Dr. Slaa amkosoa Rais Kikwete kuhusu Rwanda

Dr. Slaa amkosoa Rais Kikwete kuhusu Rwanda

hivi inaingia akilini kweli kumuona baba yako anayemtukana na kupiga mama yako kila siku nyumbani,akiwanyanyasa nyinyi watoto wake kwa kila namna kwenda kumuhubiria jirani yake jinsi ya kuishi kwa amani na familia na nyinyi watoto pamoja na mama yenu eti mumuunge mkono?

tuseme ukweli tuende vitani kwasababu jirani hataki kukaa mneza moja na mpinzani wake ? Ushauri haupokelewa inatubidi tukae kimya . Ukiwa na jirani mwenda wazimu kaa chonjo iko itakufanya mwendawazimu ndi jambo linalotokea hapo. Tuachane na jirani mwendawazimu tusije tukachekwa. Unajua kushauri lilikuwa jmbo zuri lakini ku-react kwa kuandaa mpango wa kwenda vitani hapo ni wazi hukuwa unashauri ila ulikuwa unaagiza la kufanya sasa kwakuwakuwa halijatekelezwa unaenda vitani. Kagame is like a crazy let's shit him just like that.
 
A
Huu uzi unaonesha umuhimu wa kuangalia siasa za ndani na maslahi mapana ya nchi. Tuchukulie mfano mzuri Marekani, ndani ya mwezi mmoja wamekuja marais 3 Tanzania, na marais hawa wanatoka vyama tofauti. Wanaweza kuja kwa mgongo wa taasisi zao za kusaidia watu lakini hapo hapo kwenye kujenga mazingira mazuri kwa nchi yao kufaidika kwa kuwa karibu na Tanzania.
B
Linapokuja swala la maslahi ya taifa kama hili la DRC na Rwanda tulitakiwa (kama taifa) kuwa na kauli moja. Dr Slaa hakutakiwa kuongea hayo maneno hadharani. Lakini pia, nilitegemea katika sintofahamu inayoikabili Tanzania kwa kipindi hiki, basi viongozi wa juu toka vyama vikubwa vya siasa nchini wangekutakana na kuwekana sawa kuhusu 'Tanzania'. Kama ni ushauri wangepeana humo ndani lakini nje ya nchi lazima tuwe kitu kimoja.

Kagame amefanya kazi kubwa kuinua nchi yake, lakini Kagame ana upande wa pili ambao ni 'shameful' kwa Afrika. Miaka nenda rudi sisi Waafrika tumekuwa tunalalamika kuwa machafuko yanayotokea barani kwetu yanafanywa na wazungu ili waibe rasilimali zao. DRC imakuwa ni kielelezi cha jinsi gani sisi Waafrika ni wanafiki. Kagame anang'aka, si kwa sababu kaambiwa aongee na wabaya wake, lakini anajua msimamo wa Tanzania kuhusu DRC unamuumbua. Angalia pato la taifa la Rwanda lina nini ndani yake? wana-export madini bila aibu, na sasa anajua Bandari ya Dar itakamata madini yake amekimbilia Kenya.
C
Na iweje Kagame hakumjibu Kikwete pale pale kwenye kikao badala yake ameenda kupiga kelele nyumbani kwake? Huo ujasiri anaotamba kuwa nao aliusahau wapi siku hiyo ya kikao?
Hapo A: napaacha kama palivyo kwasababu panajitosheleza.

B: Kwa maneno mengine FJM anasema kauli za Paul kumdhuru Rais wa Tanzania na nchi kwa ujumla ni kubwa kuliko mambo mawili yaliyobaki i.e Ushauri na suala la Intarahamwe.

Rais wa nchi yoyote ni alama ya taifa. Sisi Watanzania tuna haki ya kumuongelea rais kwa madhaifu au mapungufu yake kwasababu ndio waajiri wake na si raia au kiongozi wa taifa jingine.
Tishio la kumdhuru Rais ni tishio la taifa na hilo tu linatuunganisha bila kujali itikadi zetu za kisiasa.

Dr.W.Slaa
alipaswa kuliona kama kiongozi kwanza na Kauli ya kwanza ilipaswa kulaani matishio ya Paulo dhidi ya viongozi (akiwemo yeye) na nchi . Hakulaani kauli za Paulo akaliona la JK, kuna tatizo!!

C: Hapa ndipo watu wengi ima wanapakwepa au hawajui kuwa ni sehemu muhimu sana ya mtafaruku huu.
Jk hakutoa kauli zile Washington au Abuja wakati PK akiwa hayupo,ameitoa kauli mbele ya PK na Museveni akiwepo na kuunga mkono. Paulo Kagame hakusema lolote.

Aliporudi Kigali akutuma mawaziri na wala si yeye kusema pamoja na kuwa alikuwa na nafasi hiyo.
Mawaziri wakaanza kuiongelea kwa ushabiki wa ajira bila kujua hata kilichosemwa katika mkutano.
Kagame akamalizia kwa kuita wanajeshi na baadaye kutoa kauli za vitisho

Na kuonyesha kuwa PK hakujua ajibu nini na kwanini na wapi, yeye na mawaziri wake walianza kuongelea barua ya Mtikila na kumhusisha JK bila kufuatilia au kujua Mtikila mi mtu wa aina gani.

Hoja ilipokosa mashiko wakaamua kuvamia diplomasia kwa njia ya kauli za zisizo na chembe ya ustaarabu.
Kwani PK angesema hakubali ushauri wa JK katika mkutano au kuita press conference kingeharibika nini?

Tukirudi kwa Dr Slaa, ni lazima ajue kuwa zipo domestic na international politics.
Wanachama na mashabiki wa chadema walisimamam kidete na kusema uwepo wa Mbowe katika hafla ya Togwa na Obama ulikuwa ni sehemu ya Utaifa, na kutetea kuwa mambo ya kitaifa ni lazima utaifa kwanza.

Leo nauliza je, hili la kutishiwa viongozi na nchi si suala la taifa? na je, Dr Salaa hakupaswa kusimama kidete na kauli za kutishiwa kwetu kama alivyosimama kidete na utaifa wa Mbowe katika Togwa na Obama.

Lakini pia lazima wanchama wa CDM na mashabiki wao waelewe kuwa CDM ni chama cha upinzani na ni mbadala wa serikali iliyopo madarakani kama wananchi wakiamua. CDM wanapaswa kujipanga na kuhakikisha kauli zao katika majukwaa ya kimataifa zinapimwa na kuchujwa vema.

Ni kwa vile CCM kumebaki vichwa wazi, kama kungekuwa na vichwa vizuri suala hili lingerudi katika domestic politics na kuwaumiza sana Chadema.

Hivi leo hii mtu wa Karagwe, Ngara na Kagera anayepata adha kutokana na ujambazi wa Wanyarwanda pamoja na tishio la Kagame na kumbu kumbu ya Idd Amin atajisikiaje akisikia kuna kiongozi anyesimama pamoja na PK dhidi ya taifa hili?

Leo mwanasiasa akienda na kufanya spinning kuwa Chadema inaunga mkono PK na Rwanda, nafasi ya CDM maeneo hayo ni ipi? Je, tutawaulaumu wananchi kutokana na mkanganyiko huu

Na mwisho, Watanzania! tunajua hatuna natural leader kama tuliokuwa nao.
Hawa waliopo ni wa kupika na kutengeneza, tuna wajibu wa kuwa ''grill na groom' kabla hawajaingia magogoni ili wakifika huko wawe wameiva tayari.

Hakuna sababu za kuoneana haya wala kuleta ushabiki wa Simba na Yanga katika masuala serious kama haya. Akikosea JK tunampa za uso akikosea Slaa tunampa za uso kwa manufaa ya Tanzania. Period

cc JokaKuu Jasusi @Dr Kitila Mkumbo
 
Mimi naipenda CHADEMA na namkubari Dr Slaa, kiukweli CCM siipendi kwa sababu ya kushindwa kufanya yale tunayoyataka, mwanzoni nilikuwa namkubari Rais wetu Jakaya Kikwete, lakini baada ua kushindwa kuchukua hatua mbalimbali kwa wezi, wauza madawa ya kulevya na nk, silipoteza imani na Kikwete.

Kwa hili Dr Slaa amekosea kumkosoa Kikwete hadharani na kumpa kicha Paul Kageme, hata kama ni mpinzania lakini kwa mambo ya interest ya nchi lazima tuwe pamoja kama nchi hata kama Rais wetu amekosea. siamini km Dr Slaa hajui mgogoro wa Rwanda, na siamini km Dr Slaa hajui kama kabla ya 1994 hapakuwa na mgororo huko Rwanda, siamini kmDr Slaa hajui kama tuna makambi ya wakimbizi wa Rewanda kablya ya 1994 yaani miaaka ya 89 kurudi nyuma, kuna kambi za mishamo kule Rukwa na nk. Siamini km Dr Slaa hajui kama Paul Kagame ndiye aliyedungua Ndege iliyokuwa imewachukua Rais wa Rwanda na Burundi? je si chanzo cha genocide?

Dr Slaa anataka kusema kuwa kwa kuwa kule afrika kusini kwa Babu Mandela ambako waafrika waliuawa na kuteswa kwa muda mrefu sana kama siyo karne ao zaidi, je wale akina Mandela na watawala wa sasa walitakiwa kulipiza kisasi? jibu siyo kweli kwa sababu amani ya africa kusini imepatikana kwa maridhiano.

Hao RPF wanaotawala kwa sasa Rwanda si walikuwa msituni wakipigana kutokea Uganda mbona Rais aliyeuawa alikubari mazungumzo na akina Kagme?

Kwa maoni yangu sidhani km Dr slaa alikuwa sahihi kumkosoa Kikwete kwa ushauri wa Rwanda.
 
Kwa kweli hapa Dr. slaa amekosea, maana linapokuja suala la nchi wananchi wote tunakuwa pamoja bila kujali itikadi za kisiasa au za aina yoyoye ile. Lakini naamini Dr. slaa anataka kutuma ujumbe kwa JK kuwa kitendo cha kutokuchukua hatua yeyote kwa kamuhanda na badala yake kumpandisha cheo hakijawapendeza wananchi. pengine niseme njia aliyotumia kufikisha ujumbe sio sahihi. Kwa maoni yangu JK yupo sahihi katika suala la kagame lakini hayupo sahihi katika suala la Kamuhanda. na kwa upande wa Dr. slaa yupo sahihi katika suala la Kamuhanda lakini hayupo sahihi katika suala la nchi. Nahitimisha kwa kusema tumsamehe Dr. slaa kwa sababu ni kosa la kwanza ndani ya miaka mitano na kwa kweli linatokana na hasira.
 
Hapo A: napaacha kama palivyo kwasababu panajitosheleza.

B: Kwa maneno mengine FJM anasema kauli za Paul kumdhuru Rais wa Tanzania na nchi kwa ujumla ni kubwa kuliko mambo mawili yaliyobaki i.e Ushauri na suala la Intarahamwe.

Rais wa nchi yoyote ni alama ya taifa. Sisi Watanzania tuna haki ya kumuongelea rais kwa madhaifu au mapungufu yake kwasababu ndio waajiri wake na si raia au kiongozi wa taifa jingine.
Tishio la kumdhuru Rais ni tishio la taifa na hilo tu linatuunganisha bila kujali itikadi zetu za kisiasa.

Dr.W.Slaa
alipaswa kuliona kama kiongozi kwanza na Kauli ya kwanza ilipaswa kulaani matishio ya Paulo dhidi ya viongozi (akiwemo yeye) na nchi . Hakulaani kauli za Paulo akaliona la JK, kuna tatizo!!

C: Hapa ndipo watu wengi ima wanapakwepa au hawajui kuwa ni sehemu muhimu sana ya mtafaruku huu.
Jk hakutoa kauli zile Washington au Abuja wakati PK akiwa hayupo,ameitoa kauli mbele ya PK na Museveni akiwepo na kuunga mkono. Paulo Kagame hakusema lolote.

Aliporudi Kigali akutuma mawaziri na wala si yeye kusema pamoja na kuwa alikuwa na nafasi hiyo.
Mawaziri wakaanza kuiongelea kwa ushabiki wa ajira bila kujua hata kilichosemwa katika mkutano.
Kagame akamalizia kwa kuita wanajeshi na baadaye kutoa kauli za vitisho

Na kuonyesha kuwa PK hakujua ajibu nini na kwanini na wapi, yeye na mawaziri wake walianza kuongelea na barua ya Mtikila na kumhusisha JK bila kufuatilia au kujua Mtikila mi mtu wa aina gani.

Hoja ilipokosa mashiko wakaamua kuvamia diplomasia kwa njia ya kauli za zisizo na chembe ya ustaarabu.
Kwani PK angesema hakubali ushauri wa JK katika mkutano au kuita press conference kingeharibika nini?

Tukirudi kwa Dr Slaa, ni lazima ajue kuwa zipo domestic na international politics.
Wanachama na mashabiki wa chadema walisimamam kidete na kusema uwepo wa Mbowe katika hafla ya Togwa na Obama ulikuwa ni sehemu ya Utaifa, na kutetea kuwa mambo ya kitaifa ni lazima utaifa kwanza.

Leo nauliza je, hili la kutishiwa viongozi na nchi si suala la taifa? na je, Dr Salaa hakupaswa kusimama kidete na kauli za kutishiwa kwetu kama alivyosimama kidete na utaifa wa Mbowe katika Togwa na Obama.

Lakini pia lazima wanchama wa CDM na mashabiki wao waelewe kuwa CDM ni chama cha upinzani na ni mbadala wa serikali iliyopo madarakani kama wananchi wakiamua. CDM wanapaswa kujipanga na kuhakikisha kauli zao katika majukwa ya kimataifa zinapimwa na kuchujwa vema.

Ni kwa vile CCM kumebaki vichwa wazi, kama kungekuwa na vichwa vizuri suala hili lingerudi katika domestic politics na kuwaumiza sana Chadema.

Hivi leo hii mtu wa Karagwe, Ngara na Kagera anayepata adha kutokana na ujambazi wa Wanyarwanda pamoja na tishio la Kagame na kumbu kumbu ya Idd Amin atajisikiaje akisikia kuna kiongozi anyesimama pamoja na PK dhidi ya taifa hili?

Leo mwanasiasa akienda na kufanya spinning kuwa Chadema inaunga mkono PK na Rwanda, nafasi ya CDM maeneo hayo ni ipi? Je, tutawaulaumu wananchi kutokana na mkanganyiko huu

Na mwisho, Watanzania! tunajua hatuna natural leader kama tuliokuwa nao.
Hawa waliopo ni wa kupika na kutengeneza, tuna wajibu wa kuwa ''grill na groom' kabla hawajaingia magogoni ili wakifika huko wawe wameiva tayari.

Hakuna sababu za kuoneana haya wala kuleta ushabiki wa Simba na Yanga katika masuala serious kama haya. Akikosea JK tunampa za uso akikosea Slaa tunampa za uso kwa manufaa ya Tanzania. Period

cc JokaKuu Jasusi @Dr Kitila Mkumbo
Mkuu Nguruvi nimekusoma umeandika kwa ustadi mkubwa sana japokuwa tunapishana kimtazamo kwenye mambo mengine lakini kwa hili uko vizuri BIG UP umeonyesha mawazo yako yako huru, kwasababu kuna watu mawazo yao yamepigwa pingu.CC Ben Saanane
 
Kwa namna Wanyarwanda walivyoupokea ushauri wa JK bila shaka kuna walakini.Lakini hata kwa logic ya kawaida mfano; Jirani yako anapokushauri ukae chini mzungumze na watu waliowaua wazazi wako,ndugu na jamaa utajisikiaje?
na pale inapoonekana kuwa hawakuwaua kwa bahati mbaya bali ni sehemu ya 'sera' ya existence yao. Haya mambo siorahisi kama tunavyodhani na kuongelea vita maana yake mwathirika mkuu kwa Tanzania ni Kagera, tuongelee zaidi amani tafadhali.

 
Mkuu Nguruvi nimekusoma umeandika kwa ustadi mkubwa sana japokuwa tunapishana kimtazamo kwenye mambo mengine lakini kwa hili uko vizuri BIG UP umeonyesha mawazo yako yako huru, kwasababu kuna watu mawazo yao yamepigwa pingu
Boko haram ha ha ha ha, siku zote nasema kuwa na mitazamo tofuati ni jambo jema kabisa.
Hatuwezi kuwa na ulekeo au mtazamo mmoja hivyo kuofautiana kimisimamo liskutie wasi wasi.

Jambo la muhimu ni kuwa tofauti hizo zijengwre katika misimamo ya kuheshimiana katika kukubali kukubaliana au kukubaliana kutokubaliana na huo ndio wito wangu kwa wanajmvi kila mara

Ahsante
 
Dr Slaa,
Mimi sileti ushabiki mzee wangu,ninachojaribi kukweka sawa hapa ni kwamba kuna mambo ya msingi ambayo sisi kama taifa tunatakiwa kuwajibika regardless tuna yetu ya ndani ambayo tunaweza kuyatatua muda wowote,au kwa maana nyingine mtoto huwezi kususa na kuacha wajibu wako wa msingi wa kulinda nyumba,kuua nyoka anayehatarisha usalama wa nyumbani,au kwenda machungani eti kwa sababu,eti kwa sababu baba ni mlevi-anatumia pesa yote aliyopata mnadani/gulioni kulewea,au huwezi kutoboa ngalawa unayosafiria eti sababu nahodha amekutusi 'two wrongs don't a right'.
Alichokifanya JK ni kujaribu kutoa suggestion tu,katika kujaribu kuokoa nyumba ya jirani inayowaka moto(nadhani hata ukilala njaa,ikitokea ajalia ya moto kwa jirani huwezi kukaa bila kusaidia eti kwa kuwa umelala njaa,lazima utoe msaada hata wa mawazo tu).
Lakini matusi aliyeyatoa PK ni dhahiri huyu mtu ni mshari,ametumia nguvu kubwa mno kujibu swala dogo kwa jazba kubwa,sasa hapo umeona anaashiria nini huyu kama sio chokochoko za wazi.hana nia nzuri huyu na usalama wa maziwa makuu huyu nyoka,na akitoka Kivu atakuja Kigoma akiendelea kuchekewachekewa.
Mimi ni Chadema damu, lakini sibezi mafanikio yaliyofikiwa na CCM maana huwezi kusema hawajafanya kitu kabisa,vilevile siwezi kuacha kulaani usafirishaji wata wanyama pori,ufisadi wa ccm amabo wewe ndio uliyeuibua na kutujuza watanzania wote,rushwa katika vyombo vya serikali kama police,police kutumia nguvu kupita kiasi,usafirishaji wa madawa ya kulevya ulioibuka n.k.LAKINI LINAPOKUJA SWALA LA KUSHAMBULWA KWA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA MTU WA NJE,IWE KWA RAIA,IWE KWA KIONGOZI,IWE KWA JK,IWE KWA DR.SLAA,sitaangalia mapungufu aliyo nayo mtu huyo, nitashika mtutu kumshambulia adui kwanza,nikimalizana nae ndipo narudi kumwambia ndugu yangu-mtanzania huyo kuwa aliteleza kama ameteleza kweli na siku nyingine asirudie.
Hata wewe mathalani siku ukiwa magogoni pale,ukakwaruzana na mtu yeyote wa nje,nitakutete kwa nguvu zote bila ya kuhoji umefanya kosa lipi,halafu baadae ndipo nitarudi kwako na kukuuliza umefanya nini,lakini wakati huo adui atakuwa tayari keshakiona cha mtema kuni.
Mwisho angalia attachement ya UN inavyoonyesha kwa ushahidi PK yupoje
Asante mzee kwa uungwana wako wa kujibu ,nisamehe kama nilitumia lugha kali kidogo maana nilihamaki,lakini Mungu ibariki Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania


Kusema ukweli

Nyamafu,
Hapo ndo umeona JK amekaa anajadiliana na Upinzani. Ushabiki umelewesha kiasi cha kutoelewa kila kitu kina mazingira yake! Hayo yalikuwa matembezi ya Hiari ya CCBRT na CCBRT ni chombo cha huduma kwa walemavu. Tunachoxungumzia hapa ni lini JK kakutana kujadili mgogoro na wapinzani wake na hapa ninamaanisha Chadema. Kikao pekee ni cha Kujadili Katiba Mpya, ambako hata yaliyojadiliwa hakuyatekeleza ilivyokubaliwa
 
Dr. Slaa sio kosa lake. Uwezo wake wa kufikiri umekuwa wa kiwango cha Josephine Mushumbusi.

Anasema Kikwete haongei na wapinzani wakati Slaa ameonekana mara kadhaa Ikulu akinywa juice. Sasa sijui walikuwa wanakunywa juice kimyakimya!!!

View attachment 105628

huu ulikuwa mchakato wa awali kuhusu sheria ya marekebisho ya katiba, baada ya hapo CDM walisema kuna mambo bado hayajafanyiwa kazi na matukio kadhaa ya mauaji walitaka rais akae nao na wakubaliane kama nchi, je walikaa
 
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli ya kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake.

Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo kwa vile wanatambulika kama wauaji.

Alisema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Alimshangaa kuwataka kuzungumza na watu ambao Kagame anawaita wauaji wenye asili ya kundi la jeshi la Nterahamwe, lililokuwa linaangamiza Watutsi.

"Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani, hajachukua hatua dhidi wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi, alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda, amempandisha cheo," alisema.

Alisema Rais alitakiwa kuwaambia waje awapatanishe lakini si kuwaambia wazungumze na watu anaowatuhumu kuua Watutsi.

Kumezuka sitofahamu ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Rwanda, baada ya Rais Kikwete kutoa ushauri huo wakati wa mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia hivi karibuni.

Ushauri huo ulionekana kumchukiza Rais Kagame, anayedaiwa kuhutubia mikutano kadhaa nchini kwake na kutumia lugha ya matusi, kejeli na dhihaka dhidi ya Rais Kikwete na Tanzania.


CHANZO: NIPASHE

Huyu mwandishi wa Nipashe mbona kama karuka kitu kwenye hotuba ya Slaa? Au kuna kiswahili sijakielewa hapa. Haiwezekani msomi anayeongoza chama kikubwa na makini kama hiki asiongelee kabisa dhana ya umuhimu wa kuongea na adui kama nafasi inapatikana. Kwamba kwakwe lawama ndo limekuwa muhimu zaidi kuliko suluhisho la vita kongo. Au kuna kitu sijaelewa hapoa... Kuna kosa hapa nyumbani ndiyo, lakini je hilo linafuta umuhimu wa mazungumzo kati ya kagame na mahasimu wake?
 
Mfamaji, as I can see from your statements, I realize that you are very optimistic on the issue. The ability of the country is not judged by her size. Do you remember how Vietnam became a serious threat to US those days? Or can you tell what led to the nuclear bombing of Nagasaki and Hiroshima in Japan those years.

Size doesnt matter, I believe Kagame is well equipped to face Tanzania, that is why he is this much confident that he can hit Kikwete. We should not underestimate the power of any of our enemies when it comes to security issues. By the way, do you know why USA is so hesitant to attack North Korea, despite all her arrogance to USA?

lukolo you are very right. My point is some people ought be ignored sometimes. For the sake of reputation JK should not argue with Kagame because he could be a fool as well.
 
unaelewa maana ya ku argue au unaandika tu. Jk haku argue na Kagame,ndio akasema hakuona sababu ya kumjibu. akili yako inakufamaji kweli

I perfectly know what I mean. Kama JK angekuwa na busara hata chembe asinge bwabwaja huko Adis. Wanakutana kila mara EAC na njia nyingine za masasiliano zipo. Otherwise JK is a perpetrator of the whole unfounded saga. Sio kwamba JK hakumjibu. Alimjibu baada ya kumchokoza. WW vip huoni?
 
Kuna uwezekano Jk anatafuta vita ili aendelee kukaa ikulu?
 
Aliyoyaongea Dr Slaa ndio yalikuwa kichwani mwangu.Namuunga mkono Dr Slaa kwa hili.Tanzania hatuwezi kuingizwa Vitani kwasababu ya matatizo binafsi ya JK na Kagame.

matatizo binafsi ya jk na pk ni yepi hayo mbona hatuyajui?
 
ninamheshimu na kumkubali sana Dr.W.Slaa, kama ni kweli ametamka hivyo basi amepotoka sana ... the views presented are ill-advised and unpopular! wengi wataanza kumuangalia mzee kwa jicho la tatu ... atumie busara kurekebisha kauli yake ... vinginevyo naamini amenukuliwa vibaya!
 
Aliyoyaongea Dr Slaa ndio yalikuwa kichwani mwangu.Namuunga mkono Dr Slaa kwa hili.Tanzania hatuwezi kuingizwa Vitani kwasababu ya matatizo binafsi ya JK na Kagame.

matatizo binafsi ya Jk na Pk ni yepi hayo?
 
Jk aliongea vizuri sana hakuna mahara alipotaka vita tena katumia kauri nzuri sana ila slaa ndiyo kaharibu kwa kumuona jk kaksea na kumsapoti kagame ambaye amekuwa akitukana kila kukicha hivi jk angetoa kauri kama za kagame slaa angesemaje naona angeenda moja kwa moja icc kumshitaka jk huyu mzee kwa nini anamchukia sana jk na kwa nini akawa na roho mbaya kiasi hiki kwa jk na taifa.

Nyie wachumia tmbo wa CCM ndio taabu....yenu! Slaa kamkosoa JK, wewe unasema anaroho mbaya kwa taifa! hamna akili hapo!
JK aliropoka...! sasa ndio tuingie vitani kwa kumtetea mtu anaetukanwa kwa kuropoka kwake?
 
Aliyoyaongea Dr Slaa ndio yalikuwa kichwani mwangu.Namuunga mkono Dr Slaa kwa hili.Tanzania hatuwezi kuingizwa Vitani kwasababu ya matatizo binafsi ya JK na Kagame.

matatizo binafsi ya Jk na Pk ni yepi hayo?tusaidieni tusiokuwa na ufahamu nayo tuyaelewe ili tupate kuweka kumbukumbu zetu sawia,pia usisahau kutueleza hayo matatizo yalianza lini vile vile?
 
Back
Top Bottom