Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Kokolo, nakumbuka tulilizungumza hili na ulileta insight nzuri sana wakati tunazungumzia mambo ya UPS. Hadi hivi sasa nadhani tunachotakiwa kufanya ni kujenga hoja kuwa kupata mitambo mipya kutoka kwa watengenezaji ni bora na ina mantiki ya kifedha kuliko kununua toka kwa Dowans.

Hapa kuna mambo mawili makubwa:-
1. Kununua mitambo mikuu kuu bila kujali anayetuuzia ni nani na
2. Kufanya biashara na Dowans bila kujali inahusu mitambo mipya ama kuu kuu.

Binafsi nina tatizo na yote mawili:-
1. Si busara hata kidogo kwa serikali kuingia kwenye biashara ya mitambo kuu kuu. Kwamba tunafanya hivi ili kubana matumizi ni ujinga na ujinga gharama yale ni kubwa. Mwisho wa yote kuna hatari ya kuingia kwenye gharama maradufu ya hiyo tunayojaribu kui"save".
2. Kufanya biashara yoyote ile na Dowans ni kujidhalilisha wenyewe kwa kuhalalisha vitendo vya utapeli. Tukubali tusikubali tulitapeliwa na Richmond na kama vile haitoshi wakapokezana vijiti na Dowans na bado hatukugutuka. Hakuna ujuha zaidi ya kitendo chetu hicho.

Dowans waambiwe waondoe hiyo mitambo yao tuweze kuagiza mitambo mipya na kuifunga pale, period. Sijui baada ya mkataba wao (ambao hata haukuwapo kwa kuwa wenyewe hawajulikani) kufutwa bado wanafanya nini pale. Nina wasiwasi kuwa ukweli ambao hatuambiwi ni kuwa wamiliki wa Dowans ndio hao hao watawala wetu na hawana pa kupeleka mitambo yao - hivyo ni lazima tuinunue tu kama asemavyo MKJJ akiungwa mkono na Zitto. Hawa watu lao moja na asikudanganye mtu kuwa kuna vita inaendelea baina yao - yote ni changa la macho - please Zitto, the time to get out is NOW !!
 
Mh. Zitto.

Nimefurahishwa sana na msimamo wako na hoja zako za kisomi. Katika mjadala huu mawazo ya wengi ni Taneso wasinunue mitambo ya Dowans lakini ukiangalia hoja zinazotolewa hakuna hata moja yenye nguvu. Wachache akina sisi tunaunga mkono hoja hii kwa sababu za msingi kabisa.

Sasa hawa jamaa wasikuingize katika mambo ya kitoto kama vile issue za Hammer, kugombea ubunge na ufisadi. Hoja hizi zinaonyesha wazi kuwa wamefilisika na hoja za msingi na wanakimbilia kuleta issues za kukutibua. Lakini nafurahi kuwa umewatambua kutokana na umakini wako katika kuwajibu. Sababu ya yote hayo ni roho ya korosho.

Nakuhakikishia kuwa endapo ununuzi huu hautokamilishwa na ikabidi uwepo mgao wa nguvu huko baadae, ni hao hao wanaotoa hoja za kupinga ndio watakaokuwa msitari wa mbele kupiga kelele na kulalamika. Mark my words. Wewe waandike tu majina yao pembeni na utaamini ninayo yasema.

Nakushauri achana nao. Sisi tumekuelewa na natumai serikali itakuelewa zaidi.
 
hii inaitwa hekima.

Ok, I will reserve my judgement.


Pamoja na hayo, nadhani MKJJ hukuweza kumuuliza kuwa hiyo Dowans ni ya nani kwani si mahali pake hapo, ila pia tujiulize:
Iweje DOWANS (ambayo haijulikani ni kampuni ya nani wala ya wapi Dubai, Costa Rica, South Africa au Mauritius) iliyorithi mkataba HARAMU toka kwa kampuni HARAMU ya ki-tapeli Richmond (TANESCO na serikali waliuvunja huo mkataba kuwa ni batili, kwa maana pia hata Dowans walirithi mkataba batili), leo hii iwe HALALI kumiliki na kuuza mitambo yake kwa gharama takribani mara 2?

Katika kuuza na kununua, kuna mmoja humfuata mwenzie. Ama muuzaji humfuata mnunuzi au mnunuzi humfuata muuzaji. Hapa ni nani kamfuata nani?

Ama kweli kichwa cha mwendawazimu!

Na ndugu yangu Zitto naye, au basi nitasema zaidi baada ya Cheche ........
 
Mh. Zitto.

Nimefurahishwa sana na msimamo wako na hoja zako za kisomi. Katika mjadala huu mawazo ya wengi ni Taneso wasinunue mitambo ya Dowans lakini ukiangalia hoja zinazotolewa hakuna hata moja yenye nguvu. Wachache akina sisi tunaunga mkono hoja hii kwa sababu za msingi kabisa.

Sasa hawa jamaa wasikuingize katika mambo ya kitoto kama vile issue za Hammer, kugombea ubunge na ufisadi. Hoja hizi zinaonyesha wazi kuwa wamefilisika na hoja za msingi na wanakimbilia kuleta issues za kukutibua. Lakini nafurahi kuwa umewatambua kutokana na umakini wako katika kuwajibu. Sababu ya yote hayo ni roho ya korosho.

Nakuhakikishia kuwa endapo ununuzi huu hautokamilishwa na ikabidi uwepo mgao wa nguvu huko baadae, ni hao hao wanaotoa hoja za kupinga ndio watakaokuwa msitari wa mbele kupiga kelele na kulalamika. Mark my words. Wewe waandike tu majina yao pembeni na utaamini ninayo yasema.

Nakushauri achana nao. Sisi tumekuelewa na natumai serikali itakuelewa zaidi.


wewe nawe ndiyo umeandika nini sasa?kwani lazima uonekane umechangia?
 
Zitto umekwepa swali langu mara kadhaa. Ninakuuliza tena. Tukiweka pembeni siasa za kamati and all that, wewe kama informed representative utasimamia upande gani katika mjadala huu? Utaunga mkonoi ununuzi au lah? au bado hauna taarifa zinazokuwezesha kuwa na uamuzi?

Usipojibu this time sitakuuliza tena.

Ndugu yangu sikwepi kukujibu hata kidogo. Mie sifichi kitu na ndio maana nipo hapa ninajibu kila ninaloona naweza kujibu au kujieleza licha ya watu kufanya judgements zao (which is very unfair).

Kwa sasa siwezi kujibu moja kwa moja msimamo wangu binafsi kwa sababu nitaweza kusababisha tatizo la kikanuni maana ni vigumu watu kutofautisha na msimamo wa Kamati ya Bunge ninayoongoza.

So far ninasimamia msimamo wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma. Tumeandika kwa Spika na pia kwa Waziri wa Nishati na Madini kwa mujibu wa kanuni za Bunge. Tumezingatia sheria za nchi na Mahitaji ya nishati ya Umeme kwa Taifa. Tumezingatia umuhimu wa Shirika la Umeme la Taifa kujiendesha kibiashara na kuanza kupata faida.
 
Hahahahahaa..Mwanakijiji wawekee tu watu hayo mahojiano...wengine hawana subira
 
wewe nawe ndiyo umeandika nini sasa?kwani lazima uonekane umechangia?

Watu wengine bwana................. yaani humu jamvini watu hawana uhuru mpaka wawe na mawazo kama yako?
 
Snapshots:

- Asema siyo lazima kununua mitambo ya Dowans, ni ulazima wa hali ya mahitaji iliyopo

- Asema Dowans ndiyo wametangaza tenda ya kuuza mitambo yao hivyo sheria ya PPRA inaingia kwa namna tofauti
- Arudia suala la kununua mitambo iliyotumika, asema siyo 'geni'

- Atolea mfano hali ya kiuchumi Marekani na jinsi serikali ya huko ilivyoingilia hali ya uchumi wake..


Kwa majibu hayo machache tu inaonyesha kuwa kwa msimamo wa Serikali, Dr. Mwakyembe na kundi lake wameanguka na Mh. Zitto na kundi lake wameibuka kidedea.

Lakini tusubiri filimbi ya mwisho..
 
Ebana Zitto eeh? Hivi bongo hatuna wahandisi wanaoweza kuunda hiyo mitambo ya kuzalisha umeme hadi tuende majuu kuinunua?
 
Ebana Zitto eeh? Hivi bongo hatuna wahandisi wanaoweza kuunga hiyo mitambo ya kuzalisha umeme hadi tuende majuu kuinunua?

Hakuna kampuni ya kutengeneza mitambo ya kuzalisha umeme. Tunao mafundi wa kukarabati. Hata wataalamu wa kuchunguza kama inafanya kazi au sio wanatoka nje. Bado kauchumi ketu sio kazuri kiasi cha watalaamu wetu kuanzisha consultancy firms na kushindana kwa kazi hizi na wageni. Hata sheria ya manunuzi inatoa upendeleo kwa makampuni ya ndani. Tutafika tu, tuamue kaka
 
Hakuna kampuni ya kutengeneza mitambo ya kuzalisha umeme. Tunao mafundi wa kukarabati. Hata wataalamu wa kuchunguza kama inafanya kazi au sio wanatoka nje. Bado kauchumi ketu sio kazuri kiasi cha watalaamu wetu kuanzisha consultancy firms na kushindana kwa kazi hizi na wageni. Hata sheria ya manunuzi inatoa upendeleo kwa makampuni ya ndani. Tutafika tu, tuamue kaka

Sidhani kama umelielewa swali langu.....basi tu tuendelee na mjadala
 
Watu wengine bwana................. yaani humu jamvini watu hawana uhuru mpaka wawe na mawazo kama yako?

mkuu huyo ndugu aliponichanganya ni pale aliposema hoja zote zilizotolewa humu na kina moelex,mkandala,keil nk eti hazina nguvu manake anawapa greenlight muendelee na huo mchakato wa kununua mitambo ya rostam,ala?
ndipo nikashtuka kidogo
 
Hapana Mama. Kamati inataka tuwe pragmatic.

Is being pragmatic means kununua zigo lililiopatikana kifisadi? Kwa hiyo kamati yenu inakubaliana na ufisadi? Kisheria inakuwaje?
 
Is being pragmatic means kununua zigo lililiopatikana kifisadi? Kwa hiyo kamati yenu inakubaliana na ufisadi? Kisheria inakuwaje?

Swali gumu, halijibiki. Siwezi kujibu bila kusema tuliachoamua na kuandika kwa Spika na Waziri.

- Kamati yangu haikubaliani na Ufisadi hata kidogo na inapiga vita ufisadi

- Kisheria - una maana sheria ya manunuzi? Nimeomba msaada kujua kipengele cha sheria. Tusubiri mahojiano ya MwanaKijiji na Ngeleja, inaweza kusaidia swali hilo

-kama ni sheria ya rushwa, PCCB wanapaswa kuchukua hatua. PCCB wanaweza kutuhoji wajumbe wote wa Kamati kuona kama kuna mjumbe yeyote aliepata mlungula kutoka kwa yeyote.

Pragmatism ni kuwa na umeme na kuepula mgawo. Mfano Mwalimu Nyerere alikuwa pragmatic wakati wa nationalization kwa kuacha kutaifisha Mwadui diamond mine kwani angetaifisha asingeweza kuuza almasi popote na hivyo kufanya kazi na DeBeers (makaburu). Je Mwalimu aliunga mkono apartheid? Hapan, alikuwa pragmatic
 
Kwa nini nchi ing'ang'anie sana mitambo ya Dowans? Kuna nini kinafichwa hapa? naona kama ni lazima tuinunue hiyo ya Dowans tu!Habari ya kutafuta kununua mali nzee eti kwa sababu ni cheap, sidhani kama ina maana hapa, labda kama kuna hoja nyingine nyuma yake! Unapoamua kupambana na ufisadi na kuutokomeza kabisa, na baadaye unafanya biashara na fisadi huyohuyo sidhani kama inaeleweka kwa mantiki ya kawaida.
 
Back
Top Bottom