Eti uchochezi, uchochezi gani?

Eti uchochezi, uchochezi gani?

Kiukweli sikuwa nafahamu kama CHADEMA wanatisha na wanaogopeka kiasi hiki, umarufu weka umepaa ndani ya wiki tatu ndani na nje ya mipaka ya Tanzania kuliko wakati mwingine wowote tangu kusajiliwa kwake, mbinu hii imefanikiwa kwa 100%.
Kabisa, siku ya leo BBC swahili Ukuta, Voa kiswahili ni Ukuta, DW Ukuta, yaani wewe acha tu
 
Ni upumbavu mtupu, kurupuka ya kapuku
Uzamivu wa wivu, uza mbivu kwa saba buku
Baba kakaba LUKU, siasa kahaba shuku
Sio Wamakonde Maraba lakini kwa mahaba ya kuku
Tutakula mpaka panya buku chukuchuku
Dukuduku, OSS, aliye juu mpandie, usimngoje hukuhuku
Chai kwa pipi, sukari kiki
Elimu bure vipi huku redio unafungia?
Misukule pipi wenzio unatuungia?
Idi Amin asiye makini, nyama la baharini
Majina manne ubini, diva kwini, kingi wa magirini
Pol Pot, Ze Comedy Joti, baba mkusanya noti
Gusa shoti, samasoti, mwendo wa speedboti
Baba bwabwaja, jinga la haja, baja kaja
Paji kaa paja, Opobo Jaja, Black Maharajjah
Bwabwa kiporo, watu kihoro, limelala doro
Chini godoro, Dar mpaka Moro, twapitia Muhoro?
Serikali kali, bila uhalali, kwa mtaji wa shari
Hii manuwari, itenda muhali, vipi hadi dahari?
Chama mrama, ndama kapama, maziwa yahama
Hili drama la karma kama Obama na Osama
Nimeipenda hii
 
Hizi habari za uchochezi mimi sizielewi kabisa.

Hao watu wanaotuhumiwa sijui kuchochea, wamechochea kitu gani?

Kumpindua Magufuli?

Huyu jamaa asipoangalia anaweza kutumia muda wake mwingi kupambana na watu wenye maoni na hisia ambazo zipo kinyume na atakavyo au apendavyo yeye.

Katika viongozi ambao Tanzania imewahi kuwa nao tokea tuanze kutawaliwa na CCM huyu jamaa atakuwa anaongoza kwa kutokuwa na busara wala hekima.

Hovyo kabisa!

Sitashangaa JF nayo ikifungiwa kwa kupromoti uchochezi wa akina Ngabu😉.

Nakuelewa sana Nyani.

Binafsi nampenda na kumuheshimu binadamu asiyeogopa kuelezea hisia zake juu ya jambo fulani hata kama ni haki yake kisa tu anawaogopa watu flani.

Ndio maana hata kati ya wabunge wote wa ccm waliopo, Musukuma is my fovorite kwa sababu anasimamia anachokiamini na kukisema bila kugopa mtu.

Kuhusu huyu mheshimiwa mtukufu malaika mkuu tulienae, anachofanya ni kutumia intimidation kuwatawala kwanzia hao wasaidizi wake kiasi kwamba hata wao wenyewe sasa wanazitafsri kauli zake kwa namna itakayompendeza yeye.

Nna huakika wengi wao zaidi ya 90% akiwemo mkuu mwenyewe, ukiwauliza haya maneno ya mtandaoni yanachochea vipi uvunjifu wa amani hawawezi kutoa majibu sahihi.
 
Anaweza akawa Rais wa awamu moja.

Watu kama akina January usione wapo kimya, waswahili wanasema ukiona Kobe kainama ujue anatunga Sheria.

Miezi 10 madarakani, kaharibu kila kitu. Wananchi, Wanasiasa, Wafanyabiashara hata Watumishi hawana amani na huyu jamaa!!
Akiendelea kufanya "anachofanya" vizuri ataendelea na kuwa wa maisha kama mu7, PK na RM. Wengine haya tuliyajua mapema tukaonya lakini tuliambulia kuitwa watetezi wa mafisadi.

Nani anaisoma namba? Wote kabisa!!
 
Guys we have to be patient, presidaa yashamuwia magumu ndio maana anasema tumwombee.Tuweni watulivu tu pengine mabo yatanyooka ingawa sina uhakika.
Bora uendelee kutokuwa na uhakika hivyo hivyo, kuliko kujipa moyo.
 
Hizi habari za uchochezi mimi sizielewi kabisa.

Hao watu wanaotuhumiwa sijui kuchochea, wamechochea kitu gani?

Kumpindua Magufuli?

Huyu jamaa asipoangalia anaweza kutumia muda wake mwingi kupambana na watu wenye maoni na hisia ambazo zipo kinyume na atakavyo au apendavyo yeye.

Katika viongozi ambao Tanzania imewahi kuwa nao tokea tuanze kutawaliwa na CCM huyu jamaa atakuwa anaongoza kwa kutokuwa na busara wala hekima.

Hovyo kabisa!

Sitashangaa JF nayo ikifungiwa kwa kupromoti uchochezi wa akina Ngabu😉.
I can assure you...so muda mrefu jf itapigwa pini
 
Taifa ninajenga watu wa kujipendekeza na wanafiki....ukimsikiliza AG unaweza sema afadhalo ya mwenyekiti wa mtaa
Alooo.... kwa nilivyo mskia akiongea hata Makonda ana nafuu.
 
Tanzania ambayo Africa nzima tuliheshimika tumegeuka mara hii kuwa kichekesho. Nchi inaendeshwa na matamko ya viongozi tu. Taratibu za kila siku zimeshindikana. Jamani huyu mtu hana watoto wa kumwambia. Tafadhali wasanii wamtungie wimbo kama ule wa "Riziwan ongea na mshua......."
 
Jaman naombeni maana ya neno uchochez na kwenye katiba yetu wapi limetamkwa? Na kwa mantiki ipi?

Na je sasahivi hairuhusiwi kujadilinia chochote kuhusu siasa unaitwa mchochezi
 
"Magufuli is the real deal" , per PLO Lumumba. [I only know of one Real Deal and that's Evander Holyfiled - 5 time heavyweight champion of the world]

That was some 8 or 9 months ago.

Akiba ya maneno jamani...akiba ya maneno!

Hahaaa...hivi huyu PLO Lumumba leo hii bado ataweza kusema hayo maneno kweli?

Magufuli is the real deal? Really?

Angalia video kwenye dakika ya 1:20.

 
Back
Top Bottom