Hivi kweli Lowassa anaweza kushiriki mdahalo wa urais na mtu kama Dr. Slaa na akamudu kujibu hoja na changamoto zote zitakazojitokeza katika mdahalo huo?
hawa magamba wanaishia kujiita wanyamwezi tu, usanii mpaka mwisho. Litakuwa ni kosa kubwa sana kumpata rais bila kupitia mdahalo. Ikitokea hiyo ndipo wanaomshabikia watajua kuwa ni lyatonga wa pili.
Tuliona lilivyotusaidia wakati wa Mkapa na jinsi lilivyotugharimu kwa JK.
Watanzania tusivyo serious tunaweza kuruhusu hili tena na kuuziwa mbuzi kwenye gunia maana tangia ratiba ya tume ya uchaguzi itolewe nilitegemea pia kuona ratiba za midaharo japo mitatu kutoka kwa wadau lakini hakuna hadi sasa!
Mkuu,unataka kusema atakayeweza kusimama kwenye mdahalo na Dr. Slaa ndio atakuwa kiongozi bora na atakayewaletea watanzania matumaini ya kupata maendeleo wanayoyataka.
Uwezo wa kujieleza katika midahalo ni kipaji na sanaa kama vipaji na sanaa nyingine lakini kamwe haiwezi kuwa kigezo au sifa ya kiongozi bora,mwenye nia ya dhati ya kufanya mabadiliko.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.