Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Phillemon Mikael,
Mkuu walioingia mkataba na IPTL, Songas, Richmond/Dowans ni TANESCO..hivyo huwezi kutenganisha serikali na Tanesco ikiwa nchi yetu bado inaendeshwa Kikomunist.. nachokataa mimi ni pale unapotenganisha Tanesco na serikali wakati Idrissa amechaguliwa na rais kushika wadhifa huo. Hili sio shirika huru mkuu wangu, tunadanganyana tu kwani ni watu wale wale wangekuwa madarakani kama lingekuwa shirika la Umma chini ya Ujamaa.. Hawa wote wanatakiwa kulaumiwa, Toka Mwinyi, Mkapa hadi Kikwete ahadi hizi zilikuwepo hazikuanza jana, hawa wote wanakula sahani moja isipokuwa wanalala vitanda tofauti..Mwenye donge mkononi sasa hivi ni Idrissa na lazima alaumiwe yeye kwani maamuzi yake ndio yatakayo tuweka kizani - hadi lini Mungu ndiye anajua...
 
The only way out ni kutochagua CCM

Utekelezaji wa hilo ni kama ndoto za alinacha. Hakuna mbadala wa CCM for the next 10 years, Kikweke na CCM will obviously rule until 2015. Huo ndio ukweli hata kama ni mchungu.

Hakuna upinzani Tanzania ulio na nguvu kiasi cha kuweza kuongoza nchi!
 
Mtaambiwa kutoa order mpaka mitambo itengenezwe ni miaka 2 kisha kuship hiyo mitambo TZ itatumia zaidi ya mwaka 1 kutokana na ships zipo busy sana.Mtaambiwa kuja mafundi kuifunga kwenye grid ya taifa watachukua mwaka kutokana na economic crisis.Watakwambia ndo maana tunataka mitambo ya DOWANS kwa vile ipo hapa hapa TZ.Ukipiga hesabu hapo tayari uchaguzi mwingine

Gizaa 2010? atakuwa katusaidia ................. twalitaka giza neneeeeeeee mpaka 2012!!!
 
Kipa,
Kikwete ana makosa na mapungufu yake lakini sio ktk hili..Ikiwa sisi tumeshindwa hata kutumia vizuri fedha zilizotolewa kwa dharura kweli tunaweza jenga nchi ktk miradi ya muda mrefu..Trust me vyama vinginevyo vilivyoletea Uhuru barani..waliobakia wote ni madikteta tu!

....kaka kikwete ana lawama zake kwa kuwa makaburasha ya mahitaji ya tanesco alipewa tangu mwaka 2006 ....hajatekeleza hata moja ........so tumuiteje???

hali ya tanesco kifedha ni hohehahe wanategemea kutukamua sisi wanachi...

for that i have a reason kuendelea kumpenda mwalimu nyerere...kwani hadi sasa uwanja wa ndege tunaotumia arusha,kilimanjaro,dar,mtwara everywhere alijenga yeye....

umeme wa bei nafuu tunaotumia leo wa mabwawa ya maji alijenga yeye...na mengine mengi..baada ya hapo ni sarakasi tu..!!
 
Phillemon Mikael,
Mkuu walioingia mkataba na IPTL, Songas, Richmond/Dowans ni TANESCO..hivyo huwezi kutenganisha serikali na Tanesco ikiwa nchi yetu bado inaendeshwa Kikomunist.. nachokataa mimi ni pale unapotenganisha Tanesco na serikali wakati Idrissa amechaguliwa na rais kushika wadhifa huo. Hili sio shirika huru mkuu wangu, tunadanganyana tu kwani ni watu wale wale wangekuwa madarakani kama lingekuwa shirika la Umma chini ya Ujamaa.. Hawa wote wanatakiwa kulaumiwa, Toka Mwinyi, Mkapa hadi Kikwete ahadi hizi zilikuwepo hazikuanza jana, hawa wote wanakula sahani moja isipokuwa wanalala vitanda tofauti..Mwenye donge mkononi sasa hivi ni Idrissa na lazima alaumiwe yeye kwani maamuzi yake ndio yatakayo tuweka kizani - hadi lini Mungu ndiye anajua...


hizi ndizo zile fikra potofu za mwenyekiti kikwete pale anaposema kuwa kwwa kuwa wenzake walikosea pia huko nyuma hawana haki ya kumuambia anapokosea...yaani leo mkandara kijana wako akatae unapomkosoa ili asitumbukie pale ulipotumbukia kwa kuwa tu kuna jirani alimuambia kuhusu ukorofi wako ulipokuwa kijana!

hata ukianza kulaumu tangu 1985 up....haisaidii kwa kuwa wale wameshastaafu hawawezi kurekebisha ..mwenye jukumu la kurekebisha sera ya nishati ni kikwete...tena hizi lawama za kuangalia nyuma hazisaidii ...ukipewa kazi unaaipokea pamoja na changamoto na failures za watangulizi wako...

nadhani unajuwa kuwa TANESCO inaingiliwa sana na wanasiasa,,...hata wakati ule wa richmond waliingiliwa sana....wenzetu kenya shirika lao la umeme walilikwamua wakauzia hisa wananchi...leo hii bodi inaendeshwa na wananchi...hakuna siasa tena!

siasa inadumaza .....njia za umeme zisizokuwa na faida kwa shirika zinajengwa kisiasa..nk....

shirika hili linatakiwa kuutadhiminiwa na mtaji unaohitajika ujulikane ....wananchi wazawa wauziwe hisa...tuliendeshe...sio sehemu ya kuchukulia pesa za kampeni pale....wajumbe wa bodi wawe wasomi sio wanasiasa.....
 
As long as Rashid is the Tanesco managing Directoir, he is going to make sure that he creates power shortage so that he can justify his stand for wanting to buy Dowan's generatos; the sooner Rashid is flashed out of Tanesco the more likely we shall not have any power rationing soon!! I stand to be corrected but if Rashid remains in Tanesco ,by next month this country will experience severe power shortage inspite of the abundant rains currently available in many parts of the country!!
 
Kama kukaa gizani tumekwisha zoea, huku mijini tumelowea tu; moreover the majotity of our people who live in rural Tanzania have no electricity!! Hawa mafisadi safari hii lazima tuwakomalie wale wa chuya swine!!
 
No. Hakuboronga huko kote na ndio maana kapewa Tanesco aiweke sawa, ilikuwa hoi bin taabani, Dr. Rashid ndio aliyoi-save, na madudu yote ya Tanesco kayakuta na ndio anajaribu kuiweka sawa.

Kama hajaboronga huko kote alikotoka na kaletwa kuokoa shirika hili, haya madudu yote tunayoyaona ni ya nini?

BOT hali kadhalika, aliyakuta madudu akaweka sawa na alipoondoka tu, madudu yakaanza upya, matokeo yake nadhani mnayafahamu.

Matokeo ya BOT siyafahamu. Kama unayo tupatie. Lakini kubwa ninalojua ni pesa alizowekewa na Chenge kwenye account yake.

Voda, kaifanyia kuwa kampuni ya mawasiliano yenye nguvu (kwa idadi ya wateja na mapato) kuliko kampuni nyingine yeyote ya simu Tanzania.

Inawezekana. Hata hivyo Voda ni kitu kingine kabisa. Watanzania hatushindwi kuendesha mashirika yetu hata siku moja. Pia tunapenda kujikomba sana kwa waajiri, na hasa hasa kama ni wageni. Hebu angalai jinsi tunavyojikomba kwa wahindi na wazungu. Kwa hiyo sitashangaa kama alifanya maajabu Voda lakini anafanya vituko TANESCO!. Hata hivyo ni wakubwa wale wale waliofilisi mashirika ya umma ambao sasa ni matajiri wakubwa katika nchi hii na wanaendesha makapuni yao kwa faida ya kutisha!🙄

Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni!
Hilo sina taabu nalo kwa sababu sina chuki na mtu binafsi, bali kiongozi anayefanya fyongo kwenye mambo ya muhimu kwa nchi yetu. Nikiridhishwa bila shaka yoyote kuwa hana maslahi binafsi kwenye yale anayoyafanya nitampigia hata saluti!!🙂
 
This is a great opportunity for us to show Taifa and everyone that we are not vihiyo and we will not be taken for granted.

Swali la kwanza, je mahitaji ya Umeme Tanzania ni kiasi gani kwa mwaka?
Pili, mabwawa yetu ya umeme yanazalisha umeme wa kiasi gani?
tatu umeme wa Songosongo, Agreko na IPTL ni wa kiasi gani kwa mwaka?
nne, umeme wa kutumia mafuta ni kiasi gani kwa mwaka na ni asilimia gani katika gridi zima la umeme wa Taifa?

Tukishamalizana na haya, tujiulize, ni kwa nini mabwawa ya Mtera, Kidatu, Pangani, Nyumba ya Mungu na mengineyo yanayozalisha umeme hayawezi kutosheleza umeme nchi nzima? je yanazalisha kwa uwezo gani sasa hivi kuwiana na uwezo kamili?

Tukishapata haya majibu, ndipo tuje kwenye majibu ya ama kununua mitambo mipya, au kutumia fedha zilizopo au ambazo zingetumika kununua hii mitambo ya dharura kwa kufufua na kuboresha vizalisha nishati vilivyopo.

Kama sikosei, Richmond ulikuwa mradi wa umeme wa dharura. Wakati huo huo, IPTL inazalisha umeme wa ziada (dharura) ambao hatuuhitaji. Je iweje leo tukimbilie kuongeza umeme wa dharura kwa gharama za milele?

Kwa nini hizo pesa za kununua mitambo chakavu zisitumike kununua mitambo ya umeme wa upepo au jua kama si kwenda Siemens, GE au Mitsubishi?

Kwa nini tusijenge basi power plant mpya kama tutakaa tukikwepa kuijenga hoover dam yetu pale Rufiji kama Rubada wanavyotuambia?

Nimekwend Siemens, kuna mitambo powa ya kutusaidia and so is GE. I would rather see that we spend money to build a reliable and durable power plant and not patch our energy shortages through dubious deals like IPTL or Richmond.

The fact is the cost of money spent to pay IPTL and Richmond, could have as well be spent to purchase a Siemens SST-6000 which could generate up to 500 mw http://www.powergeneration.siemens.com/products-solutions-services/products-packages/steam-turbines/scale+larger+150mw/sst-6000-series/sst-6000-series.htm or Ge H system capable of producing up to 520 mw http://www.gepower.com/prod_serv/products/gas_turbines_cc/en/h_system/index.htm

This coming Monday if not Tuesday, I will call siemens and GE and ask for pricing of their 200+ megawats turbines and then we can compare notes with Dr. Rashid and Minister Ngeleja!

But who am I to talk power and energy while I am not an expert in engineering or energy but mbwabwajaji?
 
This is a great opportunity for us to show Taifa and everyone that we are not vihiyo and we will not be taken for granted.

Swali la kwanza, je mahitaji ya Umeme Tanzania ni kiasi gani kwa mwaka?
Pili, mabwawa yetu ya umeme yanazalisha umeme wa kiasi gani?
tatu umeme wa Songosongo, Agreko na IPTL ni wa kiasi gani kwa mwaka?
nne, umeme wa kutumia mafuta ni kiasi gani kwa mwaka na ni asilimia gani katika gridi zima la umeme wa Taifa?

Tukishamalizana na haya, tujiulize, ni kwa nini mabwawa ya Mtera, Kidatu, Pangani, Nyumba ya Mungu na mengineyo yanayozalisha umeme hayawezi kutosheleza umeme nchi nzima? je yanazalisha kwa uwezo gani sasa hivi kuwiana na uwezo kamili?

Tukishapata haya majibu, ndipo tuje kwenye majibu ya ama kununua mitambo mipya, au kutumia fedha zilizopo au ambazo zingetumika kununua hii mitambo ya dharura kwa kufufua na kuboresha vizalisha nishati vilivyopo.

Kama sikosei, Richmond ulikuwa mradi wa umeme wa dharura. Wakati huo huo, IPTL inazalisha umeme wa ziada (dharura) ambao hatuuhitaji. Je iweje leo tukimbilie kuongeza umeme wa dharura kwa gharama za milele?

Kwa nini hizo pesa za kununua mitambo chakavu zisitumike kununua mitambo ya umeme wa upepo au jua kama si kwenda Siemens, GE au Mitsubishi?

Kwa nini tusijenge basi power plant mpya kama tutakaa tukikwepa kuijenga hoover dam yetu pale Rufiji kama Rubada wanavyotuambia?

Nimekwend Siemens, kuna mitambo powa ya kutusaidia and so is GE. I would rather see that we spend money to build a reliable and durable power plant and not patch our energy shortages through dubious deals like IPTL or Richmond.

The fact is the cost of money spent to pay IPTL and Richmond, could have as well be spent to purchase a Siemens SST-6000 which could generate up to 500 mw http://www.powergeneration.siemens.com/products-solutions-services/products-packages/steam-turbines/scale+larger+150mw/sst-6000-series/sst-6000-series.htm or Ge H system capable of producing up to 520 mw http://www.gepower.com/prod_serv/products/gas_turbines_cc/en/h_system/index.htm

This coming Monday if not Tuesday, I will call siemens and GE and ask for pricing of their 200+ megawats turbines and then we can compare notes with Dr. Rashid and Minister Ngeleja!

But who am I to talk power and energy while I am not an expert in engineering or energy but mbwabwajaji?
 
This is a great opportunity for us to show Taifa and everyone that we are not vihiyo and we will not be taken for granted.

Swali la kwanza, je mahitaji ya Umeme Tanzania ni kiasi gani kwa mwaka?
Pili, mabwawa yetu ya umeme yanazalisha umeme wa kiasi gani?
tatu umeme wa Songosongo, Agreko na IPTL ni wa kiasi gani kwa mwaka?
nne, umeme wa kutumia mafuta ni kiasi gani kwa mwaka na ni asilimia gani katika gridi zima la umeme wa Taifa?

Tukishamalizana na haya, tujiulize, ni kwa nini mabwawa ya Mtera, Kidatu, Pangani, Nyumba ya Mungu na mengineyo yanayozalisha umeme hayawezi kutosheleza umeme nchi nzima? je yanazalisha kwa uwezo gani sasa hivi kuwiana na uwezo kamili?

Tukishapata haya majibu, ndipo tuje kwenye majibu ya ama kununua mitambo mipya, au kutumia fedha zilizopo au ambazo zingetumika kununua hii mitambo ya dharura kwa kufufua na kuboresha vizalisha nishati vilivyopo.

Kama sikosei, Richmond ulikuwa mradi wa umeme wa dharura. Wakati huo huo, IPTL inazalisha umeme wa ziada (dharura) ambao hatuuhitaji. Je iweje leo tukimbilie kuongeza umeme wa dharura kwa gharama za milele?

Kwa nini hizo pesa za kununua mitambo chakavu zisitumike kununua mitambo ya umeme wa upepo au jua kama si kwenda Siemens, GE au Mitsubishi?

Kwa nini tusijenge basi power plant mpya kama tutakaa tukikwepa kuijenga hoover dam yetu pale Rufiji kama Rubada wanavyotuambia?

Nimekwend Siemens, kuna mitambo powa ya kutusaidia and so is GE. I would rather see that we spend money to build a reliable and durable power plant and not patch our energy shortages through dubious deals like IPTL or Richmond.

The fact is the cost of money spent to pay IPTL and Richmond, could have as well be spent to purchase a Siemens SST-6000 which could generate up to 500 mw http://www.powergeneration.siemens.com/products-solutions-services/products-packages/steam-turbines/scale+larger+150mw/sst-6000-series/sst-6000-series.htm or Ge H system capable of producing up to 520 mw http://www.gepower.com/prod_serv/products/gas_turbines_cc/en/h_system/index.htm

This coming Monday if not Tuesday, I will call siemens and GE and ask for pricing of their 200+ megawats turbines and then we can compare notes with Dr. Rashid and Minister Ngeleja!

But who am I to talk power and energy while I am not an expert in engineering or energy but mbwabwajaji?
 
Rev. Kishoka,

Mbona kama TANESCO wamejibu mengi ya maswali yako? Soma tena statement ya TANESCO.

Muhimu sasa ni wapi kwa kupata mtambo mpya kwa bei poa ambao utaokoa taifa kutoka kwenye hasara ambayo tunaingia sasa.

Wakati tunaendelea kulumbana kuna watu wengi tunaendelea kuathirika na ukosefu wa umeme kwenye shughuli tunazofanya. Matokeo yake serikali inakosa pesa kupitia kodi na pia mnunuzi anaishia kulipa pesa zaidi kufidia gharama za generators na mafuta pamoja na kupungua kwa uzalishaji.

Inabidi serikali ije na jibu la haraka vinginevyo tishio la TANESCO huenda kweli likatokea. Kuna sehemu ambazo nazijua mimi tayari zinapata umeme 20% ya muda na hiyo ni March, sijui ikifika September itakuwaje?

Nafikiri njia nzuri kwa sasa ni kuikabidhi hii tender kwa bunge ili watatua matatizo ya umeme Tanzania. They have talked the talk, may be it is a right time to let them walk the walk. Sisi tunachotaka ni umeme, longo longo zingine hazitusaidii kitu.
 
Rev. Kishoka,

Mbona kama TANESCO wamejibu mengi ya maswali yako? Soma tena statement ya TANESCO.

Muhimu sasa ni wapi kwa kupata mtambo mpya kwa bei poa ambao utaokoa taifa kutoka kwenye hasara ambayo tunaingia sasa.

Wakati tunaendelea kulumbana kuna watu wengi tunaendelea kuathirika na ukosefu wa umeme kwenye shughuli tunazofanya. Matokeo yake serikali inakosa pesa kupitia kodi na pia mnunuzi anaishia kulipa pesa zaidi kufidia gharama za generators na mafuta pamoja na kupungua kwa uzalishaji.

Inabidi serikali ije na jibu la haraka vinginevyo tishio la TANESCO huenda kweli likatokea. Kuna sehemu ambazo nazijua mimi tayari zinapata umeme 20% ya muda na hiyo ni March, sijui ikifika September itakuwaje?

Nafikiri njia nzuri kwa sasa ni kuikabidhi hii tender kwa bunge ili watatua matatizo ya umeme Tanzania. They have talked the talk, may be it is a right time to let them walk the walk. Sisi tunachotaka ni umeme, longo longo zingine hazitusaidii kitu.

Ndugu yangu Mtanzania,

Majibu ay tanesco unayoyazungumzia ni viraka, ambavyo tulivifanyia kazi 1993-95 tukaleta IPTL, kisha tukarudia tena 2006-2007 na Richmond.

Kama ni hasara, mbona tunaingia hasara kubwa wala si kupitia uzalishaji bali ni ufujaji mali na ufisadi?

Hao hao Tanesco na Serikali si ndio waliotuingiza hasara na mikataba ya IPTL na Richmond na wananchi tunabebeshwa mzigo wa uzembe na uroho wa wachache kwa kulipia gharama kubwa bila sababu?

Au turudi nyuma zile enzi za Mzee Ruksa walipokataa kusafisha Mtera na Kidatu kisha kukafunguliwa uhuru wa kununua majenereta?

Ninachopinga mimi ni ngonjera kila baada ya miaka miwili au mitatu, aah kuna gharika inakuja, tuoeni pesa tuzipe ukuta wa mashua, kwa nini tusinunue mashua mpya au kujenga kingo thabiti kukabili mawimbi ya gharika?

That is why narudi kuhoji kiwango cha mahitaji yetu ya umeme kwa ujumla, si tulichoambiwa na Dr. Rashidi kuwa tutakuwa na upungufu wa megawati 100!

Infact hata power rationing ikifanyika vizuri na kwa mipango sahihi, tunaweza kudunda vilevile bila karaha mpaka pale tutakapokuja na suluhisho la kudumu na si kila siku kuweka plasta mpya!
 
Nasikitika kusema kuwa uwezo wa Dr Rashid kuendesha TANESCO umefikia mwisho, kwa kuwa TANESCO haina Strategic Plan yake ya miaka walau 5 tu? Ni aibu kwanini kila siku wanakimbilia zima moto, hawakuwa na fall back position baada ya mafisadi kuvunjiwa mikatana yao? hapa ndipo nashindwa kuwaelewa WaTZ. Jamaa amedeclare kuwa ameshindwa pia na TANESCO kwa kushindwa kuweka malengo ya muda mrefu na ndio maana anatutishia. WaTZ tuamke, MJOMBA mtimue kazi Dr Rashid (yawezekana PhD yake pia ni kama za wale wa CCM wanaojaribu kuzihalalisha)
 
Kasheshe,
Mkuu unakosea hapa unaposema wa kulaumu ni serikali wakati aliyetaka kununua mitambo hii ni TANESCO hali fedha zinatoka serikalini ambako wewe unasema huchukua forever..

Mkandara,

Siamini mchambuzi makini kama wewe, unataka kusema uwekezaji wote ule mkubwa haukuwa unafanywa na serikali... in short fedha nyingi za uwekezaji zimekuwa zinapatikana kwa njia ya mikopo ambayo serikali ndio ikilipa.

Siku zote mikataba mikubwa ilikuwa ikisainiwa na serikali na nadhani bond zote zimekuwa hivyo.

TANESCO hawakusema wanataka kununua mtambo wa DOWANS walisema wanaomba serikali inunue mtambo wa DOWANS.

Tuwe makini TANESCO hawana fedha za uwekezaji fedha walizonazo ni za operations and maintenance.

Bado sijaona kwa nini lawama zinapelekwa TANESCO yet serikali ndio haikuwekeza kwenye sekta ya UMEME kwa muda mrefu,.
 
Nasikitika kusema kuwa uwezo wa Dr Rashid kuendesha TANESCO umefikia mwisho, kwa kuwa TANESCO haina Strategic Plan yake ya miaka walau 5 tu? Ni aibu kwanini kila siku wanakimbilia zima moto, hawakuwa na fall back position baada ya mafisadi kuvunjiwa mikatana yao? hapa ndipo nashindwa kuwaelewa WaTZ. Jamaa amedeclare kuwa ameshindwa pia na TANESCO kwa kushindwa kuweka malengo ya muda mrefu na ndio maana anatutishia. WaTZ tuamke, MJOMBA mtimue kazi Dr Rashid (yawezekana PhD yake pia ni kama za wale wa CCM wanaojaribu kuzihalalisha)

Bado mnarukia mambo...

TANESCO wanayo master plan... lakini serikali haitoi resources za kuitekeleza! TANESCO imekuwa kama mwendeshaji tu wa kilichopo of course kama mwenye mali haleti hela.
 
Rev. Kishoka,

Mbona kama TANESCO wamejibu mengi ya maswali yako? Soma tena statement ya TANESCO.

Muhimu sasa ni wapi kwa kupata mtambo mpya kwa bei poa ambao utaokoa taifa kutoka kwenye hasara ambayo tunaingia sasa.

Wakati tunaendelea kulumbana kuna watu wengi tunaendelea kuathirika na ukosefu wa umeme kwenye shughuli tunazofanya. Matokeo yake serikali inakosa pesa kupitia kodi na pia mnunuzi anaishia kulipa pesa zaidi kufidia gharama za generators na mafuta pamoja na kupungua kwa uzalishaji.

Inabidi serikali ije na jibu la haraka vinginevyo tishio la TANESCO huenda kweli likatokea. Kuna sehemu ambazo nazijua mimi tayari zinapata umeme 20% ya muda na hiyo ni March, sijui ikifika September itakuwaje?

Nafikiri njia nzuri kwa sasa ni kuikabidhi hii tender kwa bunge ili watatua matatizo ya umeme Tanzania. They have talked the talk, may be it is a right time to let them walk the walk. Sisi tunachotaka ni umeme, longo longo zingine hazitusaidii kitu.

NO.. NO.. NO.. Sir! Kazi ya bunge sio hiyo. Kama uongozi wa tanesco umeshindwa na ujiondoe upishe wenye kuweza. Wapo Watanzania wengi tu wanaoweza kuiongoza tanesco kwa ufanisi.
 
Kweli Rev this is the time to source brand new generators from reputable companies in the international scene. Due to current economic problems in west, companies will bend backwards to build generators from ground up (even off shelf if possible) and a good price can be negotiated to our advantage. Anything to offer them business in these difficult times they'll take.

And why the conflicting message Idris, how come all of a sudden this has turned in a power scare and giza litaingia kesho? When Ngeleja himself said the other day, we are fine at the moment and buying Dawan is meant to help address foretasted increase. Which is a regular planned increase of capacity than an emergency if I understood correctly.

I tend to agree that a power rationing regime can take us through until such a time when new generators are acquired to address mid term power requirements. In the current climate, it is a slow time worldwide so there is no need for much for heavy duty local needs such as industrial (if we have any) which can be channelled to other use.

The long term plans that Tanesco has been talking about can then be phasened in as conditions change.
 
Mkandara,
TANESCO hawakusema wanataka kununua mtambo wa DOWANS walisema wanaomba serikali inunue mtambo wa DOWANS.

Tuwe makini TANESCO hawana fedha za uwekezaji fedha walizonazo ni za operations and maintenance.

Bado sijaona kwa nini lawama zinapelekwa TANESCO yet serikali ndio haikuwekeza kwenye sekta ya UMEME kwa muda mrefu,.

Kasheshe, serikali inabidi kulaumiwa kwa sababu inafanya manunuzi ambayo hayana maendeleo yoyote kwa Watanzania. Kwa mfano uamuzi wa kununua mashangingi kati ya 800 mpaka 1,000 na shangingi moja lina gharama kati ya shilingi milioni 100 mpaka milioni 150. Hizi pesa zingeelekezwa TANESCO basi tungeweza kabisa labda kununua mitambo mipya ya kuzalisha umeme.

Pia ni sawa kabisa kuilaumu serikali kwemye huu mkanganyiko. Kama utakumbuka Waziri wa Nishati William Ngeleja November 2008 alitwambia Watanzania kwamba serikali imeamua kutonunua mitambo ya Dowans. Kigeugeu chake miezi minne baadaye kwamba serikali inabidi inunue mitambo ya Dowans kinastahili lawama. Pia taratibu za manunuzi serikalini haziruhusu kununua mitambo ambayo ni michakavu.

Hebu fikiria hasara ambayo serikali itapata kama inanunua mitambo hiyo michakavu kwa shilingi 60 billioni haijulikani mitambo hiyo imeshafanya kazi kwa muda gani maana Dowans hawakuinunua ikiwa mipya, haina warranty halafu baada ya mwaka mmoja inashindwa kufanya kazi. Serikali itakimbilia wapi kama hilo likitokea!?

Hapa Idrisa Rashid, William Ngeleja wote wamechemsha vibaya sana. Niliwahi kusema hapa kwamba Ngeleja wizara ya nishati imemshinda na kwa mara nyingine tena imethibitika hivyo. Huyo Idrissa Rashid kwa maoni ya Watanzania wengi alitakiwa kuondolewa TANESCO siku nyingi sana hatuelewi ni kitu gani kinachoendelea cha kumfanya aendelee kuwepo TANESCO kama Mkurugenzi Mtendaji. Kauli aliyoitoa kwamba TANESCO isiulamiwe pindi nchi itakapoingia kizani inatosha kabisa kumfukuzisha kazi labda mkuu wake wa kazi atamuomba ajiuzulu haraka ili aendelee kulipwa mafao yake maana akimfukuza kazi basi hastahili kulipwa chochote.
 
Back
Top Bottom