Dr.Slaa: Zitto anaweza kufukuzwa kabisa

Dr.Slaa: Zitto anaweza kufukuzwa kabisa

Status
Not open for further replies.
Hivi Ritz ndani ya CCM una bifu na Kamati Kuu ya CCM, unaenda Kigoma kufanya Mkutano Mabango yana wadhalilisha viongozi wa CCM na mabango yote hayana bendera ya CCM bali ya Taifa (Ila huna cheo chochote serikalini cha kukupa status ya kututumia bendera ya Taifa) na unasema unaipenda CCM sana ila unapambana dhidi ya uhafidhina ndani ya CCM, na isitoshe unadai wewe utakuwa wa mwisho kutoka CCM kwa hiyari yako siyo kufukuzwa, hivi CCM hii unayoijua wewe unadhani itakufanyaje?????


you wont get honest answer from this individual....there members of CCM who can reason but not him and the team
 
Tangu ameanza kuhutubia kanda ya Huko Magharibi, ni mikakati gani ameongelea ya Kuunda serikali makini,kuongeza pato la taifa,kuongoza kwa sheria na kanuni, kudhibiti uvunjifu wa amani, kuwaunganisha watanzania, kuwezesha pato la mmoja mmoja!? Kutwa ni kupambana tu, kupambana tu,kuandamana,kusaka wahaini na wasaliti ndani ya chama! Kubaini wanaohujumu chadema! Ha ha ha!

Huwezi kufanya hayo yote huku unaishi na nyoka mwenye sumu kali chumbani mwako na muda wowote ukicheza anakuua.tutawasaka nyoka wote na kuwaua huku programu za chama kama CDM NI MSINGI NA ILE YA M4C ZIKIENDELEA!
 
Na afukuzwe tu

attachment.php
 
Huyo Zitto amejulikana akiwa Chadema...alipewa fursa ,nashangaa leo kusikia ni maarufu kushinda taasisi iliyomfanya maarufu.

Chadema fanyeni zikao vyenu ...mmutimue kwa kura this dude is cancer ..kura zisipotosha ABORT the mission excute VETO clean the mess.Dont make a mess in the name of democracy UN kuna kura za VETO is that democracy?
 
Ha ha ha kwani anahusika na hiyo petition? Haha woga mwingine huo. Zitto is a decent.

Nani asiyejua kuwa yeye ndiye mfadhili wa lile kundi la masalia pm7? na ndilo amekuwa akilitumia kurubuni watu na kutoa matamko ya kisheenz dhidi ya chama.SIKU ZAKE CDM KAZIFUPISHA MWENYEWE KWA UJINGA WAKE.
 
Wadau, nimejaribu kufuatilia matukio ya hivi karibuni na coverage yake ninaona kama sisi tuliokuwa wagumu kuamini kama ZZK anatumiwa na mahasimu wa CHADEMA, kuanza sasa kuamini kuwa ni kweli huyu bwana anatumiwa.

Matukio ya kupigiwa chapuo kwa nguvu na wana CCM, na kupata corerage kuubwa kwa msaada wa wana CCM, inatupa wasiwasi sisi matomaso na kupata majibu dhahili kuwa sasa tunaona ZZK akiwa upande wa pili na akitumiwa kweli kuiangamiza CHADEMA, Tumeona coverage ya Star TV, na redio pamoja na magazeti kadhaa ambayo kwa kawaida ni vyombo vya habari hasimu kwa CHADEMA, sasa dhahili vikimuunga mkono na kutoa coverage ya bure, kama ni bure kweli, kwa ZZK and company, kweli sasa tumeanza kufunguka macho na kuona jinsi bwana Zitto alivyo na mpango mkakati wa kuiangamiza CHADEMA.

Maandamano na mikutano ambayo asilimia 90 ni wana CCM wa mkoa especially wa Kigoma yanatia wasiwasi, je Zitto hajui kuwa wanachama wa CCM ndio wana mbackup? Kama anajua lengo lake ni nini? Je anadumisha chama au anasambaratisha chama?

Kwa viongozi wa CHADEMA mikoani na mawilayani, ninajua wengi wenu mtakuwa mmepata pesa japo kidoogo kutoka kwa wale waendesha mpango wa ondoa CHADEMA, Mwigulu and the likes, lakini jueni tuu, mambo ya usaliti mwisho wake daima sio mzuri! Tunajua baadhi ya misemo ya viongozi wa juu wa CHADEMA ni kula CCM kura CHADEMA, hebu changanyeni akili na mle tuu CCM, kama wakiwaletea vijihela vyao, lakini roho ya uasi muachane nayo kabisa, ZZK you are a backslider, slide back and come into your senses common!

Maajabu, thread plus vitu vingi tuu, wawakilishi wakuu ni wana CCM, Tunaona mtu kama Mohamed Mwaupete, Hamm-d, Mwampamba, Machange, Ifweero na wengine wa design hiyo ndio haswa wanaopata habari za kina toka kwa zitto, kwanini? Je organizers wa mikutano ya Zitto ni wana CHADEMA? Hebu jiulizeni ndugu, kama ni wanaCCM ni kwanini? Au ni kwa sababu Zitto ni mzalendo, kweli inaweza ikawa ni hivyo?

Sasa kwa kamati kuu, kosa kubwa mnalolifanya ni kuacha hili jambo lidumu kwa muda mrefu, hebu fanyeni mambo kwa haraka na yaishe kuliko kukaa hivi huku adui akitekeleza mambo yake kwa umakini, mnatakiwa musurprise msisubili surprise! Fanyeni haraka , kama ni kumfukuza mtuhumiwa on which naona ndio best option fanyeni hivyo, na kama ni msamaha kama mtaweza fanyeni hivyo, kukaa kwenu kimya mnakiangamiza chama! Mnakumbuka ya NCCR Tanga? Mkutano wenu unaweza ukatibiliwa na Mayuda watakaowasaliti kwa tamaa za hela hivyo utabiri wa Sheik Wassira kuwa chama kitasambaratika kabla ya 2013 ukawa kweli!

Nawasilisha!
 
Wadau, nimejaribu kufuatilia matukio ya hivi karibuni na coverage yake ninaona kama sisi tuliokuwa wagumu kuamini kama ZZK anatumiwa na mahasimu wa CHADEMA, kuanza sasa kuamini kuwa ni kweli huyu bwana anatumiwa.

Matukio ya kupigiwa chapuo kwa nguvu na wana CCM, na kupata corerage kuubwa kwa msaada wa wana CCM, inatupa wasiwasi sisi matomaso na kupata majibu dhahili kuwa sasa tunaona ZZK akiwa upande wa pili na akitumiwa kweli kuiangamiza CHADEMA, Tumeona coverage ya Star TV, na redio pamoja na magazeti kadhaa ambayo kwa kawaida ni vyombo vya habari hasimu kwa CHADEMA, sasa dhahili vikimuunga mkono na kutoa coverage ya bure, kama ni bure kweli, kwa ZZK and company, kweli sasa tumeanza kufunguka macho na kuona jinsi bwana Zitto alivyo na mpango mkakati wa kuiangamiza CHADEMA.

Maandamano na mikutano ambayo asilimia 90 ni wana CCM wa mkoa especially wa Kigoma yanatia wasiwasi, je Zitto hajui kuwa wanachama wa CCM ndio wana mbackup? Kama anajua lengo lake ni nini? Je anadumisha chama au anasambaratisha chama?

Kwa viongozi wa CHADEMA mikoani na mawilayani, ninajua wengi wenu mtakuwa mmepata pesa japo kidoogo kutoka kwa wale waendesha mpango wa ondoa CHADEMA, Mwigulu and the likes, lakini jueni tuu, mambo ya usaliti mwisho wake daima sio mzuri! Tunajua baadhi ya misemo ya viongozi wa juu wa CHADEMA ni kula CCM kura CHADEMA, hebu changanyeni akili na mle tuu CCM, kama wakiwaletea vijihela vyao, lakini roho ya uasi muachane nayo kabisa, ZZK you are a backslider, slide back and come into your senses common!

Maajabu, thread plus vitu vingi tuu, wawakilishi wakuu ni wana CCM, Tunaona mtu kama Mohamed Mwaupete, Hamm-d, Mwampamba, Machange, Ifweero na wengine wa design hiyo ndio haswa wanaopata habari za kina toka kwa zitto, kwanini? Je organizers wa mikutano ya Zitto ni wana CHADEMA? Hebu jiulizeni ndugu, kama ni wanaCCM ni kwanini? Au ni kwa sababu Zitto ni mzalendo, kweli inaweza ikawa ni hivyo?

Sasa kwa kamati kuu, kosa kubwa mnalolifanya ni kuacha hili jambo lidumu kwa muda mrefu, hebu fanyeni mambo kwa haraka na yaishe kuliko kukaa hivi huku adui akitekeleza mambo yake kwa umakini, mnatakiwa musurprise msisubili surprise! Fanyeni haraka , kama ni kumfukuza mtuhumiwa on which naona ndio best option fanyeni hivyo, na kama ni msamaha kama mtaweza fanyeni hivyo, kukaa kwenu kimya mnakiangamiza chama! Mnakumbuka ya NCCR Tanga? Mkutano wenu unaweza ukatibiliwa na Mayuda watakaowasaliti kwa tamaa za hela hivyo utabiri wa Sheik Wassira kuwa chama kitasambaratika kabla ya 2013 ukawa kweli!

Nawasilisha!

Kinachokusumbua ni wivu, tunasema kwamba ZZK anamvuto na watu wengi achilia vyama, kule kigoma wanaomshabikia kwa taarifa yako wapo wa cdm wengi na vyama vingine pia. zzk msimfukuze angalieni jinsi ya kuhandle maadam ameshajulikana kwamba anatumiwa jambo ambalo hakuna mwenye uhakika kama upo weka hadharani tuuone. Zzk ni kifaa, ameijenga cdm na yy amesema kuna jasho lake hivyo hawezi kuondoa ingawa naona anatangaziwa kuondolewa
 
Zitto ni kiongozi mzuri kwa kuwa si mwoga. Ila haaminiki katika kila anachokipigania. Ni mtu wa kupenda kusimamisha ufalme wake yeye mwenyewe na si mtu wa kusimamisha ufalme wa wengi. Sifa za nelson mandela zitto kamwe hawezi kuwa nazo, na sifa za zitto nelson mandela anaweza kuwa nayo moja ya kutokuwa mwoga lakini hawezi kuwa nazo zingine; nadhani hapa nitakuwa nimeweka vizuri.
 
Kinachokusumbua ni wivu, tunasema kwamba ZZK anamvuto na watu wengi achilia vyama, kule kigoma wanaomshabikia kwa taarifa yako wapo wa cdm wengi na vyama vingine pia. zzk msimfukuze angalieni jinsi ya kuhandle maadam ameshajulikana kwamba anatumiwa jambo ambalo hakuna mwenye uhakika kama upo weka hadharani tuuone. Zzk ni kifaa, ameijenga cdm na yy amesema kuna jasho lake hivyo hawezi kuondoa ingawa naona anatangaziwa kuondolewa

JK pia alikuwa na mvuto back in 2005!
 
Kinachokusumbua ni wivu, tunasema kwamba ZZK anamvuto na watu wengi achilia vyama, kule kigoma wanaomshabikia kwa taarifa yako wapo wa cdm wengi na vyama vingine pia. zzk msimfukuze angalieni jinsi ya kuhandle maadam ameshajulikana kwamba anatumiwa jambo ambalo hakuna mwenye uhakika kama upo weka hadharani tuuone. Zzk ni kifaa, ameijenga cdm na yy amesema kuna jasho lake hivyo hawezi kuondoa ingawa naona anatangaziwa kuondolewa

Mkuu mimi sina wivu, wala si mwana siasa, circumstantial evidence zina muumbua Zitto, why coverage Star TV bure? Au ana mvuto saana? Au ni tool ya kukiangamiza chama chake? Kwa kigoma watu wenye upeo waliopo huko wanatujuvya kuwa maCCM woote karibu walikuwepo kumpokea ZItto, na wa vyama vingine ambao kimsingi walitaka kujau huyu bwana atasema nini, lakini wana CCM motive yao ilikuwa tofauti, no research no right to speak mkuu, fanay utafiti utajua! ZZK ana tuonyesha sisi matomaso dhahili jinsi alivyo patwa na roho ya usaliti zaidi ya ile ya YUDA!
 
Zitto ni kiongozi mzuri kwa kuwa si mwoga. Ila haaminiki katika kila anachokipigania. Ni mtu wa kupenda kusimamisha ufalme wake yeye mwenyewe na si mtu wa kusimamisha ufalme wa wengi. Sifa za nelson mandela zitto kamwe hawezi kuwa nazo, na sifa za zitto nelson mandela anaweza kuwa nayo moja ya kutokuwa mwoga lakini hawezi kuwa nazo zingine; nadhani hapa nitakuwa nimeweka vizuri.

Uepetia mkuu, Zitto kakosa uvulilivu na Mikakati, hajui wapi kufanya nini? muda gani? niseme nini? Tumeona wakosoaji wake humu siku nyiingi, si katika sakata hili tuuu, ni mbinafsi kupita kiasi, poor quality for a leader!
 
Kinachokusumbua ni wivu, tunasema kwamba ZZK anamvuto na watu wengi achilia vyama, kule kigoma wanaomshabikia kwa taarifa yako wapo wa cdm wengi na vyama vingine pia. zzk msimfukuze angalieni jinsi ya kuhandle maadam ameshajulikana kwamba anatumiwa jambo ambalo hakuna mwenye uhakika kama upo weka hadharani tuuone. Zzk ni kifaa, ameijenga cdm na yy amesema kuna jasho lake hivyo hawezi kuondoa ingawa naona anatangaziwa kuondolewa

Zitto alishajifukuza kabla ya kufukuzwa.Ndiyo maana kwenye mikutano yake hapeperushi bendera ya CHADEMA mikutano anayofanya ni ya kivyake vyake tu wala haina baraka za chama.Wanao mfuata ni wale wanaohadaika na hadaa za Zitto anazo sema kuwa bado niko CHADEMA nitakuwa wa mwisho kutoka CHADEMA nina pigania demokrasia ya kweli nina jasho langu ndani ya CHADEMA anajifanya kuwa na uchungu hata kuwazidi waasisi wa chama aliowakuta kumbe ndiye muuaji mkubwa.Yalele ya kina Shonza mimi bado ni makamu mwenyekiti wa BAVICHA wakati alishafukuzwa siku nyingi kumbe zilikuwa ni gia za kutimukia magambani.Zitto ana pima upepo ili ajue ataungwa mkono kiasi gani atakapotimukia huko aendako.Ukweli ni kwamba Zitto yuko CHADEMA kimwili kiakili na kiroho hayuko CHADEMA ndiyo maana hawezi kujisahihi hata anapo ambiwa na wenzake kuwa amekosea.
 
Jembe Zitto atamkonfsha Slaa, Mbowe na vibaraka wao.

Dr Slaa na Mbowe wanafanya kazi ya kukipalilia chama ili kisitawi hawawezi wakafanana na jembe Zitto anae chimba kaburi ili kukizika chama.
 
mkuu sijaelewa hapa kabisa, kwa maana yeye ndo alfa na omega katika kamati kuu na baraza kuu?
Maana ninachojua ni kuwa hivyo vyombo ndo vyenye maamuzi ya mwisho.
Anyway tusuburi tuone hiyo nguvu yake.

Katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Dr.Wilbroad Slaa amesema Zitto anaweza kufukuzwa kabisa na amewaonya wafuasi wake waache kutumika kwa kusainishwa document fake, "nawaonya mnaomshauri mnaweza kumpoteza huyu kijana", alisema Dr.Slaa.

Pia, Dr.Slaa amesema yeye kama katibu mkuu hajatoa form zozote zinazodaiwa kuoka makao makuu ambazo zinasambazwa ili zisainiwe.

Dr. Slaa katoa kauli hiyo leo mkoani Tabora wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara.

CHANZO:ITV
 
Zitto alishajifukuza kabla ya kufukuzwa.Ndiyo maana kwenye mikutano yake hapeperushi bendera ya CHADEMA mikutano anayofanya ni ya kivyake vyake tu wala haina baraka za chama.Wanao mfuata ni wale wanaohadaika na hadaa za Zitto anazo sema kuwa bado niko CHADEMA nitakuwa wa mwisho kutoka CHADEMA nina pigania demokrasia ya kweli nina jasho langu ndani ya CHADEMA anajifanya kuwa na uchungu hata kuwazidi waasisi wa chama aliowakuta kumbe ndiye muuaji mkubwa.Yalele ya kina Shonza mimi bado ni makamu mwenyekiti wa BAVICHA wakati alishafukuzwa siku nyingi kumbe zilikuwa ni gia za kutimukia magambani.Zitto ana pima upepo ili ajue ataungwa mkono kiasi gani atakapotimukia huko aendako.Ukweli ni kwamba Zitto yuko CHADEMA kimwili kiakili na kiroho hayuko CHADEMA ndiyo maana hawezi kujisahihi hata anapo ambiwa na wenzake kuwa amekosea.
hayatulah mtei.
 
Zitto huhu hapa FB

Zitto Kabwe

Nitapambana kutetea uanachama wangu. Kwa upinzani ni lazima tufanye tofauti na CCM. Tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma kwa upinzani ni mbaya zaidi kuliko. Hivyo uwajibikaji kwa wote bila kujali vyama. Uwajibikaji sio msamiati kwa watawala tu bali kwa viongozi wote. Namna tunavyotaka nchi iendeshwe ndivyo hivyo tuendeshe vyama vyetu. Tuhuma dhidi ya Kiongozi wa Upinzani kuhusu masuala ya uadilifu zinapaswa kuhukumiwa kwa namna ile ile wanayohukumiwa watawala. Ninarudia kuwaambia ndugu zangu kwamba sitoki CHADEMA. Chama kina jasho langu na nitapambana mpaka dakika ya mwisho kutetea haki ya uanachama wangu. Mimi ni CHADEMA toka ujana. Niliingia CHADEMA kwa kuchagua na sio wengine walioingia kwa Mazingira Ya kupata fursa za kugombea. Wengine wangepitishwa na chama walichokuwa kuwa wagombea Leo wasingekuwa upinzani na inawezekana wangekuwa mawaziri mizigo au waendesha operesheni tokomeza
 
Kama ni SACCOS kwa nini huyo yuda anang'ang'ania kubaki? si mngemshauri akaacha kupeleka utetezi wake? kwa nini muhangaike kutwa kucha na CDM? Au kama ni saccos inawahusu nini? mlisema imeshakufa lakini wenye akili tunajiuliza kuwa kwa nini muhangaike nayo? huo ni utoto mkikua mtaacha!
Zitto kasema anajasho lake. haiwezekani nguvu yote aliyoiwekeza aje aondolewe na watu kutoka tlp akina mini kabang.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom