Infact hata power rationing ikifanyika vizuri na kwa mipango sahihi, tunaweza kudunda vilevile bila karaha mpaka pale tutakapokuja na suluhisho la kudumu na si kila siku kuweka plasta mpya!
Mkuu Kishoka,
Wacha utani bwana! Matatizo ya Tanesco yameniongezee gharama ya zaidi ya 25% kwenye kamradi kangu.
Mimi ni mmoja tu na si ajabu kuna Wafanyabiashara zaidi ya milioni ambao ni real victims wa haya malumbano.
Halafu eti tunatakiwa tuzalishe ili tushindane na wenzetu wengine wa dunia? Sahau, kila tunachofanya Watanzania kitakuwa bei juu mno kuliko nchi nyingi.
Binafsi sina huruma yoyote na mafisadi ila ifike mahali tunaposhughulikia masuala ya kitaifa tuangalie faida ya nchi na wala sio hasara kwa mbaya wetu mmoja.
Ni sawa tumeachana na Dowans lakini pia tutafute njia nyingine za uhakika kwa haraka.
Mfano Kiwira inakufa kwasababu ya ufisadi wa Mkapa, mimi ningeona wabunge wetu wako serious kama wangeilazimisha serikali kuutaifisha huo mradi mara moja ili uongozwe na wananchi wasio na scandal na uweze kupata baraka za kuzalisha umeme kwa faida ya nchi.
Sasa mitambo inakufa, wanaoweza wanachota vyao na kuvunja vunja mali mbalimbali za mgodi. Sawa tumewakomoa MKapa na rafiki yake Yona, lakini je kwanini tuendelee kuwakomoa pia mamilioni ya Watanzania?
Kuna haja ya kuwapa Tanesco meno na hizo nafasi zote za uongozi hapo kutangazawa ili wenye sifa waombe na kupewa majukumu ambayo inatakiwa wayatekeleze. NI muhimu kufuata ushauri wa wataalamu wetu, wakichemsha wawajibike hapo hapo.
Hii ya wanasiasa kutuamulia kwenye mambo makubwa kama sera ya nishati naona itatuletea matatizo mengi sana.
Kwa mimi kama raia ninachotaka ni umeme, kwenye haya malumbano kuna real victims wengi sana ambao hata hatuna sauti kwenye sera ya nishati Tanzania.
Mimi siamini katika hii miradi mikubwa mikubwa ya nishati maana ina matatizo yake mengi sana. Tungegawa nishati yetu hata kwenye maeneno kama 100 madogo madogo na ambayo yanaungana pamoja. Tuna makaa ya mawe, tuna jua la kutosha, tuna bahari kuanzia kaskazini mpaka kusini, lakini bado tunataka generator moja lizalishe umeme wa robo nchi huku hata uwezo wa kutengeneza hizo generator hatuna?