Farewell-Kwaheri Regia: A Tribute Page

Farewell-Kwaheri Regia: A Tribute Page

Asante sana kwa salam za rambramb, ila utan na nyie hatuna huwa tunawapnga kwelkweli so sisi sio watan wenu, watan wenu ni Cuf
Na NCCR mageuzi basi na si vinginevyo, tunapokea pole yako ingawa haitabadilisha chochote ila achana na masuala ya utani hapa sisi tuko serious.
 
Great idea. But I would suggest that we all hold all the over excitement together, bury her and then listen to her family first and see what else to do. We are still in a shock and too many promises might make us look ridiculous.
 
Inasikitisha kwa kweli miaka 32 tu kuondoka na ndoto zote zile inasikitisha sana, kilichobaki kumuombea kwa MUNGU apumzike kwa amani.
 
Sawa mkuu, ni wazo zuri ila kwa utaratibu utakaopangwa baada ya mazishi na iwe kweli ni mfuko wa uhakika na kwa kazi iliyokusudiwa na si vinginevyo
 
I would suggest that we all hold all the over excitement together, bury her and then listen to her family first and see what else to do. We are still in a shock and too many promises might make us look ridiculous.


True King'asti.
 
Mimi mpaka nakosa cha kuandika....kiukweli inaumaa sana
Mimi ni machozi tu kuanzia jana, kila nikimfikiria naona uchungu sana tena sana, machozi hayanikauki, namwomba Mungu atupe mtu atakayeweza kuziba pengo hili kubwa namna hii. Bwana amlipe sawa na kazi yeke. Amen
 
RIP Regia, maisha yako mafupi hapa duniani yalikuwa ya faida. Wengine wenye akili nzuri wataiga yale yote mazuri kwako na daima utakuwa mfano kwao.
 
Wana JF,

Wakati wa uhai wake ndugu yetu Mh Regia (RIP) aliwahi kuonyesha uchungu wake juu ya watoto wenye ulemavu wa mwili wanaokosa fursa ya kupata elimu. Napendekeza tumuenzi kwa kuanzisha REGIA MTEMA MEMORIAL FUND ili iweze kusomesha watoto wenye ulemavu kwa utaratibu utakaokubaliwa.

Naomba kutoa hoja.

sasa we ndugu, manyzi yote haya kumhusu Regia bado mnaanzisha mapya? Acheni ubinafsi na mwende mkaweke mawazo yenu hayo kwenye nyuzi husika. Kule premium ungeweza kuyaweka haya mawazo yako
 
Tulitegemea mengi kutoka kwako, na ulionyesha jinsi utakvyo kidhi mahitaji yetu sisi Watz kwa sasa na siku zijazo. Kwa hiki kifo chako, Mungu ana kusudi lake na kwa namna yoyote kazi yake haina makosa. RIP kipenzi chetu
 
Timing Timing Timing is everything! tuwafaraji wafiwa na kuwaombea amani ya Mungu katika kipindi hiki kigumu kwao
Mungu awape Amani na Faraja.
 
Ushupavu wako,tabasamu lako na ucheshi wako havitasahulika kamwe! Utabakia kama bint shupavu na mfano kwa mabint wengine. Upumzike kwa Amani. Panapo majaliwa nitakuja siku ya junne hapo Karimjee kukuaga mdogo wangu!
 
rest in peace gender sensitive.

wewe unaetuita watani ukome na ukomae,ccm wanaiba mali za umma na kuzigawa kama wenyewe wamefariki chadema imedhamiria kukamata mwizi unakuja unatuita watani?
utani unaanzia wapi?
ngoja tumalize msiba tuanze na wewe.
 
MM umenena yote,kwa kweli tumepoteza mtu makini sana,hasa hapa JF..hoja zake nzito zenye kuhitaji kusugua kichwa na kufikiria kwa dhati kabla ya kuchangia tutazikosa,tutazikosa comments zake,tutamkosa pale bungeni wakati wa kuchangia hoja kwa maendeleo ya nchi yetu...tutamkosa Regia! Ni jambo lisilovumilika kirahisi,nitamkosa Dada Regia,nitamkosa mum Regia!! Nani wa kutuzibia hili pengo,tutampata wapi mtu mvumilivu na makini kama Regia jamani? Tutayapata wapi mawazo yake chanya ya kujenga chama chetu wakuu? Regia hayupo jamani,nani? nani? nani? oh!! mum Regia mbona umetuacha wenzio,hapana naumia wakuu!!
 
Hivi vitu{mauti} havizoeleki aisee.....
rest in peace madam wa ukweli!!!
 
rest in peace dear Regia,
I cant wait to meet you again in gloryland.
 
Back
Top Bottom