Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Mh.Zitto Kabwe kwa siku za hivi karibuni amewachanganya Watanzania kutokana na misimamo yake yanayokanganya.Kwanza kabisa ni kwenye uchaguzi wa Tarime kuhusu vurugu juu ya kifo cha Chacha Wangwe.Pili malumbano na kamati ya bunge ya nishati na madini kwa kamati yake kuingilia kazi za kamati hiyo.Tatu kuunga mkono ununuzi wa mitambo iliyopatikana kwa njia ya utapeli na kukiuka maazimio ya kamati teule ya bunge aliyoshiriki maamuzi yake.Kutokana na hayo niliyoyataja hapo juu Mheshimiwa huyu inaonekana anapewa sifa asizostahili kwani hata operesheni fichua ufisadi na sangara yeye si mwasisi kahusishwa tu.Sasa ilituendelee kumwamini kuna haja zozote zinazowezesha hiyo? Wana JF karibuni mchangie.
 
Nashukuru kwa kuanzisha huu mjadala,tunamuomba Zitto atueleze hapa jamvini mazungumzo aliyoyafanya na Rostam pale TILAPIA Hotel pale Mwanza wiki chache kabla ya yeye kuanza kutetea mpango mzima wa manunuzi ya mitambo tata ya DOWANS (dada yake RICHMOND).
 
Nashukuru kwa kuanzisha huu mjadala,tunamuomba Zitto atueleze hapa jamvini mazungumzo aliyoyafanya na Rostam pale TILAPIA Hotel pale Mwanza wiki chache kabla ya yeye kuanza kutetea mpango mzima wa manunuzi ya mitambo tata ya DOWANS (dada yake RICHMOND).

Nikisema huu ni upumbavu mtasema ninatukana members. Huu ni ujinga wa siasa za Tanzania za kuzusha kitu ambacho mtu unajua kabisa ni uongo. Mara ya mwisho nimeenda Mwanza ni Disemba 5 wakati wa operesheni sangara. Sijarudi Mwanza tena.
Mara ya mwisho nimefika Hotel Tilapia ni mwaka 2005. Nikiwa Mwanza ninakaa hotel moja tu.

Kwa nini watu wanapenda kusema uongo?
 
Nikisema huu ni upumbavu mtasema ninatukana members. Huu ni ujinga wa siasa za Tanzania za kuzusha kitu ambacho mtu unajua kabisa ni uongo. Mara ya mwisho nimeenda Mwanza ni Disemba 5 wakati wa operesheni sangara. Sijarudi Mwanza tena.
Mara ya mwisho nimefika Hotel Tilapia ni mwaka 2005. Nikiwa Mwanza ninakaa hotel moja tu.

Kwa nini watu wanapenda kusema uongo?

Zitto ! Zitto ! Zitto ! The first time I saw you ilikuwa ni mwaka 2002/2003 Katika Maandamano yaliyolenga kupinga Marekani kuivamia Iraq pamoja na watu wengine nadhani walikuwepo wahadhiri kadhaa wa plae mlimani pamoja na watu wengi ambao niliwaita ni Wapambanaji. From there Zitto you inspired me a lot, sio mimi tu hata watu wengi unawa inspire. Do you remember Zitto during Operesheni Sangara, Watu walikulaki kama Mfalme, Watu waliimba Obama Obama Obama, Wakawachangia, mwenye ndizi akatoa ndizi, mwenye muhogo haya, mwenye mia tano sawa lakini watu walihamasika sana!

Siyo watu wote wanapenda hiyo hali ukizingatia wengi wanapokelewa kwa Matusi na Kuzomewa! Zitto hata watoto wadogo wanakujua na wanapenda kukusikiliza wewe! Wewe ni kama role model yao, vijana wengi umewasaidia kujenga moyo wa kizalendo sasa Naomaba Usituangushe Mkuu

Anaglizo! Simlaumu sana Ndanda to Lomwe, ni post yake ya sita tu naamini hajajiandisha kimakosa na anajua nini anafanya, anajua kile anachozungumza ni Uongo but huyo hawezi kuwa wa Mwisho ku take advantage ya Kukumaliza kama ni Ndege basi upo kwenye Target Nzuri situ ya Mafisadi bali hata ya Maadui zako kisiasa!

USHAURI! Soma Signature yangu hapo chini na uelewe kwamba UMESIMAMA JUU YA MABEGA YA WAZALENDO WENGI SANA!
 
Nikisema huu ni upumbavu mtasema ninatukana members. Huu ni ujinga wa siasa za Tanzania za kuzusha kitu ambacho mtu unajua kabisa ni uongo. Mara ya mwisho nimeenda Mwanza ni Disemba 5 wakati wa operesheni sangara. Sijarudi Mwanza tena.
Mara ya mwisho nimefika Hotel Tilapia ni mwaka 2005. Nikiwa Mwanza ninakaa hotel moja tu.

Kwa nini watu wanapenda kusema uongo?

Zitto,

Mheshimiwa mmoja aliyekupa thanks hapo juu aliwahi kutuambia hivi: Waziri Masha asijitetee kwamba we have the wrong date za siku alipokuwepo hotelini Ulaya ambapo anashutumiwa kukutana na kampuni ya vitambulisho. Asituonyeshe passport eti mara ya mwisho alisafiri lini, no no no, aseme hivi: aliwahi kukutana nao au hajawahi?

Sasa basi, Mkuu huyo, anaekutetea hapa kuhusu msimamo wako wa Dowans ni kwamba anakuonea aibu. Ungekuwa wewe ni Masha, angesema hivi: Umewahi kukuatana na the controversial political financier Rostam Aziz? Jibu ndio au sio. Lini mara ya mwisho? Na Mliongelea nini? Kwa nini?

Hatutaki kujua, hatujali, kama ni hotelini, vichochoroni, usiku, Jumapili, siku iliyotajwa au the wrong date, No!

Umewahi kukutana na the controversial political financier Rostam Aziz? Ndio ama hapana?

Ukimaliza hilo, eleza imekuwaje Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mahesabu, Mh. Kilasi, amekuruka kwamba uliyodai kwamba mmekubaliana kwenye kamati yenu yamemshangaza? Hayajui!


IPP MEDIA
09 Mar 2009
By Simon Mhina


Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Estherina Kilasi ambaye pia ni Mbunge wa Mbarali (CCM)...alisema maneno ambayo yamemkariri Mwenyekiti wao (Zitto Kabwe) yalikuwa maoni yake binafsi na wala sio ya kamati kwa vile hakuna hata kikao kimoja ambako walikubaliana na ombi la kununua mitambo hiyo.

``Wala hatujawahi kutoa ushauri wowote juu ya suala hilo, zaidi ya kuwaelekeza Tanesco walifikishe kwa kamati husika ya Nishati na Madini,``alisema

Akifafanua, alisema kilichotokea siku hiyo ni semina ambayo Tanesco waliiandaa na kuwakaribisha wajumbe wa Kamati hiyo kwa lengo la kuwaelezea mipango ya kununua mitambo ya Dowans kwa kuwa wana kiasi cha Sh. bilioni 60 kwa ajili hiyo.

``Sisi tuliwahoji kama mnazo Sh Bilioni 60 mnashindwajwe kuongezea kidogo ili mnunue mitambo mipya? Vilevile tukawahoji hivi mambo haya mnayotuambia kwenye semina wameyapeleka kwa wahusika ambao ni Kamati ya Niashati inayoongozwa na William Shelukindo?,`` alisema Kilasi na kuongeza:

``Baada ya hapo tuliwashauri suala hilo walifikishe kwa wahusika (Kamati ya Madini) na hakuna hata mahali pamoja tulipolitolea uamuzi suala hilo kwa vile halituhusu.``

Mbunge huyo alisema kufuatia kauli za Zitto ambazo zimezua malumbano, na kuifanya Kamati yao ionekane ina `walakini` wanamsubiri kwa hamu arejee ili wamuweka kiti moto.

``Unajua baada ya semina ile mimi nilienda Zambia, huku nyuma ndo nikasikia malumbano, lakini baada ya kurejea nimewauliza wenzangu na hasa makatibu wanaoandika muhtasari, kama kuna kikao kingine kimeketi na kutoa uamuzi, lakini wakasema hapana. Sasa tunamsubiri Zito arejee safarini ili tumuulize kulikoni? ``Alisema.

 
Zitto,

Sasa basi, Mkuu wako anakuonea aibu. Ungekuwa wewe ni Masha, angekuuliza hivi: Umewahi kukuatana na the controversial political financier Rostam Aziz? Jibu ndio au sio. Lini mara ya mwisho? Na Mliongelea nini? Kwa nini?

It'll be the stupidist question ever! Rostam ni mbunge, Zitto ni Mbunge! akijibu "tulikutana Bungeni, tukazungumza mambo ya Bunge na kwa sababu ni Mbunge mwenzangu" halafu niseme nini?

Sasa kama haya ndiyo maswali yako ya kiuandishi, kwa kweli inasikitisha. Zamani maswali haya yalikuwa yanaitwa "maswali ya jela". Umeenda jela halafu umemkuta rafiki yako yuko kafungwa halafu unamuuliza "na wewe umefungwa?" akujibu kuwa yuko picnic?

Umewahi kukutana na the controversial political financier Rostam Aziz? Ndio ama hapana?

Hili naweza kumjibia hata kwa kufumba macho "ndiyo!" Halafu "controvesial political financier Rostam" what on earth is that.. RA is more than that, he is the Member of Union Parliament. Hata mimi nimezungumza naye mara mbili does that mean what?

This is clumsy and pathetic! You better elevate your game bwana kama unataka kukosoa waandishi.

Ukimaliza hilo, eleza imekuwaje Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mahesabu amekuruka kwamba uliyoyasema yametokea kwenye Kamati yenu yamemshangaza? Hayajui.

hili angalau ni swali ambalo unaweza kuhitaji majibu yake.
 
Nikisema huu ni upumbavu mtasema ninatukana members. Huu ni ujinga wa siasa za Tanzania za kuzusha kitu ambacho mtu unajua kabisa ni uongo. Mara ya mwisho nimeenda Mwanza ni Disemba 5 wakati wa operesheni sangara. Sijarudi Mwanza tena.
Mara ya mwisho nimefika Hotel Tilapia ni mwaka 2005. Nikiwa Mwanza ninakaa hotel moja tu.

Kwa nini watu wanapenda kusema uongo?

Ya uongo ni mengi sana yamesemwa na yatasemwa. Waliosemwa uongo ni wengi na wataongezeka. Walioumia kwa uongo ni wengi na wataongezeka. Lakini pia Zitto nimjuaye si huyu anayekasirika. Sitaki kuamini Zitto anaweza kukasirika na akaweka hasira katika maandishi. Sentesi ya kwanza haikuwa na sababu kabisa ya kuwapo. Wanasiasa vijana hebu tusaidieni kwa kutulia. Masha alikasirika na kumtimuwa mwandishi wa Nipashe kwenye mkutano wake na waandishi. Haikuwa dawa. Zitto bado unaheshimika na wanaokulalamikia wapongeze kwa kuwa wote ni wale wanaokupenda sana.

Leo kuna mtu nimemsikia akisema, "Mtu unayempenda sana akikosea/akikukosea utaumia sana na uzito wa maumivu ni mkubwa mno"... na humu hasira zote unazoziona ni kwa sababu tu unapendwa na si kwa chuki. Sikatai wapo wachache sana (hasa JF) wanaokuchukia. Wengi wanaandika kwa mapenzi mema na wanataka uwabebe katika hii vita.

Niliwahi kusema na sasa nasema WAZI kwamba hii ni VITA na VITA HAINA MACHO. Vita si kitu kizuri, maana watu wanauana wao kwa wao. Na katika hii vita ujue kuna MAUAJI na kwa kweli hakuna kitu cha KUHALALISHA MAUAJI kwa namna yoyote ile. Hata muuaji huwa anahitaji kuishi hadi AHADI yale ifike. Sasa wameuwawa wengi katika hii vita. Wako waliokufa na sasa tunashuhudia makaburi yao. Wako waliokufa bila HATIA (kwa sababu tunaamini wako upande wetu wa vita) na sasa tunaomboleza. Wako waliokufa kwa HAKI (kwa sababu wako upande wa ADUI) na sasa tunachekelea.

Vita hii imeanza muda mrefu sana, tokea mwaka 1995. Wengi sana wamejeruhiwa na wengine KUFA. Mwaka 2000 wakajeruhiwa wengi na wengine KUFA. Mwaka 2005 wakajeruhiwa wengi na wengine KUFA. Baada ya mwaka 2005 vita iliendelea na ikaua na kujeruhi makamanda kadhaa wa upande mmoja pale Dodoma. Sasa vita imepamba moto na tunakaribia kuteka MJI MKUU (mwaka 2010) na vita inapamba moto sana, nakuona ZITTO kama majeruhi wa kwanza na usipoangalia UTAKUFA. Sitaki na sitokubali (wengi wataniunga mkono) tupoteze JEMADARI mzuri tena KIJANA katika hii VITA.

Vita ni kali sana na maadui zetu wamenunua silaha kadhaa kukabiliana na silaha zile zile ambazo zimeonakana kuwa kali katika siku za karibuni na kwa kweli wanapambana sana usiku na mchana. Zitto angalia sana, VITA haina macho, risasi, mabomu, na hata mitego hutumika usiku na mchana.

Kwa kujua hii ni VITA kuwa makini zaidi na kila hatua uwe unaangalia chini maana kuna mabomu ya kutegwa ardhini na angani kuna ndege zinadondosha mabomu usiku na mchana. Kuna makamanda wanaoshambuliwa kutoka kila kona na sasa wanaogopa hata mlio wa ng'ombe wakijua ni kifaru. Usishituke kwa hilo maana maadui wamechanganyikiwa wanatumia kila mbinu.
 
Kitila,

Bodi ya TANESCO haikukataa. Kamati yetu ilipokutana na TANESCO mwenyekiti wa Bodi alikuwapo na swali hilo liliulizwa na kujibiwa kuwa Bodi haina tatizo.

Tatizo ni kuwa Kamati ya Nishati na Madini iliomba TANESCO wawapeleke wabunge 2 kutoka kamati hiyo kwenda Texas kutafuta mitambo. MD wa TANESCO akakataa.


Zitto,
1. Sababu alizotoa MD wa Tanesco kukataa wabunge kwenda US ni zipi na majibu yenu kuchalenji hoja yake yalikuwa yepi?

2. Hivi sasa msimamo wako juu ya hili suala ni upi,
  • Kununua DOWANS
  • Kutafuta njia nyingine?
 
Nimepata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. William Ngeleja kuhusu suala la ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme ambayo inauzwa na kampuni ya Dowans. Snapshots:

- Asema Dowans ndiyo wametangaza tenda ya kuuza mitambo yao hivyo sheria ya PPRA inaingia kwa namna tofauti

Mwanakijiji inaelekea waziri anatufnya sisi wajinga tusioweza kufikiria,
  1. Ngeleja anaweza kuonyesha ni wapi DOWANS walipotangaza kuuza hiyo mitambo?
  2. Tunanunua kwa vile wanauza au kwa vile tunahitaji mitambo? Kama ni kwa mahitaji yetu kwa nini tuling'ang'ania DOWANS?
  3. DOWANS watauzaje mitambo ambayo TANESCO ndio wanayoishikilia?

- Arudia suala la kununua mitambo iliyotumika, asema siyo 'geni'
Kunua mitumba sio shida tatizo ni kwa nini inunuliwe toka DOWANS tena kwa bei kubwa na bila kuangalia uwezekano wa kununua mipya ya bei nafuu?
- Atolea mfano hali ya kiuchumi Marekani na jinsi serikali ya huko ilivyoingilia hali ya uchumi wake..

Hili inauhusiano gani na DOWANS? Je anaweza kufafanua? (unfortunately mazungumzo yenu yameshapita-next time)
 
ndugu watanzania.kama hali halisimlivyoiona hatiame mpambano umemalizika baada ya upande mmoja kukiri kushindwa kuhusu swala la dowans;
Kwa kweli kama binadamu ningeweza kumwita zitto ana matatizo tena makubwa sana sana;;ni kaka yangu rafiki yangu na nampenda kwa baadhi ya misimamo yake laikini kwa hili ametutia aibu kabisa;hakuna alieamini kama kweli leo hii zitto anaweza kununulika kirahisi namna hiyo;
OK!!kama kosa limeshafanyika;ni wakati wa kujipanga upya na kuangalia wapi wapinzani mmekosea;je mnavyoambiwa mnaangalia sana matumbo yenu ni kweli??jiulizeni mambo kama haya mtajua wapi pa kujirekebisha;
Onyo;
tunaomba asitokee tena kwenye kambi ya upinzani akawa kigeugeu kama huyu bwana zitto;leo hii ndio nimejua kwa nini mh sitta alimwita""(>>>)"
kule bungeni...nadhani hatuitaji watu kama hawa wanaokuwa na mamlaka ya kuwaokoa watanzania na kuishia kuwauza watanzania;
SHUKRAN
shukrani za pekee ziwaendee MH mwakyembe kwa kupigania haki za watanzania na kusahau kununuliwa!!nilimshangaaa sana zitto mbona kama kula pesa mwakyembe nae alikula na akaamua kuwageuka;iweje wewe zitto unakuwa mhuni kutuuza kirahisi hivyo;haya ndugu 2010 inakusubiri jua hakuna mtanzania atakaekusahau;;;na kama kweli una nnia njema na watanzania ulikuwa ukipiga makeelele ya richmond ya nini??au ulikuwa ukitafuta umaarufu
iweje kampuni ulioipigia debe bungeni ya majambazi inahamisha mitambo kwa kampuni nyingine na weewe unakuwa kimbeleembele kuwashauri serikali wanunue;pole zitto mitambo imekwama,na klwa taarifa yako mitambo ni bomu;
na inadaiwa madeni kibao na benki za nchini
 
UMEKOSEA SANA kumpa pole bwana zitto......! huyu haitwi zitoo anaitwa 'DOWANS'
anajitahidi kurekebisha kauli yake lakini ulimi wake ulisha tamka .....!
na wanaojaribu kurekebisha ndo wanatupa mwanya wa kuwaunganisha vizuri na 'MR.DOWANS'
 
Sweetbaby/Mahesabu
Someni gazeti la Raiamwema la jana wametoa barua ya Zitto aliyomwandikia Ngeleja,sijasoma popote aliposhauri ununuzi wa dowans.Hizi nimebaini ni njama za "So-called Anti-fisadi crusaders" wa CCM ambao wameapa kumaliza umaarufu wa Zitto.Nashangazwa na msimamo wa watu hawa mbona wameshindwa kujenga hoja zao bungeni kuhakikisha kuwa serikali inatekeleza maazimio ya bunge?Badala yake nguvu nyingi wanelekeza watu kumuona Zitto ndio tatizo inasikitisha sana.
Mimi ninaona tatizo ni serikali inayosita kuwawajibisha watendaji walioleta kadhia hii.
 
Someni gazeti la Raiamwema la jana wametoa barua ya Zitto aliyomwandikia Ngeleja,sijasoma popote aliposhauri ununuzi wa dowans

Si dhani kama kuna haja ya kuangalia magazeti kujua msimamo wa Zitto katika suala la hili Dowans. Zitto mwenyewe ametoa msimamo/mawazo yake humu jamvini (tunaweza kusoma post zake na kupima). Pia Zitto tumemsikia/ kumwona akihojiwa na ITV kuhusiana na Dowans. Nadhani source hizi mbili ni bora zaidi kuliko habari zilizo ripotiwa na magazeti.

Tunaodhani Zitto amekengeuka katika sula hili la Dowans tumesoma post zake na pia tumemsikia akihojiwa (na ITV) hivyo tunajua amesimama wapi.

Zitto ameshauri kamati yake ikutane na ile ya Shelukindo ambayo ilitoa ushauri wa kutonunua mitambo ya chakavu ya Dowans. Tanesco walionesha nia ya kutaka kununua mitambo ya Dowans kwa sababu za 'kitaalamu' ambazo Zitto anadai kamati ya Shelukindo haikuzisikiliza. Hapa kuna tatizo, je unaliona? Amekuwa wakala wa menejimenti ya Tanesco? Kwa nini menejimenti na Bodi ya Tanesco zinaelekea kutifautiana katika suala hili? Nini kinaizuia kamati ya Zitto kutoa ushauri wao kwa mujibu wa data walizo nazo hata kama ushauri huo unatofautiana na kamati nyingine? Kwa nini wanaogopa?

Zitto anasema ni kanuni (na si sheria) inayouzuia ununuzi wa mitambo chakavu. Kanuni zinatolewa na waziri katika kutekeleza sheria. Hapa Zitto anaashiria zinaweza kubadilishwa bila kuhitaji maamuzi ya Bunge. Hili ni kweli lakini kwa manufaa ya nani? Hapa pia kuna tatizo, tena kubwa. kimantiki, Zitto anatuambia tubadilishe kanuni ili tuweze kununua mitambo chakavu! (mbaya zaidi kutoka kwa 'binamu' wa Richmond, yaani Dowans).

Zitto anasema hanatuna haja ya kujua Dowans ni kina nani. Tunachohitaji ni mitambo yao ambayo ipo tayari na inafanya kazi. Dowans (kwa maoni yangu, unaweza kuita ya kishabiki) ni Richmond isipokuwa imegeuzwa jina tu. Ni mafisadi wale wale wanatuvuruga tu. Hapa pia pana tatizo kwani inaelekea amesahau yaliyotokea kwenye Richmond!

Zitto ametoa kile anachokiita msimamo wa kamati yake. Lakini taarifa za karibuni zinaonesha huenda si maoni ya kamati yake. Makamu wake amekanusha msimamo uliotolewa na Zitto. Hapa pia pana tatizo.

Kwa kifupi nilivyowaelewa Zitto pamoja na Dr Rashid, ni kwamba tatizo la umeme ni imminent na ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans ni kwa 'maslahi ya taifa'.

Kama kweli Zitto anapinga ununuzi wa mitambo ya Dowans, mbona hakuna mahali ambapo ameweka wazi msimamo huo? Au yupo neutral?
 
Waheshimiwa;

Kuachia mafisadi na mbinu zao ziendelee kushamiri katika jamii kwa madai ya kujikita katika kutatua tatizo la ukosefu wa umeme kwanza, ni dalili za woga na uzandiki. Tukubaliane kwamba kununua mitambo ya DOWANS ni kuwastawisha na kuwapa ushindi MAFISADI. Next time, they will find better tactics and weapons against our weak efforts.
Let's lose a bit by not buyinging from DOWANS but not help them off-hook!
 
Siri ya Zitto na Ngeleja yavuja

Mwandishi Wetu Machi 11, 2009
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo​

WAKATI hali ya umeme nchini ikiwa bado tete, barua ya siri kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Zitto Kabwe kwenda kwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kuhusiana na sakata la umeme na hali ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), imevuja.

Barua hiyo inagusia ushauri wa kamati ya POAC kwa Serikali kuhusiana na kukabiliana na hali ya umeme, ikiwa ni pamoja na kuishauri Serikali kuingilia kati na kuinusuru Tanesco kifedha, bila kugusia mitambo ya Dowans ambayo imekua gumzo kwa sasa.

Ndani ya barua hiyo ya mwishoni mwa mwezi uliopita, ambayo Raia Mwema imeiona, Zitto, kwa niaba ya kamati yake, ameishauri Serikali kuhakikisha kwamba kunakuwapo msaada wa dharura kwa Tanesco ili ijikwamue katika tatizo kubwa la kifedha na kuisaidia kununua mitambo ya kuzalishia umeme inayofaa bila kukiuka sheria za nchi.

“Kamati inawasilisha kwako ushauri wa kuiomba Serikali iiwezeshe Tanesco kununua mitambo ya umeme inayoona inafaa kulingana na mahitaji yake na bila kukiuka sheria za nchi ili kuliokoa Taifa kuingia kwenye giza na hivyo kuathiri uchumi wa taifa letu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo kutoka kwa Zitto.

Zitto, ambaye yuko mkoani Kilimanjaro kwa shughuli za chama chake, alikataa jana kuzungumzia kuhusiana na kuvuja kwa barua hiyo akisema: “…nilikuwa nje ya nchi na nimekuja moja kwa moja huku Machame kwa shughuli za chama.”

Kuvuja kwa barua hiyo kunakuja wakati Zitto anatajwa kama mmoja wa wanasiasa wanaoiunga mkono Tanesco katika mpango wake wa kununua mitambo ya Dowans, msimamo ambao umezua utata na kumuweka pabaya kisiasa, lakini alipoulizwa kuhusiana na msimamo wake kwa sasa alisema: “Msimamo wangu ni kuona nchi haipati giza na Watanzania wajifunze kuwa na viongozi ambao wana mawazo tofauti na wengi.”

Ndani ya barua hiyo, ambayo nakala yake imepelekwa kwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, kuna maelezo yanayoonyesha jinsi shirika hilo la umeme lilivyo na hali mbaya kifedha kutokana na sehemu kubwa ya mapato kutumika kununua umeme kutoka kampuni binafsi zinazozalisha umeme nchini.

Kuhusiana na ushauri wa serikali juu ya ununuzi wa mitambo barua hiyo inaeleza: “Kamati inapenda kuikumbusha Serikali kuwa maamuzi ya kununua mitambo ni maamuzi ya Serikali na si ya Kamati ya Bunge. Kazi ya Bunge ni kuisimamia Serikali na si utendaji wa kila siku. Kamati yangu imetoa ushauri huu kuisaidia Tanesco kupunguza gharama za kununua umeme na kuongeza mapato yake kwa kutekeleza mpango wake wa wateja 100,000 kwa mwaka. Tanesco hawataweza kuunganisha umeme kwa wateja 100,000 kwa mwaka kama hakuna umeme wa kuwapatia.”

Habari zaidi kutoka ndani ya Kamati ya Zitto zinaeleza kwamba baadhi ya wajumbe wameonyesha kuchanganywa na taarifa za vyombo vya habari zilizomnukuu Mwenyekiti wao akizungumzia Dowans wakati kamati haikuwa na maamuzi kuhusiana na kampuni hiyo.

Miongoni mwao ni Makamu Mwenyekiti wa Zitto, Mbunge wa Mbarali, Esterina Kilasi, ambaye alinukuliwa wiki hii akisema kwamba kamati haikuwa na maamuzi yoyote kuhusiana na Dowans.

Mjumbe mwingine wa kamati hiyo aliliambia Raia Mwema kwamba wajumbe wengi waliozungumzia suala la mitambo walibainisha kwamba Tanesco ni lazima inunue mitambo mipya na izingatie sheria.

“Baada ya Tanesco kuzungumzia dhamira yake ya kutaka kununua mitambo ya Dowans, tuliwaambia kwamba suala la kununua ama kutonunua ni suala la kiutendaji linalotakiwa kuzingatia sheria, ubora wa kitu kinachotakiwa kununuliwa na taratibu zifuatwe na tuliwasisitizia kwamba kazi ya Kamati na Bunge ni kusimamia,” alisema Mbunge huyo.


Mbunge huyo ambaye alikataa kutajwa jina kwa kuwa si msemaji wa Kamati, alisema waliwaeleza Tanesco waziwazi kwamba kitendo chao cha kufika katika Kamati kutaka mpango wao wa kununua mitambo upate baraka, hakikua sahihi.

“Tulisikiliza nia ya shirika dhidi ya mitambo hiyo lakini hatukubariki ununuzi huo. Uamuzi wa kamati ni kuishauri Serikali kununua mitambo mipya kwa ajili ya tahadhari na kukabiliana na tatizo la umeme linaloweza kujitokeza kama Tanesco walivyoonya, lakini kwa kuzingatia ubora, sheria, kanuni na taratibu za manunuzi,” alisema.

Mbali ya Zitto na Kilasi, wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Felister Bura, Diana Chilolo, Raphael Chegeni, Bahati Abeid, Emmanuel Luhahula, James Musalika, Peter Serukamba, Juma Njwayo, Tatu Ntimizi, Hafidh Ali Tahir, Elisa Mollel, Zaynab Vullu, Mwanawetu Zarafi, Mwadini Abass Jecha na Shally Raymond.

Mbali ya kutoa ushauri kwa Serikali, Kamati ya Zitto ilipendekeza kuwapo kwa kikao cha pamoja na kamati ya Nishati na Madini, maombi ambayo yalikataliwa na Spika Sitta, ambaye alibainisha wazi kwamba hakukuwa na sababu ya kikao hicho baada ya Kamati ya Nishati na Madini, inayoshughulikia sekta hiyo, uamuzi ambao unaelezwa kukubalika na kamati zote.

Tayari Tanesco wamekwishasitisha mpango wao wa kununua mitambo ya Dowans, lakini kwa taarifa ambayo ilitoa kitisho kwa wananchi kwamba kutakuwa na tatizo kubwa la umeme litakaloathiri sekta nyingi za huduma na uzalishaji.

Taarifa ya Tanesco iliyotolewa na Mkurugenzi wake Mkuu, Dk. Idris Rashid iliibua mjadala mpya wa kumtaka ajiuzulu kutokana na kutowajibika na kuutisha umma.

Katika tamko lake Dk. Rashid alisema: “Tanesco inatangaza rasmi kujitoa kwenye nia yake ya kununua mitambo hii. Ni imani yetu kwamba tumekwisha kujieleza na kujenga hoja za kutosha, na wananchi wa Tanzania, watafanya maamuzi yao hapo ambapo nchi itakapokuwa imegubikwa na kiza, hospitali hazitoi huduma, viwanda havizalishi, wanafunzi vyuoni wanashindwa kusoma kwa sababu tulishindwa kufanya maamuzi".

Sakata la Dowans limeibua mjadala mkali nap engine mgawanyiko wa wazi uliotokana na kauli za kukinzana kati ya wabunge wa kamati mbili ya POAC na ile ya Nishati na Madini inayoongozwa na Mbunge wa Bumbuli (CCM), William Shellukindo, anayesaidiwa na mwanasiasa machachari, Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe tofauti ambazo zimejitokeza zaidi katika vyombo vya habari.

Shellukindo na Mwakyembe wote walionyesha kushitushwa kwao na taarifa za kamati ya Zitto kujihusisha na masuala ya kisera badala ya kupitia hesabu huku wakihusisha hatua hiyo na mikakati ya kisiasa.

Dk. Mwakyembe ndiye aliyesema kwamba upo uwezekano wa suala hilo kutumika kama sehemu ya kampeni za kisiasa za Chadema ambako Zitto ni Naibu Katibu Mkuu wake, lakini Zitto akanukuliwa akisema suala hilo halina chembe ya siasa mbali ya maslahi ya Taifa.

Baada ya kauli za wabunge hao, Spika Sitta alifunga mjadala kwa kuishauri serikali kuachana na ununuzi wa mitambo ya Dowans kwa kuwa hauna maslahi kwa Taifa.
 
Ok, I will reserve my judgement.


Pamoja na hayo, nadhani MKJJ hukuweza kumuuliza kuwa hiyo Dowans ni ya nani kwani si mahali pake hapo, ila pia tujiulize:
Iweje DOWANS (ambayo haijulikani ni kampuni ya nani wala ya wapi Dubai, Costa Rica, South Africa au Mauritius) iliyorithi mkataba HARAMU toka kwa kampuni HARAMU ya ki-tapeli Richmond (TANESCO na serikali waliuvunja huo mkataba kuwa ni batili, kwa maana pia hata Dowans walirithi mkataba batili), leo hii iwe HALALI kumiliki na kuuza mitambo yake kwa gharama takribani mara 2?

Katika kuuza na kununua, kuna mmoja humfuata mwenzie. Ama muuzaji humfuata mnunuzi au mnunuzi humfuata muuzaji. Hapa ni nani kamfuata nani?

Ama kweli kichwa cha mwendawazimu!

Na ndugu yangu Zitto naye, au basi nitasema zaidi baada ya Cheche ........

Asante kwa ukweli.
 
Hongera serikali kwa kuitosa Dowans

2009-03-16; 10:24:26
Na Mwandishi Wetu


Baadhi ya wabunge waliokuwa wajumbe katika Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa utoaji wa zabuni ya kufua umeme wa dharura kwa Kampuni ya Richmond, wameipongeza serikali kuachana na mpango wa kununua mitambo ya kufua umeme ya Kampuni ya Dowans.

Mbunge wa Nzega CCM, Lucas Selelii, amesema anapongeza uamuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kujitoa katika ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya Dowans kwa sababu ilikuwa ni kashfa kubwa.

Alisema iwapo matakwa ya kununua mitambo hiyo yangetekelezwa, kitendo hicho kingeleta picha mbaya.

Alisema Sheria ya Manunuzi ya Umma (PPRA) ya mwaka 2004 hairuhusu kununua vifaa, mitambo au mashine ambazo zimekwishatumika, hivyo, kufanya uamuzi tofauti na sheria hiyo ni sawa na kuhalalisha kashfa.

Selelii, hata hivyo, alisema serikali inaweza kukodi mitambo iliyokwishatumika lakini sio kuinunua.

Alisema uamuzi huo ni wa busara na umechukuliwa kwa ujasiri hivyo ni vema kama utaendelea kuwa thabiti.

Akifafanua azma ya kununua mitambo hiyo na ile ya kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Selelii alisema kuna tofauti kubwa kati yake.

Alisema uamuzi wa kununua mitambo ya IPTL uliridhiwa na Bunge wakati uamuzi wa kununua mitambo ya Dowans ulikuwa ni wa watu binafsi na wa siri.

``Nia hiyo ilikuwa ni ya mtu binafsi, haikuridhiwa na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na wala Bunge lenyewe, lakini uamuzi wa kununuliwa kwa mitambo ya IPTL uliridhiwa na Bunge,`` alisema na kuongeza kwamba IPTL tayari ilikuwa inauza umeme wake kwa Tanesco kwa bei mbaya na nia ya kununua mitambo yake ilikuwa na lengo la kupunguza `maumivu`.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum, Stella Manyanya, alipongeza hatua hiyo akisema: ``Naunga mkono serikali kujitoa katika ununuzi wa mitambo hiyo, kinachotakiwa sasa ni kuzingatia hatua mbalimbali zilizoainishwa na Waziri Ngeleja mwishoni mwa wiki za kuhakikisha kwamba nchi inapata umeme wa kutosha... Taifa lina vyanzo vingi vya umeme, hivyo, vizingatiwe,`` alisema.

Manyanya alisema hoja ya mitambo ya Dowans imemchosha na asingependa kuizungumzia mara kwa mara na badala yake aliwataka wadau na wajasiriamali mbalimbali, hasa wa ndani, kujitokeza kwa wingi kuwekeza katika sekta ya umeme.

Alisema wadau hao wakiwa kama makampuni au watu binafsi, wanayo nafasi kubwa ya kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo vingi vya umeme vilivyopo nchini na kuwauzia wananchi moja kwa moja, badala ya kila mmoja kutaka kuuza umeme wake kwa Tanesco.

Alisema kwa kufanya hivyo, kutakuwa na ushindani katika utoaji wa huduma hiyo na kuleta ushindani unaowiana kama ilivyo katika makampuni ya simu nchini.

Alisema kujitokeza kwa wajasiriamali wengi katika huduma ya umeme kutaondoa ukiritimba wa muda mrefu wa kutegemea shirika moja tu kuzalisha na kusambaza umeme, hali ambayo inasababisha kuleta ugumu katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Waziri Ngeleja, alitangaza uamuzi wa serikali wa kujitoa katika ununuzi wa mitambo hiyo, uamuzi ambao ulitangazwa siku kadhaa baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Dk. Idris Rashid, kutangaza kuwa shirika hilo limeamua kuachana na ununuzi wa mitambo hiyo.

Wakati Dk. Idris akitangaza uamuzi wa Tanesco kusitisha mpango wake, alitishia kuwa nchi itaingia gizani na kusema kuwa Tanesco isije kulaumiwa.

Hata hivyo, Ngeleja alipinga madai ya mtendaji huyo mkuu wa Tanesco kuwa nchi itaingia gizani.

SOURCE: Nipashe
 
Jamani umeme ni tatizo tanzania.tuache ushabiki usiokuwa na mbele wala nyuma.ile mitambo inunuliwe kama ni ufisadi umeshafanyika hakuna tena jambo hiyo.tukisema tunununue mipya utafanyika ufisadi na hatutaweza.
hakuna haja ya nchi kubaki gizani kwa ajuli ya ushabiki usiokuwa na mbele wala nyuma.
 
Jamani umeme ni tatizo tanzania.tuache ushabiki usiokuwa na mbele wala nyuma.ile mitambo inunuliwe kama ni ufisadi umeshafanyika hakuna tena jambo hiyo.tukisema tunununue mipya utafanyika ufisadi na hatutaweza.
hakuna haja ya nchi kubaki gizani kwa ajuli ya ushabiki usiokuwa na mbele wala nyuma.

Msaranga hujui unachoongea ndugu yangu. Nchi haina tatizo la umeme kabisa kwa sasa. Mabwawa yana maji ya kutosha na mvua zinaendelea kunyesha. Tatizo lilinalozungumziwa hapa ni suala la baadaye kwa kuzingatia ongezeko la wateja. Kumbuka Dowans na Richmond ni mtu mmoja na mikataba yake yote imesainiwa na kampuni ya uwakili ya Ringo Tenga. Kama Richmond ilionekana kuwa ni kampuni feki ndo ilivyo hata kwa Dowans ambayo mpaka leo haitaki kutaja wamiliki wake waziwazi japo twajua ni Rostam Azizi na washirika wake ambaye sasa kwa kutumia magazeti yake ya Mtanzania ameanza kumshambulia Mwakyembe. Kwahiyo hapa si suala la kisiasa bali ni integrity and dignity.
 
Kuweza kupata upana wa habari yote hakikisha unajipatia pia nakala ya Tanzania Daima, na MwanaHalisi na Raia Mwema; I don't know. Mambo mengine yanaendelea, sehemu ya pili yake itaendelea wiki ile nyingine Inshallah!

toleola31.jpg


KAMA BABU HAJAZALIWA, WEWE HAUJAZALIWA!
 

Attachments

Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom