Dr. Slaa Vs Lowassa Urais 2015

Dr. Slaa Vs Lowassa Urais 2015

Nani unaona anafaa kuwa Rais kati ya Wawili hawa?

  • Edward Lowassa

    Votes: 103 13.0%
  • Dr. Willibrod Slaa

    Votes: 640 80.6%
  • Wote hawafai/sijaamua

    Votes: 51 6.4%

  • Total voters
    794
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.
Kama ni kwalinganisha Dr. Slaa na Lowasa basi ni ukweli uliowazi kuwa Dr. Slaa atachukua nchi. Ila tukija katika mizania inayoangalia usawa hiyo comparison sio sahihi hata kidogo. Dr. Slaa ni mzalendo kwelikweli na mpinga ufisadi kwa maneno na vitendo wakati Lowasa ni Fisadi aliyekubuhu. mimi nadhani ungempambanisha Dr. Slaa na mtoto wa mkulima (Pinda) hapo angalau tungekuwa na mizania sawa kwa sababu mtoto wa mkulima hatujasikia kashfa za ufisadi kwake.

Sijakubaliana nawe: Dr Slaa Vs Mzee wa kudhania tu... Pinda ambaye taarifa za kiintelijensia zinasema si mkulima tena bali mfanyabiashara anayemiliki Kampuni ya Mabsi ya Sumry???

Dr Slaa bado hana mpinzani. Watanzania wengi wanakosa chumvi, sukari na dizeli; wanaona ni kawaida maana hawajawahi kuonja maisha mazuri tokea kuzaliwa, uhuru hadi leo. Utajuaje kuwa hali ni ngumu wakati hujawahi kuona hali nzuri???
 
CDM hawana desturi ya kusimamisha mgombea wa urais zaidi ya mara moja, sasa ni zamu ya Prof Safari au Hamad Rashid, Zitto ajipange 2020 na Sibuda 2025.

na cuf wakifanya kosa tu Hamad anaingia cdm na ndio mwanzo wa kuiteka zanzibar
 
Kweli wao wan a dola sisi tuna Mungu tangulia hamad rashid tulikupenda sana lkn tango uliposaliti nguvu ya umma Siasa uchwara na kujivua gamba jipya lijulikanalo kama uanachama lilikupenda zaidi Kweli wao wana Dola Sisi tuna Mungu Nikilinganisha ya kafulila na haya ya hamad nazidi kuikubali hii kauli na Mungu analipa hapa hapa
 
Kama ni kwalinganisha Dr. Slaa na Lowasa basi ni ukweli uliowazi kuwa Dr. Slaa atachukua nchi. Ila tukija katika mizania inayoangalia usawa hiyo comparison sio sahihi hata kidogo. Dr. Slaa ni mzalendo kwelikweli na mpinga ufisadi kwa maneno na vitendo wakati Lowasa ni Fisadi aliyekubuhu. mimi nadhani ungempambanisha Dr. Slaa na mtoto wa mkulima (Pinda) hapo angalau tungekuwa na mizania sawa kwa sababu mtoto wa mkulima hatujasikia kashfa za ufisadi kwake.

Pinda hafai kwani anatetea mafisadi na ufisadi! Alitetea posho za kinyonyaji za wabunge. Kama yeye analinda mafisadi na yeye ni fisadi tu.
 
mkristo vs mkristo hahahahaa. "kama kuna wagombea wengi na katika hao kuna waislamu wawili basi ukiona muislamu mmoja anaelekea kushinda mchague huyo huyo"
Nchi masikini kama tanzania inapofikiria udini mimi inanisikitisha sana,kupata maendeleo katika nchi hii kama tutaendelea na mawazo mgando kama haya,basi itakuwa ndoto ya mchana!
 
nahisi kafulila atakuwa amejifunza yakuwa hakutakiwa atukane chama kikubwa kama chadema wakati bado mwanasiasa kijana na huku akijua hakuna chama kingine chenye uhuru wa kutoa hoja kama chadema pole sana kafulia nahisi umejifunza kitu
 
Fafanua mkuu, wewe unadhani nani ataibuka kidedea na kwa nini?

slaa ataibuka kidedea kwa sababu sio mwizi,.lowassa ni mwizi na wezi hawatakiwi kwenda kuishi ikulu,.wezi wanachomwa moto..dada magdalena(if you really are a woman)
 
mie kwangu wote ni sawa tu. Tunachotaka ni mabadiliko ya ukweli na kiongozi anayethubutu.

Kwenye CCM hamna kama Lowassa

Huko kwenye CDM nachelea kusema kama wakimweka Mzee Dr Slaa basi wajue urais wamekosa. Nina sababu. anayetaka jibu ani PM.

Kweli mitanzania ndivyo tulivyo,yaani tutoke kwenye mjadala wa wazi,tuende kwenye mjadala wa siri,haina mashiko hata kidogo!
 
Msimsahau Jaji Lubuva yupo katikati yao! tafakari
 
nahisi kafulila atakuwa amejifunza yakuwa hakutakiwa atukane chama kikubwa kama chadema wakati bado mwanasiasa kijana na huku akijua hakuna chama kingine chenye uhuru wa kutoa hoja kama chadema pole sana kafulia nahisi umejifunza kitu
Karimu mgeni!hoja ya msingi hapa ni Re: 2015 - Dr Slaa Vs Edward Lowasa ,nakushauri uwe unasoma kichwa cha habari cha mada kabla ya kujadili hoja husika!
 
Sr. Magd,usimfanye Lowassa aanze kukosa usingizi mapema. Dr. Slaa anakubalika!Yeye Lowaasa labda aendelee tu kufanya izo kampeni za makanisani ambazo zimeanza kwa nguvu kwa uzinduzi wa albums,uzinduzi wa ujenzi wa makanisa mapya kwa kuchangia n.k. Du,ila sijaona uzinduzi wa ujenzi wa misikiti,,,,,,nako ajitaidi!January,2012 Lowassa atakuwa Shinyanga kuzindua ujenzi wa kanisa Kuu la Jimbo litakalojengwa kwa thamani ya TZS 500 millions!
 
Dr. Slaa atashinda kwani yeye ndiye aliyevumbua ufisadi wa LOWASA hvy Lowasa ni km mtoto kwake
 
Hkuna hata mmoja anayefaa kuongoza nchi hii.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom