Heshima mbele sana wakuu,
Najaribu kuichungulia 2015 miezi ya october endapo mchuano utakuwa ni kati ya hawa vinara wawili ni nani atakuwa na nafasi kubwa ya kuukwaa urais wa nchi hii.
Wote ni wanasiasa wa siku nyingi wenye heshima zilizotofautiana kutokana na historia na nyadhifa tofauti walizowahi au wanazozikalia hivi sasa,
Je come 2015 nani ataibuka kidedea endapo team hizi zinakutana kwenye viwanja sawa vya haki na usawa, bila zengwe wala mizengwe.
hao ni ngumu kuwa marais wote bomu hawana jipya,,tunajua mnaoposti hizi ni kanda ya kaskazini ambao tayari mmekubaliana CCM Lowasa na Slaa CDM kuwa rais bila kujali itikadi atoke kaskazin huko kaskazini ndiko kunaongoza kutoa mawaziri wakuu wengi mpaka wengine mafisadi bado mnataka tu pamoja na utajiri mlionao
Kama ni kwalinganisha Dr. Slaa na Lowasa basi ni ukweli uliowazi kuwa Dr. Slaa atachukua nchi. Ila tukija katika mizania inayoangalia usawa hiyo comparison sio sahihi hata kidogo. Dr. Slaa ni mzalendo kwelikweli na mpinga ufisadi kwa maneno na vitendo wakati Lowasa ni Fisadi aliyekubuhu. mimi nadhani ungempambanisha Dr. Slaa na mtoto wa mkulima (Pinda) hapo angalau tungekuwa na mizania sawa kwa sababu mtoto wa mkulima hatujasikia kashfa za ufisadi kwake.
huyu Pinda hivi ana uadilifu gani?mi naona kakaa kama shati tu hapo,kero tu,hana sauti na ananyamazia maovu!!!
Wewe unadhani nani ni mwadilifu?
hii ni kama mechi ya Barca na man U............babu fagasoni kazi unayo kwenye mechi
Nini maana ya mwadilifu na nini maana ya fisadi?
Na nani kati ya hao hapokei posho.
hawa wote kutoka Arusha, rais 2015 hatoki Arusha
Hii kitu bado ni ngumu sana mkuu Sr. Magdalena
Kuna uwezekano mkubwa sana kwa vyama vyote hivi kupandisha sura ngeni kabisa kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Unaonaje kama kwa mara ya kwanza CDM wapandishe mtu kutoka znz, Hamad Rashid kwa mfano?
Wasalaam
Hatuwezi kuwa na rais asiyelipa kodi, kati ya hawa kuna mmoja analipwa posho ya 7m ambayo haikatwi kodi.