MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,604
[h=2]Re: Eti Wazungu -nyie dada zetu chonde![/h]Pengine hii mada ingekuja vyengine, badala ya-nyie dada zetu chonde!- ikawa -nyie kaka (au na dada) zetu chonde!- tungeona response tafauti na hizi tulizoweka hapa. Ninaheshimu mawazo ya wote, lakini kila mara huwa ninapata tabu kuchangia pale "generalization" inapotumika. Tukiwachia dada zetu wanaopapatikia wazungu, je akina kaka wanapofanya hivyo, huwa sababu ni kwa sababu "mapenzi ya kidhungu?" au maslahi?
Kwa mawazo yangu sioni tafauti kubwa sana baina ya mapenzi na maslahi, nikimaanisha kuwa kuna - maslahi katika mapenzi na mapenzi katika maslahi-. Kwa hivyo, sioni ubaya kama mwanamke au mwanamume, awe Mwafrika au Mzungu, kuvutiwa na aliye tafauti naye, pengine kwa mapenzi ya dhati au kwa kutaka kujiridhisha tu na "myths" za Waafrika wako hivi, Wazungu wako vile.
Kwa mawazo yangu sioni tafauti kubwa sana baina ya mapenzi na maslahi, nikimaanisha kuwa kuna - maslahi katika mapenzi na mapenzi katika maslahi-. Kwa hivyo, sioni ubaya kama mwanamke au mwanamume, awe Mwafrika au Mzungu, kuvutiwa na aliye tafauti naye, pengine kwa mapenzi ya dhati au kwa kutaka kujiridhisha tu na "myths" za Waafrika wako hivi, Wazungu wako vile.