Eti uchochezi, uchochezi gani?

Eti uchochezi, uchochezi gani?

[HASHTAG]#hapakazitu[/HASHTAG] Mwaka huu mtanena kwa lugha zote lakini lazima mnyooke...hakuna maigizo hapa ni kazi tu.
Wewe mwenyewe umeishanyooka ila unajikaza tu kwa kuwa akili hauna na huo Ujinga wako wa kijingalao.
 
Kabisa, siku ya leo BBC swahili Ukuta, Voa kiswahili ni Ukuta, DW Ukuta, yaani wewe acha tu

Wanadai UKUTA ni neno la kichochezi & kigaidi. Na haitashangaa BBC, Voa & DW zikafungiwa na Nape kurusha matangazo yao TZ kwa kutangaza uchochezi
 
Nakuelewa sana Nyani.

Binafsi nampenda na kumuheshimu binadamu asiyeogopa kuelezea hisia zake juu ya jambo fulani hata kama ni haki yake kisa tu anawaogopa watu flani.

Ndio maana hata kati ya wabunge wote wa ccm waliopo, Musukuma is my fovorite kwa sababu anasimamia anachokiamini na kukisema bila kugopa mtu.

Kuhusu huyu mheshimiwa mtukufu malaika mkuu tulienae, anachofanya ni kutumia intimidation kuwatawala kwanzia hao wasaidizi wake kiasi kwamba hata wao wenyewe sasa wanazitafsri kauli zake kwa namna itakayompendeza yeye.

Nna huakika wengi wao zaidi ya 90% akiwemo mkuu mwenyewe, ukiwauliza haya maneno ya mtandaoni yanachochea vipi uvunjifu wa amani hawawezi kutoa majibu sahihi.
Kuna Mbunge aliwahi kusema bungeni kuwa "wateule wa Raisi wanafanyakazi kwa mzuka wa Rais" Waziri mmoja alipinga kwa kunung'unika sana.
 
Hivi ni kweli kuwa vijana wasomi wa ccm kweli wanamwona kuwa anafanya sawa?

Mkuu ulishawahi kusikia hadithi ile tamu ya mfalme juha? aliyeshonewa suti hewa wasaidizi wake wote walikuwa wakimsifia kwamba suti imempendeza, kumbe yu uchi .
Bahati nzuri au mbaya kwao wapambe na mfalme wakati wanapita kukagua maendeleo ya raia wake kuna katoto fulani kakaushitua umma na kumuuliza mama yake mbona mfalme yuko uchi?
 
Tanzania ambayo Africa nzima tuliheshimika tumegeuka mara hii kuwa kichekesho. Nchi inaendeshwa na matamko ya viongozi tu. Taratibu za kila siku zimeshindikana. Jamani huyu mtu hana watoto wa kumwambia. Tafadhali wasanii wamtungie wimbo kama ule wa "Riziwan ongea na mshua......."
Watakamatwa kwa kosa la uchochezi na kuambulia kipigo cha polisi.
 
Nyani katika siku zote leo umeandika point ilonisababisha nikukubali...., he is the worst president ever had. Hana vision, vijana na wazee tumkosoe tusisupport kutokana na vijisent tunavyopata. Sie wazee wa zamani tunamuona kama tatizo
 
[HASHTAG]#hapakazitu[/HASHTAG] Mwaka huu mtanena kwa lugha zote lakini lazima mnyooke...hakuna maigizo hapa ni kazi tu.
Hili nalo linasadifu jina lake. Vijana wenye njaa na wabinafsi wenye kujali matumbo yao tuu bila ya kuangalia kizazi kijacho
Mungu ibariki TANZANIA wape vijana wake akili sio tope
 
Toka kina Lissu waanze kukamatwa kisa Uchochezi mbona hakuna hata mmoja ameshawahi kuhukumiwa???



Wakati mwingine naona Polisi wanahujumu serikali... Wanatumika kuwatangaza Upinzani....
 
ngoja uletewe arrest warrant na interpol ndiyo utaelewa kama kiswahili ni lugha ya taifa ama la! !
na hapo ndipo utakapoanza kutunga tafakari za semi ukiwa nguvuni!
 
Anaweza akawa Rais wa awamu moja.

Watu kama akina January usione wapo kimya, waswahili wanasema ukiona Kobe kainama ujue anatunga Sheria.

Miezi 10 madarakani, kaharibu kila kitu. Wananchi, Wanasiasa, Wafanyabiashara hata Watumishi hawana amani na huyu jamaa!!

Mkuu umesahau katiba inasema tume ya uchaguzi haihojiwi. Pia kumbuka mkuu wa tume anateuliwa na rais (which means rais ni boss wake). hawezi toka hadi amalize miaka 10
hata akipigiwa kura na familia yake tu lazima utaambiwa kashinda.
 
Ngabu

Yesu alisema rudi nyuma shetani we, na shetani akarudi, na sisi tuseme rudi nyuma ccm.....kwa kukataa uvunjifu wa katiba.

Mungu tena akaufanya moyo wa farao uwe mgumu aliamuadhibu. Hakika adhabu ya Mungu ni kubwa kuliko maanadamano na makelele ya wapinzani.
Hapa tukimtegemea yesu tumeumia dadangu,ye mwenyewe mpaka leo hatujuwi anarudi lini.
 
Mwendo wa sasa ni

[HASHTAG]#kwani[/HASHTAG] we chama gani ?
 
Ina
Ajabu kabisa Kaka, Uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM Polisi walitanda kial kona kuhakikisha hakuna njama na kumzuia Magu kuwa Mwenyekiti wa Chama,
Lakini kwenye Mkutano waCUF, Polisi ndio waliokuwa wanamuingizakwa Nguvu Mjumbe (Lipumba) asiyestahili kuingia kwenye mkutano ule, na hata fujo zilipotokea hakunaPolisi aliyeingia kuzuia fujo zile, sasa hapo nani ni mvunjifu wa Amani?
inasikitisha sana
s
 
Serikali ndiyo yenye mamlaka na uchunguzi wa vyombo husika vimeipa ripoti serikali kuwa maandamano hayo ni Ya uchochezi tu na wala siyo ya kupinga udikteta.Hakuna udikteta Tanzania ndio maana kuna jamii forum.
 
Kuna Mbunge aliwahi kusema bungeni kuwa "wateule wa Raisi wanafanyakazi kwa mzuka wa Rais" Waziri mmoja alipinga kwa kunung'unika sana.
Bila shaka hata huyo aliyepinga alipinga huku akilenga kuongeza credibility kwa raisi. Yaani hata yeye mwenyewe pia alipinga kwa mzuka wa raisi
 
Back
Top Bottom