Eneo kubwa la Pori la Jeshi kuanzia Nzuguni mpaka Mji wa Serikali Dodoma, kunaharibu mandhari ya Jiji la Dodoma

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,035
144,387
Kwa wanaoifahamu Dodoma, bila shaka watakuwa wanaelewa eneo hilo la Jeshi ambalo ni pori kubwa na sasa linageuka pori katika ya Jiji la Dodoma baada ya mji huu kuendelezwa kama Makao Makuu ya Nchi.

Kwa sasa, eneo hilo la Jeshi, linakuwa pori linalotenganisha makazi ya watu baada ya viwanja kupimwa kuzunguka eneo hili na pia linatenganisha eneo ambalo uwanja mkubwa wa mpira umepanga kujengwa.

Iwapo huo uwanja utajengwa, na watu wakaendeleza viwanja vilivyo jirani/ vinavyozunguka pori hili, basi hili pori linakwenda kuharibu madhara ya mji huu wa Dodoma .

Tukumbuke ni katika eneo hilo la jirani na hili pori, mji wa serikali ndio unaendelezwa mita chache kutoka yale magorofa ya Jeshi pale Ihumwa na ukienda mbele kilomita chache unasogelea iipo Ikulu ya Chamwino (Ukanda mmoja).

Kwahiyo huko baadae, mtu utakapokuwa unaingia katika jijil la Dodoma kutokea Morogoro/Dar-es-Salaam, utaanza kukutana na nyumba au majumba mazuri ya makazi ya watu na majumba ya serikali kisha unakutana na pori kubwa ambalo ni eneo la Jeshi halafu mita chache unakutana na uwanja mkubwa na wa kisasa wa mpira(iwapo utajengwa).Sasa vita picha ya huo muonekano wa pori katika hayo mazingira.

Binafsi nashauri Jeshi wakabidhi hilo eneo kwa serikali kwa maana ya Manispaa ya Dodoma ili eneo hilo libadilishiwe matumizi na Jeshi litengewe eneo lingine ambalo litakuwa mbali na makazi ya watu. Faida nyingine ya kuhamisha eneo hili la Jeshi mbali na makazi ya watu itakuwa ni kuondoa hatari ya watu kukaa karibu na makambi/maeneo ya Jeshi (tukumbuke mabomu ya Mbagala na athari zake).

Kwa mtazamo wangu, matumizi bora kwa eneo hili itakuwa ni kupima viwanja kwa ajili ya ujenzi wa makazi ya watu au kutenga eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa majumba ya kibiashara kama vile shopping malls,n.k.Pia sehemu ya eneo hilo wanaweza kupewa National Housing wajenge magorofa na baadae wayapangishe au wayauze.

Sioni logic ya kuzuia wananchi kulima mazao marefu kama mahindi katika ya miji/majiji, halafu tukaruhusu mapori/vichaka katika ya Jiji kisa tu malori hayo yanamilikiwa na Jeshi unless Jeshi litaendeleza hayo maeneo na si vinginevyo.
 
Kuna JW & Police
Ina Pori Ni Kubwa Sana Na Sura Ya Jiji Haivutii
Ngoja Viongozi Wamalize Kuchanjwa Johnson And Johnson
 
Mkuu ungesindikizia na picha.
11-december-2010-riwoto-eastern-equatoria-south-sudan-aerial-view-of-riwoto-eastern-equatoria-...jpg
 
Mkuu New York marekani katikaki ya mji kuna msitu hadi vicheche wapo panaitwa central park so sio kitu kibaya usifanye kila kitu kikawa siasa huo msitu haupo kwa bahati mbaya
 
Mkuu sio kwamba napingana na wewe kuhusu kuhamisha Jeshi, lakini napingana na wewe kwenye kuondoa eneo hilo la pori.Ujenzi wa majiji ya kisasa duniani unahitaji kuwa na maeneo kama hayo kwa sababu za kuregulate hali ya hewa.

Majiji kama Delhi na singapor nimetaja kwa uchache yana mapori katikati na bado yanamvuto, kujaza majumba na maghorofa kila sehemu kunasababisha hali ya joto na hivyo kulazimisha matumizi makubwa ya nishati.

Kinachohitajika ni kuwa na miundombinu bora.
 
Mkuu sio kwamba napingana na wewe kuhusu kuhamisha Jeshi, lakini napingana na wewe kwenye kuondoa eneo hilo la pori.Ujenzi wa majiji ya kisasa duniani unahitaji kuwa na maeneo kama hayo kwa sababu za kuregulate hali ya hewa.

Majiji kama Delhi na singapor nimetaja kwa uchache yana mapori katikati na bado yanamvuto, kujaza majumba na maghorofa kila sehemu kunasababisha hali ya joto na hivyo kulazimisha matumizi makubwa ya nishati.

Kinachohitajika ni kuwa na miundombinu bora.
Hayo maeneo ni vichaka na mapori mafupi mafupi yanayokera machoni.
 
Ombi lako limefika mahali penyewe. Ngoja niwasiliane kwanza na Kamanda Mamboshasha. Na yeye yupo Dodoma. Anaweza kitusaidia kitu.
 
Kwa wanaoifahamu Dodoma, bila shaka watakuwa wanaelewa eneo hilo la Jeshi ambalo ni pori kubwa na sasa linageuka pori katika ya Jiji la Dodoma baada ya mji huu kuendelezwa kama Makao Makuu ya Nchi.

Kwa sasa, eneo hilo la Jeshi, linakuwa pori linalotenganisha makazi ya watu baada ya viwanja kupimwa kuzunguka eneo hili na pia linatenganisha eneo ambalo uwanja mkubwa wa mpira umepanga kujengwa.

Iwapo huo uwanja utajengwa, na watu wakaendeleza viwanja vilivyo jirani/ vinavyozunguka pori hili, basi hili pori linakwenda kuharibu madhara ya mji huu wa Dodoma .

Tukumbuke ni katika eneo hilo la jirani na hili pori, mji wa serikali ndio unaendelezwa mita chache kutoka yale magorofa ya Jeshi pale Ihumwa na ukienda mbele kilomita chache unasogelea iipo Ikulu ya Chamwino (Ukanda mmoja).

Kwahiyo huko baadae, mtu utakapokuwa unaingia katika jijil la Dodoma kutokea Morogoro/Dar-es-Salaam, utaanza kukutana na nyumba au majumba mazuri ya makazi ya watu na majumba ya serikali kisha unakutana na pori kubwa ambalo ni eneo la Jeshi halafu mita chache unakutana na uwanja mkubwa na wa kisasa wa mpira(iwapo utajengwa).Sasa vita picha ya huo muonekano wa pori katika hayo mazingira.

Binafsi nashauri Jeshi wakabidhi hilo eneo kwa serikali kwa maana ya Manispaa ya Dodoma ili eneo hilo libadilishiwe matumizi na Jeshi litengewe eneo lingine ambalo litakuwa mbali na makazi ya watu. Faida nyingine ya kuhamisha eneo hili la Jeshi mbali na makazi ya watu itakuwa ni kuondoa hatari ya watu kukaa karibu na makambi/maeneo ya Jeshi (tukumbuke mabomu ya Mbagala na athari zake).

Kwa mtazamo wangu, matumizi bora kwa eneo hili itakuwa ni kupima viwanja kwa ajili ya ujenzi wa makazi ya watu au kutenga eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa majumba ya kibiashara kama vile shopping malls,n.k.Pia sehemu ya eneo hilo wanaweza kupewa National Housing wajenge magorofa na baadae wayapangishe au wayauze.

Sioni logic ya kuzuia wananchi kulima mazao marefu kama mahindi katika ya miji/majiji, halafu tukaruhusu mapori/vichaka katika ya Jiji kisa tu malori hayo yanamilikiwa na Jeshi unless Jeshi litaendeleza hayo maeneo na si vinginevyo.
Weka sehemu ya kupumzika watu kama pale Nairobi kuwa uwanja mkubwa watu wakichoka kutembea wanakwenda kupumzika. Sijaona mjii wo owte Tanzania unaojali wananchi kuwa na sehemu ya kupumzika
 
Back
Top Bottom