo kumwelimisha Regia kuhusu swali lake la awali.
Julius: Regia unaona kule?
Regia: Ndio!!!! Babu Nyerere,mbona kunatisha sana? ,sitamani hata kuangalia, nasikia sauti za vilio na mayowe yasiyoisha pia sauti za kuomba msaaada,si mgeenda kuwasaidia.
Julius: Regia mama ulichouliza kule tulipokuwa, ya kuwa yuko wapi Bwana Mungu na ungependa kumuona .Jibu langu kwako kwa ufahamu wangu Bwana Mungu yuko Upande huu mimi na wewe tulipo na kule unakosikia wanapiga kelele za kilio cha mayowe ndio kwa shetani na wafuasi wake ambako wana mateso ya milele.Hatima ya uwepo wako hapa ulishaichagua wewe mwenyewe toka ulipokuwa huko ugenini yaani duniani kwa kuwa tiketi ya kusafilia uliyochagua ya ujio wako huku ndio iliyokuchagua wewe kuja huku aliko yeye.Matendo yako na maisha yako duniani ndio yamempendeza Mungu akakuchagua wewe ukaja upande huu wa Bwana Mungu, ulipotamani haki kwa wote ulimpendeza Bwana Mungu wako, ulipotamani kutatua shida za wengi na matendo mengineyo yaliyokusukuma kukufikisha kuwa mwanasiasa wa kujali watu na kuthamini utu wa mwanadamu ndio umempendeza Bwana Mungu wako, kwa kuwa hesabu ya maisha yako anayo yeye toka alivyokuumba wewe kwa mfano wake.
Regia: Aaahaa Sasa nimeelewa Babu Nyerere,siuniombee ruksa kwa Bwana Mungu niende nikawaambie niliyoyaona huku.Ili wajifunze wasije wakaenda kule kwenye lile bonde linalowaka kwa kunakoitwa kwa Shetani na wafuasi wake.
Julius: Aaaaaaah Regia unanichekesha kweli mjukuu wangu!! Kwani wewe nani alikwambia?Wewe umetimiza kusudio la Bwana kwa wanadamu. Na Bwana kawaachia uamuzi wao wenyewe kuchagua kama wewe uklivyomaliza uchaguzi wako.Umetimiza nao waache watimize wajibu wao kwa Bwana kwa kuwa aliwaaumba kwa mfano wake ambao ni mimi, wewe na baba yako Sokoine hapa tulio tulishatimiza huko ugenini.Na kwa kuwa wakati nilipokuwa nimetumwa na Bwana Mungu huko ugenini nikawa Rais wao wa kwanza wa Taifa lao niliwaachia mwongozo kwa kuunda na kulinda Taifa lenye kusamini UTU WA MTU, HAKI SAWA KWAO WOTE NA KUTHAMINI WANYAONGE WASIO NA SAUTI.Na wewe Regia pia umetimiza wajibu wako hivyo hawana wa kumlalamikia cha msingi umewaachia jina lako.
Regia: Jamani Babu Nyerere jaribu kuongea nae hata sekunde chache tu kisha narudi.
Julius: Polepole utanielewa najua unawapenda sana kwa kuwa nilipotumwa mimi kuja huko nilichotumwa nilifundisha na Wananchi walio wengi walinielewa, watu wa aina yako ndio wanakazi ya kusimamia mafundisho hayo ya utu na haki, lakini kama ni kuwafundisha na kuwakumbusha kuhusu kumtumikia Bwana Mungu siku zao za maisha yao duniani basi Makanisa, Misikiti na Imani zote zinazojua Mungu mmoja zipo wanazo tele zinawakumbusha kila siku. Kwenye hayo Makanisa ,Misikiti, Madhehebu na Jadi zao wana Maaskofu,Mapadre,Wachungaji,Masheikh na Wazee wao wa Jadi.Kwa kuwa Bwana Mungu aliwapenda ndio maana akawatumia mkombozi Yesu kristu kwa ajili yao kwa wale walio wakristu na kwa Waislamu alimtuma Mtume Muhamad kwa ajili ya mafundisho ya kiimani,kuwajenga kumtumikia Mungu katika sura ya uwanadamu.Na nyie Wanasiasa wajibu wenu kusimamia na kuongoza ustawi wa jamii katika misingi ya haki na utu kwa kuwa Bwana Mungu awezi kushusha Malaika kuja kuwaongoza na kuonyesha jinsi ya kuishi bali Mungu kwa kutumia wanadamu anatoa baraka za binadamu kujiongoza na kuendesha maisha yao.
Rose Muhando kwenye mmoja ya wimbo wake anasema Regia hayumo katika miongoni mwa wajutao,hayumo miongoni mwa wenye mashaka, hayumo miongoni mwa wasitao, amemtumaini yeye Bwana Mungu kwa sasa yuko kwa Mungu ana nguvu tele.RIP Regia.
Tukipima siku za maisha yetu hapa dunia ni chache sana kwa kuishi, lakini ni nyingi sana kwa binadamu mwenye kumjua Mungu kwa kuwa Mungu ndiye mpangaji wa maisha yetu hivyo ulefu au ufupi ni kudra zake Mungu.Regia ameondoka lakini kaacha jina na jina hilo tafsiri yake inaonekana kwenye michango yetu ya maombolezo yetu humu ndani ya Jamii Forum, kwa kuwa Mungu anasema usitumaini akili zako bali mtumaini yeye Mungu kwa kuwa ndiye anayejua sababu ya uwepo wetu sisi wanadamu hapa duniani.
Mungu alisema anamuumba Mwanadamu kwa mfano wake,hivyo yaliyosemwa na sisi wote kama Wanajamii forum,Viongozi, Wanandugu na Wananchi wote juu ya Mtoto, Dada, Ndugu, Mwanasiasa, Kiongozi, Rafiki, Askari Mpiganaji huyu ni kielelezo tosha cha Mungu kuongea nasi jinsi gani Mungu alikusudia kuwapa Baba na Mama yake Regia mtoto mwema na ambae kwetu Watanzania alikuwa Mwanasiasa na Kiongozi aliyetutumikia kwa muda mfupi lakini, kwa sauti yenye mwangi mkubwa sana ambayo ilisambaa kwenye nyika na kufikisha ujumbe popote pale ilipostahiki.
Regia kaacha jina lake kwenye vinywa vyetu kwa kuwa katimiza kazi aliyotumwa na Mungu kwetu,ndio maana wanafalsa [Philosophers] wanasema kwa Wanasiasa na Viongozi wazuri duniani ubora na uzuri wa uongozi wao si kuacha mali kwa walithi wao,bali kuacha jina ambalo kila mtu akilisikia na kukumbuka anapata mwamko wa kufuata mazuri ambayo mwanasiasa au kiongozi huyo aliyapigania na kusimamia wakati wa wote wa uhai wake hapa duniani.Ndio maana kwa sisi vijana wa dotcom ambao hatukupata kuushuhudia utawala wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lakini wanadotcom hao wa sasa wanamjua na kumfuata nyayo zake kuliko wale Mwalimu aliowatumika na kuwafundishawakati wote wa maisha yake hapa duniani.
Hakika napata picha ya kibinadamu lakini ambayonatumani nawe ndiyo unayoijenga.Mungu alipomuita kiumbe wake Regia, wakati anaitikia wito wake kufika mbinguni Mungu nae ananena na mmoja wa makarani wake kwa Nchi yetu Tanzania [Baba wa Taifa] Mwalimu Nyerere.Maneno ya Mungu na mmoja wa makarani wake Mwalimu Nyerere,hakika mimi binafsi nayaona ni kama ifuatavyo:
Mungu: Julius
Julius: Naaaaaaaaam Bwana
Mungu: Kuna kiumbe wangu anakuja yuko upande wako wa wanasiasa kampokee
Julius: Ndio Bwana nitatenda ulivyonena Bwana.
Mungu: Utanena nae
Julius: Ndio Bwana
Mwalimu anaelekea langoni kule wageni wanakoingilia,naam katika tizama yake kutoka kundi la wageni anawaona kwenye mlango wa wanasiasa anashanga kuwa anaona binti,ambae kwa umri huo anamuona kwenye faili ni mjukuu wake.Kibinadamu Mwalimu amini kuwa binti aliye mlangoni mwake ni mgeni wake toka Tanzania hasa upande wa siasa, Mwalimu anaamua kupiga magoti na kunena na Bwana tena ili apate jibu kwa kuwa ajaamini.
Julius: Bwana Mungu wangu mbona mgeni ulie nena nami,ninae muona mbele yangu ni mjukuu wangu Bwana.
Mungu: Julius unaniuliza nini tena fuata nilichokuagiza
Julius: Ndio Bwana
Mwalimu anampokea Regia na kuanza kuelekea nae makazi ya Mwalimu,mazungumzo ya Mwalimu na Regia yanaanza kama ifuatavyo
Regia: Shikamoo Babu
Julius: Marahaba ujambo,karibu sana umefika hapa ndio kwenu nyumbani kwa maisha ya milele.
Regia: Asante Babu, nimepapenda kuzuri sana sijapata kuona mfano wake natamani Watanzania wangepaona.
Julius: Mshukuru Bwana Mungu aliyekufanya mteule kuja huku.
Baada ya mapumziko na kupumzika,jioni Mwalimu anamazungumzo na mjukuu wake huyo:
Julius: Regia mjukuu wangu ujambo na heri ya safari yako njema na salama,japo najua ugenini uko ulikotoka wanakulilia.
Regia: Babu Umekosea kule ndio Nyumbani,
Julius: Aaaaaaaaah mjukuu wangu Regia, kule sio kwenu huku ndio kwenu kule ni ugenini huku ndiko nyumbani kwenu.
Regia: Kumbe !!!!!!!,natamani hata walioko kule wangekuona kulivyo kuzuri.
Juliis: Baba na Mama yako, Bibi zako akiwemo Maria Nyerere natumai ni wazima ila najua wanakulilia
Regia: Wazima Babu.
Julius: Eeeeeeeeeeh Nchi yenu ikoje manake mimi mwenyewe,nimestuka sana pale Bwana aliponena nami na kuniagiza nikapokee mgeni,lakini wewe katika makarabrasha yangu ya wanasiasa niliowafundisha na kuwaagiza kufuata maadili ya UTU NA KUTENDA HAKI, HASA KWA MASKINI NA WANYONGE nakisha nikawaachia jukumu la kuongoza maisha ya Watanzania na vizazi vyao, viumbe wa Bwana, wewe ulikuwa kichanga tena wakati mimi naaawachia madaraka wao wewe ulikuwa na umri wa miaka mitano.
Regia: Mmmmmmh Babu kwani wewe ujui!!!!!!!!!.
Julius: Regia mimi nitajulia wapi mjukuu wangu,kwa kuwa kuna ukuta mkubwa sana kati yangu mimi na watu walioko Duniani,na mwenye funguo za mawasiliano hayo ni Bwana, ambae nyie duniani mnamuita Mungu.Sana sana taarifa ya mwisho kuhusu huko kanipa Babu yako Rashid tena alitoka hapa asubuhi, karibu ataludi.
Regia: Aaaaaaaaah Kumbe!!!!!!!!. Na mimi nataka kumuona Bwana Mungu.
Julius: Aahhhhhhaaa Regia Bwana Mungu unae hapa hapa ulipo anakujua, anakusikia anakugusa wewe hata kabla ujafikiliwa utazaliwa na kwenda kuishi ugenini huko duniani na kisha yeye kukuita tena kwake,anakujua wewe tangu alivyokuumba yeye.
Regia: Babu mbona duniani walinimbia wanaokuja huku wanamuona Bwana Mungu.
Julius: Ndio hawakukosea unamuona Bwana Mungu yeye ni Alpha na Omega yani mwanzo na mwisho kwa kuwa wewe kuja kwako uku tayari umemuona ndio maana mimi na wewe tumeonana,na tunaongea, kwa kuwa yeye ndie aliyeyafanya haya yote.
Mara mlangoni aningia Sokoine, Mwalimu anamkaribisha ndani,
Sokoine: Shikamoo Mzee
Julius: Marahaba Edward karibu,tuna mgeni, kwani nilinena na Bwana akaniagiza nikampokee anaitwa Regia
Regia: Shikaamo nafurahi kukuona Baba
Sokoine: Aaaaaaaha Marahaba Regia,karibu sana Nyumbani. Kisha Sokoine anataka kutoka,kumuacha Mwalimu aendelee na maongezi yake na mjukuu wake Regia,Mwalimu anatoa kauli
Julius: Edward,usitoke ebu,twende hapo kilimani na mgeni huyu manake kaniuliza swali la mwisho hapa wakati wewe unaingia kumuhusu Bwana Mungu,ya kuwa anataka kumuona !!
Sokoine: Sawa Mzee
Wanatoka na kuelekea kilimani,wakati wakielekea huko Regia anavutiwa na uzuri wa maua na hali ya hewa ya mazingira ya wenyeji wake na sauti nzuri za ndege,wenye rangi nzuri za kuvutia kupita Tausi wa Ikulu, Regia amepapenda sana.Ghafla wanafika kilimani Regia anaona kwa mbali mwanga mkali wa moto na miale mikali ambayo kwa macho yake hakuna athari zozote anazopata ila inatisha kwa kuangalia.Mwalimu anatumia muda huo kumwelimisha Regia kuhusu swali lake la awali.
Julius: Regia unaona kule?
Regia: Ndio!!!! Babu Nyerere,mbona kunatisha sana? ,sitamani hata kuangalia, nasikia sauti za vilio na mayowe yasiyoisha pia sauti za kuomba msaaada,si mgeenda kuwasaidia.
Julius: Regia mama ulichouliza kule tulipokuwa, ya kuwa yuko wapi Bwana Mungu na ungependa kumuona .Jibu langu kwako kwa ufahamu wangu Bwana Mungu yuko Upande huu mimi na wewe tulipo na kule unakosikia wanapiga kelele za kilio cha mayowe ndio kwa shetani na wafuasi wake ambako wana mateso ya milele.Hatima ya uwepo wako hapa ulishaichagua wewe mwenyewe toka ulipokuwa huko ugenini yaani duniani kwa kuwa tiketi ya kusafilia uliyochagua ya ujio wako huku ndio iliyokuchagua wewe kuja huku aliko yeye.Matendo yako na maisha yako duniani ndio yamempendeza Mungu akakuchagua wewe ukaja upande huu wa Bwana Mungu, ulipotamani haki kwa wote ulimpendeza Bwana Mungu wako, ulipotamani kutatua shida za wengi na matendo mengineyo yaliyokusukuma kukufikisha kuwa mwanasiasa wa kujali watu na kuthamini utu wa mwanadamu ndio umempendeza Bwana Mungu wako, kwa kuwa hesabu ya maisha yako anayo yeye toka alivyokuumba wewe kwa mfano wake.
Regia: Aaahaa Sasa nimeelewa Babu Nyerere,siuniombee ruksa kwa Bwana Mungu niende nikawaambie niliyoyaona huku.Ili wajifunze wasije wakaenda kule kwenye lile bonde linalowaka kwa kunakoitwa kwa Shetani na wafuasi wake.
Julius: Aaaaaaah Regia unanichekesha kweli mjukuu wangu!! Kwani wewe nani alikwambia?Wewe umetimiza kusudio la Bwana kwa wanadamu. Na Bwana kawaachia uamuzi wao wenyewe kuchagua kama wewe uklivyomaliza uchaguzi wako.Umetimiza nao waache watimize wajibu wao kwa Bwana kwa kuwa aliwaaumba kwa mfano wake ambao ni mimi, wewe na baba yako Sokoine hapa tulio tulishatimiza huko ugenini.Na kwa kuwa wakati nilipokuwa nimetumwa na Bwana Mungu huko ugenini nikawa Rais wao wa kwanza wa Taifa lao niliwaachia mwongozo kwa kuunda na kulinda Taifa lenye kusamini UTU WA MTU, HAKI SAWA KWAO WOTE NA KUTHAMINI WANYAONGE WASIO NA SAUTI.Na wewe Regia pia umetimiza wajibu wako hivyo hawana wa kumlalamikia cha msingi umewaachia jina lako.
Regia: Jamani Babu Nyerere jaribu kuongea nae hata sekunde chache tu kisha narudi.
Julius: Polepole utanielewa najua unawapenda sana kwa kuwa nilipotumwa mimi kuja huko nilichotumwa nilifundisha na Wananchi walio wengi walinielewa, watu wa aina yako ndio wanakazi ya kusimamia mafundisho hayo ya utu na haki, lakini kama ni kuwafundisha na kuwakumbusha kuhusu kumtumikia Bwana Mungu siku zao za maisha yao duniani basi Makanisa, Misikiti na Imani zote zinazojua Mungu mmoja zipo wanazo tele zinawakumbusha kila siku. Kwenye hayo Makanisa ,Misikiti, Madhehebu na Jadi zao wana Maaskofu,Mapadre,Wachungaji,Masheikh na Wazee wao wa Jadi.Kwa kuwa Bwana Mungu aliwapenda ndio maana akawatumia mkombozi Yesu kristu kwa ajili yao kwa wale walio wakristu na kwa Waislamu alimtuma Mtume Muhamad kwa ajili ya mafundisho ya kiimani,kuwajenga kumtumikia Mungu katika sura ya uwanadamu.Na nyie Wanasiasa wajibu wenu kusimamia na kuongoza ustawi wa jamii katika misingi ya haki na utu kwa kuwa Bwana Mungu awezi kushusha Malaika kuja kuwaongoza na kuonyesha jinsi ya kuishi bali Mungu kwa kutumia wanadamu anatoa baraka za binadamu kujiongoza na kuendesha maisha yao.
Rose Muhando kwenye mmoja ya wimbo wake anasema Regia hayumo katika miongoni mwa wajutao,hayumo miongoni mwa wenye mashaka, hayumo miongoni mwa wasitao, amemtumaini yeye Bwana Mungu kwa sasa yuko kwa Mungu ana nguvu tele.RIP Regia.