Farewell-Kwaheri Regia: A Tribute Page

Farewell-Kwaheri Regia: A Tribute Page

Kwaheri kamanda umetutangulia nasi tuko nyuma tunakuja, sina namna ya kuelezea msiba huu maana kwa namna ratiba yake ya kazi ilivyokuwa jana kwa kweli ni mpiganaji aliyefariki akiwa katika harakati za kujiletea maendeleo ya familia na Taifa kwa ujumla. Tuko pamoja na familia yake ktk kipindi hiki kigumu na Mungu awape moyo wa subira
 
Regia umetangulia nakutuacha wakiwa. Watz, vijana na wapenda maendeleo wote kuwa uliloacha si pengo la kawaida japo tumezoea kusema halitazibika hili halizibiki kweli. Umekuwa si mbunge tunaowafahamu nakuwazoea mara wapatapo ubunge huwa si watz bali wageni kwetu baada yakuwapa nafasi. Nenda pumzika kwa amani na kwa machozi ya watz wengi mungu atkupokea kwakuwa ulitumikia wananchi tena walala hoi.

Kwa waliobaki, mh ama waheshimiwa wabunge wa CDM nawaomba japo alichokuwa anakifanya Mh Regia kilikuwa ni cha kipekee chakuhabarisha wananchi wanayotoke bungeni na nje ya bunge yaliyokuwa yanatokea tupatieni watz mtu ambae atatupa updates hizo japo anaweza kutoziba kabisa pengo hilo.

Kwako dada yetu, mh mbunge wa cdm na mwenyekiti wa mkoa wa morogoro, pole kwa msiba huu wakuondokewa na mbunge na mtu uliekuwa unashirikiana nae kuhudumia wana morogoro na watz. Jipe moyo umeniliza kwa huzuni uliyokuwa nayo natambua kakuachia pengo
 
Nilishakwaruzana nawe sana Regia, but hii ni kwasababu ya tofauti ya itikadi zetu..nilisikitika sana kupata habari za kifo chako, bado nilikuwa nakuhitaji ili tumalize tofauti zetu, but mungu amekuhitaji zaidi. Pumzika kwa amani Regia.
 
Wakati mwingine najiuliza "Why Regia?". Kwa nini Mungu kakuchagua Regia? Mbnona ndo kwanza ulianza kukusanya kero zetu kupitia humu mtandaoni kuziwasilisha bungeni na kwingineko. Why now?.


Binafsi bado naikumbuka Hotuba yako bungeni ulipochangia kwa mara ya kwanza, ambapo ulisema "Nawashukuru Wananchi wa Kilombero kwa kunichagua kwa kura nyingi kuwa mbunge wao ingawa sikufanikiwa kutangazwa mshindi" Maneno haya yamenifikirisha na yana ujumbe mzito. Kwa maneno haya ulitoa ujumbe mzito kwa Tume yetu ya Uchaguzi, lakini kwa unyenyekevu.
RIP REGIA.
 
Tumeguswa sana. Mungu amlaze na kumpumzisha pamoja na wapiganaji wenzake. lakini tuliobaki TUISHI NDOTO ZAKE kwani lengo na nia yake kwa TAIFA aliiweka bayana.
 
Toka moyoni mwangu Nasikitika sana,

Rest in Peace beloved Regia.:shock:

My heart is feeling pain for this fatal accident that has claimed your life especially at this stage that we needed you most. Regia, you will remain in my heart forever for your unprecedented commitment to your people and Tanzanians.
 
Hii ni kwa ajili ya tributes za Regia; kama unalo zuri la kusema kumhusu yeye au kumbukumbu yako njema tushirikishe.

Nyota Imezimika


Ni pigo limetufika
Nashindwa la kutamka
Ilikuwa inawaka
Sasa nyota yazimika
Nabaki natetemeka
Machozi yanadondoka!
Namlilia Regia, ni nyota imezimika!

MMM

R.I.P mheshimiwa
 
Tutakukumbuka milele regia tulikupenda sana mpendwa wetu ,lakini mungu kakupenda zaidi,
nyota yako ilikuwa ndo imeanza kung'ara mpendwa wetu.pumzika kwa amani,,kila nikiwaza nakuwa kama naota vile
kweli maisha ya mwanadamu ni mafupi yanachanua na kunyauka tutengeneze mapito yetu siku zote kwani hatujui siku wala saa mwenyezi mungu atakapoamua kutuita
 
Mungu, ampumzishe kwa amani Regia; legacy aliyoiacha naamini kina dada wengi watakutumia kama role model.

Pumzika dada!
Amen
 
Regia dada.Nakumbuka ulipokuwa umekuja mkoa wa Ruvuma ukiwa umeambatana na katibu wa kawe katika kutoa elimu ya kuhusiana na katiba mpya,na mimi nikajitahidi kutoa yale yote uliyotufundisha na kutuelekeza hapa jamvini na watu wengi wakafurahi kwa jinsi ulivyo washa moto wa mabadiliko kwa vijana,wazee na hata kina mama.Dada Regia nakumbuka ulipo sema atakama watakufunga wewe hautojali ila utaendelea kuelimisha watu mpaka kieleweke.Watu wa Ruvuma tulifurahi sana kwakuona sasa tumepata mtu wakutuongoza katika harakati izi.Ehe mwenyezi MUNGU kweli kazi yako haina makosa lakini kamanda huyu bado tulimuhitaji zaidi katika kipndi hiki.Dada Regia kumbe ndio ulikua umekuja kutuaga wana Ruvuma?ukweli tutakukumbuka nasi tutakuenzi kwa kushika na kufata ujasili ule uliotufundisha pindi ulipokuja Ruvuma tulijua ungeja rudi tena na tena kumbe dada ndio ulikua umekuja kutuaga!MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI DADA REGIA.
 
oooh Mungu,
imekua ghafla kwangu,hata bado siamini,na kuzingatia ni wakati mwafaka tunakuitaji.........nashindwa kusema zaidi nasema,''tutakuenzi kisiasa, kiuharakati, kiukamanda, kiupambanaji, kiutoaji hoja,mungu akulaze mahara pema AMEN
 
"Bwana ametoa na Bwana ametwa jina lake libarikiwe"
Ameen.
 
RIP Regia,nashukuru kwa mchango wako kwa taifa ili la Tanzania,Bwana alitoa Bwana ametwaa jina lake libarikiwe.
 
Buriani dada Regia tulikuwa tukikwaruzana sana na tofauti zetu za mtazamo wa mambo ya nchi. Ama kweli moyoni ni simanzi kubwa kuondoka kwako tumekosa mpiganaji. Ukapumzike salama. Zile ID zako nyengine tunaomba moderator uzihifadhi pia kwa heshima ya Mheshimiwa.
 
Mh Regia, Hakuna hata mbunge mmoja aliyeanza kukusanya kero kwa ajili ya kikao kijacho lakini wewe ulianza ! Ulikuwa unaipenda hiyo kazi ya Utumishi sana.......Uliichukua kero yangu una uka i " like " humu JF nlijua utaifikisha magogoni kwa kutumia ile anuani ya Bunge ! MIPANGO YA MUNGU haina makosa, Nakupenda sana..............!!
 
Dada Regia tulikupenda lakini Mungu alikupenda zaidi hatuna jinsi pengo ulilotuachia ni kubwa kazi ya Mungu haina makosa raha ya milele umpe ee bwana na mwanga wa milele umwangazie apumzike kwa amani
 
Back
Top Bottom