DOWANS wawasha Mitambo yao

DOWANS wameingilia mlango wa nyuma. Wameingia mkataba na SONGAS. Umeme wao wanawauzia SONGAS. Kisha SONGAS inaiuzia TANESCO. Tafakari.

Nimekupata mkuu at least umeandika kitu cha maana badala ya porojo kila siku,nilipatwa na mshangao speed ya TANESCO na DOWANS kuingia mkataba ilikuwa kubwa sana kumbe wazee wa dili walitafuta njia rahisi kama kawaida yao.
 
Al Adawi amesema amekuja kuongea na tanesco, wala hana shida na ngeleja. Na amesema yuko tayari kupunguza gharama badala ya bilioni 94 tulizotakiwa kumipa basi atatuunguzia kidogo waau tupate kiasi cha kuwalipa waathirika wa makombora gongo la mboto.
sasa kama jana tu ametangaza kuongea na tanesco na leo mtambo umewashwa, hiyo ni kusema aliitisha waandishi wa habari huku akiwa amemaliza mazungumzo na tanesco, vinginevyo watakuwa wamezungumza fasta kama kawaida yao inapokuja suala la dharura ni wepesi wa kufanya negotiation na kufikia maamuzi.

Braza... sisi hatutaki walipwe kabisa na sio kupunguza deni... we unafikiri atapunguza kwa kiasi gani??
 
Nadhani huajielewa dahana ya soko huria. IMF ilisema serikali ijotoe katika kufanya biashara na iruhusu private sectort kufanya shughuli. IMF haimaanishi kuachia wezi wapore au mikataba ya hovyo, wanachosema ni serikali isimamie shughuli na isijishirikishe kama mfanyabiashara.
Marekani waliachia soko huru bila serikali kuingilia matokeo yake ni economical crisis tunayoiona. Obama ameingilia kati na sasa pale Wall street kuna rules and regulations.
Margreth Sacher alipobinafsisha kila kitu UK, ilifika mahali wananchi wake wakamwambia no! kaa pembeni, hawezi kubinafsisha Posta na Reli. Elewa kuwa soko huria si soko holela na serikali lazima iwajibike kuhakikisha wananchi wake wanatendewa haki na wenye pesa.
Hakuna tatizo la shirika binafsi kuuzi umeme TANESCO, tatizo ni kuwa akina RA hawafanyi biashara ni matapeli wanaotaka kulipwa kwa hila mabilioni ya fedha. Bado serikali ingeliweza kuwa ''BAIL OUT'' TANESCO wanunue mtambo kama wa Dowans, lakini kwa hila BoT wame bail out Richmond/Dowans kwa sababu tu kuna watu wachache wanafaidika na mgao wa RA. hapa ndipo hasira za wananchi zilipo, si privatisation! Kutokana na madudu ya RA/EL leo tunapandishiwa bei ya umeme ili tumlipe RA. Jiulize, hivi kama TANESCO haina pesa za kujiendesha, inapata wapi pesa billion 100 kumlipa Dowans! huu si upuuzi wa kutufanya matutusa.

Sasa, tunasikia umeme umewashwa, maana yake ni kuwa Dowans inatambuliwa na kama inatambuliwa Richmond inapata uhalali, na ni kwa uhalali huo Lowasa anakuwa safi, Zigo linakwenda kwa Mwakyembe na Sitta wazalendo wenye uchungu na nchi hii.
Kwa taarifa tu, hujuma za umeme zimeingia Mabwawani, Songas n.k ili kujenga mazingira ya Dowans kuzalisha umeme. Tulijua kuna jambo pale January alipoteuliwa kuwa mwenyekiti wa nishati, akaanza na safari mtera, akaja na wazo la mkataba w miezi 6, Ngeleja akasema kunnuua Dowans si tatizo na kama watauza umeme hakuan shida, jenerali kaingia kinyemela Dar, jenerata zinawashwa siku inayofuata!
Tukimruhusu RA aendelee hivi tujue kuwa tunamuandaa Jenerli Farah Aideed, naye alikuwa na power kama ya RA.
Bora tukae gizani kuliko kumhalalisha fisadi huyu. Tusimfundishe panya kula sufi ipo siku atatafuna vidole.

sad!

Umeandika habari nzuri, ila basi wakati mwingine uangalie spelling unapondika, ina udhi sana kusoma maneno na majina yaliyokosewa kuandikwa. Inavuruga mtiririko wa usomaji. Tafadhali sana.
 
Tukiendelea kuruhusu mediocre performance toka kwa hizi Serikali za CCM miaka nenda miaka rudi nchi yetu itabaki nyuma sana kimaendeleo huku hao wanaojiita Viongozi wakijiendelea kujilimbikizia mali wao, familia zao na marafiki wao wa karibu. Rwanda waliuana kwa mamilioni mwaka 1994 lakini sasa hivi nchi hiyo katika maendeleo inafanya vizuri sana ukilinganisha na sisi "wenye amani" ya miaka nenda miaka rudi. I am not demanding too much ninachotaka kuwe na kuwajibika pale hawa wanaojiita Viongozi wanaposhindwa kutimiza wajibu wao kama Viongozi wa nchi au wizara mbali mbali. Tumeona kwa mfano mabomu ya Mbagala miaka miwili iliyopita hakuna aliyewajibika kwa kujiuzulu au kufukuzwa kazi, miaka miwili baadaye mabomu ya gongo la mboto wamekuwa na kiburi cha kuweza hata kutamka kwamba "sijiuzulu" si ajabu miaka miwili mingine mabomu hayo yatalipuka tena katika moja ya sehemu hizo au inaweza kuwa Lugalo.

Rais anasimama na kuwadanganya Watanzania kwamba hawajui wamiliki wa Dowans wakati ni uongo wa hali ya juu. Hivi wewe kama Rais wa nchi baada ya sakata lote hili la Dowans hata kama huwajui wamiliki wa Dowans huwezi kuwauliza wasaidizi wako toka wizara ya nishati wakupe briefing kuhusu Dowans na hatimaye uwajue wamiliki wa Dowans? Iweje Ngeleja awajue wamiliki wa Dowans wakati Kikwete anadai hawajui? Kama wewe unaruhusu uzembe na ufisadi wa hali ya juu unaofanywa na hii Serikali iliyopo madarakani kila la heri lakini wengine hatukubaliani na hali hiyo na hivyo tuna haki ya kujadili hapa bila wewe kutaka kuonyesha kwamba...we're demanding too much from them.

Nilipokuwa darasa la pili ukiniuliza tano toa tau, najibu inabaki mbili. Lakini ukiniuliza tatu toa tano, nilikuwa najibu HAIWEZEKANI. Nilipofika darasa la sita, nilijua kumbe tatu toa tano ni hasi mbili.
Ukimuuliza Kikwete 'tatizo la umeme (na mengine) Tz litatatuliwaje, atakujibu HAIWEZEKANI, lakini kwa mtu mwenye upeo kama walio nao watanzania wengi, atakupa jibu rahisi tu na sahihi. Tatizo la umeme linatatulika lakini kwa uwezo na upeo wa viongozi tulio nao, HAIWEZEKANI.
 
Mramba alisema hata watanzania tule majani ilikuwa lazima ndege ya raisi inunuliwe, mimi nimefikiwa uamuzi wa kukaa gizani kusubiri mvua ya Mungu ijaze mabwawa ya Mtera na Kidatu kuliko umeme wa RA, JK na serikali yake wametusaliti na kututupa kamwe si Mungu, na njia pekee ya kutuokoa watanzania kwa sasa nikupitia matatizo.

umenifurahisha sana kwakweli nilikuwa sijafurahi siku nyingi
 
kwa hiyo mgao umeisha? kwangu hawajakata umeme tangu juzi, watueleze imekuwaje ni mabwawa yamejaa au ndo kimya kimya dowans wanakamata mshiko wao
 
AM WAITING KWA HAMU KUBWA SIKU TUTAKAYOINGIA BARABARANI KUWATOA HAWA WATAWALA BOMU....:rain:


watanzania tulishalogwa tiyari....KILA MTU ANAKULA 10 YEARS ANAVUNA NA KUONDOKA,SISI TUNASEMA TUNA DEMOKRASIA VIONGOZI WANAACHIANA MADARAKA...KUMBE SISI TUMEKUWA KM SHAMBA..VILE,WANAVUNA NA KUMRUSHIA MPIRA MWINGINE.HAWANA WANALOTUFANYIA....LA MSINGI NI KUANDAMANA KUONDOA SISIEM.SI KIONGOZI.
 
nchi inaendeshwa vipi na majenereta?
maduka kariakoo yatumie majenereta, na nchi nayo inatumia majenereta? hii kali..
 
Endapo shida zetu (kama hii ya mgao wa umeme) zikitufanya tuhalalishe mambo ambayo ni haramu basi Taifa limekwisha.

Nauliza; uko tuendako tukiwa na matatizo mengine si tutapokea hata hela za madawa ya kulevya hili tuondokane na hilo tatizo?

Watu binafsi ndiyo uendesha maisha kwa mtindo huo hili kuokoa nafsi yao lakini serikali zinatakiwa kuendeshwa kwa principles!

Ni makosa kuendesha serikali kama familia kwa sababu unalolifanya leo linakuwa ni msingi wa yatakayotokea kesho.

Tukiruhusu hili la Dowans ipo siku tutasikia serikali inaingia tena mkataba na kampuni kama KAGODA!


TAFAKARI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Huuu ni usenge jazz band, hivi serikali yetu chini ya sisiemu na mkwere wanashindwa kununua mitambo kama ya dowans? Mbona wanaweza kununua mashangingi VX V8 kwa mawaziri, makatibu, wakurugenzi na juzi tu wamewalipa wabunge 90mil*310, huu ni ujinga kabisaaaaaaa, sijui viongozi wetu wanafikiri kwa kutumia ubongo au kamasi.Pumbavuuuuuuuuuuuuuuuuu.
 
Wakuu hivi ninavyoandika ni kuwa mtambo mmoja wa Dowans aina ya LM6000 PD 40MW uliopo site A nyuma ya ghorofa la Tanesco umewashwa na hadi sasa unazalisha 37MW.

Nitawaletea habari zaidi lakini nina uhakika kuwa hawataweza kutembeza mitambo yao yote kutokana na sababu ambazo nitazieleza hapo baadae. Kiufundi mtambo huo kwa sasa ume-substitute mtambo wa Songas ambao kwa sasa upo down kutokana na kupata ajali ya moto hapo jana.

Habari kamili baadae.
...thanks for the infomation!!! i'm eager for more and more infoz!
 
Wakuu hivi ninavyoandika ni kuwa mtambo mmoja wa Dowans aina ya LM6000 PD 40MW uliopo site A nyuma ya ghorofa la Tanesco umewashwa na hadi sasa unazalisha 37MW.

Nitawaletea habari zaidi lakini nina uhakika kuwa hawataweza kutembeza mitambo yao yote kutokana na sababu ambazo nitazieleza hapo baadae. Kiufundi mtambo huo kwa sasa ume-substitute mtambo wa Songas ambao kwa sasa upo down kutokana na kupata ajali ya moto hapo jana.

Habari kamili baadae.

Updates, 22.02.2011:
Wafanyakazi wa Dowans wapo katika pilikapilika za kufanya marekebisho madogo madogo katika mashine zao ambazo bado hazijawashwa nazo ni mashine tatu zenye uwezo wa kuzalisha 20-25MW kila moja. Pilikapilika hizi zinaonesha huenda wanataka kuwasha mashine nyingine zaidi. Lakini bado nasisitiza Gesi haitoshi. Tusubiri tuone!
 
:A S 13::decision:sasa hichi kizungumkuti,
mi naomba kuelewesha,iwapo kesi imeisha,mahakama imeamua tumlipe,sisi tumevunja agizo la mahakama,mdai kakaa na mdaiwa kaamua amlipe+ kuikodi hiyo mitambo,
yani hapa kama sielewi akili inazunguka tuu
sheria ya wapi hiyo???:A S 20::bowl:
 
<p>
Hiii nchi kweli kiraka...
</p>
<p>&nbsp;</p>JAMANI JAMANI MBONA MABABU ZETU KINA MKWAWA MELI KINJIKITILE NK TUNA AMBIWA WALIKUWA MAJASIRI MPAKA WAKOLONI WANAKIMBIA SISI TUNA LAANA GANI ??? MPAKA TUNATAWALIWA NA WAKIMBIZI KAMA ROSTAM ??
 
Mkuu jana nilikupinga sana, samahani.... nimeuliza the same question, KUUNGUA SONGAS NA KUWASHWA DOWANS KUNATUAMBIA NINI??

INAKUAJE MTU MWENYE KESI NA SISI AND ALL SORTS OF TROUBLES AKUBALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SISI?? HOW COME MITAMBO ILIUZWA KWA KAMPUNI YA KIGENI IBAKI UBUNGO? ILIKUA INALINDWA KWA GHARAMA YA NANI?

Kwenye red:
Capacity charge mkuu.
Mitambo kuwepo tu pale hata kama haizalishi, inaigharimu Tanesco zaidi ya USD 200,000 kwa siku. Na hii si kwa Dowans tu bali ni kwa makampuni yote yanayoiuzia umeme Tanesco. Wakizalisha, mahesabu mengine ambapo huwa wanauza umeme kati ya sh. 90-120 kwa unit.
Alstom kule Mwanza haijawahi kuzalisha lakini walikuwa wanalipwa kiwango kama hicho kwa kipindi cha zaidi ya miaka mi3. Sina hakika kama wameshaondoa mitambo yao.
Tatizo letu ni lile lile; Mikataba iliyosababishwa na tamaa ya baadhi ya watu ambao siwezi kuwaita "Watanzania".
 
Kwa utawala huu ndugu zangu tutakoma! Yaani mpaka miaka mitano iishe sijui tutakuwa na hali gani?? Viongozi wameshindwa kuwa wabunifu!! Kama hawawezi kubuni vya kwao si waige basi kutoka kwa wenzetu!!
 
Back
Top Bottom