Zitto, huyo anaeitwa Omary Ambaye kila saa anajitia kukusafisha ama kukutetea hafai hata kidogo kuwa mshauri wako kwani ni kama wale ambao wanaweza kumwambia mfalme umependeza kumbe yuko uchi.
Huyu jamaa anapaswa kuwashauri watu wapenda sifa kama Mzee wa kiraracha pamoja na Mtikila ambao wanapenda kusifiwa kila wanalolifanya ila ukimwendekeza atakupotezea mbali sana .
Huyu jamaa anajifanya kujua kuwa wewe unamsimamo gani ,na anafika mbali zaidi kuwaona wengine ambao wanajaribu kukuonyesha upande wa pili wa shilingi kuwa hawajui wanalolifanya , jiepushe na washauri wa aina hiyo kwani ni watu hatari na hata siku moja ukikosea hawatakuwa tayari kukueleza ukweli wa mambo.
Sijawahi kujiunga humu Jf ila tangu mjadala huu uanze , nimekuwa nikisoma na nimemwona kuanzi thread za mwanzo kabisa akimshambulia kila mtu ambaye anajaribu ama kukuonyesha feeling za jamii na haswa watanzania wengi ambao walikuamini.
Anafika mahali anaandika eti wewe uko tayari kuchukua maamuzi magumu , na anaita hilo unpopular decisions , kwenye ulimwengu huu anayechukua maamuzi magumu sharti awe na uwezo wa kuyatekeleza , wewe unauwezo gani wa kuamua kununuliwa kwa hiyo mitambo kama huo ndio uamuzi mgumu?
Bush alichukua unpopular decisions , na alikuwa na mamlaka ya kufanya yatekelezeke, wewe hizo mamlaka huna mpaka sasa , sasa hao wanaokushauri hivyo jua kuwa ni watu ambao hawakutakii mema , jitahidi sana kuwa msikivu,mpole ila mwerevu kama nyoka .
Nimejiunga humu leo ili niweze kuandika ujumbe huu, niko mbali sana na huko nyumbani ila leo niliongea na watanzania walioko huko na wamenieleza kusononeshwa sana na msimamo wako huo, tafuta njia ya kutoka kwenye mtego.
Namshukuru aliyeanzisha mtandao huu kwani ni wa afya pamoja na wengine kujiandikia tuu kwa sababu wanajua kuwa majina yao sio halisi hivyo hawako responsible kwa chochote watakachoandika.