Dr.Slaa: Zitto anaweza kufukuzwa kabisa

Dr.Slaa: Zitto anaweza kufukuzwa kabisa

Status
Not open for further replies.
Fukuza haraka sana huyu msaliti, kuendelea kwake kuwa mwanachama ni hatari sana kwa mshikamano ndani ya CHADEMA.
kuhusu huyo zitto mfukuzeni tu haina haja ya kumtungia uongo kwenye mitandao. kwani kamati kuu si yenu, hata mkimfukuza hamna wa kuwahoji.
na kwa bahati mbaya kabisa kumbe na nyinyi ni wachumia tumbo tu kama haya maccm a.k.a chama cha majizi.
eti mnatetea wanyonge! wanyoge wawapi wanafiki wakubwa nyie.
 
Hujitambui weye!!! Fuatilia mijadala kwa kina ili uelewe kinachoendelea badala ya kukurupuka na kuropoka ropoka bila mpango. Upo ushahidi wa kutosha kuhusu usaliti wa Zitto humu ndani kaupitie kwa utulivu badala ya kutoa povu bila mpango.

kuhusu huyo zitto mfukuzeni tu haina haja ya kumtungia uongo kwenye mitandao. kwani kamati kuu si yenu, hata mkimfukuza hamna wa kuwahoji.
na kwa bahati mbaya kabisa kumbe na nyinyi ni wachumia tumbo tu kama haya maccm a.k.a chama cha majizi.
eti mnatetea wanyonge! wanyoge wawapi wanafiki wakubwa nyie.
 
"nawaonya mnaomshauri mnaweza kumpoteza huyu kijana" Kama haya maneno yamenenwa na Dr Slaa basi inabidi yafafanuliwe vyema ili yasitafsiriwe ndivyo sivyo. Je, alikuwa na maana gani aliposema hayo? Ina maana zito ni tishio kiasi cha kudhamiria "kumpoteza"?
 
kuhusu huyo zitto mfukuzeni tu haina haja ya kumtungia uongo kwenye mitandao. kwani kamati kuu si yenu, hata mkimfukuza hamna wa kuwahoji.
na kwa bahati mbaya kabisa kumbe na nyinyi ni wachumia tumbo tu kama haya maccm a.k.a chama cha majizi.
eti mnatetea wanyonge! wanyoge wawapi wanafiki wakubwa nyie.

Hamasa imepungua kutokana na malumbano yanayo endelea ndani ya chama huku hakuna kiongozi anaye onesha kupata busara ya kuutatua mzozo huu. Kwa maoni yangu ni kwamba hata Dr. Slaa ni tatizo.

Sielewi ni vipi katika mazingira ya sasa yalivyo kama Zitto akiomba kufanya mkutano kwa taratibu za chama atakubaliwa! Na ktk mazingira haya sioni hata uwezekano wa CDM hata ikimvua uanachama Zitto kama watafanikiwa kumuondoa Bungeni. Wajifunze kutoka kwa Kafulila na NCCR MAGEUZI na Hamad Rashid na CUF.
 
Afukuzwe tu huyu ndondocha kazidi sana haheshimu Chama chake wala viongozi wake hivi hawaoni kina Mwingulu Mchemba na ugonjwa wake wa akili lakini anaheshimu chama chalke na viongozi wake japokuwa ni wango'a kucha na meno ya waandishi wa habaari na Ma Dr ambao wanataka nchi iwe na uhakika wa wagonjwa na kuwe na vitu ambavyo vinakizi mahitaji kwenye Mahospital.

Sasa kwa Zitto Zuberi Kabwe hakuna la zaidi AFUKUZWE TU na ATAFUKUZWA TU kama mtabisha basi tieni pesa.Huyu jamaa kapoteza channel kwa kwenda kwa kuamini wale Ma DR wa tunguli na ndio wanaomharibia kila uchao mkumbuke wale Wachawi hawawezi kufanya mambo mazuri hata siku moja kwa wao wenyewe hali mbaya sasa watakufanyiaje wewe uwe kamili kado.

Wao wanaweza kuharibu tu na si kutengeneza.

Atamuheshimuje mtu ambaye hajiheshimu?Viongozi wa CDM hawajiheshimu ndio maana hawaheshimiwi na mwana CDM yeyote mwenye akili timamu
 
zito anatapa tapa ya mwisho .kwani kwa tuhuma alizo nazo ndani ya chadema hawezi kuzipinga mbele ya uongozi cdm .kwa hali hiyo sasa yuko kati kurudi cdm tabu kwenda ccm tabu .maana itakuwa ni fedhea kubwa itakayo thibitisha usaliti mkubwa aliokuwa anawafanyia wanachadema na watanzania wote wapenda mabadiliko .hapana shaka huu ndio mwisho wake .ni swala la muda tuu
 
Zito sio mtu wa kuaminiwa kwa madaraka makubwa iwe ndani ya Chama ama madaraka makubwa ya Kitaifa,Mpaka sasa ZZK ameprove failure ndani CHAMA CHAKE. Izingatiwe kwamba mtu wa nia mbili siku zote hutangatanga katika maamuzi yake,Zito anaonesha kuipenda CHADEMA na kwa wakati huo huo kwa usalama wa tumbo lake Na kwa kutafuta kujiongezea umaarufu anaitumikia CCM kwa kufuata maelekezo yote bila kukosea,Ni vigumu mtu aina hii ya akina Zito kutimiza ndoto zake,Na mwisho wa yote ni kukataliwa na pande zote na kubakia kama Garasha mbele ya UMMA WA WATANZANIA.
Tusisahau sio tu uwezo wake Zito ndio uliomfanya akubalike sana hasa kwa Vijana bali Kule kuji-conect na chama makini na sahihi chenye kujali maslahi ya Wananchi kumechangia kwa 75% kujenga na kumtangaza ZZK kukubalika kwa UMMA.
Shida kubwa aliyonayo Zito ni kujiamini sana kunako changanyikana na KIBURI CHA FEDHA,KIBURI CHA UMAARUFU NA TAMAA YA MADARAKA Huku akitabainisha wazi kukosa minofu ya Uaminifu na Uadilifu ndani ya chama chake. Shauku na matamanio ya kutaka kufikia ndoto yake vinam-drive ovyo mpaka kumtoa nje mwendo halali uliosimikwa kwenye misingi ya UADILIFU na kubakia kufuata MISISIMKO inayoletwa na kiu yakutaka kushika nafasi fulani kubwa ndani chama ama Kitaifa.
Ni wazi tena ni ukweli usiyopingika kijana huyu ana Ndoto kubwa kwa siku zijazo ila kwa kukosa Hekima,Utulivu (SUBIRA) amejikuta ameangukia mikononi mwa watu wabaya wenye kujionesha wema macho pake mwenyewe kumbe ni nyoka wenye sumu kali walioshindikana kuvuana magamba. Wako hapo pamoja na Zito kwa kusudi moja kubwa KUIZIMA NDOTO KUBWA YA ZITO,Nitawapa mfano wa mdudu mmoja:- Kwa Lugha ya Kabila langu mdudu huyo anaitwa CHALUNGU.Mdudu huyo hupenda sana kuchimba shimo ama katikati ya njia au kando ya njia na kufanya kashimo (katundu) hako ndio makao yake ya kuishi,Na mdudu ni maarufu sana kwa jina la Kinyaturu CHALUNGU kama nilivyomtaja hapo juu. Tulipokuwa Watoto kila tulipoona nyumba ya CHALUNGU tulifanya hima kuhakiki tumemtoa nje ya nyumba yake hio.Kazi ya kumtoa CHALUNGU ni rahisi sana,unapaswa uwe na zana zifuatazo Macho,mdomo ,Mate,Mikono na Unyasi mwembamba mrefu kwa wastani.
Ukishaukata huo unyasi utautafunatafuna kwa kuulainisha mwisho wa Ncha kisha utauingiza kwenye lile shimo aliko CHALUNGU,mara atakatambua kuna jambo jipya limeingia ndani nyumba yake kwa hasira atang'ata ule unyasi kisha CHALUNGU ATAUSUKUMA kwenda juu ili kuhakikisha kautoa nje ya makao yake,kwa kuwa CHALUNGU hajui kinachoendelea juu ya silaha hio aina ya Unyasi atabakia kuung'ata kwa hasira,Hatimaye mmoja ya vijana akiwa na wenzake watagundua CHALUNGU yupo kwa ishara ya unyasi kucheza cheza huku ukitolewa nje kwa kuja juu.
Kabla CHALUNGU hajautoa huo unyasi kijana mmoja kwa haraka sana ataushika unyasi na kuuvuta kwa haraka kwa vile CHALUNGU AMEUNG'ATA TENA BADO AMEUNG'NG'ANIA KINYWANI MWAKE watafanikiwa kumtoa nje ya nyumba yake huku wakimbamiza chini ya ardhi ngumu njiani.
Baada tu ya kufanikiwa kumtoa CHALUNGU nje ya nyumba yake Kijana au Vijana watacheka kwa dharau na kufurahia kazi walioifanya ya kumtoa CHALUNGU ndani ya makao yake sahihi.Wamemuweza hawezi kurudi tena huko nguvu zake zimekwisha kwa kubamizwa chini ya Ardhi ngumu,hana ujanja tena wakurudi mwenyewe kwenye shimo lake (hio nyumba ya CHALUNGU) Sasa atapigwa na jua kali na kwa kuwa mafuta mengi mwilini mwake atakufa kwa joto kali la jua,Pia sisimizi watamshambulia na kumwuua kabisa na kuitafuna Nyama yake,huo ndio utakuwa mwisha CHALUNGU yule mwenye Kichwa kigumu na mwili laini,Vijana mtaani watabakia na msemo tu,SASA CHALUNGU BASI-KWISHA HABARI YAKE.
"ZITO ZUBERI KABWE TAFADHALI JIFUNZE KWA MDUDU CHALUNGU"
Zito unakumbuka jinsi ulivyoanza siasa kwa mara ya kwanza? kwa vyovyote vile wewe huwezi kuwa mtu mkuu na maarufu kuliko CHADEMA uliyoikuta. Mimi nikukumbushe jambo hili; Usisahau katika Ndoto zozote alizonazo mtu awaye yote kwenye maisha yake ANAHITAJI WATU SAHIHI ILI KUFIKIA LENGO NA HATMA NJEMA YA NDOTO ZAKE.
Zito unaonekana umejisahau umejiruhusu kuingia mikononi mwa watu wanaotamani Vipawa vyako wanakuchekea, huku wanakutumia isivyostahili, Wanakusifia kinafiki wewe ni Kichwa sana mpaka kufikia nawe kubweteka wakati kiukweli wewe bado ni kijana mwororo sana kwenye siasa za Nchi yetu,Bado unahitaji uangalizi mzuri na Mashauri ya watu wengine walikutangulia kwenye mambo ya siasa.Na watu hao sahihi wanapatikana kwanza CHADEMA kabla ya kuinua macho kwenye vyama vingine kikiwemo CCM WANAOONEKANA KUKUPENDA SANA KWA WAKATI HUU.Zito wewe sio wakuwapuuza CHADEMA, maana wao ndio wamekufanya uwe kama ulivyo sasa.Baadhi ya Wana CCM na watu wa TISS wanakufurahia na kukushabikia kwa sababu wamekukuta uko ndani ya nyumba salama CHADEMA.
Zito wa Kabwe kwanini umekubali kirahisi vile kulainishwa kwa vijisenti kwa kutumainishwa makubwa wakati wewe mwenyewe una ndoto kubwa na ndio inayotafutwa KUZIKWA MAPEMA KABLA YA KUTIMIA? Hivi ni kweli hii inaingia Akilini??? CCM ndio wanaokupenda kuliko CHADEMA? Mahusiano hayo mmeanza nao lini? Hivyo ulivyo ndo walivyokukuta umesoma na kupendeza na umaarufu huo? kama sivyo kwanini leo wakusifie? KIJANA SHITUKA!!! LA SIVYO IMEKULA KWAKO.
Zito unapaswa kuelewa kanuni ya maisha iko hivi.Ukipendwa Jipende,Ukithaminiwa Jithamini,Ukiaminiwa Aminika.
Kwa mwenendo anayoenda nayo Zito sitashangaa akituachia Hadithi kuwa Tulikuwako na kijana machachari ajuaye kujenga hoja (ZITO) Lakini kwa kukosa SUBIRA,UAMINIFU NA UADILIFU ALISHAWISHIKA KIRAHISI AKATUMIKA VIBAYA CHADEMA WAKAMDAMPO CCM WAKACHEKELEA WANANCHI TUKAMSAHAU MPAKA WA LEO,NACHELEA YASIJE KUMKUTA ZITO ZUBERI KABWE YALE YALIYOMKUTA MR.KABURU ALIYEKUWA KATIBU MKUU WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) Mwenye macho na Masikio na asome na kulielewa Andiko hili la 12STONE MwanaJF mwenzenu, Nawasilisha.
Mungu akitujalia kuiona 31 Dec. 2013 na Kuingia Jan.1,2014 WOTE TUWE NA SHUKRANI KWAKE MOLA.
 
Dah! makala ndefu sana halafu hujaruka mistari inakuwa shida kidogo kuisoma yote
 
Muondoeni zito haraka ama myamalize haraka. Maamuzi ndio swala siku zote linarotesha mambo. Ni vyema wanachama wakajua kuwa Zito bado ni mbunge na mwanachama wa chadema au sio, kwasasa hii sintofahamu inazidi kuchanganya wengi.

Ni kweli kabisa mbunge wa chadema ana haki zote kikatiba kukutana na wananchi wake, na wa majimbo mengine. Sasa hili swala lazima litaleta usumbufu kwa viongozi wa ngazi za mkoa jinsi ya kum-handle Zito. Je wamuone kama mtuhumiwa mtu asiyefaa kushiriki kazi za chama, au mbunge wa Chadema anayejenga chama.

Kauli za ZZK akipanda majukwaani ni sumu kali sana inayoingamiza chama. Inaweza kuwa anafanya makusudi au hasira za kuona anakaribia kufukuzwa hiuvyo bora tukose wote. Haya yote sio hasara kwa zito labda na viongozi wengi bali hasara kubwa ni kwawananchama walioipa cdm imani kubwa ya kuwatoa matongotongo.

Kikundi cha ZZK kinachokifanya kwa sasa kwenye media, mitandao na mikutano ya hadhara ni hatari sana ikiachwa bila kuchukuliwa hatua kwa muda mrefu. Kwa hali iliyopo ni lazima udharura ulioainishwa kwenye katiba utumike ili kuweka hali ya utulivu sawa.

ZZK and the team, mnadhihirisha wazi nia yenu ni kuidhoofisha cdm na sivinginevyo hamna mapenzi na hiki chama hata kidogo. Wapo wengi waliowahi kupewa adhabu kali sana kwenye vyama vyao ila walijitahidi kukilinda chama chao mpaka mawimbi yakapita. Kwa matendo yenu sasa mnaonekana wazi nia yenu haikuwa mabadiliko ya kidemokrasia au kujenga chama imara zaidi, kwani manaonekana mapandikizi kama wale wa Mobutu.

Matendo yanasema zaidi kuliko maneno.
 
Mpaka hapa Zito alipofikia sidhani kama ana uthubutu wa kuomba msamaha na kukubalina na makosa yake,zaidi sana tajitahidi kujihesabia haki kwa kujionyesha machoni pa Wanachama wa CHADEMA na jamii yote kwa ujumla kuwa yeye ni mtu safi asiye na kasoro ama doa lolote.

Njia bora ya kufanya hivi sasa ni KUMFUKUZA ZITO ASIWE MWANACHAMA WA CHADEMA TENA VINGINEVYO Huruma za CC YA CHADEMA itakuwa na mchango mkubwa wa Kukiua chama kwa kushiriki dhambi za Zito.
 
Mpaka hapa Zito alipofikia sidhani kama ana uthubutu wa kuomba msamaha na kukubalina na makosa yake,zaidi sana atajitahidi kujihesabia haki kwa kujionyesha machoni pa Wanachama wa CHADEMA na jamii yote kwa ujumla kuwa yeye ni mtu safi asiye na kasoro ama doa lolote.

Njia bora ya kufanya hivi sasa ni KUMFUKUZA ZITO ASIWE MWANACHAMA WA CHADEMA TENA VINGINEVYO Huruma za CC YA CHADEMA itakuwa na mchango mkubwa wa Kukiua chama kwa kushiriki dhambi za Zito.
 
wee zitto! haya bhaana! yaani unavuruga chama ambacho ndio kinajiandaa kuingia ikulu kubadili mfumo wa maisha ya Wa-tz! Endelea na huo usaliti maana
mwisho wake ni Aibu na fedheha kwako na kwa wafuasi wako.
 
Hujitambui weye!!! Fuatilia mijadala kwa kina ili uelewe kinachoendelea badala ya kukurupuka na kuropoka ropoka bila mpango. Upo ushahidi wa kutosha kuhusu usaliti wa Zitto humu ndani kaupitie kwa utulivu badala ya kutoa povu bila mpango.

umekamatwa mkuu

matusi na povu la nini?? kama umeamua kuweka akili mfukoni kwa chuki zako kwa zitto

sio wote wajinga
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom