Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Hakuna
Mtu kakosea anaambiwa kakosea kuomba radhi ni yeye na utashi wake utakavyomtuma.

mimi nafikiri huu mtindo wakusema eti kusimamia unachoamini hapa hatupo ktk dini hiki ni chanzo cha udikiteta.

Dikteta kwa kuamini mawazo yake zaidi kuliko yaliyo ya wengi ndicho humponza dikteta,Mimi nafikiri kiongozi umetumwa umepewa dhamana ya kuwakilisha kusimamia mawazo ya walio wengi yani wananchi na sio mawazo yako.

Mara nyingi japo si mara zote kiongozi yoyote anayesimamia mawazo yake badala ya wananchi hata kama mawazo yake yapo sahihi mwisho wa mwisho huishia kuwa dikteta na kutoa vitosho anavyoviona yeye vinamfaa maana anaamini mawazo yake siku zote yapo sahihi.
 
Last edited:
Tanzania ni nchi yenye umakini sana katika suala la kuwa na mipango ya muda mrefu. Matatizo yapo katika maeneo kadhaa kama yafuatayo:
  1. Ukosefu wa ushirikishaji wa wananchi katika kufikia mipango hiyo na hivyo mipango hiyo kukosa uhalali na uchangiaji chanya wa wananchi katika utekelezaji wake.
  2. Kutumika kwa wataalamu walio na mahusiano maalumu na wanasiasa zaidi ya kigezo cha utaalamu uliokubuhu.
  3. Utegemezi wa mataifa na asasi za nje katika kugharamia utekelezaji wa mipango hiyo.
  4. Uingiliaji wa maslahi binafsi na ya kisiasa ya muda mfupi katika utekelezaji wa mipango hiyo ya muda mrefu.

Pia ni utamaduni wa watanzania kuacha kujishughulisha kutafuta na kufuatilia taarifa za mipango hiyo kutoka serikalini. Tuna tatizo kubwa la upashanaji habari lakini pia hatuna utamaduni wa kujisumbua kutafuta habari hizo.

Haya ni matatizo ya kimfumo ambayo ni uthubutu wa kubadili mfumo wetu wa kisiasa, kijamii na kiuchumi tu ndio utakaotutoa hapa tulipo lakini sio vinginevyo.

Tuthubutu kuwa sehemu ya mabadiliko na sio kuendelea kusubiri MASIHA FEKI ndio watuletee mabadiliko tunayoyataka. Kupiga kelele tu haitoshi. Watanzania tulipiga na tunaendelea kupiga kelele dunia nzima ikatusikia lakini bado tupo katika lindi la matatizo ambayo yanazidi kuongezeka badala ya kupungua.

omarilyas

Bubu
.......naomba umsome vema Mkuu Omarilyas, anachoongelea hapo juu ni sahihi kabisa...........
 
Hakuna
Mtu kakosea anaambiwa kakosea kuomba radhi ni yeye na utashi wake utakavyomtuma.

mimi nafikiri huu mtindo wakusema eti kusimamia unachoamini hapa hatupo ktk dini hiki ni chanzo cha udikiteta.

Dikteta kwa kuamini mawazo yake zaidi kuliko yaliyo ya wengi ndicho humponza dikteta,Mimi nafikiri kiongozi umetumwa umepewa dhamana ya kuwakilisha kusimamia mawazo ya walio wengi yani wananchi na sio mawazo yako.

Mara nyingi japo si mara zote kiongozi yoyote anayesimamia mawazo yake badala ya wananchi hata kama mawazo yake yapo sahihi mwisho wa mwisho huishia kuwa dikteta na kutoa vitosho anavyoviona yeye vinamfaa maana anaamini mawazo yake siku zote yapo sahihi.

Nakushauri usome insha moja inasema "the tyranny of the majority".. utaelewa kuwa mawazo ya wengi siyo lazima yote yawe sahihi! Na kuhusu dhamira mawazo ya majority hayalazimishi mtu ukane dhamira yako ndiyo maana kuna watu wameenda na kuwa mashahidi kuliko kukana kile walichokiamini katika dhamira zao.

Sasa kama wewe unapenda kufuata mawazo ya wengi kwa vile yana mvuto zaidi hilo jingine lakini mtu anayefuata mawazo yake kwa vile dhamira yake inamtua kuwa ni sahihi huyo ni mtu huru.
 
Mkjj,

Binadamu wote hatuko perfect na huwa tunafanya makosa mbali mbali hata katika utu uzima wetu. Siyo siri kwamba Zitto kwa kuipigia debe mitambo ya Dowans amefanya kosa. Na hakuna yeyote aliyemshinikiza Zitto atamke amekosea. Na wala kutamka kwa amekosea si kutaka kumsabaratisha Zitto ili asivume tena kwenye nyanja za siasa au nyanja nyingine zozote zile katika nchi yetu. Lakini kwa maoni yangu atakuwa in a better position kusema amekosea kuliko kung'ang'ania kwamba hakukosea and time will tell. Tumewaona viongozi mbali mbali Ulimwenguni ambao walikubali makosa yao na wananchi wakawasemehe, hivyo Watanzania kumsamehe Zitto, kwa wale ambao hawajafanya hivyo, hakitakuwa ni kitu kigeni.
 
Kaka hiyo haina maana kuwa hatuna mipango ya muda mrefu. Ipo tena mingi tu. Hata katika sekta ya KILIMO kaka. Ukitoa mipango mingi ya miaka ya nyuma hivi sasa kuna Mpango wa ASDP (Agriculture Sector Development Programe) ambao ulipaswa kupatiwa shilingi trilioni moja kila mwaka kwa miaka saba. Kaka ukipitia kwa umakini mpango huu wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo huo utashangaa sana inakuwaje tunaanza kuja na mipango ya bandikabandua kama ule wa mbolea na fedha za EPA na kuacha kuuwezesha mpango huu ili ufanikiwe.

Tatizo kubwa katika mpango huu ni kuwa haukushirikisha wadau wengi katika kuuandaa, umekosa uhalali kwa upande wa walengwa halisi, unategemea msaada wa nje kuweza kuugharamia na zaidi wanasiasa wengi hawaujui kwa undani na hivyo kuuona hauna maslahi yao kisiasa haswa katika kutimiza malengo yao ya muda mfupi.

Fuatailia mpango huo pamoja na mabadiliko ya kisera yanayoendelea uone ni jinsi gani watanzania tunavyopenda kuja na mipango ya muda mrefu lakini hatuko tayari kukomaa nayo kutokana na mapungufu yetu kimfumo na kibinfsi.

omarilyas

Omarilyas, ndiyo hapo nasema huwezi kuwa na mpango nzuri kwenye makabrasha tu halafu ukija katika utekelezaji ni sifuri. Kwa maoni yangu mipango ya muda mrefu ambayo unaiweza kuiita mizuri ni ile ambayo utekezaji wake pia unakamilika 100%, vinginevyo hiyo mipango ni mizuri tu ikiwa kwenye makabrasha lakini mafanikio yake Watanzania hatuyaoni kwa sababu utekelezaji wa mipango hiyo hakuna.
 
Nakushauri usome insha moja inasema "the tyranny of the majority".. utaelewa kuwa mawazo ya wengi siyo lazima yote yawe sahihi! Na kuhusu dhamira mawazo ya majority hayalazimishi mtu ukane dhamira yako ndiyo maana kuna watu wameenda na kuwa mashahidi kuliko kukana kile walichokiamini katika dhamira zao.

Sasa kama wewe unapenda kufuata mawazo ya wengi kwa vile yana mvuto zaidi hilo jingine lakini mtu anayefuata mawazo yake kwa vile dhamira yake inamtua kuwa ni sahihi huyo ni mtu huru.

Mwanakijiji kuna jambo ambalo mnanishangaza, nalo ni kwamba kwenye hesabu 2+2=4 , whether wengi wanataka hivyo au la, sasa katika suala la Dowans au suala la umeme Tanzania Dowans sio dawa ya matatizo yetu, hivyo mtu yoyote yule atakayeliongelea suala hilo hivyo au kulielekezea hivyo atakuwa amepotoka. Period hakuna kusimamia msimamo hapa. Labda uniambie katika umeme wa Maji au nuklia au Solar au wa Upepo au hata wa Gesi hapo ndipo unaweza kufanya analysis ya advantage na dis-advantage ya upi unatufa kutokana na mazingira, fedha etc. Lakini hila la Dowans from the word Go ni batili.Kwa sababu za kiuchumi na kuogopa nchi kuingia Giza, hapa mtu anaongelea uchumi upi? wa kuibiwa? au hiyo ndio za best solution?
 
Last edited:
Kifupi kama mimi ndiye Kikwete basi huyu Idrissa anatakiwa kuwakilisha barua yake ya kujiuzuru mara moja.. maneno yake tu yanatosha kuonyesha hawezi kazi alokabidhiwa..
Hata hivyo labda kwa wale wasiomjua, huyu mkuu tunampa heshima yake lakini... Lol! salaaleh! hafai hata kwa kulumangia..

Usingeweza kufanya hivyo kwani alikuletea barua ya kujiuzulu hapo nyuma ukampigia magoti na kumbembeleza abatilishe uamzi wake na akafanya hivyo. Sasa tangu wakati huo akagundua hata akiboronga atakuwepo mpaka atakapoamua kuwa hataki tena.
 
Last edited:
Nakushauri usome insha moja inasema "the tyranny of the majority".. utaelewa kuwa mawazo ya wengi siyo lazima yote yawe sahihi! Na kuhusu dhamira mawazo ya majority hayalazimishi mtu ukane dhamira yako ndiyo maana kuna watu wameenda na kuwa mashahidi kuliko kukana kile walichokiamini katika dhamira zao.

Sasa kama wewe unapenda kufuata mawazo ya wengi kwa vile yana mvuto zaidi hilo jingine lakini mtu anayefuata mawazo yake kwa vile dhamira yake inamtua kuwa ni sahihi huyo ni mtu huru.


Kazi sana kwa hiyo
Zito humo Bungeni anawakilisha mawazo yake na msimamo wake ama anawakilisha mawazo yawaliyomtuma??

Kama waliomtuma wanasena hayo mawazo yake anayotilia msimamo sio waliomtuma sasa sijui hapo imekaa je?
Swali rahisi Zito ktk uenyekiti wake humo kwenye kamati ya bunge anasimamia mawazo yake ama ya wananchi?
 
Mkandara, Zitto akitambua ni wapi alipotoka na akaja kuomba radhi mimi sina tatizo; siyo hapa tu bali hata kwa hadhara ya Watanzania. Ni sehemu ya uungwana na ukomavu. Tatizo langu ni kuwa baadhi ya watu wanaonekana kukwazwa kupita kiasi kana kwamba Zitto hatakiwi kufanya makosa, kupotoka au kwenda nje ya mstari fulani. Kwamba, akichukua msimamo basi ni lazima uwe sahihi wakati wote. Hilo haliwezekani. Hakuna mwanadamu anayeweza hivyo.

Ndiyo maana kwa maoni yangu, nashangazwa na ukali wa maneno ya watu kwani naelewa kuna wale ambao wanatambua kuwa kijana amekosea na wamejaribu kumshawishi aone makosa hayo; bado hilo hatujui kama ameona makosa hayo.

Tatizo ni kuwa watu wanataka Zitto akubali tu kuwa amekosea hata pale ambapo dhamira yake na akili yake haimshawishi kuona makosa hayo. Dhamira ya mwanadamu iko juu ya sheria n.k NI lazima afanye kile ambacho dhamira yake ambayo imejengwa vizuri (well formed conscience) inamuambia kuwa ni kitu sahihi.

Nadhani tukimpa muda wa kutafakari na kupitia taratibu hoja hizi zote na ushahidi ambao utazidi kutokea huko mbeleni ataweza kuona ni wapi alipoenda pembeni na kwa kiasi gani. Kwa sababu naamini kama alivyosema Halisi yawezekana kabisa kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo hayakuripotiwa sahihi. Uzuri ni kuwa wengi wetu waliouelewa msimamo wa Zitto siyo kutokana na magazeti bali tumesoma aliyoyaandika yeye mwenyewe.

Ombi langu ni kuwa watu wasiwe wakali sana kulazimisha mtu achukue msimamo wao kama mtu huyo hajashawishika kufanya hivyo. Vinginevyo tutamfanya achukue uamuzi wa kinafiki. Tumpe nafasi apime na kuona uzito wa ushahidi uliopo kwanini hatulazimiki na hatuna sababu ya kununua majenereta yaliyoletwa na Dowans, na akishashawishika hivyo basi yeye mwenyewe atajua achukue hatua gani. Vinginevyo, atakuja hapa na kuomba radhi na watu watasema "haitoshi, inabidi ujiuzulu"; na wengine watasema "haitoshi kujiuzulu, itabidi ujivue uanachama" (tayari kuna watu wameshatoa mapendekezo hayo humu humu).

Ninachoelewa ni kwamba kuna wale ambao wanamkosoa Zitto kwa ni nzuri lakini siwezi kushangaa kuna wale ambao wanamkosoa ili kumfanya duni na kumharibu kuliko ukweli wa hali halisi.

Mwanakijiji,
Hapa unajichanganya mwenyewe;
  1. Zitto hatakiwi aombe msamaha kwa vile tu amekuwa tofauti na wengi, hell NO! Mashabiki wake wanamtaka afanye hivyo kwa vile conclusion ni kuwa amekosea kutetea ubadhirifu.
  2. Kama ingekuwa tu ni tofauti ya pande mbili, upande wa pili ungekuwepo lakini hapa haupo. This is not tirany of the majority, it is just between wrrong and wright. Kama alikuwa hajaona kosa, hivi sasa ni lazima atakuwa ameelewa na msimamo wake mpya ndio unaotakiwa kueleweka.
 



..tungeitumia vema tusingenunua madege mabovu,mapantoni na mitambo mingine.....!!!!

Kumbe unafahamu kila kitu halafu unajifanya hamnazo. Wameshatangaza hawanunui tuone kama tutakufa kwa kutonunua hiyo mitambo. Na wakijitokeza kina zito na idirisa wengine tutawakatalia vilevile.
 
Bubu
.......naomba umsome vema Mkuu Omarilyas, anachoongelea hapo juu ni sahihi kabisa...........

Hiyo mipango ya muda mrefu mbona hatujaiona? Au ni siri?

Nijuavyo mimi ni kuwa kuna viji-program wanavyotengeneza kwa ajili ya kuwadanganya wahisani kupata misaada, lakini mipango ya taifa haipo.

Anayedai ipo ailete tuione na kujadili.
 
Halisi,
Zitto nimemsoma kw amakini sana kauli zake hapa JF

1. Zitto alizungumza kwa niaba ya Kamati

3.Kosa lake kisiasa ni kukubali kuburuzwa na msimamo wa kamati yake.......kama alivyotuonyesha awali kuwa anasimama na kamati yake

4.Nia yake ya kukutana na Kamati ya Shelukindo...naweza kuelewa ilikuwa ni opportunity nzuri kwake...

Aliyosema Zitto Kabwe kwamba yametokea kwenye kamati yake wenzake wamemruka! Makamu Mwenyekiti amesema Kamati ya Hesabu haikuwa na mpango wa kukutana na Kamati ya Madini kwa sababu "halituhusu."

Sasa najiuliza, ni kwa nini Dr. Slaa alisema kwamba hatujui yaliyotokea kwenye kamati ya Zitto? Hata Dr. Slaa hakumwamini Zitto? Duuuh, hii inatisha mbona!

Makamu Mwenyekiti wa Zitto kasema hivi:

IPP MEDIA
09 Mar 2009
By Simon Mhina


Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Estherina Kilasi ambaye pia ni Mbunge wa Mbarali (CCM)...alisema maneno ambayo yamemkariri Mwenyekiti wao (Zitto Kabwe) yalikuwa maoni yake binafsi na wala sio ya kamati kwa vile hakuna hata kikao kimoja ambako walikubaliana na ombi la kununua mitambo hiyo.

``Wala hatujawahi kutoa ushauri wowote juu ya suala hilo, zaidi ya kuwaelekeza Tanesco walifikishe kwa kamati husika ya Nishati na Madini,``alisema

Akifafanua, alisema kilichotokea siku hiyo ni semina ambayo Tanesco waliiandaa na kuwakaribisha wajumbe wa Kamati hiyo kwa lengo la kuwaelezea mipango ya kununua mitambo ya Dowans kwa kuwa wana kiasi cha Sh. bilioni 60 kwa ajili hiyo.

``Sisi tuliwahoji kama mnazo Sh Bilioni 60 mnashindwajwe kuongezea kidogo ili mnunue mitambo mipya? Vilevile tukawahoji hivi mambo haya mnayotuambia kwenye semina wameyapeleka kwa wahusika ambao ni Kamati ya Niashati inayoongozwa na William Shelukindo?,`` alisema Kilasi na kuongeza:

``Baada ya hapo tuliwashauri suala hilo walifikishe kwa wahusika (Kamati ya Madini) na hakuna hata mahali pamoja tulipolitolea uamuzi suala hilo kwa vile halituhusu.``

Mbunge huyo alisema kufuatia kauli za Zitto ambazo zimezua malumbano, na kuifanya Kamati yao ionekane ina `walakini` wanamsubiri kwa hamu arejee ili wamuweka kiti moto.

``Unajua baada ya semina ile mimi nilienda Zambia, huku nyuma ndo nikasikia malumbano, lakini baada ya kurejea nimewauliza wenzangu na hasa makatibu wanaoandika muhtasari, kama kuna kikao kingine kimeketi na kutoa uamuzi, lakini wakasema hapana. Sasa tunamsubiri Zito arejee safarini ili tumuulize kulikoni? ``Alisema.

 
Namtazama Zitto kama mwanasiasa ambaye amepanda jukwaani anahutubia uzuri wa Dowans kwa watanzania wa leo! Halafu wanaanza kumzomea (kama mawaziri wa JK) yeye anaamua kukomaa na msimamo wake! Ajabu kweli - hii si kawaida katika ulimwengu wa siasa!

Na hii excuse kwamba hakumaanisha Dowans ila anataka TANESCO wanunue mitambo kokote si ya kweli! Zitto alijua kuwa akina Shelukindo hawakuwakataza TANESCO kununua mitambo (hata ya Dowans) sas iweje leo yeye atake kamati zikutane! Wajadili nini!

Hakuna haja ya kumtetea Zitto kwa hili hakuna cha kusema wengi wanamlazimisha akubali hoja zao ILA tunamshangaa huyu aliyekuwa shujaa wetu ghafla kawa kipofu lakini anataka kutuamisha kuwa anaona wakati ni wazi haoni! Hakuna haja ya kumlazimisha Zitto kuomba radhi! Ameshakuwa kipofu na sisi tunaona kama atapata kuona tena tutamwona. Leo ni mbunge tu anabishana na watu hivi, je angekuwa na madaraka kama ya rais si angekuwa dictator! Kila siku tunamshangaa JK na kuwaacha akina RA et al kwa nini ni tusimshangae na huyu sasa!

Naamini wengi wa wana JF ni wazalendo na wengi wetu si wanasiasa ila tunaipenda nchi yetu - sasa yeye ambaye ni mwanasiasa hata hayuko sensitive kusikiliza maoni ya watu! Amekomaa! Hajui wanasiasa hujengwa na watu! Angeamua kuwa mchumi huko ni ruksa kukomaa na hoja yako almradi una ushahidi wa kisayansi lakini kwenye politics! Bila watu (wapiga kura - iwe wa Kigoma au UDSM nani angemjua Zitto!). Degree za Economics hazijampa huu umaarufu kwa sababu ni wazi kuna economists wazuri kuliko Zitto na hawajawa maarufu. He is indeed becoming a liability - anatufundisha tusiwe wepesi wa kuwaamini sana watu, hasa wanasiasa!
 
Aliyosema Zitto Kabwe kwamba yametokea kwenye kamati yake wenzake wamemruka! Makamu Mwenyekiti amesema Kamati ya Hesabu haikuwa na mpango wa kukutana na Kamati ya Madini kwa sababu "halituhusu."

Sasa najiuliza, ni kwa nini Dr. Slaa alisema kwamba hatujui yaliyotokea kwenye kamati ya Zitto? Hata Dr. Slaa hakumwamini Zitto? Duuuh, hii inatisha mbona!

Makamu Mwenyekiti wa Zitto kasema hivi:

Kaka kamati ina wajumbe zaidi ya kumi na tano hivyo kuwa makini katika kusema kuwa wenziwe wamemruka. Lakini pia ulitegemea nini kutoka kwa Mbunge wa CCM katika hali kama hii ambayo ni rahisi kumaliza udhia wa wapinzani na haswa mtu kama Zitto ambaye wanamuona kama kiungo muhimu wa mabadiliko ya mwendo wa kisiasa nchini tangia wakati wa BUZWAGI. Pia unadhani kuwa CCM wangekuwa hawalazimiki kikanuni kuchagua upinzani katika nafasi ya uenyekiti wangemchagua Zitto. Lakini zaidi unajua siasa za ndani za kamati hizi?

Hata ningekuwa mimi ni CCM ama CUF ambao wanaona CHADEMA ni adui wao mkubwa kuliko CCM hivi sasa nisingelisema tofauti na huyu mama ama kina Lipumba.

Vilevile tujitayarishe kuona sakata hili ndani ya kamati kwani CCM wako mtegoni haswa maana wakati wanaona wana sababu nyepesi ya kuondokana na uenyekiti wa Zitto lakini kazi inakuja pale itakapowalazimu kuwachagua CUF kitu ambacho wanakiepuka zaidi ya kuwa mtu wa CHADEMA.

omarilyas
 
Omarilyas, ndiyo hapo nasema huwezi kuwa na mpango nzuri kwenye makabrasha tu halafu ukija katika utekelezaji ni sifuri. Kwa maoni yangu mipango ya muda mrefu ambayo unaiweza kuiita mizuri ni ile ambayo utekezaji wake pia unakamilika 100%, vinginevyo hiyo mipango ni mizuri tu ikiwa kwenye makabrasha lakini mafanikio yake Watanzania hatuyaoni kwa sababu utekelezaji wa mipango hiyo hakuna.

Kama ninakuelewa ni kuwa Tanzania hatuna mipango MIZURI ya muda mrefu na sio kuwa HATUNA mipango ya muda mrefu....hapo nakubaliana nawe 100%.

omarilyas
 
Zitto kabwe nitasema kweli daima nilikushabikia sana nilikuenzi sana nilikupenda sana tuliongea sana na tulijadiliana sana. niliona faraja kuongea na kijana mwanamapinduzi mtetezi wa taifa mzalendo wa kweli. mimi na wenzangu tulikuwa tayari kujitolea zaidi ya mwanzo kwa ajili yako uli-inspire wengi.
sichelei kukwambia hufai jiuzulu ujijengee heshima. sio unafiki kusema umekula mlungula na kwa sababu hiyo ugonjwa huu ni mkubwa sana kiasi kwamba akili yako haiwezi kuwa sawa tena utatetea ujinga uozo fisadi na ufisadi umekwisha . na kila atakaye jitahidi kukutetea mwishowe atajikuta kajimaliza mwenyewe kwani huwezi kumtetea mla rushwa na fisadi.

timeline ya richmond/dowans iko wazi wamiliki wake waliojificha wako wazi walikuwa wanapigia debe mitambo mibovu wako wazi waliopigia debe mitambo mizima wako wazi wanajulikana sasa ulikuwa unashikia bendera kwa lipi??
Tulikupa mzunguko wa richmond /dowans na mwisho wake leo unajifanya hujui tulikueleza wazi watakuja na gia ya kuuza mitambo ile sasa lipi geni unatetea giza kwa maslahi ya Rostam.

Najua vitisho vimekuweka pamaya. jiuzulu ulinde heshima yako iliyoptea.
 
Topic ni Zitto au Dowans?

Kama Mtanzania Zitto is entitled to whatever he said. Sielewi kelele zinatoka wapi!
 
Topic ni Zitto au Dowans?

Kama Mtanzania Zitto is entitled to whatever he said. Sielewi kelele zinatoka wapi!

Ni kwasababu thread zaidi ya nne zimeanzishwa zikimtaja Zitto na sio Dowans lakini zote zimeunganishwa hapa,mimi sielewi kinakwepwa nini.
 
kuna sababu ya kuwaachia wataalam wa tanesco, ambao wanashauri mitambo inunuliwe. Sioni sababu ya kuwepo wataalamu halafu tuanze kuwafundisha. mambo yakienda vibaya tutamlaumu nani?
 
Kipa,
Kikwete ana makosa na mapungufu yake lakini sio ktk hili..Ikiwa sisi tumeshindwa hata kutumia vizuri fedha zilizotolewa kwa dharura kweli tunaweza jenga nchi ktk miradi ya muda mrefu..Trust me, matukio yote haya nadhani ni bora ungewatazama viongozi wetu wanaoendesha shughuli hizo kabla ya rais..Kikwete atafukuza wangapi..
Huko CCM karibu asilimia 80 wameoza sasa Kikwete ni ktk fungu la kaa walioko ktk kapu wanasubiri kuchomwa..Binafsi naanza kuamini kabisa kwamba hakuna mtu yeyote anayeweza kuibadilisha CCM na Ufisadi ni ukweli ambao hatutaki kuukubali..
The only way out ni kutochagua CCM wameshindwa kama KANU, ZAPU, UPC na vyama vinginevyo vilivyoletea Uhuru barani..waliobakia wote ni madikteta tu!
Mkandara,

Ni lazima Kikwete alaumiwe kwa hili, yeye ni mkuu wa nchi tuliomchagua sisi anawajibika kwetu ( Wananchi ), Yeye ndiye anateua (Wasaidizi wake ) Mawaziri, wakuu wa mikoa, wa wilaya na wakurugenzi wakuu wa mashirika ya umma kutokana na ushauri wa wizara husika, wakurugenzi hao wanawajibika moja kwa moja kwa waziri wa wizara husika, sasa kama wakina Mgawe, Dr Idris Rashidi ( huyu sijui cheti chake ilipata wapi , mbona anafanya mambo kawa wakina kihiyo ) , mataka hawatekelezi majukumu yao na bado wapo kwenye nafasi zao na mawaziri husika wanazidi kutumia pesa zetu tu bila ya kupendekeza kwake( Rais ) wawajibishe anatakiwa ( Raisi ) awawajibishe mawaziri hao.
ni lazima watanzania tuanze utamaduni wa kuwajibishana bila hivyo ni ndoto kufikia maendeleo yeyote
 
Back
Top Bottom