Uchunguzi wangu wa awali kuhusu mgodi wa siri uliopo ndani ya pori la hifadhi Singida-Tabora

Mdude_Nyagali

Member
Dec 11, 2022
60
1,237
Watanzania wenzangu mtakumbuka kwamba 4 March 2024 niliripoti kuhusu uwepo wa mgodi wa siri huko Singida - Tabora baada ya kupewa taarifa na mmoja wa wachimbaji wadogo.

Timu yangu ilifanikiwa kufika eneo hilo kwa lengo la kujiridhisha. Baada ya kufika eneo la tukio ikawa ngumu timu yetu kuingia kwenye huo mgodi baada ya kugundua kwamba mgodi huo uko ndani ya pori la Kizigo Game Reserve lililoko mkoani Singida na hakuna njia wala barabara inayoweza kukupeleka ndani ya mgodi huo. Na pori hilo hilo linalindwa na askari wanaohusika kulinda mapori na hifadhi za taifa.

Kutokana na mazingira hayo timu yetu ililazimika kutumia technology ambayo ilisaidia kujua mambo yafuatayo.

1. Ni kweli mgodi huo uko ndani ya hifadhi au pori la Kizigo Game Reserve lililopo Singida na linaingia mpaka Tabora.

2. Ni kweli kwamba karibu na mgodi huo kuna uwanja wa ndege (airstrip) kilomita 1.3 kama ambavyo technology imetuonyesha pamoja na picha za uwanja huo.

3. Kwa muda ambao timu yetu iliweka kambi ya wiki moja ndege ilitua na kuondoa mara 2. Kwa hiyo kwa wiki ndege hutua na kuondoka mara mbili kwa ajili ya kushusha na kubeba mizigo.

4. Tumejiridhisha kwamba Kizigo Game Reserve pia inapakana na hifadhi zingine mbili Muhesi Game Reserve na Rungwa Game Reserve.

5. Kuna njia zinatoka kwenye huu uwanja wa ndege kwenda kwenye hayo hizo hifadhi za jirani nilizozitaja hapo juu. Hii inaashiria kuwa kuna biashara nyingine haramu ya kusafirisha wanyama Wildlife trafficking katika eneo hilo. Ndio maana kuna njia za kuingia kwenye mapori mengine ya hifadhi katika eneo hilo.

6. Kuna nyumba zimejengwa umbali wa mita 800 kutoka katika uwanja huo wa ndege.

7. Hakuna barabara yoyote inayoingia katika mgodi huo isipokuwa huo uwanja wa ndege ambao sijui kama unatambulika rasmi.

Katika mazingira tuna mashaka kwamba serikali au viongozi wa serikali binafsi wanaweza kuwa wanahusika na biashara haramu zinazoendelea katika eneo hilo. Kwa sababu hizo Game Reserve zina askari wanaozilinda muda wote hivyo ni ngumu serikali kutokujua uwepo wa mgodi huo.

Bado timu yangu inaendelea na uchunguzi ili kupata picha clear lakini na wamiliki wa biashara haramu ndani ya msitu huo pamoja na washirika wake. Tutajua tu kama biashara hiyo wameuziwa wazungu au waarabu na wahusika wenye mamlaka ya kuuza au kukodisha eneo ndani ya nchi.

Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
IMG-20240325-WA0007.jpg
IMG-20240325-WA0004.jpg
 
๐—จ๐—ฐ๐—ต๐˜‚๐—ป๐—ด๐˜‚๐˜‡๐—ถ ๐˜„๐—ฎ๐—ป๐—ด๐˜‚ ๐˜„๐—ฎ ๐—ฎ๐˜„๐—ฎ๐—น๐—ถ ๐—ธ๐˜‚๐—ต๐˜‚๐˜€๐˜‚ ๐—บ๐—ด๐—ผ๐—ฑ๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐˜€๐—ถ๐—ฟ๐—ถ ๐˜‚๐—น๐—ถ๐—ผ๐—ฝ๐—ผ ๐—ป๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐—ฝ๐—ผ๐—ฟ๐—ถ ๐—น๐—ฎ ๐—ต๐—ถ๐—ณ๐—ฎ๐—ฑ๐—ต๐—ถ ๐—ต๐˜‚๐—ธ๐—ผ ๐—ง๐—ฎ๐—ฏ๐—ผ๐—ฟ๐—ฎ-๐—ฆ๐—ถ๐—ป๐—ด๐—ถ๐—ฑ๐—ฎ.

Watanzania wenzangu mtakumbuka kwamba 4 March 2024 niliripoti kuhusu uwepo wa mgodi wa siri huko Singida - Tabora baada ya kupewa taarifa na mmoja wa wachimbaji wadogo.

Timu yangu ilifanikiwa kufika eneo hilo kwa lengo la kujiridhisha. Baada ya kufika eneo la tukio ikawa ngumu timu yetu kuingia kwenye huo mgodi baada ya kugundua kwamba mgodi huo uko ndani ya pori la Kizigo Game Reserve lililoko mkoani Singida na hakuna njia wala barabara inayoweza kukupeleka ndani ya mgodi huo. Na pori hilo hilo linalindwa na askari wanaohusika kulinda mapori na hifadhi za taifa.

Kutokana na mazingira hayo timu yetu ililazimika kutumia technology ambayo ilisaidia kujua mambo yafuatayo.

1. Ni kweli mgodi huo uko ndani ya hifadhi au pori la Kizigo Game Reserve lililopo Singida na linaingia mpaka Tabora.

2. Ni kweli kwamba karibu na mgodi huo kuna uwanja wa ndege (airstrip) kilomita 1.3 kama ambavyo technology imetuonyesha pamoja na picha za uwanja huo.

3. Kwa muda ambao timu yetu iliweka kambi ya wiki moja ndege ilitua na kuondoa mara 2. Kwa hiyo kwa wiki ndege hutua na kuondoka mara mbili kwa ajili ya kushusha na kubeba mizigo.

4. Tumejiridhisha kwamba Kizigo Game Reserve pia inapakana na hifadhi zingine mbili Muhesi Game Reserve na Rungwa Game Reserve.

5. Kuna njia zinatoka kwenye huu uwanja wa ndege kwenda kwenye hayo hizo hifadhi za jirani nilizozitaja hapo juu. Hii inaashiria kuwa kuna biashara nyingine haramu ya kusafirisha wanyama Wildlife trafficking katika eneo hilo. Ndio maana kuna njia za kuingia kwenye mapori mengine ya hifadhi katika eneo hilo.

6. Kuna nyumba zimejengwa umbali wa mita 800 kutoka katika uwanja huo wa ndege.

7. Hakuna barabara yoyote inayoingia katika mgodi huo isipokuwa huo uwanja wa ndege ambao sijui kama unatambulika rasmi.

Katika mazingira tuna mashaka kwamba serikali au viongozi wa serikali binafsi wanaweza kuwa wanahusika na biashara haramu zinazoendelea katika eneo hilo. Kwa sababu hizo Game Reserve zina askari wanaozilinda muda wote hivyo ni ngumu serikali kutokujua uwepo wa mgodi huo.

Bado timu yangu inaendelea na uchunguzi ili kupata picha clear lakini na wamiliki wa biashara haramu ndani ya msitu huo pamoja na washirika wake. Tutajua tu kama biashara hiyo wameuziwa wazungu au waarabu na wahusika wenye mamlaka ya kuuza au kukodisha eneo ndani ya nchi.

Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
#@ moderator msifute huu uzi naona siku hizi mnatumika nyie#
 

Attachments

  • FB_IMG_1711605931766.jpg
    FB_IMG_1711605931766.jpg
    64.7 KB · Views: 2
huu uchunguzi hautoshi
nafikiri ukae kama tetesi na wahusika waje na majibu

kwa Tanzania hili linawezekana maana hii nchi watu huiendesha wanavyo taka na sisi tupo kama makondoo tu

utashangaa badala wafanye uchunguzi waje na majibu, watamchukia mtoa bandiko na kuanza kumuwinda
 
๐—จ๐—ฐ๐—ต๐˜‚๐—ป๐—ด๐˜‚๐˜‡๐—ถ ๐˜„๐—ฎ๐—ป๐—ด๐˜‚ ๐˜„๐—ฎ ๐—ฎ๐˜„๐—ฎ๐—น๐—ถ ๐—ธ๐˜‚๐—ต๐˜‚๐˜€๐˜‚ ๐—บ๐—ด๐—ผ๐—ฑ๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐˜€๐—ถ๐—ฟ๐—ถ ๐˜‚๐—น๐—ถ๐—ผ๐—ฝ๐—ผ ๐—ป๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐—ฝ๐—ผ๐—ฟ๐—ถ ๐—น๐—ฎ ๐—ต๐—ถ๐—ณ๐—ฎ๐—ฑ๐—ต๐—ถ ๐—ต๐˜‚๐—ธ๐—ผ ๐—ง๐—ฎ๐—ฏ๐—ผ๐—ฟ๐—ฎ-๐—ฆ๐—ถ๐—ป๐—ด๐—ถ๐—ฑ๐—ฎ.
Tatizo nini?
 
Mdude_Nyagali waovu na wala nchi watakusaka Weeknd hii wakukamate kwa kuandika hii habari,wataanza na kusaka drone iliyotumika na kukutaka utoe kibali Cha lurusha drone hiyo.

Tulivyo na Taifa la kishenzi,hawatodili na kuhoji waziri wa Ardhi ama kamishina wa madini mkoa husika. Jiandae wasiharibu pasaka yako
 
Back
Top Bottom