Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Dowans wanauwezo wa kuzalisha hiyo 100MW kwa namna gani?

Mwanakijiji, kwenye hili swala la Dowans, Mkuu hueleweki.

Mwanzoni ulisema tuwaachie huru wa kina Gire na nunue mitambo, na kwamba Rostam ameshatushinda and what not.

Baadae ukamtetea Zitto, japo ukasema hukubaliani na mahitimisho yake.

Ulipoulizwa mahitimisho yako wewe ni yapi ukasema tukasome Cheche.

Kwenye Cheche kuna mahitimisho ya Jessica Fundi na Fred Katunzi.

Sasa basi, kwa sababu kwenye hili swala wewe kama Mwanakijiji unaogopa kuchukua msimamo mimi nadhani sio busara kujadili kitu na ghosti Jessica na ghosti Fredi!

Sijaona swali lilipojibiwa!
 
Na Mwandishi wetu

SUALA la ununuzi wa mitambo ya umeme ya Dowans, linazidi kuchukua sura mpya baada ya Waziri Mkuu Mstaafu, Joseph Warioba kusema malumbano yanayoendelea kati ya Kamati za bunge na wabunge yanaonyesha kuna mgawanyiko ndani ya bunge.


Katika majibu yake kwa Mwananchi Jumapili, Warioba alisema malumbanano kuhusu suala la mtambo wa umeme ni jambo la kushangaza kwani ununuzi wa bidhaa na huduma ni kazi ya serikali.


Alisema sheria, kanuni na taratibu zipo, hivyo serikali inaweza kuzitumia bila ya kutaka maoni ya bunge na kwamba hata kama ni dharura pia kuna kanuni na taratibu zake.


" Inakuwa vingumu kuelewa kwa nini Serikali ilipeleke suala la ununuzi wa mtambo wa umeme kwenye kamati ya Bunge. Inaonekana kama ni njia ya kukwepa lawama za kisiasa au kukwepa wajibu," alisema.


Maoni hayo ya Warioba yamekuja wakati kamati mbili za bunge tayari zikiwa katika mvutano mzito, moja ikitaka inunuliwe na nyingine ikipinga.


Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, chini ya Mwenyekiti wake, William Shelukindo imeshakataa kulipa baraka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco ) kununua mitambo hiyo kwa madai kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria ya manunuzi, huku kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, chini ya Mwenyekiti wake, Zitto Kabwe imeamua inunuliwe ili kunusuru taifa na giza.


Warioba alisema cha kushangaza zaidi kuhusu jambo hili ni jinsi wabunge walivyochangamkia suala hili huku wanajua kwamba siyo kazi ya Bunge kujihusisha na maamuzi ya utekelezaji.


Warioba alihoji " Kwa nini Kamati za Bunge zimekubali kupokea na kuzungumzia suala ambalo haliwahusu?


Hata hivyo, alisema tatizo kubwa la nchi ni kupata umeme wa kutosha hivyo, tuzungumzie hilo badala ya malumbano ambayo hayatuongezei umeme.


Alishauri bunge na wabunge wafanye kazi ya kusimamia, siyo kutenda na kwamba wasihangaike kusaka nyaraka za serikali ili wapeleke hoja bungeni kwa mambo ambayo ni ya utendaji.


Warioba alisema hoja binafsi ni kitu kizuri, lakini bunge ni lazima liwe makini kuangalia ni hoja gani zinaambatana na kusimamia utendaji na ni hoja zipi zinaliingiza bunge jikoni.


Alionya kwamba bunge limeanza kuingilia madaraka ya serikali na mahakama ingawa limekuwa likijitetea ukweli ni kwamba Bunge limekwenda nje ya madaraka yake limejichukulia hata madaraka ya kutafasiri sheria ili kuhalalisha maamuzi yake.


Hata hivyo, jana Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk Idrisa Rashid juzi alitangaza rasmi kujitoa katika ununuzi wa mitambo yenye utata wa kufua umeme ya dharura Dowans Tanzania na kueleza kuwa hospitali zitakaposhindwa kutoa huduma asilaumiwe.


Alisema wamefikia hatua hiyo baada ya kuona mwelekeo wa suala hilo linatupeleka kwenye ugonvi wa wanasiasa, jukwaa ambalo sisi hatuna mamlaka nalo.


Warioba pia alivionya vyombo vya habari kuwa navyo hivi sasa vimekumbatia suala moja tu la ufisadi kwa kiwango cha ajabu.


Alisema mahakama zinazosikiliza kesi za ufisadi zimegeuka kuwa ni kumbi za kupatia habari habari kwa waandishi na kwamba taarifa kutoka mahakamani zinapewa kipaumbele katika vyombo vyote na zinaandikwa kwa kirefu.


Alisema upungufu wa chakula, kushindwa kuuza marobota ya pamba, Kampuni ya Barrick kujitoa kwenye mradi wa umeme wa kusini ni habari za kupita ambazo hazipatiwi umuhimu unaostahili.


Warioba alisema uchumi wa dunia utakuwa katika matatizo kwa kipindi cha miaka miwili mitatu au zaidi, kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania utapungua na mfumko wa bei utapanda.


"Watu watapoteza kazi na wahitimu wa elimu watakosa kazi. Wateja wa wafanya biashara watapungua kwa sababu ya kupanda bei. Bei ya mafuta imepungua lakini uchumi wa nchi kubwa ukitulia mafuta yatapanda bei na nchi ndogo zitapata matatizo zaidi,"alisema .


Alisema katika hali hii tuweke pembeni tofauti zetu za itikadi, makundi na mitandao kila taasisi ielekeze nguvu kwenye matatizo ya uchumi ili watu wengi wakatumia matatizo ya njaa katika uchaguzi mkuu kununua wananchi.


" Mwaka kesho ni mwaka wa uchaguzi. Katika mwaka wa uchaguzi maamuzi magumu hukwepwa. Lakini tusipolivalia njuga suala la uchumi tunaweza kuingia kwenye kipindi cha uchaguzi wakati watu wana njaa, wengine watakuwa wamepoteza kazi na wengine wanashindwa kupata kazi.


" Tunaweza kuwa na uchaguzi wenye uchafu kuliko ilivyotokea huko nyuma. Wenye fedha watatawala na kununua uchaguzi kwa takrima," alisema.
 
Ni za kuwatetea wananchi. ... yaani mnataka niamini kwamba Watanzania hawawezi kumwamini mtu, na kutofautiana mtazamo katika jambo fulani ndo unakuwa uadui au? Binafsi ninampongeza sana Mhe.Zito kwa kuonyesha mtazamo/msimamo wake wazi. Hawa ndiyo viongozi tunaowahitaji. Tatizo la Watanzania ni 'opportunism' yaani msimamo wa mtu unaangalia upepo, huu ni udhaifu mbaya sana. Ninapata shida juu ya uwezo wetu wa kujua na kuchambua mambo. Lazima tujue kuwa kila mtu anaakili yake na hatuwezi kuwa na mawazo mamoja.
 
Ni za kuwatetea wananchi. ... yaani mnataka niamini kwamba Watanzania hawawezi kumwamini mtu, na kutofautiana mtazamo katika jambo fulani ndo unakuwa uadui au? Binafsi ninampongeza sana Mhe.Zito kwa kuonyesha mtazamo/msimamo wake wazi. Hawa ndiyo viongozi tunaowahitaji. Tatizo la Watanzania ni 'opportunism' yaani msimamo wa mtu unaangalia upepo, huu ni udhaifu mbaya sana. Ninapata shida juu ya uwezo wetu wa kujua na kuchambua mambo. Lazima tujue kuwa kila mtu anaakili yake na hatuwezi kuwa na mawazo mamoja.

Bado sijaelewa unamaanisha nini?
 
Ni za kuwatetea wananchi. ... yaani mnataka niamini kwamba Watanzania hawawezi kumwamini mtu, na kutofautiana mtazamo katika jambo fulani ndo unakuwa uadui au? Binafsi ninampongeza sana Mhe.Zito kwa kuonyesha mtazamo/msimamo wake wazi. Hawa ndiyo viongozi tunaowahitaji. Tatizo la Watanzania ni 'opportunism' yaani msimamo wa mtu unaangalia upepo, huu ni udhaifu mbaya sana. Ninapata shida juu ya uwezo wetu wa kujua na kuchambua mambo. Lazima tujue kuwa kila mtu anaakili yake na hatuwezi kuwa na mawazo mamoja.

Kutofautiana kupo!! Ila hili Mh Zitto alichemka vibaya sana..
 
Bado sijaelewa unamaanisha nini?

Jitihada za ZITTO ni zakuwatetea wananchi ama ni za kimangimeza

hili ndilo swali lako kuu katika thread hii au siyo?
ukisoma vizuri na kuwa tayari kuyakubali mawazo ya wengine, utanielewa.
 
Zitto kachemsha inabidi atafute namna ya kurudisha reputation nzuri aliyokuwa nayo miongoni mwa Watanzania walio wengi. Siku zote Zitto alikuwa anasimama upande mmoja na wananchi katika vita dhidi ya mafisadi, kwenye hili la kushawishi serikali inunue mitambo chakavu ya Dowans alikuwa upande mmoja na mafisadi.
 
Let me pitch in a radical idea. If Serukamba and others feel the need to buy the Dowans lousy turbines, they should give their entitlements for the next 22 months to foot the expenses and this is how we will measure their patriotism. Give up the car, masurufu, imprest and mshahara for next 22 months and thy should add their re-election campaign money so that Watoto wasife hospitali!
 
Kutofautiana kupo!! Ila hili Mh Zitto alichemka vibaya sana..

Zitto kachemsha atafute inabidi namna ya kurudisha reputation nzuri aliyokuwa nayo miongoni mwa Watanzania walio wengi. Siku zote Zitto alikuwa anasimama upande mmoja na wananchi katika ya vita dhidi ya mafisadi, kwenye hili la kushawishi serikali inunue mitambo chakavu ya Dowans alikuwa upande mmoja na mafisadi.

inayetofautiana na wewe au wengi anakuwa amekosea... hiyo ndiyo shida yetu. tunatakiwa kuwapa watu nafasi ya kuonyesha wanachokiwaza au kukiamini sasa sisi tunataka wawe 'opportunists'
 
inayetofautiana na wewe au wengi anakuwa amekosea... hiyo ndiyo shida yetu. tunatakiwa kuwapa watu nafasi ya kuonyesha wanachokiwaza au kukiamini sasa sisi tunataka wawe 'opportunists'

Lakini siyo hili la kubadilisha taratibu zilizowekwa kila kukicha. Sasa hivi Zitto alitaka taratibu za manunuzi ya mitambo michakavu ibadilishwe. Je, hiyo mitambo baada ya mwaka kama ingeshindwa kufanya kazi na haina warranty serikali ingekimbilia wapi ili kuinusuru nchi toka kizani wakati imeshatumia bilioni 60 kununua mitambo chakavu?
 
Ni za kuwatetea wananchi. ... yaani mnataka niamini kwamba Watanzania hawawezi kumwamini mtu, na kutofautiana mtazamo katika jambo fulani ndo unakuwa uadui au? Binafsi ninampongeza sana Mhe.Zito kwa kuonyesha mtazamo/msimamo wake wazi. Hawa ndiyo viongozi tunaowahitaji. Tatizo la Watanzania ni 'opportunism' yaani msimamo wa mtu unaangalia upepo, huu ni udhaifu mbaya sana. Ninapata shida juu ya uwezo wetu wa kujua na kuchambua mambo. Lazima tujue kuwa kila mtu anaakili yake na hatuwezi kuwa na mawazo mamoja.

Zittto hajaonyesha msimamo wowote, na wala hajafanya jitihada zozote. Kinachofanyika sasa ni kuamua kutumia opportunity hii kuongea about Zitto. Kilichozungumzwa na kamati ya mahesabu ya mashirika ya umma ni msimamo wa kamati nzima na si msimamo wa Zitto kama Zitto. Hapa JF alisema wakati muafaka ukifika atatoa views zake kama Zitto. HIvyo kama mnahitaji kujua views zake juu ya hili inabidi mjiunge nami katika kuwa na subira.
 
Sikonge, hueleweki. Kwanza, fahamu kwamba Nyambala kasema tununue vimitambo vya 1.6MW, wewe unasema tununue mitambo ya 20-50MW. Kwa hiyo hata wewe unacho ki advocate hakiendani na alichosema Nyambala. Kwa kweli umeunga tela pointi kichwa kichwa wakati na wewe mwenyewe huonekani kui support. Pili, kuhusu faida na hasara za mitambao mikubwa na midogo, mimi sikusema ubaya na uzuri wake, ile nimesema Nyambala katoa mfano irrelevant, misrepresented, wa vi generator vya 1.6MW akasema vinafanana na nguvu ya Dowans. Si kweli!

Lakini tukiachana na mifano misreprented wa vijimitambo vya Nyambala, hata wewe umejichanganya. Umesema kuna faida ya kununua vijimitambo vidogo kama vya power plant ya Nyambala, halafu hapo hapo unasema utatoa 300MW na ni poa: "...Hii inafaida kubwa kuwa ukiharibika moja ya mtambo mdogo nchini, nchi haiteteleki. Ila sasa mkiwa na mtambo kama huu wanasema ujengwe Rufiji, na unaanza kutoa 300MW, loo ni poa ..." Una maana gani hapo, vimitambo hivi vitatoa 300MW? Hueleweki.

Kuhani,
Naona unakuwa 2PAC sana yaani "Me against the World" na hapo unaacha kusoma massage kwa uhakika. Mie niliandika "...Kama mgodi wanaunganisha unganisha hizo 1.6 MW, kama nchi tunatakiwa tuunganishe unganishe 20-50MW."

Kama ulisoma hesabu, inajulikana kuwa ukifanya interpolation ya harakaharaka utajua kwa vipi Mgodi wa dhahabu unaunganishaunganisha 1.6MW na kama inchi iunganishe kiasi gani? advantage kubwa ya kuwa na vigenerator vidogo ni kuwa kikifa hampati pressure. Ila kama lile la 300MW likafa hapo ndipo nchi inakuwa giza. Ila nikasema kama mkiwa na hayo makubwa kadhaa na vidogo kadhaa na zinafanya kazi kwa kupokezana basi hii ni safi sana. Hata kama kukitokea maongezeko ya utumiaji umeme somewhere basi ni kiasi cha kuwasha generator nyingine zaidi na wakati huohuo mnaanza kutafuta sehemu nyingine ya kuwa na umeme wa akiba.

Sijakataa kuwa na mashine kubwa. Kama zikiwepo hata za 1300MW ni safi tu ila hii ikiwepo si kubweteka kuwa umemaliza kazi. Inatakiwa ziwepo nyingine kukidhi haja ya mahitaji kama Big Brother likiharibika. Ila ukiangalia POCHI letu, tuna hela ya kuwa na hivyo vyote? Ndiyo maana tunasema heri kuwa na nyingi ndogondogo kuliko na mbili kubwa sana.
 
inayetofautiana na wewe au wengi anakuwa amekosea... hiyo ndiyo shida yetu. tunatakiwa kuwapa watu nafasi ya kuonyesha wanachokiwaza au kukiamini sasa sisi tunataka wawe 'opportunists'

Hapana mtu mtetea wananchi na msomi mie binafsi nafikiri alitakiwa kujadili jinsi yakupatikana kwa suluhu ya kudumu.

Kitu kingine mkuu wangu ASSUME wewe una shati lako jamaa lenye maguvu limekuja likakunyang'anya shati lako la bei kali tuseme 20000,mkaenda kwenye baraza la wazee Rafiki yako Juma akawa upande wako kama shaidi mthibitisha ya kwamba hakika lile shati ni lako,Lakini ktuokana na mabavu ya lile jambazi wazee wa baraza wakaamuwa lile shati si lako.

Harafu siku wa siku ikawaidia ukahitaji kununuwa shati maana ktk droo yako huna shati ,Juma akageuka akawa dalali wa lile jamaa akakushawishi ulinunue lile shati lako jambazi alilokukwapua ,Duuuuuuuuuuuuuuu

Totally Confused .
 
Zittto hajaonyesha msimamo wowote, na wala hajafanya jitihada zozote. Kinachofanyika sasa ni kuamua kutumia opportunity hii kuongea about Zitto. Kilichozungumzwa na kamati ya mahesabu ya mashirika ya umma ni msimamo wa kamati nzima na si msimamo wa Zitto kama Zitto. Hapa JF alisema wakati muafaka ukifika atatoa views zake kama Zitto. HIvyo kama mnahitaji kujua views zake juu ya hili inabidi mjiunge nami katika kuwa na subira.
mkuu umesikia mahojiano waliofanya Zitto na Mwakyembe na ITV? Mwakyembe kasema live msimamo wa Zitto si wa kamati yake.....ni wake binafsi na anamshangaa kama ndio Zitto anaemfahamu.....Zitto hakubisha....
 
Zittto hajaonyesha msimamo wowote, na wala hajafanya jitihada zozote. Kinachofanyika sasa ni kuamua kutumia opportunity hii kuongea about Zitto. Kilichozungumzwa na kamati ya mahesabu ya mashirika ya umma ni msimamo wa kamati nzima na si msimamo wa Zitto kama Zitto. Hapa JF alisema wakati muafaka ukifika atatoa views zake kama Zitto. HIvyo kama mnahitaji kujua views zake juu ya hili inabidi mjiunge nami katika kuwa na subira.

Kupenda sana ni ujinga!! Hakutakiwa kukubaliana na kamati kama yeye alikuwa na mtizamo tofauti...nadhani yeye ni mwenyekiti wa hii kamati sina uhakika thou!
 
Hatutaweza kuendelea kabisa kama mtindo ndio huu.

Mtu akudhulumu mali yako kwa round ya kwanza tena arudi kwa raudi ya pili akudhulumu kwa kuuzia kilicho chako hata kama ni bure mimi sikubali ,mimi nitakubali kwa kumnyaganya tu si kunipa bure ama kuniuzia kwa bei nafuu kilicho changu.
 
Sawa,

Kwa hiyo msiseme - maana si kweli - kwamba mashine za 1.6MW za power plant ya kazini kwa Nyambala "zinalingana lingana na za Dowans" ambao wanatoa 100MW. Itabidi muunge unge vijigenerator 62 na ushee! Semeni ukweli. Tatizo la Dowans, again, ni kwamba wako linked to Richmonduli, wana kesi dhidi yetu France, kuna court injuction dhidi yao Tanzania, na mitambo yao michakavu inazua legal quandaries.

Kuhusu 2Pac's "me against the world" mentality, well, inawezekana ndio predicament ninayoi face all the time jamvini, our lifestyles be close captioned, against all odds we carry on. Hata hivyo, I ain't mad at cha!
 
........... Ubaya wa Dowans ni legacy ya ufisadi wa Richmond na kanuni zinazokataza kununua vifaa chakavu.............

PERIOD! maelezo mengine kutaka ku-justfy Dowans ni uhuni uliokubuhu
 
Back
Top Bottom