Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Mimi nafikiri kutokana na mazingira ya ununuzi wa awali wa mitambo hiyo michakavu kutoka kwenye kampuni feki ya Richmond...Kusapoti ununuzi wa mitambo hiyo bila vigezo vitakavyojitosheleza mbele za wananchi kunaweza kupelekea mitizamo kwamba there is some sort of ufisadi....Honestly hata kama ni uamuzi wake wa kisiasa..Kuwapa hao watu mipesa yote hiyo na wakti kuna maswali yanaoyotakiwa kujibiwa ni swala linalohitaji maelezo ya kina.
Naona umezungumzia sana kuhusu "kutofautiana naye kimaelezo" Kumbuka ni tofauti za maamuzi na utekelezaji na si tu "maelezo" Malezo aliyoyatoa bado hayawezi kuhalalisha ununuzi wa mitambo hiyo na hivyo basi atueleze nia yake haswa ilikuwa ni nini na si tu kusema haogopi kuitwa fisadi ama kuonekana ana mtizamo wa tofauti.
Na pia unaposema mmetofautiana kisiasa una maana gani? Yani Zitto a lobby kumsadia Rostam na Lowassa na Karamagi halafu useme ni utofauti wa kisiasa tu, well kama wewe ni CHADEMA kama Zitto then utofauti wenu wa kisiasa unahitaji maelezo zaidi.
Ukishindwa kuwaelesha wana JF utaweza vipi kuwaelewesha wananchi kama si kuwadanganya na wizi mtupu?

Zitto ana uamuzi gani katika suala la ununuzi wa majenereta? akiamua yanunuliwe yatanunuliwa? na akiamua yasinunuliwe je?
 
Zitto ana uamuzi gani katika suala la ununuzi wa majenereta? akiamua yanunuliwe yatanunuliwa? na akiamua yasinunuliwe je?

Akitaka kujitetea kuwa hana uamzi,basi inabidi awaombe wanakamati wake radhi kwa kuongea kama vile anawawakilisha. Pia kama yeye ni mwenyekiti halafu anatowa maelezo yanayopingana na msimamo wa kamati yake then ndio maana watu wanahoji kwanini.
MKJJ umesema ana uamuzi gani na wakati huo huo ulisema huo ni uamuzi wake wa kisiasa...Sasa si ina maana alikuwa na nia ya kuwasaidia watu flani flani kisasa? Vipi kuhusu kifedha?
Naona unazidi kuleta siasa kwasababu toka huo msimamo uwe wake na si wa kamati basi tunataka kupuuzia na kuleta taswira ya kwamba kwasababu alichokizumgumzia hakina uzito kwenye maamuzi...Sasa vikao na kina Dk Rashid vilikuwa vya nini?
Kama ushauri wake usingehojiwa si ungefuatwa? Na kama ulikuwa ni uamuzi wake binafsi ambao ana uhakika kuwa hauta affect uamuzi wa ununuzi then kwanini aliutoa? Nani alimuuliza?
Tukiangalia vizuri, the guy has to offer some sort of akcnowledging that there is screwing up.
 
Akitaka kujitetea kuwa hana uamzi,basi inabidi awaombe wanakamati wake radhi kwa kuongea kama vile anawawakilisha. Pia kama yeye ni mwenyekiti halafu anatowa maelezo yanayopingana na msimamo wa kamati yake then ndio maana watu wanahoji kwanini.

Umeuona msimamo wa Kamati yake?

MKJJ umesema ana uamuzi gani na wakati huo huo ulisema huo ni uamuzi wake wa kisiasa...Sasa si ina maana alikuwa na nia ya kuwasaidia watu flani flani kisasa? Vipi kuhusu kifedha?

Unasoma mengi kuliko kilichosemwa.
Naona unazidi kuleta siasa kwasababu toka huo msimamo uwe wake na si wa kamati basi tunataka kupuuzia na kuleta taswira ya kwamba kwasababu alichokizumgumzia hakina uzito kwenye maamuzi...Sasa vikao na kina Dk Rashid vilikuwa vya nini?

Unaujua msimamo wa kamati hasa ni nini?

Kama ushauri wake usingehojiwa si ungefuatwa? Na kama ulikuwa ni uamuzi wake binafsi ambao ana uhakika kuwa hauta affect uamuzi wa ununuzi then kwanini aliutoa? Nani alimuuliza?
Tukiangalia vizuri, the guy has to offer some sort of akcnowledging that there is screwing up.

Hana sababu kama haamini hajakosea. Kama atatambua alikosea na dhamira yake itamuonesha hivyo basi atajua cha kufanya lakini asiombe radhi kwa sababu ya kuturidhisha mimi na wewe au kuwa politically correct.
 
Zitto hawezi omba msamaha, hilo litamwaribia zaidi..Ni matamanio ya walio wengi kwa nia tofauti kuona Mh Zitto anaomba msamaha...

Je endapo Zitto bado anaamini kuwa msimamo wake ulikuwa sawa ingawa unaweza ukawa umemharibia kisiasa kama ambavyo wengu hapa wanavyodai ni sawa akiomba radhi? Hivi hatakuwa anaendeleza usanii wa kisiasa. Hivi kweli Tanzania tunayoitaka ni ile ya kuendeleza siasa hohehahe zilizojaa usanii?

Kipi muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu. Kusimamia maamuzi yako unayoamini kuwa ni sahihi ama kusema maneno yanayolenga kuwafurahisha wafuasi wako ama wale watu unaowaamini?

Kama ni hivyo basi naamini wapo wanasiasa wa kufuata na kuwaamini kuliko Zitto na wamejaa tele kule hatika madhabahu ya UFISADI.

omarilyas
 
yanayotokea nchi hii yanasikitisha sana. Hivi kweli nchii tumeshidwa kuwa na mipango ya muda mrefu ya kupata umeme wa kutosha. Upungufu wa umeme unaotokana na kukosekana kwa mvua umekuwa ukitokea karibu kila baada ya miaka miwili. Tumeshidwa namna ya kuliondoa taifa katika tatizo hili?. Ebu tujifunze wenzetu wamewezaje pata umeme wa kudumu. Kama kukopa tufanye hivyo tuondokane na tatizo hilo. Inawezekana suala la kutafuta umeme wa dharula imekuwa miradi ya wanasiasa na chama tawala!!!. Naomba JF members tuendelea Kupiga kelele sana juu ya ufisadi uliokidhiri ndani ya serikali hii. Ama sivyo nchi hii hakuna future.

Tanzania ni nchi yenye umakini sana katika suala la kuwa na mipango ya muda mrefu. Matatizo yapo katika maeneo kadhaa kama yafuatayo:
  1. Ukosefu wa ushirikishaji wa wananchi katika kufikia mipango hiyo na hivyo mipango hiyo kukosa uhalali na uchangiaji chanya wa wananchi katika utekelezaji wake.
  2. Kutumika kwa wataalamu walio na mahusiano maalumu na wanasiasa zaidi ya kigezo cha utaalamu uliokubuhu.
  3. Utegemezi wa mataifa na asasi za nje katika kugharamia utekelezaji wa mipango hiyo.
  4. Uingiliaji wa maslahi binafsi na ya kisiasa ya muda mfupi katika utekelezaji wa mipango hiyo ya muda mrefu.

Pia ni utamaduni wa watanzania kuacha kujishughulisha kutafuta na kufuatilia taarifa za mipango hiyo kutoka serikalini. Tuna tatizo kubwa la upashanaji habari lakini pia hatuna utamaduni wa kujisumbua kutafuta habari hizo.

Haya ni matatizo ya kimfumo ambayo ni uthubutu wa kubadili mfumo wetu wa kisiasa, kijamii na kiuchumi tu ndio utakaotutoa hapa tulipo lakini sio vinginevyo.

Tuthubutu kuwa sehemu ya mabadiliko na sio kuendelea kusubiri MASIHA FEKI ndio watuletee mabadiliko tunayoyataka. Kupiga kelele tu haitoshi. Watanzania tulipiga na tunaendelea kupiga kelele dunia nzima ikatusikia lakini bado tupo katika lindi la matatizo ambayo yanazidi kuongezeka badala ya kupungua.

omarilyas
 
Tanzania ni nchi yenye umakini sana katika suala la kuwa na mipango ya muda mrefu.
omarilyas

Omarilyas, hapa sikubaliani na wewe. Nitakupa mfano mmoja tu pamoja na kuwa kuna mifano mingi sana. Viongozi wetu hupiga kelele kila kukicha kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu, lakini vitendo vyao siku zote haviendani na kauli hiyo. Katika bajeti ya nchi ya kila mwaka Wizara ya kilimo hupata asilimia ndogo sana ambayo haiendani na kauli hiyo kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu. Na matokeo yake kilimo chetu kimekuwa ni kile kile cha kutumia jembe la mkono miaka nenda miaka rudi.
 
Hana sababu kama haamini hajakosea. Kama atatambua alikosea na dhamira yake itamuonesha hivyo basi atajua cha kufanya lakini asiombe radhi kwa sababu ya kuturidhisha mimi na wewe au kuwa politically correct.

Zitto anaweza kuamini hajakosea, lakini umma wa Watanzania haukubaliani na aliyoyasema kwa maana nyingine Watanzania wengi tunamuona kakosea. Wakati mwingine ni bora ukubali kwamba umeteleza na kauli uliyoitoa ilikuwa na kasoro. Kama Obama Rais wa Taifa kubwa anaweza kukubali makosa basi Zitto naye anaweza kukubali makosa.

Binadamu hatuko perfect na unapojikwaa ni bora kukubali badala ya kung'ang'ania kwamba sikujikwaa. Credibility na Reputation ya Zitto imeingia dosari kubwa sana kama ataendelea kung'ang'ania kwamba hakukosea basi atakuwa na wakati mgumu sana siyo tu kwenye nyanja za siasa bali nyanja zozote atakazotaka kushiriki baadaye.
 
Omarilyas, hapa sikubaliani na wewe. Nitakupa mfano mmoja tu pamoja na kuwa kuna mifano mingi sana. Viongozi wetu hupiga kelele kila kukicha kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu, lakini vitendo vyao siku zote haviendani na kauli hiyo. Katika bajeti ya nchi ya kila mwaka Wizara ya kilimo hupata asilimia ndogo sana ambayo haiendani na kauli hiyo kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu. Na matokeo yake kilimo chetu kimekiwa ni kile kile cha kutumia jembe la mkono miaka nenda miaka rudi.

Kaka hiyo haina maana kuwa hatuna mipango ya muda mrefu. Ipo tena mingi tu. Hata katika sekta ya KILIMO kaka. Ukitoa mipango mingi ya miaka ya nyuma hivi sasa kuna Mpango wa ASDP (Agriculture Sector Development Programe) ambao ulipaswa kupatiwa shilingi trilioni moja kila mwaka kwa miaka saba. Kaka ukipitia kwa umakini mpango huu wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo huo utashangaa sana inakuwaje tunaanza kuja na mipango ya bandikabandua kama ule wa mbolea na fedha za EPA na kuacha kuuwezesha mpango huu ili ufanikiwe.

Tatizo kubwa katika mpango huu ni kuwa haukushirikisha wadau wengi katika kuuandaa, umekosa uhalali kwa upande wa walengwa halisi, unategemea msaada wa nje kuweza kuugharamia na zaidi wanasiasa wengi hawaujui kwa undani na hivyo kuuona hauna maslahi yao kisiasa haswa katika kutimiza malengo yao ya muda mfupi.

Fuatailia mpango huo pamoja na mabadiliko ya kisera yanayoendelea uone ni jinsi gani watanzania tunavyopenda kuja na mipango ya muda mrefu lakini hatuko tayari kukomaa nayo kutokana na mapungufu yetu kimfumo na kibinfsi.

omarilyas
 
Last edited:
Kama Obama Rais wa Taifa kubwa anaweza kukubali makosa basi Zitto naye anaweza kukubali makosa..[/B]

Kaka nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sana siasa za OBAMA na "MABADILIKO WANAYOAMINI" haswa kwa muda wa miezi mitano ambayo nimekuja huku US kwa minajili kadhaa mojawapo ikiwa ni kusoma siasa za uchaguzi katika nchi hii. Ukweli ni kuwa tukitoa kuwa OBAMA ni "A" brainer kuna usanii mwingi sana katika siasa zake. tuwe makini tunapojaribu kuchukua WANASIASA mahiri kama OBAMA alivyojithibitishia kama BLUE PRINT ya mabadilko tuyapiganayo nchini mwetu....

"I screw up" ina maana nyingi kisiasa jamani....

Kumbuka kuna wasanii walikubuhu nyuma yake ambao wana sura ya imani lakini ni wajanja mno kisiasa. Walio maarufu ni Rahm na Axelroid. Wapo wengine wanatisha ukiwajua na OBAMA anaamini sana kutumia mbinu zao kisiasa.

omarilyas
 
Umeuona msimamo wa Kamati yake?
Wapi nimesema msimamo wake ni sawa na wa kamati yake? Kuna yule mwanamama aliyekuwa nje ya nchi ambaye na yeye alisema ameshtushwa na uamuzi wa Zitto na akasema wazi kuwa si msiamo wa kamati,na Mwakyembe alishampigia Zitto kelele kuwa anaingilia kazi ambazo si zake..Kwa hiyo mlipoamua kuitoa kamati yake na kudai ni uamuzi wake binafsi then tubaki hapo..Kwenye mjadala kuhusu uamuzi wake "binafsi wa kisiasa" Ama "maelezo" kama unavyotaka tuelewe.



Unasoma mengi kuliko kilichosemwa.

Ni hapo unapopiga chenga za kisiasa kwenye kuhusu "maelezo ya kisiasa" na "uamuzi binafsi"


Unaujua msimamo wa kamati hasa ni nini?
Msimamo wa kamati siujui ila ni tofauti na msimamo wa Zitto.



Hana sababu kama haamini hajakosea. Kama atatambua alikosea na dhamira yake itamuonesha hivyo basi atajua cha kufanya lakini asiombe radhi kwa sababu ya kuturidhisha mimi na wewe au kuwa politically correct.

Kutoa maelezo kuwa ni sahihi kununuwa mitambo chakavu ya kampuni hewa si kuturidhisha wana JF....Ni kuwakosea wananchi kwa maamuzi mabovu yanayoitwa misimamo...Kuwa politically correct si muhimu kwenye utekelezaji wa maamuzi yenye kuwagusa wananchi moja kwa moja? Issue hapa si kuwa "politically correct" Bali ni kuwa ethicall wrong. Angekuja na alternative nyingine kabla ya hapo then nia ingekuwa wazi...Sasa 2010 hiyo hapo...Another EPA on the make...Sasa radhi haina maana kwa wananchi?
 
My point ni kuwa Zitto haitaji kutoa maelezo zaidi ya aliyoyatoa. Wote tunajua alichosema. Wapo ambao hawakubaliani naye na wapo wanaokubaliana naye.

Hana sababu kama haamini hajakosea. Kama atatambua alikosea na dhamira yake itamuonesha hivyo basi atajua cha kufanya lakini asiombe radhi kwa sababu ya kuturidhisha mimi na wewe au kuwa politically correct.

Mwanakijiji,
Nafikiri humfanyii vema Zitto kwa kumuweka mahali pabaya zaidi kwa kuongeza pressure ya yeye kutokutoa angalau samahani kwa alivyochemsha. He is alone on his side with the exception of some few whom we know well their everlasting positions on Richmond+Dowans.

Nitakubali kuwa hapo awali Zitto atakuwa hakuona tatizo lililopo kwenye uamuzi aliofikia kwa kuwa alikuwa na upeo mdogo kwenye hili suala. Lakini kama hadi hivi sasa baada ya midahalo chungu zima na kelele kebe kebe atakuwa bado hajafunguka macho, basi atakuwa ana lake na wala sio kuwa anamtazamo tofauti au hata kiburi haiwezi kuwa kinga yake kama unavyoonyesha kupendekeza.

Anachotakiwa Mh. Zitto kufanya sio kuomba msamaha bali kuelezea wafuasi wake kuwa mtizamo wake wa awali ulikuwa na makosa (He Screwed Up), na kwa sasa hivi anamtazamo upi. Vinginevyo asije akatushangaa walewale tuliokuwa tunamshangilia tukimpiga mayai viza kama mafisadi wengine.

He only need to acknowledge that he errored in his previous stance.
 
Kaka hiyo haina maana kuwa hatuna mipango ya muda mrefu. Ipo tena mingi tu. Hata katika sekta ya KILIMO kaka. Ukitoa mipango mingi ya miaka ya nyuma hivi sasa kuna Mpango wa ASDP (Agriculture Sector Development Programe) ambao ulipaswa kupatiwa shilingi trilioni moja kila mwaka kwa miaka saba.

Omarilyas,
Sidhani kama umelielewa vema suala la mipango ya muda mrefu. Kwa ujumla hatuna mipango ya muda mrefu na ndio maana hakuna anayeijua. Mipango ya muda mrefu haiwi siri ya waziri au mkurugenzi fulani, inakuwa ni ya taifa na inawekwa wazi kama ilivyo bajeti ili kila mhusika aweze kuiangalia tunakoelekea. Mipango hiyo huwa na mihula (mile stones) ambayo huweza kukaguliwa kuona wapi hiyo mipango imefikia.

Kama vipo vi-program walivyoandika kwa ajili ya kuwaonyesha wahisani ili waweze kuwachuna pesa za kununulia mashangingi, hiyo sio mipango ya Taifa na ndio maana haiko wazi.

Serikali ya JK inaendeshwa kama zimamoto. Ana react kulingana na nini ni news wakati huo. Kazi yake kubwa anafikiri ni kutafuta misaada na sio kutoa mwelekeo wa maendeleo na mabadiliko na kuyasimamia.

Husubiri news. Watu wakipiga kelele kuhusu Richmond, anafukuza mtu na kuzima makali lakini hatatui tatizo na ndio maana DOWANS wameweza kuibuka ili kutuuzia matapishi yetu, maana tatizo la umeme bado lipo pale pale. EPA nayo hivyo hivyo, sidhani kama loopholes zilizopo BOT zimezibwa au ni mpaka tupoteze bilioni nyingine uchaguzi ujao. Waalimu, chuo kikuu, kudorora kwa elimu, msongamano wa magari Dar, uhaba wa chakula n.k., n.k., vyote anababaisha babaisha tu ili siku zisogee bila kutatua.

Ukweli ni kuwa hatuna mipango na Kikwete doesn't care. We are led by a blind-man and we seem to have accepted our fate.
 
Zitto anaweza kuamini hajakosea, lakini umma wa Watanzania haukubaliani na aliyoyasema kwa maana nyingine Watanzania wengi tunamuona kakosea. Wakati mwingine ni bora ukubali kwamba umeteleza na kauli uliyoitoa ilikuwa na kasoro. Kama Obama Rais wa Taifa kubwa anaweza kukubali makosa basi Zitto naye anaweza kukubali makosa.

Binadamu hatuko perfect na unapojikwaa ni bora kukubali badala ya kung'ang'ania kwamba sikujikwaa. Credibility na Reputation ya Zitto imeingia dosari kubwa sana kama ataendelea kung'ang'ania kwamba hakukosea basi atakuwa na wakati mgumu sana siyo tu kwenye nyanja za siasa bali nyanja zozote atakazotaka kushiriki baadaye.


Harafu mtu unaweza kweli kufikiri mawazo yako hayako sahihi ama mawazo ya watu wengine ndiyo yanayokuwezesha kutambuwa mawazo yako hayako sahihi.?

Ngoja nikuambieni kitu hata FISADI anapoamuwa kufuja fedha huwa anaamini mawazo yake ya kufisadi na kujenga ma hekalu yapo sahihi,na kwa kuamini mawazo yake hayo ndipo huamuwa kuyatekeleza.
HAkuna mtu mtu hapa duniani asiyeyaamini mawazo yake ,kila mmoja anayaamini mawazo yake yapo sahihi ila waungwana pembeni ndipo wanapokusituwa na kukueleza mawazo yako unayoyaamini sio sahihi ama ni sahihi.
 
Jamanie, kama CCM na Kikwete walishakopeshwa na kina hawa jamaa basi watafute njia ya kuwalipa bila kuiingiza nchi kwenye milungula ya kiajaba ajabu mwaka nenda, mwaka rudi.

Bwanae, kuna watu wengine nuksi kushinda ukoma. Hawa ni wale ambao baba na mama yao ni fedha; dini yao ni dala; kabila lao pauni au yeni; na utu wao umakini, ujinga na maradhi ya wananchi wa nchi zao. Epukaneni nao. Fungueni macho muone hao ambao kwa ujinga wao wanaamini wana akili nyingi kuliko Watanzania wote wakiwekwa pamoja.
 
Unlikely bedfellows emerge in Dowans saga
THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

PUBLIC debate on the government’s failed Dowans purchase bid continues to grow well after the state-run Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) was forced to abandon the dubious deal.

An overwhelming majority of Tanzanians seem to be fiercely opposed to the hugely controversial proposal, with just a handful of people in government and elsewhere publicly in favour of the buyout.

Most of the public debate at office corridors, street corners, radio talk shows and Internet forums now increasingly focuses on the unlikely support for the deal from the Kigoma North Member of Parliament, Zitto Kabwe (Chadema).

The youthful opposition leader, who gained nationwide popularity in the recent past after taking on the government over the controversial Buzwagi gold deal, raised many eyebrows after publicly coming out in support of TANESCO’s intention to purchase the second-hand power turbines.

Zitto stood virtually alone in supporting the relentless pursuit by TANESCO’s Managing Director, Dr Idris Rashidi, and the Minister for Energy Minerals, William Ngeleja, to land the deal.

Even as the Speaker of the National Assembly, Samwel Sitta, the chairman of the parliamentary energy and minerals committee, William Shellukindo, and several other influential MPs slammed the proposal, the opposition lawmaker remained firmly in defiance of public opinion.

And many people are now questioning the MP’s real motives for supporting the much-criticized deal, with some observers even suggesting that the image of the erstwhile respected politician could suffer irreparable damage.

At the online public forum, www.jamiiforums.com, thousands of viewers are posting critical comments on a daily basis against Ngeleja, Dr Rashidi and Zitto for supporting the proposed Dowans buyout deal.

One post that was viewed more than 500 times bestows the Chadema lawmaker with the nickname ’Dowans’ for his role in the saga.

Another post on the website titled ”The Showdown - The Gvt, Parliament, Tanesco, Dowans and the People!” dominated much of the debate on the public forum, drawing more than 18,600 views by yesterday afternoon.

’’Dowans and Richmond are not clean legal entities as they do not even have a country of origin where they have been legally registered. They are ghost companies. So we cannot negotiate with ghost companies,’’ said Susuviri, one of the JamiiForums (JF) members.

Susuviri urged members of the public to petition Rashidi for his immediate resignation or dismissal by President Jakaya Kikwete.

’’I respect Zitto a lot, but he has missed the point in this issue. It’s better for him to just keep quiet,’’ added the JF member.

Another contributor on the online forum, MTM, said: ’’Just wait and see the impact of Dowans on Zitto -- I can bet my nationality on that. There is a huge backslash coming.’’

The opposition MP was forced to post his own comments on the JF website to respond to his growing army of critics.

’’I want to state here in explicit terms that, I, Kabwe Zuberi Zitto (MP), Chairman Public Investments Committee of Parliament of Tanzania, stand with TANESCO on their desire to acquire gas fired turbines to improve electricity generation to the country,’’ declared Zitto.

He added: ’’I stand firm in my decision and ready to be held accountable to that. I do this in good faith. I am genuine and honest. People can say all what they want to say, so long as this decision is mine based on the information I have -- technical information. So long as I reached to this decision without any influence whatsoever, I stand by it.’’

The MP surprisingly lashed out at his colleagues from the parliamentary energy and minerals committee, claiming that the Shellukindo committee’s rejection of the Dowans deal was ’’politically motivated.’’

Parliamentary sources say Ngeleja and Rashidi could face tough questioning in parliament next month when the Bunge session resumes.

The parliamentary energy and minerals committee has already stated its intention to summon Ngeleja over the Dowans saga.

There have been growing calls from both politicians and members of the public alike for the resignations of the TANESCO boss and the energy and minerals minister.

It remains to be seen if the embattled Rashidi and Ngeleja will heed the mounting calls for them to step down.


Source: ThisDay
 
Kaka hiyo haina maana kuwa hatuna mipango ya muda mrefu. Ipo tena mingi tu. Hata katika sekta ya KILIMO kaka. Ukitoa mipango mingi ya miaka ya nyuma hivi sasa kuna Mpango wa ASDP (Agriculture Sector Development Programe) ambao ulipaswa kupatiwa shilingi trilioni moja kila mwaka kwa miaka saba. Kaka ukipitia kwa umakini mpango huu wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo huo utashangaa sana inakuwaje tunaanza kuja na mipango ya bandikabandua kama ule wa mbolea na fedha za EPA na kuacha kuuwezesha mpango huu ili ufanikiwe.

Tatizo kubwa katika mpango huu ni kuwa haukushirikisha wadau wengi katika kuuandaa, umekosa uhalali kwa upande wa walengwa halisi, unategemea msaada wa nje kuweza kuugharamia na zaidi wanasiasa wengi hawaujui kwa undani na hivyo kuuona hauna maslahi yao kisiasa haswa katika kutimiza malengo yao ya muda mfupi.

Fuatailia mpango huo pamoja na mabadiliko ya kisera yanayoendelea uone ni jinsi gani watanzania tunavyopenda kuja na mipango ya muda mrefu lakini hatuko tayari kukomaa nayo kutokana na mapungufu yetu kimfumo na kibinfsi.

omarilyas

Nchi haiwezi kuwa na mipango ya muda mrefu kwenye makabrasha tu lakini ikija kwenye utekelezaji ni sifuri. Na hili ndilo lililopo nchini kwetu tuna mipango chungu nzima kwenye makabrasha lakini utekeleazi hakuna ndiyo maana Watanzania tunalalamika kwamba hatuoni maendeleo yoyote ya kuridhisha miaka nebda miaka rudi.
 
Kwa namna walivyoandika ThisDay hapo juu, nimeipenda namna waliyoitumia kui-quote JF na kuonyesha kuwa wako pamoja nasi hapa.
 
Mzee Mwanakijiji,
Sawa mkuu nimekusoma lakini katika kujifunza kwako ongeza hayo majibu yangu...utaepuka mengi sana kwa sababu hata siku moja Adui yako hakutakii mema na kamwe hawezi kukusaidia isipokuwa kwa faida yake..

Nikirudi ktk issue ya Mh. Zitto nadhani anahitaji kutoa samahani hasa hapa JF kwani wapo tuliomsamehe lakini wapo ambao bado wanatia shaka sana maelezo yake humu ndani.
Mkuu mimi sina shaka kabisa na Zitto huko nje isipokuwa anapokuja hapa kijiweni na taarifa kama ile ndugu yangu ilikuwa shock!..Na hasa aliposisitiza ndio msimamo wake na kuponda watu tunaoishi nje kwamba hatulijui joto la jiwe!..

Kifupi tumalize kama alivyosema Ogah, walioelewa wameisha elewa na kama Zitto ni mtu wa kujirudi atafahamu alichemsha nje ya hapo hatuwezi kumpinda tena..

Hii issue inanikumbusha sana madai ya CCM kuhusiana na sakata la EPA.. Fedha za EPA hazikuibiwa ila zilitoka kisheria kwa mashirka feki kama Kagoda yaliyoundwa kwa minajiri ya fedha hizo. Fedha hizo zikapewa uhalali kwa sababu ya dharura, na nia ya chama CCM kushinda uchaguzi 2005....Hivyo vibali vikatolewa.... Wakachota na kuzitumia...sasa wananchi wanapolalamikia mpango mzima, chama kinatuambia kuna baadhi ya watu (kina Rostam/Lowassa ndio wabaya lakini sio chama kizima, wakati ubaya wa hawa watu unatokana na fedha zilizochukuliwa Benki kuu nje ya sheria kwa ajili ya kampeni za uchaguzi, watu wakavuta zaidi ya kiwango kilichokusudiwa...

Kisheria kila aliyezipokea fedha zile ni mshirika wa wizi huo ikiwa ni pamoja na Wabunge waliotumia fedha hizo kwa Takrima ya uchaguzi wa mwaka 2005 lakini wajanja wakahalalisha takrima (pindisha sheria)..

Well, one can argue umuhimu wa kushinda CCM uchaguzi na vigumu sana kwa mwanaCCM kuona uharamu wake ikwa takrima sio haramu kikatiba.. kwa madai kwamba wakosefu ni kina Rostam walioiba zaidi na tujifunze kutenganisha Rostam, Kagoda, EPA na Uchaguzi..
 
Mzee Mwanakijiji,
Sawa mkuu nimekusoma lakini katika kujifunza kwako ongeza hayo majibu yangu...utaepuka mengi sana kwa sababu hata siku moja Adui yako hakutakii mema na kamwe hawezi kukusaidia isipokuwa kwa faida yake..
Nikirudi ktk issue ya Mh. Zitto nadhani anahitaji kutoa samahani hasa hapa JF kwani wapo tuliomsamehe lakini wapo ambao bado wanatia shaka sana maelezo yake humu ndani.
Mkuu mimi sina shaka kabisa na Zitto huko nje isipokuwa anapokuja hapa kijiweni na taarifa kama ile ndugu yangu ilikuwa shock!..Na hasa aliposisitiza ndio msimamo wake na kuponda watu tunaoishi nje kwamba hatulijui joto la jiwe!..

Kifupi tumalize kama alivyosema Ogah, walioelewa wameisha elewa na kama Zitto ni mtu wa kujirudi atafahamu alichemsha nje ya hapo hatuwezi kumpinda tena..
Hii issue inanikumbusha sana madai ya CCM kuhusiana na sakata la EPA.. Fedha za EPA hazikuibiwa ila zilitoka kisheria kwa mashirka feki kama Kagoda yaliyoundwa kwa minajiri ya fedha hizo. Fedha hizo zikapewa uhalali kwa sababu ya dharura, na nia ya chama CCM kushinda uchaguzi 2005....Hivyo vibali vikatolewa.... Wakachota na kuzitumia...sasa wananchi wanapolalamikia mpango mzima, chama kinatuambia kuna baadhi ya watu (kina Rostam/Lowassa ndio wabaya lakini sio chama kizima, wakati ubaya wa hawa watu unatokana na fedha zilizochukuliwa Benki kuu nje ya sheria kwa ajili ya kampeni za uchaguzi, watu wakavuta zaidi ya kiwango kilichokusudiwa...
Kisheria kila aliyezipokea fedha zile ni mshirika wa wizi huo ikiwa ni pamoja na Wabunge waliotumia fedha hizo kwa Takrima ya uchaguzi wa mwaka 2005 lakini wajanja wakahalalisha takrima (pindisha sheria)..
Well, one can argue umuhimu wa kushinda CCM uchaguzi na vigumu sana kwa mwanaCCM kuona uharamu wake ikwa takrima sio haramu kikatiba.. kwa madai kwamba wakosefu ni kina Rostam walioiba zaidi na tujifunze kutenganisha Rostam, Kagoda, EPA na Uchaguzi..

Ndiyo Mkuu
Fedha za BOT hafungwi mtu maana wote wameshiriki kuzitumia,Kosa la Lowasa/Rostam ni wao kufungulia mabwawa ya maji na Lowasa kwenda sijui nchi gani akitaka Mvua artificial ili baadae waje waseme dhalula.

Tz hakuna dhalula yoyote ya umeme ila wanaiacha iwe dhalula ama kutengeneza udhalula watuibie kutokana na udhalula artificial.
 
Mkandara, Zitto akitambua ni wapi alipotoka na akaja kuomba radhi mimi sina tatizo; siyo hapa tu bali hata kwa hadhara ya Watanzania. Ni sehemu ya uungwana na ukomavu. Tatizo langu ni kuwa baadhi ya watu wanaonekana kukwazwa kupita kiasi kana kwamba Zitto hatakiwi kufanya makosa, kupotoka au kwenda nje ya mstari fulani. Kwamba, akichukua msimamo basi ni lazima uwe sahihi wakati wote. Hilo haliwezekani. Hakuna mwanadamu anayeweza hivyo.

Ndiyo maana kwa maoni yangu, nashangazwa na ukali wa maneno ya watu kwani naelewa kuna wale ambao wanatambua kuwa kijana amekosea na wamejaribu kumshawishi aone makosa hayo; bado hilo hatujui kama ameona makosa hayo.

Tatizo ni kuwa watu wanataka Zitto akubali tu kuwa amekosea hata pale ambapo dhamira yake na akili yake haimshawishi kuona makosa hayo. Dhamira ya mwanadamu iko juu ya sheria n.k NI lazima afanye kile ambacho dhamira yake ambayo imejengwa vizuri (well formed conscience) inamuambia kuwa ni kitu sahihi.

Nadhani tukimpa muda wa kutafakari na kupitia taratibu hoja hizi zote na ushahidi ambao utazidi kutokea huko mbeleni ataweza kuona ni wapi alipoenda pembeni na kwa kiasi gani. Kwa sababu naamini kama alivyosema Halisi yawezekana kabisa kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo hayakuripotiwa sahihi. Uzuri ni kuwa wengi wetu waliouelewa msimamo wa Zitto siyo kutokana na magazeti bali tumesoma aliyoyaandika yeye mwenyewe.

Ombi langu ni kuwa watu wasiwe wakali sana kulazimisha mtu achukue msimamo wao kama mtu huyo hajashawishika kufanya hivyo. Vinginevyo tutamfanya achukue uamuzi wa kinafiki. Tumpe nafasi apime na kuona uzito wa ushahidi uliopo kwanini hatulazimiki na hatuna sababu ya kununua majenereta yaliyoletwa na Dowans, na akishashawishika hivyo basi yeye mwenyewe atajua achukue hatua gani. Vinginevyo, atakuja hapa na kuomba radhi na watu watasema "haitoshi, inabidi ujiuzulu"; na wengine watasema "haitoshi kujiuzulu, itabidi ujivue uanachama" (tayari kuna watu wameshatoa mapendekezo hayo humu humu).

Ninachoelewa ni kwamba kuna wale ambao wanamkosoa Zitto kwa ni nzuri lakini siwezi kushangaa kuna wale ambao wanamkosoa ili kumfanya duni na kumharibu kuliko ukweli wa hali halisi.
 
Back
Top Bottom