DOWANS wawasha Mitambo yao

Ndugu zangu watanzania, mabibi na mabwana, vijana na watoto, huu ni usanii ulipitiliza, Je inaingia akilini mitambo yeye utata, mkataba uliokatishwa, kesi imenguruma na bado anadai fidia mitambo yake kuwashwa. Na huu ni kwa mkataba upi. Au ndo maana mhe. Kikwete kasafiri ili aje kusema simtabui mmiliki wake na wala hajapata kumuona.

Kweli tunaye raisi, ambaye hata hamjui Rostam na wala hajapata kuongea naye!!!!!!!!!!!!!!!!!:A S 13:
 
Njoo Arusha ufike kiwanda cha SUNFLAG kwanza waulize kina wafanyakazi wangapi na kutokana na ukosefu wa umeme wanafanyakazi siku ngapi kwa wiki na shift ngapi kwa hizo siku.

Hasara inayopatikana katika uchumi kwa ujumla wake kutokana na tatizo la umeme nahisi kwa muda tutakaokuwa kwenye mgao mpaka mabwawa yajae inaweze kuzidi ile bei DOWANS waliotaka kuiuzia Tanesco mitambo.

Mkuu,
Hiyo hasara tumeshapata sana, ni bora tukataabika kwa mda ile tuje na suluhu ya kudumu, haya mambo ya umeme wa dharura yatatusesa hadi mwisho tusipoangalia.

Halafu hukohuko Arusha nimesikia jana mwekezaji anavuna matawi ya msitu wa hifadhi halafu analipa Tsh.1,000/ton, huu ni uwekezaji au wendawazimu?
 
Mkuu nafikiri huu ni ushindi kwa RA na wenzake, kama wamewasha mitambo yake unategemea nini tena?

Hakuna ushindi Mkuu hapa, kwanza itabidi huo mkataba wa kuwashwa tena mitambo ya Dowans ujulikane ni nani aliyeuruhusu na details zote za mkataba ziwekwe hadharani. Pili kuwashwa mitambo hiyo hakuhusiani kabisa na malipo ya $95m.

Mhhhh! Ndiyo maana yule January Makamba alipiga debe sana hivi karibuni kwamba ni lazima mitambo iwashwe kumbe walikuwa wameshaamua hivyo maana hata wiki mbili hazijaisha tangu atoe kauli hiyo mitambo imewashwa. Uongozi wa nchi hii hovyo kabisa!

Mitambo iliyodaiwa kuuzwa nchi za nje kumbe ulikuwa ni UWONGO MTUPU!

~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~@@~

JENERETA za kufufua umeme za kampuni ya Dowans Tanzania Ltd ambazo zinatumia gesi asilia na ambazo ziliibua mjadala mkubwa wakati serikali ilipotaka kuzinunua, zimeuzwa nje ya nchi kwa zaidi ya Sh101 bilioni.

Kampuni ya kufua umeme ya Cyprus, Independent Power Corporation (IPC) ndiyo iliyonunua mitambo hiyo yenye uwezo wa kuzalisha megawati 112.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa nchini Uingereza na mkurugenzi mtendaji wa IPC, Peter Earl, kampuni yake imeshafikia makubaliano ya kununua mitambo hiyo na kampuni ya Dowans Tanzania.

Kwa mujibu wa habari za kuaminika kutoka Shirika la Umeme (Tanesco), mitambo hiyo imeuzwa kwa kampuni ya IPC kwa gharama ya dola 77 milioni za Kimarekani (sawa na zaidi ya Sh101 bilioni za Kitanzania).

Pamoja na kwamba Tanesco hawakuhusishwa katika uuzwaji wa mitambo ya Dowans, imeuzwa kwa zaidi ya dola milioni 77 za Kimarekani kwa kampuni ya IPC, kilisema chanzo chetu
Akizungumza na gazeti hili jana mbunge Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe aliitaka serikali isiruhusu mitambo hiyo kuondoka nchini.

Zitto, ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), alifafanua kwamba mitambo hiyo haipaswi kuruhusiwa kuondoka nchini kutokana na kuwepo kwa kesi baina ya Tanesco na Dowans pamoja na kampuni hiyo kudaiwa Sh12 bilioni na serikali.

Tunawezaje kuacha mitambo iondoke wakati hatuna umeme,alihoji Zitto na kuongeza: Serikali isiruhusu mitambo ya Dowans iondoke nchini kwa kuwa kampuni hiyo inadaiwa na serikali. Pia kuna kesi mahakamani.

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo alipotafutwa na Mwananchi.
Kwa sasa siwezi kusema lolote kuhusu hizo taarifa za uuzwaji wa mitambo ya Dowans, alisema Ngeleja.

Taarifa za kuuzwa kwa mitambo hiyo ziliibuliwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam katika ofisi ndogo za Bunge, wakati wa kikao cha kujadili ripoti ya hesabu za Tanesco za mwaka 2008.
Ripoti hiyo ilikuwa imewasilishwa kwa kamati ya POAC.
Taarifa ya kuuzwa kwa Dowans ilibainishwa na Zitto katika kikao hicho.

Hata hivyo mwanasheria wa Tanesco, Subira Wandiba alisema mitambo hiyo imezuiwa na Tanesco ambayo iliomba amri ya mahakama ili kama shirika hilo la serikali litashinda, mitambo itumike kama fidia. http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=19144
 
Mkuu,
Hiyo hasara tumeshapata sana, ni bora tukataabika kwa mda ile tuje na suluhu ya kudumu, haya mambo ya umeme wa dharura yatatusesa hadi mwisho tusipoangalia.

Halafu hukohuko Arusha nimesikia jana mwekezaji anavuna matawi ya msitu wa hifadhi halafu analipa Tsh.1,000/ton, huu ni uwekezaji au wendawazimu?
Only possible in our beloved mama land.
 
Mwaka jana Bunge liliagiza tanesco wakanunue mitambo yao lakini Jk aliweka ngumu kwa sababu lengo lake ni kuhakikisha anajenga mazingira ya mitambo ya DOWANS inunuliwe tu tutake tusitake...........................................

Kila Raisi wa CCM baada ya nyerere amekuwa mjasiria mali mara tu baada ya kuingia Ikulu na biashara aifanyayo ni kulipora taifa hili masikini na changa duniani.......................
 
Tunachekelea mimi nawaambia nchi inauzwa. Shida tutakayopata baada ya kukomboa nchi hii ni kwamba tutakuwa na madeni ya ajabu. Tuamke sasa. Hatuhitaji mitambo ya Dowans tunahitajia mitambo tunayomiliki sisi wenyewe nukta.
 
Mwaka jana Bunge liliagiza tanesco wakanunue mitambo yao lakini Jk aliweka ngumu kwa sababu lengo lake ni kuhakikisha anajenga mazingira ya mitambo ya DOWANS inunuliwe tu tutake tusitake...........................................

Kila Raisi wa CCM baada ya nyerere amekuwa mjasiria mali mara tu baada ya kuingia Ikulu na biashara aifanyayo ni kulipora taifa hili masikini na changa duniani.......................

Hivi kwanini Serikali isiamue kununua mitambo yake mipya ya kupunguza adha ya mgao wa umeme badala ya kuendeleza hiki kizungumkuti cha Dowans kila kukicha? Kwa mfano zile 90m ambazo wanatakiwa wapewe Wabunge ili kununua magari mapya zitasaidia sana katika ununuzi wa mitambo mipya ili kuachana kabisa na hawa mafisadi wa Dowans. Si ajabu hiki kizungumkuti cha Dowans kinaweza kuendelea mpaka 2015 au hata zaidi maana ni miaka mitano sasa mafisadi wa Dowans alias Richmond waanze ufisadi wao nchini.
 
Mkuu,
Hiyo hasara tumeshapata sana, ni bora tukataabika kwa mda ile tuje na suluhu ya kudumu, haya mambo ya umeme wa dharura yatatusesa hadi mwisho tusipoangalia.

Halafu hukohuko Arusha nimesikia jana mwekezaji anavuna matawi ya msitu wa hifadhi halafu analipa Tsh.1,000/ton, huu ni uwekezaji au wendawazimu?[/QUOTE]

Kwa uwezo wa watendaji wetu wa Serikali wamefikiri TShs. 1000 is the reasonable amount to go to the Government Confor the rest......
 
Yaani hili swala la umeme sasa limekuwa kama daktari aliyekosa maadili anabaka mgonjwa. Tutafanyaje sasa
 
Hivi kwanini Serikali isiamue kununua mitambo yake mipya ya kupunguza adha ya mgao wa umeme badala ya kuendeleza hiki kizungumkuti cha Dowans kila kukicha? Kwa mfano zile 90m ambazo wanatakiwa wapewe Wabunge ili kununua magari mapya zitasaidia sana katika ununuzi wa mitambo mipya ili kuachana kabisa na hawa mafisadi wa Dowans. Si ajabu hiki kizungumkuti cha Dowans kinaweza kuendelea mpaka 2015 au hata zaidi maana ni miaka mitano sasa mafisadi wa Dowans alias Richmond waanze ufisadi wao nchini.
Mkuu,
Kitaendelea hata baada ya 2015 kwa sababu hakuna mkakati tuliouona(unaopimika) ambao ni suluhu ya kudumu ya tatizo hili la umeme hapa kwetu. Halafu kumbuka Dowans ni mrija wa watu hivyo serikali kununua na kumilika mitambo yake ni kukata mrija huo.

Tutaendelea kuumia kwa sababu watu hawa wamekosa aibu na hakuna wanayemwogopa.
 
Ni bora wamewasha. I dont care how much they will pay them. Let them pay 100 trillions, I don't care. What I care ni kama kuwasha huko kutapunguza makali ya mgao wa umeme, basi. Tulipiga kelele wakavunja mkataba wa awali, tukaokoa mamilioni yaliyokuwa yanalipwa kila siku, then what.. maisha yalikuwa mazuri zaidi? Dawa ziliongezeka hospitali?, barabara zilijengwa zaidi? Mboga nyumbani nilibadilisha, au idadi ya bia ninazokunywa pale grocery kwa mama Manka ziliongezeka? Nimeendelea kuishi katika matatizo yale yale, yet umeme ukapungua na mgao ukaanza.

Wacha wawashe. Hii nchi ni ya kifisadi, na hata wasipowalipa Dowans, hizo fedha hawashindwa kuzila. Hii nchi inaongozwa na vilaza, na hata wasipowalipa Dowans hawataweza kuwa na njia mbadala ya ktupatia umeme. What we are demanding from them is beyond their thinking and operating capacity.

Njia ya kuepuka haya matatizo ilikuwa ni kuwaondoa madarakani, na hatukufanya hivyo, then let them do what they are capable to deliver, otherwise they will do nothing. Dowans isiwashwe, umeme ukosekane na bado hela zinaliwa. Kuliko kula hizo hela bure, bora ziliwe na Dowans angalau umeme kidogo tupate.

Wacha wawashe... sasa kesho watupe ratiba mpya inayoonyesha kupungua kwa mgao... Kudadadadadeki.
 
Hivi kwanini Serikali isiamue kununua mitambo yake mipya ya kupunguza adha ya mgao wa umeme badala ya kuendeleza hiki kizungumkuti cha Dowans kila kukicha? Kwa mfano zile 90m ambazo wanatakiwa wapewe Wabunge ili kununua magari mapya zitasaidia sana katika ununuzi wa mitambo mipya ili kuachana kabisa na hawa mafisadi wa Dowans. Si ajabu hiki kizungumkuti cha Dowans kinaweza kuendelea mpaka 2015 au hata zaidi maana ni miaka mitano sasa mafisadi wa Dowans alias Richmond waanze ufisadi wao nchini.


Hawana uwezo wa kufanya hivyo.. You are demanding too much from them Babu...
 
Kwangu siyo goodnews mpaka nijue wamewasha kwa makubaliano gani. So u better keep us informed.
 
Wakuu hivi ninavyoandika ni kuwa mtambo mmoja wa Dowans aina ya LM6000 PD 40MW uliopo site A nyuma ya ghorofa la Tanesco umewashwa na hadi sasa unazalisha 37MW. Nitawaletea habari zaidi lakini nina uhakika kuwa hawataweza kutembeza mitambo yao yote kutokana na sababu ambazo nitazieleza hapo baadae. Kiufundi mtambo huo kwa sasa ume-substitute mtambo wa Songas ambao kwa sasa upo down kutokana na kupata ajali ya moto hapo jana.
Habari kamili baadae.

hivi hakuna aliyeokota viazi vya Goms akawapa mateja mishale ya usiku wakatupia nyavuni?
 
Back
Top Bottom